
Na Mwandishi Wetu, 
WENGI
 wa watu nchini China wanapendelea ujenzi wa majengo makubwa ya 
kihistoria na magari kadhaa yenye muonekano wa alama ya uchina kama 
ishara ya kuonyesha ufanisi wao katika uvumbuzi wa vitu mbalimbali 
duniani.
Lakini
 basi tena, wachina ni watu katika jamii wanaopenda kufanya mambo 
makubwa na tofauti na ni wazalishaji wa vitu vingi vya hapa leo duniani,
 sasa wachina wanatengeneza meli kubwa kwa mfano wa meli maarufu ya 
Titanic.
Meli
 ya Titanic iliyozama mwaka 1914 karibu karne moja iliyopita na kuua 
watu karibu elfu moja, sasa kampuni kutoka uchina ya Star Investment 
Group katika mkoa wa Sichuan itatumia dola za kimarekani 165 milioni 
katika kujenga upya meli mfano wa Titanic.

Meli
 hiyo mpya ya wachina itafanana kabisa na meli ya Titanic iliyozama 
vibaya kwenye kina cha bahari karne moja iliyopita. Meli hiyo itajengwa 
kwa ushirikiano na kampuni ya serikali ya China Ship building 
Corporation ya Wuchang inatumika kama sehemu ya hifadhi ya makumbusho 
katika mkoa wa Sichuan.
Katika
 meli hii ya replica ni ishara ya uvumbuzi uliotukuka kutoka kwa wachina
 na watazamiwa kuingiza mamilioni ya fedha kama riba kutokana na alama 
ya Titanic duniani.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog