![]() |
Daladala hii ya Tabata Segerea hadi posta imeandikwa "AKILI YA NJAA HAISHINDWI KITU" |
Friday, September 20, 2013
YANGA YADAIWA KARIBIA NUSU BILIONI
Thursday, September 19, 2013
TAZAMA PENNY ALICHOSEMA KUHUSU NASEEB ABDULMALIK 'DIAMOND PLATNUMZ'
![]() |
Penny |
SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR (SMZ) YARUHUSU SHEIKH WA UAMSHO AZZAN KHALID HAMDANI KWENDA KUTIBIWA NJE YA NCHI
![]() |
Sheikh Azzan Khalid Hamdani |
PAMBANO LA SIMBA NA MGAMBO LAINGIZA SHILINGI MILIONI 58
Watazamaji 10,241 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo namba 23 ya VPL msimu wa 2013/2014 iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuibuka na ushindi wa mabao 6-0.
Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 13,839,327.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,903,135.59.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,036,946.16, tiketi sh. 2,548,890, gharama za mechi sh. 4,222,167.70, Kamati ya Ligi sh. 4,222,167.70, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,111,083.85 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,641,954.10.
MIKATABA YA MAKOCHA VPL, FDL YATAKIWA TFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa siku 14 kwa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na za Ligi ya Daraja la Kwanza (FDL) kuwasilisha mikataba ya makocha wao.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana Septemba 12 mwaka huu imebaini klabu nyingi hazijawasilisha mikataba ya mabenchi yao ya ufundi, kitu ambacho ni matakwa ya kikanuni. Siku hizo 14 zimetolewa kuanzia Septemba 17 mwaka huu.
Kwa klabu ambazo zitashindwa kuwasilisha mikataba hiyo na vielelezo vingine ndani ya mudau huo zitachukuliwa hatua kwa mujibu wa kanuni.
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
JESHI LA POLISI KUFANYA OPERESHENI MAALUMU KATIKA MAKUTANO YA BARABARA ZOTE ZA DAR
MNIGERIA ASHINDA MISS WORLD MUSLIMAH 2013
ARSENAL YAPATA USHINDI UGENINI KWA KUWAFUNGA WENYEJI WAO MABAO 2 - 1
SIMBA YAONESHA MAKUCHA YAKE NA KUTOA KIPIGO CHA MBWA MWIZI KWA KUWACHAPA MGAMBO BAO 6 KWA SINIA.

Wednesday, September 18, 2013
KASEJA AJIUNGA NA ASHANTI AKITOKEA NDANDA FC YA DARAJA LA KWANZA
NAHODHA wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars Juma Kaseja amejiunga na timu ya Ashanti United ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara akitokea timu ya Ndanda FC inayocheza daraja la kwanza kama kocha wa makipa wao na anatarajiwa kuanza kuichezea rasmi Januari mwakani, baada ya kuchelewa dirisha la usajili.
Kocha wa makipa wa timu hiyo ya Ilala, Dar es Salaam, Iddi Pazi ‘Father’ amesema jana kwamba Kaseja amejiunga na Ashanti United na amekwishaanza kazi.
Father, alisema kwamba pamoja na Kaseja, pia Ashanti imempata kipa mwingine mzoefu, Amani Simba SC ambaye naye amekwishaanza mazoezi.
“Nipo na Amani Simba na Juma Kaseja hapa Ashanti, naamini wote ni makipa wazuri na watachuana ili kurejea matawi ya juu. Nitawafanyia kazi na watakuwa makipa bora tena,”alisema Pazi, baba wa mshambuliaji wa Simba SC, Zahor Pazi.
Kaseja aliachwa Simba SC mwishoni mwa msimu baada ya kuitumikia timu hiyo tangu mwaka 2003 alipojiunga nayo akitokea Moro United.
Baada ya hapo, alipata ofa ya kwenda St. Eloi Lupopo ya DRC, lakini wakashindwa kuafikiana na kuamua kuangalia ustaarabu mwingine. Wakati wa maandalizi ya msimu mpya, Kaseja alikuwa akifanya mazoezi na Mtibwa Sugar iliyokuwa imeweka kambi Dar es Salaam.
Juhudi za kumpata Kaseja mwenyewe kuthibitisha kujiunga kwake na Ashanti hazikuweza kufanikiwa mapema.