![]()  | 
| Sheikh Suleiman Amran Kilemile | 
TAMKO LA UMOJA WA WANAZUONI WA KIISLAMU TANZANIA KUHUSU TUKIO LA SHEIKH PONDA
 
 Sisi, Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania (Hay – atul Ulamaa), 
tumepokea kwa masikitiko makubwa habari za kushambuliwa na kujeruhiwa 
kwa silaha za moto, Sheikh Ponda Isa Ponda, huko Morogoro, Jumamosi 
Agosti 10, 2013.
 
 Hay-atul Ulamaa, imesitushwa na tukio hili 
linalo uma na linaloumiza na kuleta mshtuko na fazaa katika jamii kama 
ilivyoshtushwa na matukio mengine kama hili hapa nchini. Hili ni tukio 
ambalo linaashiria kuwa walio litenda hawaitakii mema na amani nchi 
yetu.
 
 Tunalaani vikali kitendo 
hicho na tunaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchukua 
hatua kali na za haraka dhidi ya wale wote walio husika katika tukio 
hili lenye kuumiza nyoyo za wengi.
 
 Aidha tunawasihi Waislamu na
 jamii kwa ujumla kuwa watulivu, wenye subira na wenye kunyenyekea kwa 
Mola wao katika jambo hili zito, wakati tunasubiri vyombo vya dola 
vichukue hatua zinazo stahiki dhidi ya wahusika wa tukio hili.
 
 Tunamuombea Sheikh Ponda Isa Ponda Allah Amponye haraka na Am,pe baraka katika umri wake. Amin
 
 Sheikh Suleiman Amran Kilemile
 
 Mwenyekiti
 
 Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania.
 
 11/August/2013
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog
