Facebook Comments Box

Monday, September 23, 2013

TANZANIA YATWAA UBINGWA WA AIRTEL RAISING STARS KWA WANAWAKE


Mkurugenzi mkuu wa Airtel Nigeria Segun Ognsanya Katikati akiwakabithi captain wa timu ya wasichana Tanzania na kocha wa timu ya wasichana Rogacian Kaijage zawadi za ushindi mara baada ya kuibuka mabigwa wa michuano ya Airtel Rising stars ya Afrika  

 
Donisia Daniel ndio alipeleka furaha kwa upande wa Tanzania kwa kufunga bao hilo pekee la ushindi jana.
Tanzania ilikua kundi moja na Sierra-Leone, Malawi, na Uganda. Walishinda mechi moja dhidi ya Sierra-Leone 2-1, wakapoteza mchezo dhidi ya Uganda na kutoka sare na Malawi 1-1.
Malkia wadogo; Tanzania wakiwa na Kombe lao baada ya ushindi

Katika Robo Fainali, mabinti wa kibongo wakashinda 4-2 kwa mikwaju ya penalti dhidi ya DRC Uwanja wa NIS Sports, kabla ya kuifumua Uganda kwa mabai 8-1 kwenye Nusu Fainali.Mbali na ushindi huo wa wasichana wa Tanzania walijishindia zawadi mbalimbali ikiwemo , Mchezaji bora kwa upande wa wasichana Tatu Iddi, Mfungaji bora wa mashindano kwa upande wa wavulana Athanas Mdam na Mfungaji bora kwa upande wa wasichana Shelda Boniface.
 Kwa upande wa wavulana Timu ya Niger wametetea tena ubingwa  baada ya kuifunga Zambia kwa mikwaju ya penati 7-6  katika mechi ya fainali ya Airtel Rising Stars ilifanyika kwenye uwanja wa Agege nchini Nigeria.
Mkurugenzi mkuu wa Airtel Nigeria, Segun Ognsanya Katikati akimkabithi Nahodha wa timu ya wasichana Tanzania, zawadi za ushindi mara baada ya kuibuka mabigwa wa michuano ya Airtel Rising stars ya Afrika


Mwakilishi na kiongozi wa Airtel Tanzania bi Lilian Kibiriti akifurahia ushindi na Wachezaji wa timu ya wasichana ya Tanzania ya Airtel Rising stars mara baada ya kuibuka mabigwa wa michuano ya Airtel Rising stars ya Afrika


Mabingwa; Kikosi cha Tanzania wanawake

Niger wamefanya vizuri kuanzia hatua ya makundi  baada ya kushinda michezo yote katika makundi na kufikisha magoli 12 na kuruhusu magili matatu tu katika mechi sita. Jumla ya mechi 58 zimechezwa katika mashinda.

Aidha timu ya wavulana ya Tanzania imeshikilia nafasi ya nne kati ya timu zaidi ya 16 zilizoshiriki michuano hiyo Michuano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu yamefanyika nchini Nigeria katika viwanja vinne Agege, Township Stadium, Legacy Pitch, National Institute for Sports Fiels na Main Bowl.

Mashindano ya kiamataifa ya umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars yanafanyika kwa mara ya pili mwaka huu na yamekua bora kwa vijana wadogo na kwa kuzingatia jinsia.
CHANZO:BIN ZUBEIRI


Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU