Facebook Comments Box

Friday, June 28, 2013

NDEGE ZA MAREKANI ZAWASILI DAR ES SALAAM


DAR ES SALAAM.   MAKACHERO wa Marekani wameendelea na matayarisho ya mwisho ya ziara ya Rais Barack Obama, ambapo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere walikuwa na kazi ya kuunganisha helikopta za doria.
Makachero hao walikuwa wakiunganisha helikopta sita zilizosafirishwa vipande vipande kutoka Marekani, ambapo meli mbili za kivita na ndege moja pia zimewasili.
Rais Obama tayari yuko katika ardhi ya Afrika, ambapo leo anatarajiwa kwenda Afrika Kusini baada ya kumaliza ziara yake ya kwanza Senegal na anatar ajiwa kuwasili nchini Jumatatu.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa jana na Mwananchi unaonyesha Marekani imeleta helikopta hizo kwa ajili ya ulinzi wa Rais Obama, zikiwemo meli zilizobeba helikopta nyingine mbili na ndege.
Habari zilizopatikana kutoka kwa wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,zinasema kuwa helikopta sita zinaunganishwa katika sehemu ya karakana ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Mpashaji mmoja aliliambia gazeti hili kuwa helikopta hizo zililetwa kama vipande vipande vilivyosafirishwa kama mzigo kwenye meli za kivita zilizotia nanga jijini Dar es Salaam.
“Nilikaribia kwenye eneo la karakana na nikashangaa kuona jinsi jamaa walivyokuwa ‘bize’ wakiunganisha vyuma mbalimbali na kutengeneza helikopta hizo,” aliongeza mpashaji wetu, ambaye alibahatika kusogelea eneo hilo licha ya kuwepo kwa ulinzi mkali.
Inaaminika kuwa helikopta hizo zitakuwa zinasaidia kusafirisha watu na mizigo kutoka kwenye meli za kivita ambazo zimeegeshwa kwenye Kikosi cha Maji cha JWTZ.
Pia helikopta mbili zinaaminika ziko katika meli ambazo zimeegeshwa huko Kigamboni.
Meli za kivita na ndege ya kijeshi
Katika hatua nyingine, meli mbili za kivita ambazo zimetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu zimeegeshwa Kigamboni.
“Jamaa wana meli kali kwa kweli, mimi nimekuwa askari wa Kikosi cha Maji kwa muda mrefu na kufanya mazoezi na mataifa kadhaa, lakini sijaona meli kama zile.


BARACK OBAMA KUPEWA PHD YA HESHIMA NA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA

Taarifa ambazo zinasikika zikimnukuu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam zinasema ya kuwa Ocean Road itabadilishwa jina lake na kuitwa, "Barack Obama Avenue" kwa heshima ya Rais huyo wa 44 wa taifa la Marekani.

Taarifa nyingine zinasema kuwa Obama pia atatunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Heshima na Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania (OUT) kwa kutambua mchango wake katika maisha ya binadamu kwenye nyanja ya maendeleo ya kiuchumi.

Amenukuliwa Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Tolly Mbwete akisema tuzo hiyo imethibitishwa na Baraza Kuu la Chuo hicho baadaye kupitishwa na Mkuu wa OUT, Dk Asha Rose Migiro.

“Rais Obama anatunukiwa tuzo hiyo akitanguliwa na hayati Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, Rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela na Rais wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin Mkapa.

OUT imeshatoa pia shahada za heshima kwa mtafiti na mtetezi wa Sokwe wa Gombe, Dk Jane Goodall na Mhadhiri wa Mawasiliano bwana David Mellor.



HISPANIA YAFANYA KILICHOTAKWA NA WAPENZI WENGI WA SOKA PALE ILIPOING'OA ITALIA KWA PENATI 7-6 NA KUTINGA FAINALI

HISPANIA imeitoa Italia katika Kombe la Mabara kwa ushindi wa matuta wa 7-6 mjini Fortaleza, kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 katika mchezo mkali wa Nusu Fainali.

Wataliano walifungwa na Waspanyola katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana, itawakutanisha wenyeji Brazil na Hispania kama wapenzi wengi wa soka walivyokuwa wanataka ili waone soka ya uhakika ikichezwa ndani ya Maracana.

Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja ya penati yake na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na kuipeleka Hispania Fainali.


Close shave: Spain moved through to the Confederations Cup final after beating Italy on penalties in Fortaleza


Dramatic: Spain triumphed 7-6 in a dramatic shootout to set up a dream final against Brazil
Off target: Italy blinked first in the shout-out when Leonardo Bonucci fired over at 6-6
Decisive: Jesus Navas stepped up to score the winning penalty and send Spain to the final
Jesus Navas akiifungia Hispania Penati ya Mwisho na Kutinga Fainali ambapo watapambana na wenyeji Brazil ndani ya Uwanja wa Maracana.
Evens: The teams were locked at 0-0 after 120 minutes in the all European semi-final
Torres
Outnumbered: Italy's Giorgio Chiellini tries to win a header against Sergio Ramos and Gerard Pique
Effort: Fernando Torres attempts a shot on goal as Gianluigi Buffon watches
On the ball: Manchester City's David Silva attempts one of his elusive runs
David Silva
Held his nerve: midfielder Andres Iniesta slotted his penalty past Buffon in the Italian goal
Andres Iniesta.





ABASS MTEMVU AUNGURUMA TEMEKE


 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (aliyevaa miwani katikati), akifuatwa na wananchi baada ya kumaliza mkutano wa kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Kata ya Temeke, Dar es Salaam hivi karibuni.
 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Dar es Salaam, Abbas Mtemvu akihutubia katika mkutano wa hadhara wa kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Kata ya Temeke, Dar es Salaam hivi karibuni. 
 Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu akimsikiliza Mweka Hazina wa Kikundi cha Kuweka na Kukopa (VICOBA), Anjela Ndigula ambaye alipokea sh. 50,000 alizotoa msaada kwa Muya Thabit ili ajiunge na kikundi hicho, baada ya kuambiwa hana haki hivyo anashindwa kulipia pango. Msaada huo aliutoa katika mkutano wa hadhara wa kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Kata ya Temeke, Dar es Salaam hivi karibuni.
 Muya Thabit akicheza kwa furaha baada Mbunge Mtemvu kumsaidia fedha za kujiunga na vicoba
 Diwani wa Kata ya Temeke, Khamis Nsombo, akiwazawadia fedha wasanii wa kikundi cha Msimamo

Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu akikizawadia fedha kikundi cha sanaa cha Msimamo kilichokuwa kinatumbuiza katika mkutano wa hadhara wa kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Kata ya Temeke, Dar es Salaam hivi karibuni. Pia aliahidi kukipatia kikundi hicho sh. 500,000 za kununulia vifaa.
                  
                           Muya Thabit akiomba fedha kwa Mbunge Mtemvu ili alipe pango
                                    Wananchi wakiuliza maswali kwa Mbunge wao Mtemvu






Thursday, June 27, 2013

WAKILI WA MUME WA JOYCE KIRIA ATOA MAELEZO KUHUSU MTEJA WAKE

Henry John Kileo alipigiwa simu na Maafisa wa Police Makao Makuu mnamo Tarehe 17/6/2013, wakimuarifu kwamba wanataka kufanya mahojiano naye.Hawakusema ni kuhusu nini.mara moja Kilewo akawasiliana nami kama wakili wa familia yao na Joyce Kiria ,nami nikawasiliana na maafisa hao kuwaarifu kwamba kwa kuwa nina majukumu kadhaa ya kkimahakama, na kwa kuwa Kilewo yuko nje ya mkoa, basi ninaahidi kama wakili kuhakikisha ninamepeleka binafsi Kilewo Makao Makuu Police mnamo Ijumaa ya tarehe 21/6/2013.

Tarehe 21/6/2013 tuliambatana mimi, Kilewo na John Mnyika (MB) mpaka Police Makao Makuu, ambapo Mnyika alituacha na Kilewo;mahojiano yakaanza.Kwa ujumla walimuhoji Kilewo mambo mbalimbali kuhusiana na tukio la kumwagiwa tindikali kijana aitwaye Mussa Tesha katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mnamo mwaka 2011.Wakati mahijiano hayo yanafanyika,tayari kulikuwa na Case ya jinai ikiendelea huko Igunga, ambapo washtakiwa Wanne (4) ambao ni makada wa Chadema kutoka maeneo mbalimbali nchini walishtakiwa kama mshtakiwa nambari moja mpaka nne.Walishtakiwa kuhusiana na tukio hilo nililolisema, la Mussa Tesha kumwagiwa Tindikali.Walishtakiwa chini ya vifungu vya sheria ya kanuni ya adhabu, (Penal Code, na si ugaidi).

Baada ya mahojiano na Police yaliyomalizika kwa Kileo kuandikisha statement mpaka mnamo saa 11.30 hivi 
za jioni ya hiyo Tarehe 21/6/2013, Police walimnyima Kilewo dhamana, na wakampeleka remand iliyoko Central Police Station,akalala huko.

Jumamosi ya mnamo tarehe 22/6/2013, mimi wakili, Joyce Kiria na John Mnyika tulifika Central Police station, ambapo OCS wa hiyo Central Police Station alituarifu kwamba amri alizonazo ni kwamba Kilewo haruhusiwi kuonana na mtu yeyote. Kama wakili nilijadiliana masuala ya kisheria na OCS, ikalazimu kuwasiliana na maafisa wa Police Makao Makuu ambao hatimaye waliniruhusu mimi kama wakili kwa mujibu wa sheria kuonana na mteja wangu.

Tukazungumza na kupeana "moyo", nikahakikisha amekula chakula kilicoletwa na mkewe Joyce Kiria (ambaye muda wote alikuwa akimuangalia mumewe kwa mbali tu,kwani mazungumzo yangu na Kilewo yalifanyika faragha).

Mnamo saa 7.30 hivi tuliondoka sote (wakili, Kiria na Mnyika), na kukubaliana kurudi tena Central Police Station Jumapili ya Tarehe 23/6/2013 kumtembelea tena Kilewo, na pia kufahamu mipango hasa ya jeshi la Police kuhusu Kilewo kwani mpaka tunaondoka si wakili wala mkewe Kilewo aliyefahamishwa rasmi kuhusu mipango hiyo.

Nikiwa Nyumbani nilipokea simu toka kwa Joyce Kiria akiniarifu kwamba amefika Central Police Station jioni ya Jumamosi ya tarehe 22/6/2013 na kuarifiwa tu kwa mkato kwamba Henry John Kilewo "ameondoka".

Ukweli kama mke alikuwa amechanganyikiwa, na jukumu la kwanza lilikuwa kumtuliza kisaikoilojia kwani nilifahamu kina Kilewo walikuwa wamepata mtoto muda si mrefu huko nyuma;kwa hiyo hali ya Joyce ilikuwa delicate sana kiafya na kisaikolojia.

Nikapambana kama wakili kwa kutumia uzoefu na contacts (P.R) ili kupata tarifa ya aliko mteja wangu.
Niliariwa tu "off record" na maafisa wa Police kwamba Kilewo amesafrishwa kwa ndege ya Precision kuelekea Tabora kupitia Mwanza chini ya ulinzi wa maafisa Senior wa Police ili kule Tabora afunguliwe Case. Sikuwa na mawasiliano yeyote na mteja wangu, na hizo taarifa "off record" ndo cha pekee tulichokuwa nacho mimi, Joyce Kiria na uongozi wa Chadema kuhusu nini kimemsibu Henry Kileo.

Niliendelea kupambana kupata taarifa rasmi, na hatimaye Jumapili ya Tarehe 23/6/2013 majira ya saa 6 hivi (noon) ndipo nilipopigiwa simu na mmoja wa maafisa waliomsindikiza Kilewo kuelekea huko Tabora kwa utaratibu ule ule wa "off record", na kuniunganisha na Kilewo, ambapo nilizungumza naye kwa kifupi kumjulia hali na kumuhakikishia kwamba tutapigana kwa uwakili wetu wote kwa ajili yake.

Kwa hiyo mpaka muda huo hatukuwa bado na uhakika wa 100% kwamba Kilewo yuko wapi hasa. Kw wale mawakili wenzangu wanafahamu kwamba huwezi tegemea taarifa za kusikilizishwa mteja kwenye simu ambayo hata si ya kwake.Wala huo si ushahidi wa alipo mtu huyo kisheria.

Lakini ikatubidi ku-"assume" kwamba Kilewo yuko/atapelekwa Tabora kushtakiwa.mimi na Prof Abdallah Safari tukaanza maandalizi ya upesi upesi ya safari kuelekea Tabora kwa gari (kwani ndege kuulekea Tabora ni Jumamosi na Jumatatu tu). Tuliondoka kwa gari ya makao makuu ya Chadema Jumapili ya tarehe 23/6/2013, majira ya saa 11.30 hivi za jioni. Tulisafiri usiku kucha, na tulichukuwa "risk" ambazo kwa kawaida tusingechukuwa, ikiwemo kupita katika mapori maarufu kwa utakaji;kilichotusukuma na kutupa moyo ni kwamba Henry John Kilewo yuko mahali ambapo anatuhitaji sana, na hana tumaini lingine bali sisi mawakili wake.

Tukisafiri usuku kucha na kufika Tabora asubuhi ya Jumatatu tarehe 24/6/2013, majira ya saa 2.30 asubuhi;tumechoka hakuna mfano.Tukabadili mavazi upesi upesi na kuvaa suits zetu na kukimbilia mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora, ambapo turiarifiwa kuwa wao hawana taarifa zozote za Kilewo. Tukaelekea Makao Makua ya Police Tabora;jibe likawa ni lile.

Maana yake ni kwamba sisi mawakili wa Kilewo, tuko Tabora ambayo ni kubwa has, na hatujui mteja yuko wapi hasa. Nikafanya juhudi zile zile za "off record", na kufahamishwa kwamba Kilewo alishikiliwa Police Station ya Nzega (masaa matatu toka Tabora), na kwamba yuko njiani kuletwa Tabora. Hatukuwa na uhakika bado, ila ilitulazimu kushikilia hako kataarifa kasiko rasmi, na kuendelea na maandalizi ya case.

Majira ya saa 9 hivi za alasiri ya Tarehe 23/6/2013 Kilewo, akiwa chini ya ulinzi mkali sana wa FFU katika Land Cruisers Mbili za Police waliwasili Mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora; hajala tangu jana yake.
Alikuwa yeye na wenzake wanne ambao walikuwa wamefutiwa mashtaka kwa hati ya "Nolle Prosequi" huko Igunga, kisha kukamatwa tena mara moja na kusafirishwa kwa ulinzi mkali sana mpaka Tabora.

Ukweli ni kwamba tulivyoonana na Kilewo si mawakili wala KIlewo mwenyewe aliyejizuia kulengwa na machozi;yeye akimshukuru MUNGU kwamba tumepambana na yote mpaka Tabaora kwa ajili yake kwa kasi vile, nasi kwamba hatimaye tumeonana na mteja wetu.
Tukaingia Mahakamani, Kilewo na wenzake wakasomewa mashtaka mawili; moja chini ya sheria ya kuzuia ugaidi kwamba walimteka kwa nia ya ugaidi Mussa Tesha huko Igunga, Tabora na la pili kwamba walimdhuru kwa kumwagia Tindikali.

Makosa ya Ugaidi hayana dhamana.

Mawakili tulipambana na kutoa hoja za kisheria nne (4) dhidi ya uhalali wa mashtaka yenyewe na utaratibu wa kufungua case husika. Tumeoimba mahakama kufuta mashtaka ya ugaidi, au la iamuru kila mshtakiwa arudishwe kushtakiwa mahali alikokamatwa (mfano Kilewo, Dar es Salaam).

Uamuzi wa Mahakama ni tarehe 8/7/2013.

Kabla ya kuondoka Tabora jana, tulipita kumuaga Henry Kilewo na wenzake katika gereza la Uyui. Wote wako na combat zao za chama chao, na wako imara, hasa baada ya kuona mawakili wako imara.

Cha msingi ni kuomba MUNGU aipe mahakama ujasiri.

Peter Kibatala, Advocate

Source: WAVUTI

KONGAMANO LA WAZI LA UZINDUZI WA MPANGO WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

KONGAMANO LA WAZI NA UZINDUZI WA MPANGO WA KULETA MATOKEO MAKUBWA SASA KWA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (Mbunge), anawaalika wadau wote wa Sekta ya Nishati na Madini kote nchini kwenye kongamano la wazi litakalofanyika siku ya Jumatano Julai 3, 2013 kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Mwenge Jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 3.00 asubuhi hadi saa 11.00 jioni.

Mada kuu ni kujadili, kushauri na kutoa maoni juu ya miradi mikubwa ya kitaifa ya sekta ya nishati itakayotekelezwa na Wizara ya Nishati na Madini kwa kipindi cha miaka mitatu, Julai 2013 – Disemba 2015 ili kuliwezesha Taifa kufikia Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now).

Wadau wanaoalikwa ni pamoja na:

Mabenki washirika, Wakandarasi kwenye sekta ya Umeme, Wahandisi kutoka Taasisi na Vyuo Vikuu nchini, Mashirika ya Kiserikali na yasiyo ya kiserikali, Wawakilishi kutoka Makampuni mbalimbali, Migodi, Viwanda vikubwa na vidogo na wananchi wote kwa ujumla.

Hakuna kiingilio kwenye uzinduzi huo.

“Matokeo Makubwa sasa kwa maendeleo ya Mtanzania”

Imetolewa na:
Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini



Wednesday, June 26, 2013

WAKATI WACHEZAJI WENGINE WAKILA RAHA: DEMBA BA AENDA MAKKA NA MEDINA KUFANYA IBADA





ADAM JUMA WA VISUAL LAB ATANGAZA KUACHA KUTENGENEZA VIDEO


Taarifa iliyotufikia ni kwamba Adamu Juma adai kuacha kufanya video za muziki,Akiongea na mtandao wa Bongo 5 Adam juma amesema kwamba kwa sasa anafanya kazi na NGOs mbali mbali kuelimisha jami,alisema tena kwamba video production ni business yake lakini kwa sasa "right now im not doing"lakini bado kuna wasanii anawasiliana nao kuwasaidia kibiashara na kimaendeleo soim still around.Adam juma amesema haoni kama kutakuwa na pengo kwa yeye kutofanya video kwani kuna video production company nyingi zinafanya vizuri tu.

HII NDIO HALI ILIVYO NJE YA HOSPITALI ALIYOLAZWA MANDELA

UJUMBE MBALIMBALI KWAKE
UJUMBE MBALIMBALI UKIWA UMESAMBAA ENEO LOTE LA NJE YA HOSPITALI

WAANDISHI WA HABARI WAMEWEKA KAMBI MDA WOTE TANGU ALAZWE HAPO MZEE MANDELA TUNAMTAKIA KILA LA HERI APONE HARAKA





AUDIO: ZITTO KABWE: I AM TANZANIAN

\


Of blood cleaned by fresh waters of the lakes and the rivers and the streams of my great nation. A vision from the top of mount Kilimanjaro and honesty as clear as The Serengeti savannah. Pure as virgin beaches of Zanzibar. Hopeful as a product of Azimio. Sparkling as Tanzanite stone out of the Land of Maasai.

I am a Tanzanian.

Born of the peoples of Africa, of Tanzania. The Pains of the struggle of African liberation. The pains of The Revolution. Whatever the setbacks of the moment, nothing can stop me from being a Tanzanian, an African. The land of Kambarage. The state of our own creation. Whatever the difficulties, Tanzania shall remain ONE, Strong and UNITED. However improbable it may sound, Tanzania shall prevail. Amongst nations of the world. We are The United Republic of Tanzania.

I am a Tanzanian
.



HIZI NDIO SABABU ZILIZOFANYA JOSEPH MBILINYI (MB) AACHIWE KWA DHAMANA

Kuhusu Joseph Mbilinyi 'Sugu', Mbunge wa Mbeya Mjini. Ni kweli alikuwa polisi Dodoma, alikoitwa kwa madai ya kutoa lugha ya matusi kwa Ndugu Mizengo Pinda, lakini hajaandikisha maelezo, kwa sababu 3, zifuatazo:
  1. Wakili wake, Tundu Lissu, amewaambia kuwa Polisi hawawezi kumkamata na kumhoji Mbunge Sugu, iwe ukumbini, maeneo ya bunge, au nje ya maeneo ya bunge, wakati bunge likiendelea, kutokana na parliamentary immunity aliyonayo hadi polisi watakapofuata taratibu zinazotakiwa.

  2. Neno hilo wanalotuhumu kuwa ni lugha ya matusi, si tusi kwa sheria za nchi yetu, bali linaweza kutumika kwa vitu au mtu anayefanya matendo au kusema maneno yanayostahili kuitwa hivyo.

  3. Wakili wake (Tundu Lissu) kawauliza, nani mlalamikaji katika tuhuma hizo, je wamepokea malalamiko ya Ndugu Pinda mwenyewe? Majibu yalikuwa ya kigugumizi.

Wameondoka polisi kwa makubaliano ya kurudi kesho asubuhi.

Na: Tumaini Makene, Afisa Habari, CHADEMA.

Source: WAVUTI


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU