Donisia Daniel ndio alipeleka furaha kwa upande wa Tanzania kwa kufunga bao hilo pekee la ushindi jana.
Tanzania
 ilikua kundi moja na Sierra-Leone, Malawi, na Uganda. Walishinda mechi 
moja dhidi ya Sierra-Leone 2-1, wakapoteza mchezo dhidi ya Uganda na 
kutoka sare na Malawi 1-1.
![]()  | 
| Malkia wadogo; Tanzania wakiwa na Kombe lao baada ya ushindi | 
Katika
 Robo Fainali, mabinti wa kibongo wakashinda 4-2 kwa mikwaju ya penalti 
dhidi ya DRC Uwanja wa NIS Sports, kabla ya kuifumua Uganda kwa mabai 
8-1 kwenye Nusu Fainali.Mbali
 na ushindi huo wa wasichana wa Tanzania walijishindia zawadi mbalimbali
 ikiwemo , Mchezaji bora kwa upande wa wasichana Tatu Iddi, Mfungaji 
bora wa mashindano kwa upande wa wavulana Athanas Mdam na Mfungaji bora 
kwa upande wa wasichana Shelda Boniface.
 Kwa
 upande wa wavulana Timu ya Niger wametetea tena ubingwa  baada ya 
kuifunga Zambia kwa mikwaju ya penati 7-6  katika mechi ya fainali ya 
Airtel Rising Stars ilifanyika kwenye uwanja wa Agege nchini Nigeria.
![]()  | 
| Mabingwa; Kikosi cha Tanzania wanawake | 
Niger
 wamefanya vizuri kuanzia hatua ya makundi  baada ya kushinda michezo 
yote katika makundi na kufikisha magoli 12 na kuruhusu magili matatu tu 
katika mechi sita. Jumla ya mechi 58 zimechezwa katika mashinda.
Aidha timu ya wavulana ya Tanzania imeshikilia nafasi ya nne kati ya timu zaidi ya 16 zilizoshiriki michuano hiyo Michuano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu yamefanyika nchini Nigeria katika viwanja vinne Agege, Township Stadium, Legacy Pitch, National Institute for Sports Fiels na Main Bowl.
Mashindano ya kiamataifa ya umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars yanafanyika kwa mara ya pili mwaka huu na yamekua bora kwa vijana wadogo na kwa kuzingatia jinsia.
CHANZO:BIN ZUBEIRI 




