GODBLESS LEMA (MB)
Mahakama
 ya hakimu mkazi imefuta kesi iliyokuwa inamkabili mbunge wa jimbo la 
Arusha Godbless Lema na kudai kuwa upande wa mashitaka hakuwa na nia ya
 kuendeleza kesi hiyo.
Aidha kesi hiyo iliyokuwa inamkabili mbunge huyo ilikuwa ni ya uchochezi  katika chuo cha uhasibu Arusha ambapo vurugu hizo zilisababisha chuo hicho kufungwa.
Pia kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa leo mbele ya Hakimu Devotha Msofe wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ili kuweza kuitolea ufafanuzi zaidi.
Hataivyo
 mara baada ya hakimu huyo pamoja na Jopo la mawakili kuingia mahakamani
 hapo, Wakili wa Serikali Elianenyi Njiro, aliiomba mahakama kesi hiyo 
ifutwe chini ya kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya 
Jinai, kama ilivyorekebisha 2002.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa upande wa mashitaka uliona hauna haja wala tija ya kuendelea na kesi hiyo lakini pia ni vema kama kipengele
cha sheria kikaangaliwa zaidi.
Pia
 mara baada ya ombi hilo mahakama iliridhia na kudai kuwa kuanzia sasa 
Mbunge huyo yupo huru kwa mujibu wa kifungu cha sheria.
 “kwa
 mujibu wa kifungu cha sheria kuanzia sasa Lema upo huru”aliongeza 
hivyo. Awali Akisoma maelezo ya awali Julai 10 mwaka huu mahakamani 
hapo, Wakili wa Serikali Elianenyi alidai Aprili 24 mwaka huu, Lema 
akiwa eneo la Freedom Square la IAA alifanya kosa la uchochezi wa 
kutenda kosa kinyume na Sheria ya Kanuni ya Adhabu.
Akifafanua
 shtaka hilo, Elianenyi, alidai kuwa Lema aliwaeleza wanafunzi wa chuo 
hicho ambao walikuwa wamekusanyika kufuatia kuuawa kwa mwenzao na watu wasiojulikana kuwa; Upande
 wa mashtaka tayari ulikuwa umewaleta mashahidi watano ambao ni Kamanda 
wa Polisi wa Wilaya ya Arusha, Giles Mroto, Naibu Mkuu wa Chuo cha 
Uhasibu Arusha, Faraji Kasidi, Inspekta wa Polisi Bernard Nyambalya, 
Jane Chibuga na Mwadili wa Wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha, John 
Joseph Nanyaro.
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
.jpg)