JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI JESHI LA POLISI TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 
KUHUSIANA NA MAENDELEO YA UPELELEZI WA TUKIO LA MLIPUKO WA BOMU KATIKA 
KANISA LA MT. JOSEPH – OLASITI JIJINI ARUSHA LILILOTOKEA TAREHE 
05/05/2013
Ndugu wanahabari, mtakumbuka kwamba mara 
ya mwisho nilipokutana nanyi niliwaahidi kwamba nitaendelea kuwapa mara 
kwa mara taarifa juu ta maendeleo ya upelelezi wa tukio la mlipuko wa 
bomu lililotokea katika kanisa katoliki la mtakatifu joseph mfanyakazi 
parokia ya olasiti tarehe 05/05/2013 na kusababisha vifo vya watu 
watatu(3) na wengine kudhaa kujeruhiwa.
Kama nilivyowaeleza hapo awali, baada ya 
tukio hilo jumla ya watuhumiwa tisa(9) walikamatwa na kuhojiwa kuhusiana
 na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani. Watuhumiwa haoa ni victor 
Ambros Kalist, (20), dereva wa bodaboda na mkazi wa kwa Morombo; Yusuph 
Lomayani Josee (18) mwendesha bodaboda mkazi wa kwa Morombo na George 
Bathlomeo Silayo (23) mfanyabiashara na mkazi wa Olasiti.
Watuhumiwa wengine waliokamatwa ni raia 
watatu toka nchi za falme za kiaruabu (UAE) Abdul Aziz Mubrak (30) 
mfanyakazi wa mamlaka ya mapato katika falme za kiarabu, Fouad Saleem 
Ahmed Al Hareez Al Mahri (29) mfanyakazi wa kikosi cha zimamoto katika 
Falme za Kiarabu, Saeed Abdulla Saad (28) askali polisikitengo cha 
traffic katika falme za Kiarabu, pamoja na raia mmoja wa Saudi Arabia 
Al-Mahri Saeed Mohseens (29)
Rai hao wa kigeni walikamatwa pamoja na 
wenyeji wao wawili ambao ni raia wa tanzania wenye asili ya Yemen. 
 Majina ya watanzania hao ni Mohamed Suleiman Saad, (38) mkazi wa ilala 
jijini Dar es Salaam na Jasm Mubarak (29) mkaazi wa mtaa wa Bondeni 
jijini Arusha.
Uchunguzi wa kina uliofanywa na timu ya 
upelelezi ukihusisha taaasis nyingine za upelelezi FBI pamoja na 
INTERPOL kuhusiana na tukio hilo la mlipuko wa bomu kanisani umebaini 
kuwa raia hao wanne wa kigeni hawakuhusika katika shambulio hilo. Baada 
ya jalada la tukio hilo kufikishwa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali
 Arusha – divisheni ya mashtaka imeelekeza kuwa watuhumiwa hao 
wakabidhiwe ofisi za idara ya uhamiaji mkoa wa arusha ili kuona kama 
kuna taratibu zozote za kiuhamiaji ziikiukwa na wageni hao wakati 
walipoingia nchini ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa dhidi yao. Pia 
ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali imeandaa mashitaka dhidi ya victor
 S/O Ambros kalisti na amefikishwa mahakamani leo kwa tuhuma za mauaji 
na kujaribu kuua. Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa waliosalia unaendelea 
kwa sasa tunao wataalamu kutoka kenye na Uganda ambao tunashirikiana nao
 katika upelelezi wa shauri hilo.
Aidha, hadi sasa idadi ya majeruhi wa 
tukio hilo la mlipuko wa bomu wanaoendelea kupata matatibabu katika 
hospitali mbalimbali ni 31 ambao kati yao 19 wanaendelea na matibabu 
katika hospitali ya mkoa mount Meru arusha, 4 katika hospitali ya St. 
Elizabeth arusha na wengine 8 katika hospitali ya taifa muhimbili jijini
 dar es salaam na taarifa zinaonyesha hali zao zinaendelea kuimarika.
Hata hivyo jeshi la polisi linaendelea 
kufuatilia taarifa za watuhumiwa wengine wanaohusishwa na tukio hilo ili
 waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani pia jeshi la polisi 
linaendelea kuwaomba wananchi au raiayeyote mwenye taarifa 
zitakazowezesha kubaini mtandao wa kigaidi nawatuhumiwa wengine 
wanaohusika na tukio hilo wajitokeze na kuwasilisha taarifa hizo; tayari
 mkuu wa jeshi la polisi (IGP) amekwishaahidi zawadi nono ya Tshs. 
50,000,000/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa hizo za siri kwa 
kukamatwa kwa watu hao. ASANTENI KWA KUNISIKILIZA.
IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA
LIBERATUSI SABAS – ACP
TAREHE 13/05/2013.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog