Facebook Comments Box

Thursday, June 6, 2013

PICHA M TO THE P AKIMUAGA MANGWEA MOROGORO LEO




MAREKANI WAANDAA SHERIA ITAKAYO KATAZA WATU KUVAA MLEGEZO


Sina shaka umeshasikia style za uvaaji wa suruali hususan kwa wanaume zenye majina kama mlegezo au kata k, au yawezekana ukawa huzijui kwa majina lakini umeshashuhudia vijana wamevaa suruali chini ya makalio.
Kama ambavyo mabinti wamekuwa wakilaumiwa kwa mavazi ya kuonyesha miili yao hasa sehemu nyeti, na upande wa wanaume wamekuwa wakilalamikiwa kwa style hiyo ya uvaaji ambayo imeonekana kuigwa hata na vijana wadogo ambao bado wako shuleni.
Katika hali ya kukerwa na tabia ya vijana kuvaa suruali chini ya makalio uongozi wa Wildwood, New Jersey nchini Marekani umeandaa sheria mpya itakayoweza kuwadhibiti wale wote wenye tabia hiyo ya kuvaa mlegezo na kukatiza mitaani.
Sheria hiyo inaelekeza wavaaji wote wa suruali, kaptura, mavazi ya kuogelea na sketi zisivaliwe chini ya inchi 3 kutoka kiunoni mwa mvaaji.

Mayor wa Wildwood Ernie Troiano Jr. aliwaambia waandishi wa habari kuwa amechoshwa na malalamiko anayoyapata juu ya vijana wanaotembea makalio nje kwa kushusha suruali zao kupita kiasi.


HII NDIO KAULI YA M 2 THE P BAADA YA KUFIKA TANZANIA KUMZIKA MANGWEA


 Rafiki wa wa karibu wa marehemu Albert Mangwea aliyekuwa amelazwa nchini Afrika Kusini amerejea Tanzania na yuko njiani akielekea mkoani Morogoro kwaajili ya kushiriki mazishi ya swahiba wake Mangwea jioni ya leo (June 6).Akizungumza na Times Fm asubuhi hii Mgaza Pende a.k.a M 2 The P amewashukuru watanzania kwa kumuombea japo hali yake bado haijawa nzuri sana lakini ameamua kurudi Tanzania kuja kumzika ndugu yake Mangwea. “Ndugu zangu watanzania mimi ni Mgaza Pende M 2 The P nawashukuru sana kwa kuniombea mpaka muda huu, nimeweza kuwasili Tanzania salama na tutakuwa pamoja kwenda kumzika ndugu yangu kipenzi changu Albert Mangwea, nawashukuru sana watanzania kwa kuniombea asanteni na endeleeni kuniombea hali yangu bado haijawa nzuri zaidi, asanteni,” alisema. Msikilize hapa 


PICHA ZA UTOAJI WA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MANGWEA MOROGORO

Meza kuu hii ikiwa ni maandalia ya kuuwaga mwili wa msanii marehemu Albert Mangwea aliyefariki dunia na anatarajiwa kuzikwa leo mkoani morogoro.Utaratibu huu umeandaliwa katika uwanja wa jamuhuri mkoani morogoro kwa lengo la kuwapa fursa wakazi wa mji huo kupata nafasi za kuuwaga mwili huo kabla ya maziko

Umati mkubwa wa wakazi wa morogoro waliojitokeza katika zozi za kuwaga mwili wa msanii huyo mchana huu kabla ya maziko yake leo.Marehemu albert mangwea alifariki wiki iliyopita nchini afrika kusini na maziko yake yatafanyika leo mkoani hapa.


 Mama Mzazi wa Mangweha, Denisia Mangweha akiwa nyumbani kwake kabla ya safari kuelekea Uwanja wa Jamhuri.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera akiwasili nyumbani kwa Mama mzazi wa Mangweha.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera asubuhi hii amefika nyumbani kwa Mama Mangwea eneo la Kihonda Mazimbu Road na kumpa pole kwa niaba ya wakazi wote wa mkoa wa Morogoro. Baada ya kutoa pole, Mhe. Bendera aliongoza umati wa watu kutoka Kihonda kuelekea Uwanja wa Jamhuri kwa shughuli za kuaga mwili wa Albert Mangwea aliyefariki dunia Mei 28 mwaka huu nchini Afrika Kusini. Mangwea anatarajiwa kuzikwa katika makaburi ya Kihonda nje ya Kanisa la Mtakatifu Monica jirani kabisa na alipozikwa baba yake mzazi Mzee Keneth Mangwea.
943280_10152915710755525_916679441_n
 Wakazi wa mjo wa morogoro waanza kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu albert Mangwea kabla ya kumpeleka katika Nyumba yake ya Milele. Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahala Pema.




MAJANGA YAZIDI MUANDAMA MR. NICE SASA MKATABA WAKE NA GRAND PA RECORDS YA KENYA WAVUNJWA


Mwanamuziki aliyevumbua staili ya muziki ya TAKEU (Tanzania Kenya Uganda), Mtanzania Lukas Mkenda aka Mr Nice amepoteza mkataba wake na kampuni ya kurekodi muziki ya nchini Kenya, kwa kile kilichoelezwa na kampuni hiyo kuwa ni tabia ya Mr Nice ya uvivu, ulevi, asiyeaminika na asiye na ushirikiano. 
Zaidi ya maandishi yaliyoandikwa na GrandPa Records kwenye ukurasa wao wa Facebook, pia wamezungumzia suala hilo walipohojiwa na kituo cha EA Radio ambapo wamesema Mr Nice amesema ataendelea kubaki mjini Nairobi nchini Kenya akitafuta kujiweka sawa. 



Wednesday, June 5, 2013

KOCHA WA YANGA AWASILI KWA AJILI YA KUINOA TIMU KWA AJILI YA MSIMU MPYA

Kocha Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Ernie Brandts (kulia) baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam usiku wa leo akitokea kwao Uholanzi kwa mapumziko mafupi baada ya kumaliza msimu, tayari kuanza maandalizi ya kikosi chake kwa msimu mpya. Aliyemlaki kushoto ni Meneja wa Yanga SC, Hafidh Saleh.

Anaondoka Airport 

Baada ya kutua, kitu cha kwanza aliwasha simu yake

Anafungua mlango wa gari lake apakie mizigo

Anafungua mlango wa nyuma apakie mizigo

Hahitaji msaada wa mtu, anapakia mwenyewe

Anafunga mlango baada ya kupakia

BIN ZUBEIRY anaondoka baada ya kumaliza kazi yake

Brandts naye anapanda gari lake

Anapiga stata...


Anaondoka Airport 


POLISI WATUMIA MBWA KUTAWANYA WATU LEADERS BAADA MUDA WA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KUISHA

Asakari Polisi wakitumia mbwa kutawanya maelefu ya watanzania waliotaka kuuaga mwili wa Mangwea baada ya muda uliopangwa kukamilika
ASKARI wa Jeshi la Polisi walilazimika kutumia Mbwa kuwatawanya mamia ya Watanzania waliojitokeza kuuaga mwili wa marehemu Albert Mangwea lakini wakashindwa baada zoezi hilo kukatishwa.
Mangewa alifariki Dunia nchini Afrika Kusini katika Jiji la Johannesburg Mei 28 mwaka huu na kusafirishwa kuja nchini jana jioni, mamia hao wa watanzania wameshindwa kuuaga mwili wa kipenzi chao baada muda ulioapngwa kukamilka huku wakibaki katika foleni ndefu.
Kitendo cha Kamati ya maandalizi kukatisha zoezi la kuuaga mwili wa marehemu kwa sababu ya muda uliopangwa kukamilika iliwashangaza mamia ya watu waliokuwa kwenye foleni ya kusubiri kupata nafasi ya kutoa heshma zao za mwisho mbele ya Jeneza la Mangwea.
Zoezi hilo liloanza saa 2:30 asubuhi imesitishwa saa 6:30 mchana kwa saa za Afrika Mashariki na Kati, na msafara ukiongozwa na Askari wa Jeshi la Polisi pamoja na vikosi vya ulinzi na usalama waliokuwa katika Viwanja vya Leaders Club.
Barabarani Asakari wa Kikoso Cha Usalama Barabarani pia walijiapanga vizuri kuhakikisha kwamba msafara wa mwili wa marehemu unapita vizuri katika maeneo yaliokuwa yamepangwa kuelekea mjini Morogoro.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Mr Blue alifika katika viwanja hivyo akiwa amechelewa na kukosa muda wa kuuaga mwili wa Mangwea lakini alipokutana na mashabiki wa muziki wake aliweza kusimama na kuwapa pole.
Mwili wa Mangwea hivi sasa uko safarini kuelekea Mjini Morogoro ambapo utalala nyumbani kwa mama yake na kesho uwakazi wa Mji huo pia watapata nafasi ya kutoa heshma zao za mwisho

ANUSURIKA KUUAWA BAADA YA KUKUTWA AKIMBAKA BINTI WA MIAKA KUMI

Mkazi mmoja wa Mwangata katika Manispaa ya Iringa amenusurika kuuwawa na wananchi baada ya kukutwa akimbaka binti wa miaka kumi.

Tukio hilo linaelezwa kutokea jana saa nane mchana, pale ambapo mazazi wa binti huyo alipomsikia mwanaye akilia kwa uchungu, na aliposogea kujua kulikoni, alimshuudia kijana huyo akiendelea na ubakaji jambo lililosababisha apige kelele kuomba msaada wa wananchi.


 
Kutokana na kushamiri kwa vitendo vya ubakaji katika eneo hilo, mtuhumiwa huyo alijikuta akipokea hasira za wananchi kwa kupigwa na kunusurika kuchomwa moto baada ya baadhi ya wananchi wengine kushauri afikishwe polisi.

Mtuhumiwa huyo amefikishwa katika kituo kikuu cha polisi mjini Iringa akivuja damu kichwani.

PICHA ZA UWANGWAJI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEA LEO VIWANJA VYA LEADERS



Umati wa watu wakiwa wamepanga mstari tayari kwa kwenda kuaga huku kikosi cha msalaba mwekundu na polisi kikiwa stand by just incase anything happens. Sasa naskia watu badala ya kwenda na kuaga wao wako busy wanapiga picha kha hizi teknolojia aiseee tutajutaaaa 
Baadhi ya ma super star wa bongo wakiwa kwenye mstari tayari kwa kuaga.
Jeneza likiandaliwa kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho


Diamond akiwa dada yake Queen Darlin


Diamond akimuaga Ngwair









MADIWANI WAPENDEKEZA JINA LA MKOA MPYA LIWE MBOZI, MAKAO MAKUU YAWE VWAWA

KIKAO cha dharura cha Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya Mbeya kimependekeza jina la mkoa mpya wa Mbeya liwe ni Mkoa wa Mbozi badala ya mkoa wa Rungwe kama ilivyopendekezwa na wataalamu,wenye makao yake makuu wilayani Mbozi katika mji wa Vwawa. Wakizungumza katika kikao hicho Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya walisema kuwa azma ya kupendekeza kuwepo kwa mkoa mpya katika wilaya ya Mbozi umezingatia jiografia ya mkoa na fursa za kiuchumi zilizopo badala ya hamasa za siasa. ‘’Sisi ni madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya, hatuna maslahi yoyote ya kisiasa na wilaya ya Mbozi, tumezingatia fursa za kiuchumi na jiografia ya mkoa ambayo italeta tija na maslahi kwa Taifa,’’alisema Bw. Mashauri Mbembela Diwani wa kata ya Nsalaga. Awali katika mapendekezo hayo ambayo yaliwasilishwa na Ofisa Uchaguzi wa wilaya kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya Bi. Marietha Mlozi,Bw.Edward Mwaigombe alisoma taarifa ya mapendekezo ya jina la mkoa mpya kuwa ni Rungwe kama lilivyopendekezwa na wataalamu. Bw. Mwaigombe alisema kuwa, taarifa ya wataalamu imezingatia vigezo vya idadi ya watu, ukubwa wa eneo, huduma zilizopo na mawasiliano ambayo ni mapendekezo kutoka katika kamati za maendeleo za kata 14 za Ulenje, Lwanjilo, Ikukwa, Swaya, Mshewe, Igale, Iyunga Mapinduzi, Tembela, Bonde la Songwe, Utengule Usongwe, Ilungu, Ilembo na Inyala. Alisema kuwa kamati zilipendekeza mkoa wa Mbeya ugawanywe katika mikoa miwili ya Mbeya na Rungwe ambapo mkoa wa Mbeya wenye takwimu ya idadi ya watu 1,721,795 na ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 41,544 umependekezwa kuundwa kwa wilaya za Chunya,Mbozi,Momba, ambapo makao yake makuu yanatarajiwa kuwa jiji la Mbeya. Bw. Mwaigombe alisema kuwa mkoa wa pili ambao una takwimu ya watu 985,915 na ukubwa wa eneo wa kilomita za mraba 22,073 unatarajiwa kuundwa na wilaya za Mbarali, Rungwe,Kyela na Ileje na makao yake makuu yanatarajia kuwa katika wilaya ya Rungwe. Aidha katika taarifa hiyo kwa madiwani wa halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, ilipendekezwa kuanzishwa kwa wilaya mpya kutokana na jiografia na kuzingatia mgawanyo mpya wa mkoa kati ya wilaya ya Mbeya na Halmashauri ya Jiji la Mbeya na kupendekezwa wilaya hizo zigawanywe katika wilaya tatu. Hata hivyo katika mapendekezo ya madiwani wa halmashauri hiyo walisema kuwa mji wa Mbalizi ujigawe kutoka katika halmashauri ya wilaya ya Mbeya na ujitegemee kuwa wilaya kamili. Katika mapendekezo ya awali madiwani walipendekeza majina mawili ya mkoa wa Mbozi na Mkoa wa Songwe ambapo jina la mkoa wa Mbozi lilipitishwa na madiwani kwa kura 24 dhidi ya kura 3 ambapo baadaye majina mawili ya mkoa wa Rungwe na mkoa wa Mbozi nayo yalipigiwa kura na jina la mkoa wa Mbozi lilipita kwa kura 24 dhidi ya kura tatu za jina la mkoa wa Rungwe. Akizungumza katika kikao hicho Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya Bw. Mwalingo Kisemba alisema kuwa mchakato huo umekuja baada ya ushauri na mapendekezo ya kuugawa mkoa wa Mbeya ambao kwa sasa una jumla ya watu milioni 2.7 na ukubwa wa kilomita za mraba 63,617.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU