Facebook Comments Box

Sunday, July 7, 2013

PICHA ZA PAMBANO LA WABUNGE WASHABIKI WA YANGA NA WABUNGE WASHABIKI WA SIMBA

Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua…
Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua Yanga.picha zote na GPL


KOCHA WA AZAM ASEMA HAMTAKI KASEJA: MAKIPA ALIO NAO WANATOSHA

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amekiri Juma Kaseja ni bonge la kipa, lakini amesema kwamba sasa anataka Aishi Manula na Mwadini Ally wapambane kuwania nafasi ya kipa wa kwanza wa timu na hana mpango wa kusajili kipa mwingine.
Muingereza huyo amesema kipa wake mwingine, Jackson Wandwi anampeleka kucheza kwa mkopo Ashanti United ya Ilala iliyopanda Ligi Kuu msimu huu, ili kukusanya uzoefu baadaye arejee kushindana na Mwadini na Aishi.
Hatumuhitaji Kaseja; Stewart Hall kulia akiwa na Msaidizi wake, Kali Ongala

“Najua Kaseja ameachwa Simba SC, na nasikia watu wanamzungumzia sana wakimhusisha na Azam. Mimi nakubali yule ni kipa mzuri na ana uzoefu. Ila mimi nina makipa wazuri wawili, Aishi na Mwadini. Nataka hawa wagombee kuwa kipa wa kwanza wa timu,”alisema.
Hall amesema kwamba bado Azam ina makipa wengine wazuri wa timu za vijana, ambao watakuwa wakipewa nafasi ya kujifua na kikosi cha kwanza msimu ujao.
“Kama nitakuwa na Aishi na Mwadini kama makipa wawili imara wa timu ya kwanza, maana yake Wandwi ataendelea kuua kiwango chake. Nimeona bora nimpeleke Ashanti ili akakusanye uzoefu, baadaye arejee kwenye timu akiwa imara,”alisema.
Azam wakiwa mazoezini ufukwe wa Coco Dar es Salaam jana. Wandwi (katikati) anapelekwa kwa mkopo Ashanti United.

Aidha, kuhusu maandalizi ya msimu mpya, Hall amesema kwamba kwa sasa Azam ambayo itaiwakilisha Tanzania kwa mara ya pili mfululizo kwenye Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, iko katika mazoezi.
“Tunaendelea na mazoezi ya msimu mpya. Kwa sasa tupo katika programu ya ufukweni na gym. Baada ya hapo tutaanza programu rasmi ya uwanjani. Lakini wiki mbili za mwanzo za Agosti tutakwenda Afrika Kusini kuweka kambi,”.
“Tukiwa huko tutafanya mazoezi katika Uwanja mzuri na kupata mechi nne za kujipima nguvu dhidi ya timu kama Orlando Pirates, Kaizer Chiefs, Mamelodi Sundwons na nyingine,”alisema

Endelea kusoma hapa 

Saturday, July 6, 2013

HUYU NDIO MZEE ABDULLAH AL RUWEIHY ALIETEMBEA KWA MIGUU KUTOKA DAR HADI TANGA



Mwarabu aliyetembea kwa Miguu Dar es salaam mpaka Tanga.
Baba yake alitembea kutoka Dar es salaam mpaka  Kigoma
Yafuatayo ni mahojiano yaliyofanyika kati ya mwandishi  na mzee Abdullah Mohammed Alruweihy mwaka 2007 katika kijiji cha Saadani eneo la Tongoni wakati  wa uhai wake.Alifariki mwaka 2009/2010.Mwenyezi Mungu amrehemu.
Swali:Sisi pale jijini Tanga tunakufahamu zaidi kwa jina la mzee Ruwehi.Jina lako kwa ukamilifu ni nan?.
Jibu:Mimi jina langu ni Abdullah bin Muhammad bin Habiib bin Salim bin Ally bin Suleiman bin Salim Al Rawaahy.
Swali:Umezaliwa wapi?.
Jibu:Nimezaliwa kijiji cha Ndono kwa Mwana Kurwa  Tabora.
Swali:Tupe historia ya wazazi wako kwa kifupi.
Jibu:Mama yangu  alikuwa akiitwa  Zuhura kutoka kabila la Manyema.Baba yangu alikuwa ni mmoja ya wafanyaji wa biashara aliyetoka kutoka nchi ya Oman.Alikuja mpaka Zanzibar.Akaona Zanzibar hapamfai akaondoka kuelekea sehemu za bara.Akafika sehemu moja inaitwa Tabora kama nilikutajia.
Sasa baada ya kufika hapo.Huyu bwana alikuwa anafanza kazi za biashara.Wakati huo walimchunuka Majarumani.Na ikawa wanatumia vitu vingi  katika dukani kwake.
Sasa  ilipokuwa imetokea ile vita wak
awa majarumani wanashambuliwa na waiengereza.
Swali:Ni vita gani hiyo?
Jibu:Ni vita ya 1914
Swali:Jee ndiyo ile vita ya mwanzo ya dunia?.
Jibu:Hapana,haikuwa vita ya mwanzo ya dunia.Ile vita ya maji maji ni vita mbali ile.Hii ilikuwa ni vita ya pili.
Swali:Ilikuwa ni mwaka gani?.
Jibu:Ilikuwa ni  1914.
Swali:Wewe ulizaliwa mwaka gani hasa?.
Jibu:Mimi nilizaliwa tarehe 10/02/1908
Swali:Tuendelee na historia ya wazazi wako.
Jibu:Mzazi  wangu mbali na kufanza utaratibu akawa na mlahaka na wale wajarumani mpaka ilipoingia vita.
Vita iliendelea mpaka baadae akaja mmoja anaitwa bwana Robert Fonreto. Akamwambia Muhammed una habari?.Vita inaendelea vikali na sisi hapa tulipo hatukukaa vizuri.Akamwambia sasa tutafanza nini?.Akamwambia risasi imekuwa kidogo na baruti  kidogo lakini askari wapo wa kuweza kuendesha kazi.Sasa tutafanza mashauri  gani?.
Akamwambia kama shauri ya risasi na baruti mimi nitafanza taratibu ya kuweza kutafuta na maarif mengine.Akamwambia unaweza  kweli,akajibu ndio.Akamwambia haya ondoka nenda.
Akaondoka moja kwa moja mpaka akafika Dar es salaam.Wakati ule wajarumani wenyewe ndio wameikamata Dar es salaam.Akatoka Dar es salaam moja kwa moja mpaka akafika kwenye nchi ya Mukkalla,Yemen.Akatoka Mukalla akenda juu,akapata risasi na baruti jumla debe thamanini na nne (84).
Ikawa chini akaweka risasi na madebe mengine akaweka baruti,lakini juu akaweka tende.Akaajiri jahazi moja lakini mimi wakati ule bado mdogo.Lakini ile historia walivyokuwa  wananieleza wale waliiokuwa wenziwe.
Akasikilizana na nahodha kuwa hii ni tende nipelekee Dar es salaam.Nahodha akaondoka mpaka akafika Unguja.Wakati ule Unguja ilikuwa ndani ya mikono ya waarabu wenyewe.Unguja ana nduguze.Mmoja anaitwa sheikh Suleiman bin Said Alruwahiy.Anakaa sehemu moja kule Unguja panaitwa Michungwa miwili.
Walipofika kule wakamwambia habari gani uliyonayo Mohammed?.Aliwaambia sina habari yoyote.Nimekuja tu kuwasalimia.Hakuwaambia ile siri yake.
 Ile jahazi baada ya pale akamwambia chukua hii mizigo kateremshe Dari salaam.Mimi nipo kidogo hapa halafu nakuja.Nahodha akaendesha jahazi hadi Dari salaam.Wakati ule ilipofika ile jahazi Dari salaam haipo tena ndani ya mikono ya Wajarumani.Imo ndani ya mikono ya Muiengereza.Kashatawala muiengereza.     
ITAENDELEA... 

SOURSE:  ISLAMICTIDES

PICHA ZA HARUSI YA DIDA WA TIMES FM

HONGERA SANA DIDA NA MUMEO MPYA, NDOA HALALI YA KIISLAM..


VIDEO: KWA WALE WAPENZI WA WEMA SEPETU HII NDIO REALITY SHOW YAKE

Wema Sepetu alitangaza kwamba anaandaa reality show yake chini ya kampuni anayoimiliki “Endless Fame”. Muda umefika wa kuanza kuonyesha hiyo show yenyewe na Wema ameshatoa teaser au kionjo cha reality show hiyo ambayo inaonyesha baadhi ya vitu vinavyohusika kwenye show hiyo. Kwenye hii teaser inamuonyesha Wema anazungumzia kazi, mahusiano na katajwa Diamond humo,ziara za Wema na maisha ya nyumbani. 
 


Friday, July 5, 2013

MKE WA MANDELA AELEZEA HALI YA MUME WAKE


 

Johannesburg. Mke wa Nelson Mandela, Graca Machel kwa mara ya kwanza amejitokeza hadharani kuzungumzia hali ya kiafya ya mumewe kwamba kuna wakati anazidiwa lakini hajambo.

Graca alisema hayo jana kwenye sherehe za uzinduzi wa siku ya Utamaduni na Michezo ya Nelson Mandela iliyofanyika kwenye Kituo cha Kumbukumbu ya Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini.
Alieleza sababu za kuhudhuria sherehe hizo kwamba kubwa ni kuwashukuru kwa kuwa pamoja na kumwombea afya njema Mandela tangu alipolazwa hospitali Juni 8, mwaka huu.
Graca alisema pamoja na kwamba Mandela amelala akiugua hospitali, lakini ameendelea kutoa zawadi kwa wanajamii wote ya kuwaunganisha pamoja, ambayo ni michezo na utamaduni.
“Madiba kuna wakati hayuko vizuri. Wakati mwingine anakuwa na maumivu. Lakini hajambo,” alinukuliwa Graca akizungumza katika sherehe hizo.
Katika hatua nyingine mjini Pretoria, Rais Jacob Zuma juzi alisema kuwa hali ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela bado ni mbaya na hakuna mabadiliko.
Rais Zuma alisema hayo baada ya juzi (Jumatano) jioni kwenda hospitali kumjulia hali Mandela, ambapo alikuwa na msafara mkubwa.
Kiongozi huyo pia aliwaomba wananchi wa Afrika Kusini kutenga dakika 67 kwa ajili ya Siku ya Mandela ya Julai 18, ambayo ni siku yake ya kuzaliwa.
Alisema kauli mbiu ya siku hiyo ni “Chukua hatua; penda mabadiliko; fanya kila siku iwe siku ya Mandela kwa kujielekeza katika masuala ya chakula, makazi na elimu.
Wakati huohuo, kumekuwa na hali ya utulivu katika eneo la Hospitali ya Medi-Clinic aliyolazwa Mandela, tofauti na ilivyozoeleka kuwa na pilikapilika nyingi.
Kwa mujibu wa taarifa, watu wanaopita eneo hilo la hospitali wamekuwa wakionekana wakiwa na hali ya utulivu, huku wengine wakipiga picha kwenye kadi, maua, bendera, vipeperushi na mabango yaliyowekwa kandokando ya hospitali hiyo, yakiwa na ujumbe wa kumtakia nafuu ya kuumwa Madiba.
Wakati hali hiyo ikiendelea kutokea mjukuu wa Mandela, Mandla Mandela ameendelea kuikoroga familia hiyo, baada ya kuzungumza na waandishi wa habari akidai kushangazwa na mahakama ilivyoharakisha kesi hiyo kuhusu mvutano wa sehemu ya kuzikwa Mandela na siyo miaka miwili iliyopita baada ya yeye kufukua makaburi.

SOURSE: MWANANCHI


MAGUFULI: NINA UTAMANI URAIS


.
Katika hali inayoonyesha kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, anautamani urais, amesema anaweza kutangaza nia hiyo kama atakidhi masharti yatakayowekwa kwenye Katiba mpya.

Alisema iwapo Katiba ijayo itakuja na sifa ambazo atakidhi vigezo kuna uwezekano mkubwa wa kuwania nafasi hiyo na kwamba iwapo atapungukiwa sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba hataingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Dk. Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa ‘Mshikamano Saccos’, muda mfupi baada ya mzee Paschal Nyambibo (87) kumsihi agombee nafasi hiyo mwaka 2015 kutokana na sifa zake za uchapakazi ndani ya serikali. 

Nyambibo alisema kutokana na uwajibikaji mzuri aliouonyesha Dk. Magufuli tangu mwaka 2000 akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na katika wizara mbalimbali, Watanzania wamekuwa na imani kubwa na uwajibikaji wake na kwamba anastahili kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ifikapo mwaka 2015. 

Licha ya kauli hiyo kusababisha minong’ono mingi kwa wazee waliohudhuria kikao hicho, Dk. Magufuli alionekana kutuliza hali hiyo kwa kusema isubiriwe Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano iwapo itakuwa na masharti ambayo yatamfanya kujitathimini iwapo ana sifa za kugombea au vinginevyo.

Hata hivyo, Dk. Magufuli hakusita kuonyesha hisia zake za kukerwa na baadhi ya wananchi wanaobeza maendeleo aliyotekeleza katika jimbo lake tangu alipochaguliwa kuwa Mbunge. 

Alimshutumu hadharani aliyekuwa Katibu wa CCM wilaya ya Chato kabla ya kuhamishiwa wilayani Mbogwe, Gervas Stephano, kuwa hana shukrani. 

Dk. Magufuli alimwelezea katibu huyo kuwa hana fadhila kutokana na mambo mengi aliyomtendea tangu akiwa katibu wa ofisi yake ya jimbo ambapo alimsaidia kupanda ngazi na kuwa Katibu wa CCM wilaya Chato, Kwimba, Kasulu, Kilosa na kurejea tena Chato kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita  kuendelea na wadhifa huo. 

“Tatizo lenu watu wa Chato hamna shukrani…mambo mengi nimefanya hapa Chato, lakini yote mnaona ziro…hata niliowasaidia kama Gervas naye sasa hivi ananiponda…lakini nawashukuru sana wazee wangu kwa kunikumbusha niliyoyafanya kwenye jimbo letu kupitia risala yenu nzuri,” alisema Dk. Magufuli. 

“Kutokana na hali hiyo ninawazawadia Sh. 1,000,000 mfanye sherehe ya kujipongeza kwa kuwa natambua mmejitesa sana mpaka kufanikisha kikao hiki cha leo…na kwa kuwa hamna mradi wowote wa kuwaingizia kipato kama wazee, ninaahidi kuwapa Sh.   3,000,000 kutoka mfuko wa jimbo, ili muanzishe walau saccos ya kukopeshana,” alisema. 

Baadhi ya viongozi na wananchi wamekuwa wakilitaja mara kwa mara jina la Waziri Magufuli miongoni mwa watu wanaodhaniwa kutaka kugombea nafasi ya urais wa Tanzania mwaka 2015, ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha uvumi huo. 

Mbali na Dk. Magufuli, wengine ndani ya CCM wanaotajwa  ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye anajiita mtaji wa urais; Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Ushirikiano wa Kimataifa –CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Mambo ya Nje, Bernard Membe, ambaye alipata kusema anasubiri kuiteshwa na Mungu kuwania nafasi hiyo.
SOURSE: MWANANCHI


RYAN GIGGS AND PHIL NEVILLE JOIN MAN UTD COACHING STAFF


Picture
L-T: Neville, Giggs
via BBC Sports -- Manchester United have named Ryan Giggs as player-coach and Phil Neville as their new first-team coach.

Giggs, who will be 40 in November, and ex-United player Neville, 36, are the latest additions to new manager David Moyes's backroom team at Old Trafford.

"I'm delighted that Ryan has accepted the chance to become player-coach," said Moyes.

Giggs added: "It's no secret I've been taking my qualification. I see this as the first step in my future career."

Neville, 36, takes up the role vacated by Rene Meulensteen, who has now joined manager Guus Hiddink at Russian club Anzhi Makhachkala.

Giggs continued: "It's a great privilege to be appointed as player-coach. I hope I will be able to bring my experience to bear, having been both a player and part of the Manchester United family for so long.

"I'm really looking forward to working alongside David and the team."

Moyes, who was announced as Sir Alex Ferguson's successor in May, will conduct his first news conference as manager of United on Friday at 16:00 BST.


Wednesday, July 3, 2013

KIBONZO: TASWIRA ZA DAR ES SALAAM INAPOKUWA NA UGENI NA UGENI UKIONDOKA

Picture
Picture
 


MUHIMBILI KUTENGENEZA CHUO KINGINE CHA UDAKITARI

Picha onayoonesha mchoro wa jengo

Na: Belinda Kweka- MAELEZO
CHUO Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili(MUHAS)  kipo katika mpango wa kujenga chuo kipya kwa ajili ya ufanyaji mazoezi kwa wanafunzi.Ujenzi huo  unatarajiwa kuanza Agosti mwaka huu katika eneo la Mloganzila Kibamba  ambapo , ukimalizika  utachukua wanafunzi 15,000  watakaosoma  taaluma  mbalimbali za afya. Akizungumza  na
waandishi wa habari  leo kwenye   Maonesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa  yanayoendelea katika viwanja  vya  Mwalimu  J. K Nyerere  jijini  Dares Salaam (sabasaba) ,Afisa Mipango Mkuu wa chuo hicho Ulimbaga Kijobile alisema  uamuzi  huo umetokana na ongezeko la wanafunzi ni wengi.
Alisema  eneo hilo   lita wezesha wanafunzi hao kupata sehemu  za kusomea kwa ufanisi  kama vile  ya maabara za kisasa, madarasa, na sehemu za ufanyaji mazoezi.

“Tumeamua kuanzisha mradi kwa kujenga chuo kipya kwa sababu MUHAS ina sehemu ndogo na hatuwezi kuipanua kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa chuo ili kuweza kutosha kwa wanafunzi” alisema Kajobile.
Aidha alisema wanafunzi hao , walikuwa wakipata tabu katika kufanya mazoezi ,hivyo hulazimika  kwenda  hospitali za Mwananyamala na Amana.“Muda mwingine tunatumia hospitali nyingine ili kupata sehemu ya kutosha lakini hospitali hii itakayojengwa itasaidia kuchukua wanafunzi wote ili kuweza kufanya mazoezi yao bila usumbufu” alisisitiza Ulimbaga.
Alisema  ujenzi wa  chuo hicho, kinakadiriwa kujengwa ndani ya mwaka mmoja,ambapo  wanafunzi wa muhula wa kwanza wa mwaka 2015 wanatarajiwa kuanza.
Aliongeza  kuwa kitatoa huduma za kiafya kama hospitali nyingine hivyo wananchi wa eneo hilo wanashauriwa kufika mara baada ya ufunguzi wa chuo hicho ili kupata matibabu mbalimbali.


KIBONZO: ANGALIA KITUKO HIKI CHA KISARAWE

.
.
Huku tunakoishi uswahilini wengi wetu huwa hata majumba ya Cinema wanakolipia elfu kumi kutazama movie huwa hatuyafahamu au hatujawahi kwenda kabisa…. hivyo kuna kautaratibu ketu ka kuchangisha hizi mia mia na mia mbili kwa ajili ya kuingia ‘vibanda umiza’ ambavyo huwa vinatutoza hizo senti kwa ajili ya kutazama movie zilizotafsiriwa pamoja na mpira…. yani kutazama hivyo vitu viwili sehemu kama hizo ni kawaida kabisa.
Sasa bwana kwenye eneo la Kisarawe ambalo liko kwenye mkoa wa Pwani, kuna mjanja mmoja alitumia akili ya ziada kujua kwamba sio kila mmoja anaweza kwenda town kusubiria kuona msafara wa Rais Obama, hivyo akaamua kuchangisha hizo mia mia kwa kila anaetaka kutazama ujio wa Rais Barack Obama Tanzania ambao ulikua unaonyeshwa moja kwa moja na vituo mbalimbali vya TV ikiwemo ya Taifa TBC1 na Clouds TV.
Uhakika wa kuzikusanya hizo mia mia ulikuwepo sana kwa sababu kwanza Kisarawe sio kila Mwananchi anamiliki TV au nyumba yake ina umeme hivyo ni lazima tu kama angekua na shilingi 100 angejikusanya kwenye kibanda umiza kucheki hilo movie la Obama kwenye ardhi ya Tanzania.

 SOURSE:MILLARD AYO 

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU