KWA
 mara ya kwanza, kiungo Amri Ramadhani Kiemba ameibuka na kukanusha 
kusaini Yanga SC, ingawa amesema yeye bado mchezaji huru, kwa kuwa hadi 
sasa hajasaini timu yoyote baada ya kumaliza Mkataba wake Simba SC.
Akizungumza  Kiemba alisema kwamba hajasaini timu yoyote hadi sasa na anajitambua kama mchezaji huru.
Alipoulizwa
 kuhusu mustakabali wake, Kiemba alisema kwa sasa akili yake ipo kwenye 
kuisaidia timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars iweze kukata 
tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia.
“Sasa
 hivi ukiniuliza mambo ya klabu, utakuwa unanionea tu. Nipo katika kambi
 ya timu ya taifa, fikra zangu ni majukumu yangu ya kitaifa. Nadhani 
baada ya hapa, nitazungumzia hayo mambo,”alisema Kiemba.
Kiemba
 aliibua wasiwasi mkubwa kwa wapenzi wa Simba SC, baada ya kuvuma kwa 
habari amesaini Yanga SC, huku Mkataba wake ukiwa umemalizika Msimbazi.
Na anaonekana mtu asiye na wasiwasi kabisa kuhusu mustakabali wake- pengine inatokana na kiwango chake cha juu hivi sasa.
Stars inashika nafasi ya pili 
katika Kundi C, kuwania tiketi ya Kombe la Dunia mwakani Brazil, ikiwa 
na pointi sita nyuma ya Ivory Coast yenye pointi saba, ambayo kesho 
itakuwa ugenini ikimenyana na Gambia katika mchezo mwingine wa kundi 
hilo.
Stars
 ilitua hapa Jumatatu ikitokea Ethiopia ambako iliweka kambi ya wiki 
moja na kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Sudan, ulioisha kwa sare ya 
bila mabao.
Kabla
 ya kuja hapa, Stars iliweka kambi ya wiki moja katika hoteli ya 
Tansoma, Dar es Salaam ikijifua Uwanja wa Karume na siku chache kabla ya
 kuondoka ilialikwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete, aliyewapa hamasa kwa 
hotuba nzuri.
SOURSE: BIN ZUBEIRY 
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
