Facebook Comments Box

Monday, July 8, 2013

MWANAFUNZI WA VETA DODOMA AJICHOMA MOTO KISA WIVU WA MAPENZI


MWANAFUNZI wa Chuo cha Ufundi (VETA), mkoani Dodoma, Taliki Juma (22), amefariki dunia baada ya kujilipua kwa mafuta ya petroli. Mbali na mwanafunzi huyo kufariki, watu wengine wanane waliokuwa karibu na moto huo nao walijeruhiwa vibaya.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma na kusainiwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa, David Misime, tukio hilo lilitokea juzi saa 12.30 jioni katika Kitongoji cha Machaka, Kata ya Nzughuni.

Kamanda Misime alisema, katika tukio hilo marehemu alinunua mafuta ya petroli lita tano katika kituo cha mafuta cha Nanenane na kisha kujilipua.

“Juma ambaye ni mwanafunzi wa fani ya ufundi wa magari, alimwaga petroli hiyo ndani ya saluni ya Irene Mapunda na kujilipua.

“Watu waliokuwa karibu naye walijaribu kumsihi asijilipue lakini hawakufanikiwa, kwani aliwasha kibiriti ndani ya saluni hiyo na kusababisha moto mkubwa kulipuka ambao uliwaunguza wengine waliokuwa karibu naye pamoja na mali zote zilizokuwa ndani ya Saluni hiyo.

“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi, hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linaendelea na uchunguzi wa kina juu ya tukio hili,” ilieleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo waliojeruhiwa ni Mugina Hessein (32), Benson Mushi (11) Japhet Japhet (18), Meshack John (18), Swaibu Kassim (20),Ester Silau (30), Shaban Pili (20) na Fedrick Gabriel (21).

Majeruhi wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma (General) na tathimini ya hasara iliyosababishwa na moto huo bado haijafahamika.


LIVERPOOL REJECT £ 30 M ARSENAL BID FOR SUAREZ


Luis Suarez Liverpool have turned down a £30m bid from Arsenal for 26-year-old Uruguayan striker Luis Suarez. Suarez has been at the centre of transfer speculation since saying in May that it would be a "good moment for a change", and admitted it would be "difficult to say no" to Real Madrid. Liverpool refused to comment on reports of Arsenal's move and have previously insisted Suarez is not for sale. However, it is understood an approach was made and instantly rejected. Chelsea have also been linked with a move for Suarez and it remains to be seen if Arsenal take their interest further as manager Arsene Wenger continues to finalise a deal for Real Madrid's Gonzalo Higuain. Real are expected to emerge as the most serious test of Liverpool's resolve not to sell Suarez unless they receive an offer in the region of the £50m which saw Fernando Torres move to Chelsea in January 2011. Liverpool manager Brendan Rodgers remains relaxed about Suarez's situation and the striker has yet to indicate to the club that he wishes to leave. The Merseyside club's stance has always been that they have no desire to part with Suarez - and even if Liverpool's hand is forced by the player's own discontent they will not be pushed into a deal and will hold out for the maximum price.


MLIPUKO WA KIPINDUPINDU MBEYA: MIKUSANYIKO YAPIGWA MARUFUKU

UGONJWA wa kipindupindu, umeingia katika wilaya ya Kyela na kuua watu wawili na 39 wakiwa wamelazwa.

Taarifa zinasema ugonjwa huo umeibuka wilayani humo wiki iliyopita ukisadikika kuanzia katika Kijiji cha Ngonga na kisha kusambaa hadi Kilwa.

Kutokana na hofu ya kupata maambukizi kwa wananchi wengine, serikali imepiga marufuku mikusanyiko ikiwemo ya harusi, kipaimara, ngoma, michezo na sikukuu inayosherehekewa kila mwaka ya wakulima. 


--- taarifa via Kalulunga blog



SABABU ZA ZITTO KABWE KUTOSHIRIKI TAMASHA LA MATUMAINI

Kupitia account yake ya facebook Mh. Zitto Kabwe amepost hotuba hii akielezea kushindwa kwake kufika katika tamasha la siku ya matumaini.
POST YAKE AMEANZA KWA KUANDIKA HIVI.

Global Publishers leo 7.7.2013 waliandaa Tamasha la Matumaini. Bahati mbaya sana sikuweza kuwahi kutokana na safari nilizonazo. Hii ni hotuba niliyopanga kuitoa na kuwatumia waandaaji.

TAMASHA LA MATUMAINI

Leo nilikuwa niwe nanyi kwa ajili ya siku hii muhimu sana kwa nchi yetu, siku ya matumaini kama inavyoandaliwa na Kampuni ya Global Publishers. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa ndugu yangu Erick Shigongo kwa kuandaa tamasha hili kila mwaka. Nasikitika kuwa sitaweza kufanya pambano la ngumi na ndugu Ray na pia kuchezea timu yangu ya Wabunge wa Simba dhidi ya watani zetu Yanga. Hata hivyo naamini kuwa tamasha litakuwa na mafanikio makubwa na nipo nanyi japo sipo Dar es Salaam.

Ilikuwa niwepo Dar es Salaam leo, lakini nimeshindwa kuondoka Marekani kwa sababu Spika wa Bunge Mama Anna Makinda ameniagiza kwenye safari nyingine ndefu kwenda visiwa vya Cayman na baadaye Namibia kwa shughuli za Umoja wa Wabunge wa Jumuiya ya Madola. Sikuweza kukwepa jukumu hili la kitaifa maana limekuja ghafla na mimi nipo huku jirani na maeneo hayo. Naomba radhi sana kwamba sipo nanyi leo.

Nawaomba muiombee amani nchi yetu na msimamie haki kwa wananchi wote bila kubagua dini zao, rangi zao, hali yao kimaisha na ufuasi wa vyama vya siasa. Mwaka huu tumeshuhudia matukio ambayo yanatikisa msingi wa Taifa letu – Umoja. Hivi sasa msingi wetu una nyufa ambazo kwa kweli hatujajua bado nini kinacholeteleza mambo haya kama kulipua makanisa, kulipua mikutano ya vyama vya siasa na kuua viongozi wa dini.

Matukio haya yanatuelekeza kuwa makini sana na kauli zetu kwani baadala ya kuunganisha wananchi tunawezajikuta tunawagawa zaidi Watanzania na hivyo kuwa na mzunguko wa machafuko (vicious circle of violence). Ni wajibu wa viongozi wa kisiasa na wananchi kuepuka kabisa kuanza kurushiana maneno na lawama kuhusu matukio haya, kwani inawezekana lawama na maneno yetu yakawa yanampa nguvu adui wetu ambayo hatujamjua bado.

Napenda niwakumbushe kwamba ni rahisi sana kusambaza chuki na ni vigumu sana kuondoa chuki miongoni mwa wananchi. Viongozi hatari kama Hitler walitumia sana mbinu ya kueneza chuki dhidi ya jamii ya Jews na matokeo yake yalikuwa ni vita vikuu vya pili vya dunia na zaidi ya watu milioni 6 wasio na hatia kupoteza maisha. Sisi sote tuna jukumu moja la kuhakikisha tunajenga Taifa lenye kujali HAKI na lenye mshikamano mkubwa miongoni mwa raia. Kwa nia hii tu ndio tutaweza kuwa na Taifa imara lenye heshima mbele ya mataifa mengine duniani. Ni kwa njia hiyo tu ndio tutaweza kutokomeza umasikini uliokithiri mijini na vijijini hapa nchini kwa kuongeza uzalishaji na kupanua ajira. Ikumbukwe bila HAKI hakuna AMANI na bila UWAJIBIKAJI hakuna UTULIVU.

Tukiegemea siasa za CHUKI. Tukashindwa kuwa na mahusiano ya kawaida miongoni mwa viongozi kuhusu masuala ya msingi ya nchi. Tukashindwa kujadiliana kwa hoja kuhusu sera zetu. Tutapata viongozi aina ya Hitler nchini mwetu. Wote tukatae. Sisi ni Watanzania. Muwe na Tamasha jema la Matumaini.

Zitto Kabwe
7.7.2013, Aspen Colorado, USA.


Sunday, July 7, 2013

PICHA ZA PAMBANO LA WABUNGE WASHABIKI WA YANGA NA WABUNGE WASHABIKI WA SIMBA

Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua…
Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua Yanga.picha zote na GPL


KOCHA WA AZAM ASEMA HAMTAKI KASEJA: MAKIPA ALIO NAO WANATOSHA

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amekiri Juma Kaseja ni bonge la kipa, lakini amesema kwamba sasa anataka Aishi Manula na Mwadini Ally wapambane kuwania nafasi ya kipa wa kwanza wa timu na hana mpango wa kusajili kipa mwingine.
Muingereza huyo amesema kipa wake mwingine, Jackson Wandwi anampeleka kucheza kwa mkopo Ashanti United ya Ilala iliyopanda Ligi Kuu msimu huu, ili kukusanya uzoefu baadaye arejee kushindana na Mwadini na Aishi.
Hatumuhitaji Kaseja; Stewart Hall kulia akiwa na Msaidizi wake, Kali Ongala

“Najua Kaseja ameachwa Simba SC, na nasikia watu wanamzungumzia sana wakimhusisha na Azam. Mimi nakubali yule ni kipa mzuri na ana uzoefu. Ila mimi nina makipa wazuri wawili, Aishi na Mwadini. Nataka hawa wagombee kuwa kipa wa kwanza wa timu,”alisema.
Hall amesema kwamba bado Azam ina makipa wengine wazuri wa timu za vijana, ambao watakuwa wakipewa nafasi ya kujifua na kikosi cha kwanza msimu ujao.
“Kama nitakuwa na Aishi na Mwadini kama makipa wawili imara wa timu ya kwanza, maana yake Wandwi ataendelea kuua kiwango chake. Nimeona bora nimpeleke Ashanti ili akakusanye uzoefu, baadaye arejee kwenye timu akiwa imara,”alisema.
Azam wakiwa mazoezini ufukwe wa Coco Dar es Salaam jana. Wandwi (katikati) anapelekwa kwa mkopo Ashanti United.

Aidha, kuhusu maandalizi ya msimu mpya, Hall amesema kwamba kwa sasa Azam ambayo itaiwakilisha Tanzania kwa mara ya pili mfululizo kwenye Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, iko katika mazoezi.
“Tunaendelea na mazoezi ya msimu mpya. Kwa sasa tupo katika programu ya ufukweni na gym. Baada ya hapo tutaanza programu rasmi ya uwanjani. Lakini wiki mbili za mwanzo za Agosti tutakwenda Afrika Kusini kuweka kambi,”.
“Tukiwa huko tutafanya mazoezi katika Uwanja mzuri na kupata mechi nne za kujipima nguvu dhidi ya timu kama Orlando Pirates, Kaizer Chiefs, Mamelodi Sundwons na nyingine,”alisema

Endelea kusoma hapa 

Saturday, July 6, 2013

HUYU NDIO MZEE ABDULLAH AL RUWEIHY ALIETEMBEA KWA MIGUU KUTOKA DAR HADI TANGA



Mwarabu aliyetembea kwa Miguu Dar es salaam mpaka Tanga.
Baba yake alitembea kutoka Dar es salaam mpaka  Kigoma
Yafuatayo ni mahojiano yaliyofanyika kati ya mwandishi  na mzee Abdullah Mohammed Alruweihy mwaka 2007 katika kijiji cha Saadani eneo la Tongoni wakati  wa uhai wake.Alifariki mwaka 2009/2010.Mwenyezi Mungu amrehemu.
Swali:Sisi pale jijini Tanga tunakufahamu zaidi kwa jina la mzee Ruwehi.Jina lako kwa ukamilifu ni nan?.
Jibu:Mimi jina langu ni Abdullah bin Muhammad bin Habiib bin Salim bin Ally bin Suleiman bin Salim Al Rawaahy.
Swali:Umezaliwa wapi?.
Jibu:Nimezaliwa kijiji cha Ndono kwa Mwana Kurwa  Tabora.
Swali:Tupe historia ya wazazi wako kwa kifupi.
Jibu:Mama yangu  alikuwa akiitwa  Zuhura kutoka kabila la Manyema.Baba yangu alikuwa ni mmoja ya wafanyaji wa biashara aliyetoka kutoka nchi ya Oman.Alikuja mpaka Zanzibar.Akaona Zanzibar hapamfai akaondoka kuelekea sehemu za bara.Akafika sehemu moja inaitwa Tabora kama nilikutajia.
Sasa baada ya kufika hapo.Huyu bwana alikuwa anafanza kazi za biashara.Wakati huo walimchunuka Majarumani.Na ikawa wanatumia vitu vingi  katika dukani kwake.
Sasa  ilipokuwa imetokea ile vita wak
awa majarumani wanashambuliwa na waiengereza.
Swali:Ni vita gani hiyo?
Jibu:Ni vita ya 1914
Swali:Jee ndiyo ile vita ya mwanzo ya dunia?.
Jibu:Hapana,haikuwa vita ya mwanzo ya dunia.Ile vita ya maji maji ni vita mbali ile.Hii ilikuwa ni vita ya pili.
Swali:Ilikuwa ni mwaka gani?.
Jibu:Ilikuwa ni  1914.
Swali:Wewe ulizaliwa mwaka gani hasa?.
Jibu:Mimi nilizaliwa tarehe 10/02/1908
Swali:Tuendelee na historia ya wazazi wako.
Jibu:Mzazi  wangu mbali na kufanza utaratibu akawa na mlahaka na wale wajarumani mpaka ilipoingia vita.
Vita iliendelea mpaka baadae akaja mmoja anaitwa bwana Robert Fonreto. Akamwambia Muhammed una habari?.Vita inaendelea vikali na sisi hapa tulipo hatukukaa vizuri.Akamwambia sasa tutafanza nini?.Akamwambia risasi imekuwa kidogo na baruti  kidogo lakini askari wapo wa kuweza kuendesha kazi.Sasa tutafanza mashauri  gani?.
Akamwambia kama shauri ya risasi na baruti mimi nitafanza taratibu ya kuweza kutafuta na maarif mengine.Akamwambia unaweza  kweli,akajibu ndio.Akamwambia haya ondoka nenda.
Akaondoka moja kwa moja mpaka akafika Dar es salaam.Wakati ule wajarumani wenyewe ndio wameikamata Dar es salaam.Akatoka Dar es salaam moja kwa moja mpaka akafika kwenye nchi ya Mukkalla,Yemen.Akatoka Mukalla akenda juu,akapata risasi na baruti jumla debe thamanini na nne (84).
Ikawa chini akaweka risasi na madebe mengine akaweka baruti,lakini juu akaweka tende.Akaajiri jahazi moja lakini mimi wakati ule bado mdogo.Lakini ile historia walivyokuwa  wananieleza wale waliiokuwa wenziwe.
Akasikilizana na nahodha kuwa hii ni tende nipelekee Dar es salaam.Nahodha akaondoka mpaka akafika Unguja.Wakati ule Unguja ilikuwa ndani ya mikono ya waarabu wenyewe.Unguja ana nduguze.Mmoja anaitwa sheikh Suleiman bin Said Alruwahiy.Anakaa sehemu moja kule Unguja panaitwa Michungwa miwili.
Walipofika kule wakamwambia habari gani uliyonayo Mohammed?.Aliwaambia sina habari yoyote.Nimekuja tu kuwasalimia.Hakuwaambia ile siri yake.
 Ile jahazi baada ya pale akamwambia chukua hii mizigo kateremshe Dari salaam.Mimi nipo kidogo hapa halafu nakuja.Nahodha akaendesha jahazi hadi Dari salaam.Wakati ule ilipofika ile jahazi Dari salaam haipo tena ndani ya mikono ya Wajarumani.Imo ndani ya mikono ya Muiengereza.Kashatawala muiengereza.     
ITAENDELEA... 

SOURSE:  ISLAMICTIDES

PICHA ZA HARUSI YA DIDA WA TIMES FM

HONGERA SANA DIDA NA MUMEO MPYA, NDOA HALALI YA KIISLAM..


VIDEO: KWA WALE WAPENZI WA WEMA SEPETU HII NDIO REALITY SHOW YAKE

Wema Sepetu alitangaza kwamba anaandaa reality show yake chini ya kampuni anayoimiliki “Endless Fame”. Muda umefika wa kuanza kuonyesha hiyo show yenyewe na Wema ameshatoa teaser au kionjo cha reality show hiyo ambayo inaonyesha baadhi ya vitu vinavyohusika kwenye show hiyo. Kwenye hii teaser inamuonyesha Wema anazungumzia kazi, mahusiano na katajwa Diamond humo,ziara za Wema na maisha ya nyumbani. 
 


Friday, July 5, 2013

MKE WA MANDELA AELEZEA HALI YA MUME WAKE


 

Johannesburg. Mke wa Nelson Mandela, Graca Machel kwa mara ya kwanza amejitokeza hadharani kuzungumzia hali ya kiafya ya mumewe kwamba kuna wakati anazidiwa lakini hajambo.

Graca alisema hayo jana kwenye sherehe za uzinduzi wa siku ya Utamaduni na Michezo ya Nelson Mandela iliyofanyika kwenye Kituo cha Kumbukumbu ya Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini.
Alieleza sababu za kuhudhuria sherehe hizo kwamba kubwa ni kuwashukuru kwa kuwa pamoja na kumwombea afya njema Mandela tangu alipolazwa hospitali Juni 8, mwaka huu.
Graca alisema pamoja na kwamba Mandela amelala akiugua hospitali, lakini ameendelea kutoa zawadi kwa wanajamii wote ya kuwaunganisha pamoja, ambayo ni michezo na utamaduni.
“Madiba kuna wakati hayuko vizuri. Wakati mwingine anakuwa na maumivu. Lakini hajambo,” alinukuliwa Graca akizungumza katika sherehe hizo.
Katika hatua nyingine mjini Pretoria, Rais Jacob Zuma juzi alisema kuwa hali ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela bado ni mbaya na hakuna mabadiliko.
Rais Zuma alisema hayo baada ya juzi (Jumatano) jioni kwenda hospitali kumjulia hali Mandela, ambapo alikuwa na msafara mkubwa.
Kiongozi huyo pia aliwaomba wananchi wa Afrika Kusini kutenga dakika 67 kwa ajili ya Siku ya Mandela ya Julai 18, ambayo ni siku yake ya kuzaliwa.
Alisema kauli mbiu ya siku hiyo ni “Chukua hatua; penda mabadiliko; fanya kila siku iwe siku ya Mandela kwa kujielekeza katika masuala ya chakula, makazi na elimu.
Wakati huohuo, kumekuwa na hali ya utulivu katika eneo la Hospitali ya Medi-Clinic aliyolazwa Mandela, tofauti na ilivyozoeleka kuwa na pilikapilika nyingi.
Kwa mujibu wa taarifa, watu wanaopita eneo hilo la hospitali wamekuwa wakionekana wakiwa na hali ya utulivu, huku wengine wakipiga picha kwenye kadi, maua, bendera, vipeperushi na mabango yaliyowekwa kandokando ya hospitali hiyo, yakiwa na ujumbe wa kumtakia nafuu ya kuumwa Madiba.
Wakati hali hiyo ikiendelea kutokea mjukuu wa Mandela, Mandla Mandela ameendelea kuikoroga familia hiyo, baada ya kuzungumza na waandishi wa habari akidai kushangazwa na mahakama ilivyoharakisha kesi hiyo kuhusu mvutano wa sehemu ya kuzikwa Mandela na siyo miaka miwili iliyopita baada ya yeye kufukua makaburi.

SOURSE: MWANANCHI


MAGUFULI: NINA UTAMANI URAIS


.
Katika hali inayoonyesha kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, anautamani urais, amesema anaweza kutangaza nia hiyo kama atakidhi masharti yatakayowekwa kwenye Katiba mpya.

Alisema iwapo Katiba ijayo itakuja na sifa ambazo atakidhi vigezo kuna uwezekano mkubwa wa kuwania nafasi hiyo na kwamba iwapo atapungukiwa sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba hataingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Dk. Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa ‘Mshikamano Saccos’, muda mfupi baada ya mzee Paschal Nyambibo (87) kumsihi agombee nafasi hiyo mwaka 2015 kutokana na sifa zake za uchapakazi ndani ya serikali. 

Nyambibo alisema kutokana na uwajibikaji mzuri aliouonyesha Dk. Magufuli tangu mwaka 2000 akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na katika wizara mbalimbali, Watanzania wamekuwa na imani kubwa na uwajibikaji wake na kwamba anastahili kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ifikapo mwaka 2015. 

Licha ya kauli hiyo kusababisha minong’ono mingi kwa wazee waliohudhuria kikao hicho, Dk. Magufuli alionekana kutuliza hali hiyo kwa kusema isubiriwe Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano iwapo itakuwa na masharti ambayo yatamfanya kujitathimini iwapo ana sifa za kugombea au vinginevyo.

Hata hivyo, Dk. Magufuli hakusita kuonyesha hisia zake za kukerwa na baadhi ya wananchi wanaobeza maendeleo aliyotekeleza katika jimbo lake tangu alipochaguliwa kuwa Mbunge. 

Alimshutumu hadharani aliyekuwa Katibu wa CCM wilaya ya Chato kabla ya kuhamishiwa wilayani Mbogwe, Gervas Stephano, kuwa hana shukrani. 

Dk. Magufuli alimwelezea katibu huyo kuwa hana fadhila kutokana na mambo mengi aliyomtendea tangu akiwa katibu wa ofisi yake ya jimbo ambapo alimsaidia kupanda ngazi na kuwa Katibu wa CCM wilaya Chato, Kwimba, Kasulu, Kilosa na kurejea tena Chato kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita  kuendelea na wadhifa huo. 

“Tatizo lenu watu wa Chato hamna shukrani…mambo mengi nimefanya hapa Chato, lakini yote mnaona ziro…hata niliowasaidia kama Gervas naye sasa hivi ananiponda…lakini nawashukuru sana wazee wangu kwa kunikumbusha niliyoyafanya kwenye jimbo letu kupitia risala yenu nzuri,” alisema Dk. Magufuli. 

“Kutokana na hali hiyo ninawazawadia Sh. 1,000,000 mfanye sherehe ya kujipongeza kwa kuwa natambua mmejitesa sana mpaka kufanikisha kikao hiki cha leo…na kwa kuwa hamna mradi wowote wa kuwaingizia kipato kama wazee, ninaahidi kuwapa Sh.   3,000,000 kutoka mfuko wa jimbo, ili muanzishe walau saccos ya kukopeshana,” alisema. 

Baadhi ya viongozi na wananchi wamekuwa wakilitaja mara kwa mara jina la Waziri Magufuli miongoni mwa watu wanaodhaniwa kutaka kugombea nafasi ya urais wa Tanzania mwaka 2015, ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha uvumi huo. 

Mbali na Dk. Magufuli, wengine ndani ya CCM wanaotajwa  ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye anajiita mtaji wa urais; Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Ushirikiano wa Kimataifa –CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Mambo ya Nje, Bernard Membe, ambaye alipata kusema anasubiri kuiteshwa na Mungu kuwania nafasi hiyo.
SOURSE: MWANANCHI


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU