Facebook Comments Box

Sunday, September 15, 2013

TUNAOMBA UTUPIGIE KURA



TUNAPENDA KUTANGULIZA SHUKRANI ZETU KWA WALE WOTE MLIOTUCHAGUA KUINGIA KWENYE MASHINDANO HAYA YA BLOGS AWARDS,TUNAOMBA KURA YAKO ILI TUWEZE KUIBUKA WASHINDI SASA,CLICK LINK HAPO CHINI NA UTUPIGIE KURA MARA NYINGI UWEZAVYO,

TUNATANGULIZA SHUKRANI ZETU,

JINA LA BLOG YETU NI kitongoni.blogspot.com

click hiyo link hapo chini upige kura mara nyingi uwezavyoooo

Vote For The Best Sports News Blog 

 

GONGA HAPA KUTUPIGIA KURA




VIDEO: ANGALIA ARSENAL WAKIIFANYIA KITU MBAYA SUNDERLAND: OZIL AKIFANYA VITU VYAKE




MTOTO WA MIAKA SABA ACHOMWA MOTO MIKONI NA MAMA YAKE KWA TUHUMA ZA KUIBA MAYAI YA KUKU

Mtoto EMILLY GEORGE[7] Mkazi wa kijiji cha RUANDA wilaya ya Mbeya akilia kwa uchungu maumivu ya vidonda baada ya kuchomwa moto na mama yake mzazi kisa akidaiwa kuiba mayai ya kuku jamani ukatili gani huu?
Mama mzazi wa mtoto aliyechomwa moto  ELESIA MWASILE[41]  akipelekwa kituoni na wanausalama
Hapa wanausalama na mama mzazi wa mtoto huyo wakielekea kumwona mtoto huyo katika hospitali ya Rufaa Mbeya
Baada ya kukamatwa mama huyo katili alkabidhiwa kwa Dawati la Polisi Jinsia na watoto chini ya Kiongozi wa Wilaya D\SSGT PUDENSIANA BAITU akimjulia hali mtoto Emilly


Wimbi la ukatili dhidi ya watoto bado limezidi kuchukua sura mpya baada ya mtoto EMILLY GEORGE[7] Mkazi wa kijiji cha RUANDA wilaya ya Mbeya kuunguzwa vibaya mikono yote miwili na mama yake mzazi ELESIA MWASILE[41] kwa maji ya moto kisha kufungiwa ndani kwa siku saba bila matibabu yoyote.

Akiongea huku akitetemeka kwa hofu ELESIA amesema kuwa chanzo cha cha kumchoma mtoto huyo ni kutokana na malalamiko ya majirani wakimtuhumu mtoto huyo kujihusisha na vitendo vya wizi vikiwemo wizi wa pesa na mayai ya kuku.

Tukio la mwisho lililopelekea mtoto huyo hadi kuchomwa ni pale ilipodaiwa na mama huyo kuwa mtoto aliiba mayai akidai amechoshwa na tabia za malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa jirani zake.

Baada ya kuunguzwa kikatili mtoto huyo alifungiwa ndani kwa siku saba  bila matibabu yoyote hali iliyowafanya majirani kuuliza aliko mtoto kutokana na mtoto huyo kutoonekana mitaani hali iliyopelekea kutolewa taarifa ofisi ya kijiji ili kubaini aliko mtoto.

Uongozi wa kijiji baada ya kupata taarifa kwa majirani walifanya upekuzi na kumkuta mtoto amefungiwa ndani huku akiwa na majeraha makubwa katika mikono yote miwili ndipo taarifa ilitolewa kituo cha Polisi MBALIZI ambapo mama huyo alikamatwa.

Baada ya kukamatwa mama huyo katili alkabidhiwa kwa Dawati la Polisi Jinsia na watoto chini ya Kiongozi wa Wilaya D\SSGT PUDENSIANA BAITU na Mwenyekiti MARY GUMBO ambaye muda wote alikuwa akiangua kilio kutokana na kitendo alichofanyiwa mtoto na mama yake mzazi.

Hivi sasa mwanamke huyo anahojiwa na Polisi kituo kikuu cha kati na atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo na mtoto amelazwa katika Hospitali ya Rufaa wadi namba tano akiendelea kupatiwa matibabu.

Vitendo vya unyanyasaji vimendelea kukemewa Mkoani Mbeya na Asasi mbalimbali hasa kwa watoto vikiwemo vya ubakwaji,ulawiti,kazi za ndani na baadhi ya watoto wamepata ulemavu wa kudumu ikiwemo kupoteza viungo.
 
CHANZO: MBEYA YETU


WAMAREKANI WADAI KUGUNDUA CHANJO INAYO ANGAMIZA VVU


Washington. Wanasayansi nchini Marekani wamegundua chanjo ambayo wanaamini itaweza kuangamiza Virusi Vya Ukimwi (VVU) kwa binadamu.
Katika majaribio ya chanjo hiyo, wanasayansi hao wameelezea kuwa imeonyesha mafanikio kwa kuangamiza kabisa virusi wanaofanana na VVU kwa nyani.
Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) limechapisha kwenye tovuti yake kuwa baada ya kubaini hilo sasa wamekusudia kufanya majaribio ya chanjo hiyo kwa binadamu.
Likinukuu taarifa iliyochapishwa kwenye jarida la kisayansi linaloitwa; Nature, lilimnukuu Mwanasayansi wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba cha Oregon, nchini Marekani akisema walijiridhisha kuwa chanjo hiyo iliangamiza virusi vyote kwenye mwili wa nyani.
Virusi hao jamii yake inafanana sana na VVU wanajulikana kama Simian Immunodeficiency Virus (SIV) ikiwa na maana ni virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga ya kujikinga na maradhi kwa nyani.
Taarifa za kisayansi zinaonyesha kwamba SIV ni virusi ambao wamekuwa wakienea kwa njia ya kujamiiana miongoni mwa vizazi vya nyani na vilibadilika baada ya kuambukizwa kwa binadamu vikawa vimezaa VVU.
Wanasayansi hao wanasema kati ya nyani 16 waliopewa chanjo hiyo, waliyoipa jina la Cytomegalovirus (CMV),tisa walipona kabisa maradhi ya SIV.
Mtaalamu wa Taasisi ya Chanjo na Jeni katika Chuo Kikuu cha Oregoni, ambaye alihusika kwenye utafiti huo, Profesa Louis Picker aliielezea chanjo hiyo kuwa ni ya kutia moyo ukilinganisha na nyingine ambazo zimewahi kufanyika.
“Katika chanjo nyingi ambazo ziliwahi kuonyesha mafanikio ya kuangamiza virusi ni kwamba kuna baadhi ya seli virusi walibakia,” alisema Profesa Picker, akifafanua:
“Lakini kwa chanjo hii tulichunguza sehemu nyingi nyeti katika mwili wa nyani tukagundua kwamba hakuna kirusi aliyebakia.”
Alisema chanjo yao wameiamini kutokana na uwezo wake wa kupenya maeneo mbalimbali ya mwili kiasi kwamba siyo rahisi kirusi kubakia.
Wanasayansi hao walisema kwa kawaida nyani ambaye ameambukizwa SIV hufa ndani ya kipindi cha miaka miwili


YALIYOJIRI KATI YA YANGA NA MBEYA CITY

Basi la klabu ya Yanga likiwa linaingia katika uwanja wa sokoine mjini Mbeya limeshambuliwa na mashabiki wanaodhaniwa kuwa wa Mbeya City kwa kupigwa mawe, kitu kilichopelekea vioo vya gari hilo kupasuka.

Katika tukio hilo dereva wa basi la Yanga aliumizwa

Mechi iliisha kwa timu hizo kutoka suluhu ya Moja kwa Moja


 
 
 
Wachezaji wa Yanga wakimzonga refa baada ya kukataa bao lao

Wachezaji wa Yanga wakimuambia refa amuangalia mshika kibendera kakubali bao Basi la Yanga likiwa chini ya uangalizi wa Polisi Uwanja wa Sokoine lisishambuliwe zaidi
Yanafaa kula? Mayai yaliyoandikwa Kiarabu yaliyotolewa uwanjani kabla ya mchezo kuanza

Bendera ya Mbeya City na maandishi wa Kiarabu


Friday, September 13, 2013

HILI NDIO TUKIO JINGINE LA MTU KUMWAGIWA TINDIKALI LEO UNGUJA

Ikiripotiwa ni Padri wa kanisa katoliki cheju amemwagiwa tindikali leo. 


MAHAKAMA NCHINI INDIA YAWA HUKUMU KIFO WABAKAJI WANNE

Mahakama nchini India imewahukumu wanaume wote wanne kifo baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumuua mwanamke katika basi katika mji mkuu wa India Delhi mwezi Desemba mwaka jana.
Mmoja wao aliangua kilio na kuanguka baada ya kutangazwa kwa hukumu dhidi yao .
Taarifa zinazohusiana
afya
Msichana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 23 aliumizwa sana na baada ya wiki moja alifariki kutokana na majeraha .
Karibu miezi 9 baada ya ubakaji ulioitikisa India, jaji ametoa hukumu kwa wanaume wote wanne ambao tayari walikuwa wamepatikana na hatia ya uhalifu .
Wendesha mashtaka walikuwa wamewaombea hukumu ya kifo wakisema ingetoa ishara muhimu kwamba uhalifu wa aina hiyo hautakubalika kamwe .
Familia ya mwanamke huyo pia waliomba wanaume hao wanyongwe .
Lakini mawakili watetezi wa wanaume hao walipinga mapendekezo ya hukumu ya kifo , wakisema wateja wao hawakuwa na rekodi za uhalifu awali na kwamba wanastahili kusamehewa .
Kifo cha mwanafunzi huyo mwezi Disemba mwaka jana kilisababisha maandamano makubwa ya upinzani kote nchini India , yaliyoilazimisha serikali kubadili sheria zilizokuwepo za uhalifu wa ngono



Thursday, September 12, 2013

WAGENI WOTE WATAKAO INGIA ZANZIBAR KUPIMWA MALARIA

KITENGO cha kupambana na Malaria Zanzibar (ZMPC) kimesema kinatarajia kuanza kampeni ya kuchunguza malaria kwa wageni wote watakaoingia nchini kupitia uwanja wa ndege na bandari ya Malindi.

Ofisa mwandamizi wa kitengo wa ZMPC, Mwinyi Mselem akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mikakati ya kupambana na malaria nchini, alisema kitengo kimepanga kutekeleza mikakati hiyo, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha kwamba ugonjwa wa malaria unatokomezwa na hakuna njia za kuambukizwa kwa wananchi.

“Tunakusudia kuanzisha zoezi la kupima afya za wageni wote wanaoingia nchini kupitia njia za uwanja wa 
ndege pamoja na bandarini ili kujuwa afya za wageni wanaoingia nchini,” alisema.

Alisema mikakati ya kitengo cha kupambana na malaria ifikapo mwaka 2017 ni kuhakikisha ugonjwa huo umetokomezwa na siyo tishio tena kwa afya za wananchi. Kwa sasa Zanzibar imefanikiwa kushusha maambukizi ya ugonjwa huo kutoka asilimia 32 hadi kufikia asilimia moja na kupunguza vifo vya akinamama na watoto.

Hata hivyo, Mselem alisema katika kipindi cha miaka miwili sasa kumejitokeza maambukizi mapya ya malaria kutokana na kuongezeka kwa uchafuzi wa mazingira na hivyo kupelekea mbu kuzaliana zaidi.

Alisema kitengo cha kupambana na malaria kinatarajia kuanza kazi ya kupiga dawa majumbani pamoja na sehemu za mazalia ya mbu. Mselem alisema kazi hiyo inatarajiwa kuanza katika kipindi cha msimu wa mvua za vuli, ambazo huibuka kwa mazalia mengi ya mbu yanayosababisha ugonjwa wa malaria.

Zanzibar inatajwa mfano wa kupambana na ugonjwa wa malaria, ambapo hivi karibuni Rais mstaafu wa Marekani, Bill Clinton alizindua mradi wa kupambana na ugonjwa huo wa kupima damu hapo katika uwanja wa Amaan mjini hapa.

Khatib Suleiman
HabariLeo, Zanzibar


JWTZ YAKANA TAARIFA YA JAMII FORUM, TWITTER NA FACEBOOK

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO
Telex : 41051                                                      
Tele Fax  : 2153426
Barua pepe : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti : www.tpdf.mil.tz
Makao Makuu ya Jeshi,                
Simu ya Upepo  : “N G O M E”      
Simu ya Mdomo  : DSM  22150463
 Sanduku la Posta  9203,              
DAR ES SALAAM,                           

           12 Septemba, 2013. 
Taarifa kwa vyombo vya Habari

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) limepata habari kupitia mtandao wa Jamii Forumna Gumzo la Jiji  na mingineyo kuwa likizo zimesitishwa Jeshini  na waliokuwa  likizo wameitwa kurudi kazini.

          Taarifa hizo pia zimeeleza kwamba Brigedi za Tembo na Kifaru zimepewa maagizo ya kuwa katika hali 
ya utayari endapo watahitajika kusonga mbele.

          JWTZ  linapenda kuwaeleza wananchi pamoja na watumiaji wa mitandao hiyo kuwa taarifa hizo ni za upotoshaji mtupu na hazina ukweli wowote.  Aidha, taarifa hizo ni zenye nia ya kuzorotesha uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi yetu (Tanzania) na majirani zake. 

Sambamba na taarifa hii, pia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kutoa taarifa za kutohusika na viunganishi vya JWTZ kwenye mitandao ya  ‘Facebook‘ – (Facebook/JWTZ) na  ‘Twitter‘  (Twitter/ JWTZ).

Mitandao hiyo yenye viunganishi vya JWTZ imekuwa ikijihusisha na kutoa taarifa ambazo zimekuwa zikichangiwa na watu mbalimbali, ambapo baadhi yao wamekuwa wakitoa taarifa za upotoshaji  na zisizo sahihi.  Tunapenda kutaarifu kwamba akaunti za facebook na twitter zilizotajwa siyo za JWTZ.

Hatua zimechukuliwa za kuwatambua wahusika na kuwachukulia hatua za kisheria.

         Aidha inasisitizwa kwamba JWTZ lina taratibu za zake zinazotumika kufanya mawasiliano na Vyombo vya Habari, Taasisi, au mtu binafsi kuhusu utoaji wa taarifa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi
Dar es salaam, Tanzania



AKAMATWA MUDA MCHACHE KABLA YA KUTIMIZA AZMA YAKE YA KUCHOMA QUR`AN

Kiongozi mmoja wa Kanisa nchini Marekani anayeishi jimboni Florida, Terry Jones alitiwa mikononi mwa polisi jana muda mchache tu kabla ya kutimiza azimio lake la kuchoma Quran takriban elfu tatu, katika siku ambayo taifa hilo lililkuwa likiadhimisha miaka 12 tangu Marekani ishambuliwe kigaidi Septemba 11.

Magazeti kadhaa ya jimboni Florida yaliandika ifuatavyo:

The Tampa Tribune: "When he and another pastor were pulled over by Polk County sheriff's deputies near the small town of Mulberry, their pickup bed was full of kerosene-soaked Qurans - and they were towing a 
large, barbeque-style grill behind the truck. The arrest happened shortly before 5 p.m., when Jones was scheduled to burn the Qurans - one for every victim of the terrorist attacks - at a public park just outside Mulberry."

The Polk County Ledger:  County officials had previously denied a permit for the event. The paper reports that in a press conference Sheriff Grady Judd said Jones had been stopped because his trailer did not have a license plate and he has been charged with "unlawful conveyance of fuel and unlawful carry of a firearm."
Essentially, Judd said, Jones was driving a "bomb" down the road.
"We couldn't allow that vehicle to continue down that road," Judd alinukuliwa na gazeti kusema hayo.

The AP: "Jones is the pastor of a small evangelical Christian church. His congregation burned a Koran in March 2011, and last year he promoted an anti-Muslim film. His actions have sparked violence in the Middle East and Afghanistan. The U.S. Central Command, based at MacDill Air Force Base in Tampa, earlier this week had urged him not to go through with Wednesday's event."

Hii si mara ya kwanza kwa Jones kufanya jaribio la kuchoma Quran kwani miaka mitatu iliyopita, alipigiwa simu na Robert Gates, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi wa wakati huo, akimtaka aachane na mpango wake wa kuchoma kitabu hicho kitakatifu cha Waisalam, kwa sababu kufanya hivyo kungehatarisha maisha ya askari wa Marekani waliopo ng'ambo, duniani kote.

Pamoja na kuwa alitii wito huo, mwaka 2012 mwezi Aprili alitimiza azma yake hiyo
.


MESUT OZIL KUANZA KUITUMIKIA TIMU YAKE MPYA YA ARSENAL JUMAMOSI NA SUNDERLAND



KIUNGO Mesut Ozil amewasili katika klabu yake mpya, Arsenal tayari kuanza kumtumikia Arsene Wenger anayekabiliwa na tatizo la wachezaji wengi majeruhi.

Mchezaji huyo aliyenunuliwa kwa Pauni Milioni 42 ataanza mazoezi leo makao makuu ya klabu, Colney London kwa mara ya kwanza tangu ahamie akitokea Real Madrid.
 
Na Wenger anajiandaa kumtumia mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ujerumani katika mchezo dhidi ya Sunderland Jumamosi hii baada ya Tomas Rosicky kurejea kwenye mechi ya timu yake ya taifa akiwa majeruhi.
 
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech aliumia wakati timu yake ikilala 2-1 dhidi ya Italia na yuko shakani kucheza Uwanja wa Light.
 
Hiyo inaacha milango wazi mno kwa Ozil kuanza kazi Arsenal, licha ya kwanza atakuwa na siku mbili tu kamili za kufanya mazoezi na wenzake kabla ya mechi hiyo.
 
Licha ya msimu kuwa umekwishaanza kwa karibu mwezi mzima, Arsenal tayari ina idadi kubwa ya majeruhi. 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU