Rais wa FIFA Sepp Blatter akiwa
 na Rais wa TFF Leodegar Chilla Tenga walipokutana hivi karibuni makao 
makuu ya FIFA jijini ZurichShirikisho
 la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limetuma mapendekezo 10 ya 
marekebisho ya Katiba yake kwa wanachama wake kwa njia ya waraka.Mapendekezo
 hayo yametumwa kwa kila nchi mwanachama kupitia waraka namba 1320, 
ambapo wanachama kwa kupitia kwa mashirikisho yao ya mabara watapiga 
kura ya ndiyo au hapa. 
Kwa upande wa Afrika, wanachama wa FIFA 
wanatakiwa kuwasilisha kura zao kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu 
Afrika (CAF).Baadhi ya mapendekezo 
hayo ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa 
FIFA (FIFA Congress). Makamu wa Rais wa FIFA na wajumbe wa Kamati ya 
Utendaji wanaochaguliwa katika mabara ambapo itabidi wathibitishwe na 
FIFA Congress.
Muundo wa Kamati ya 
Utendaji; nafasi moja ya vyama vya mpira wa miguu vya Uingereza (British
 FAs) sasa inahamishiwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA). Pia 
Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi ya FIFA anatakiwa kushiriki vikao vya 
Kamati ya Utendaji bila kuwa na haki ya kupiga kura.Uchaguzi
 wa Rais; mgombea anatakiwa kuungwa mkono na idadi ya kutosha ya vyama 
wanachama kutoka katika mabara mawili tofauti. Ukomo wa uongozi; 
kuanzisha vipindi vya uongozi. Ukomo wa umri; ukomo wa umri usiozidi 
miaka 72 wakati wa kugombea utekelezwe.Uwakilishi
 wa kutosha kwa makundi yenye maslahi katika FIFA; makundi yenye maslahi
 katika mpira wa miguu kama wachezaji wapate uwakilishi katika Kamati ya
 Mpira wa Miguu. Uteuzi wa mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia; uteuzi
 sasa ufanywe na Mkutano Mkuu wa TFF.
SOURECE: www.issamichuzi.blogspot.com 
Facebook Comments Plugin Enhanced by Kitongoni blog