Facebook Comments Box

Sunday, January 5, 2014

SOMA ZITTO ALIVYO WACHANA LISSU NA MBOWE LIVE.



MATOKEO YA FA CUP: MAN U WACHEZEA KICHAPO



SHOTI YA UMEME YATHIRI NYUMBA ZAIDI YA MIA: MOTO MPAKA SASA BADO HAUJAZIMWA

Taarifa ilotufikia muda mfupi kua shoti ya umeme imeathiri nyumba takribani 100 katika mji wa Pemba kijiji cha Shumba mjini na mpaka hivi sasa hakujawezekana kuzimwa kwa moto huo kwa kutopatikana gari la kuzimia moto huu ni msiba mkubwa kwa ndugu zetu naomba tuwatakieni dua ili Allah awahafifishie mtihani huo


YANGA YAWAHENYESHA WAZUNGU


Kocha Msaidizi wa timu ya Yanga Boniface Mkwasa akitoa maelekezo kwenye mazoezi ya timu ya Yanga hivi karibuni  

YANGA imeuanza mwaka 2014 kwa kasi ya aina yake ambapo makocha wazungu wenye hadhi zao wanahenya usiku na mchana wakisubiri simu za viongozi tayari kuitwa kazini kuanza kibarua kipya.
Lakini Abdallah Binkleb ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano na Usajili wa Wachezaji, ameithibitishia Mwanaspoti kwamba kabla ya Jumatano ijayo lazima watakuwa wamemchagua mzungu mmoja wa maana.
Binkleb alisema: “Wapo wengi sana kila siku wanatuma maombi lakini sisi tunataka kocha mmoja tu wa maana ambaye ni fundi na anayeweza kutufanyia kitu kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na analijua soka la Afrika.
“Tumemchukua Mkwasa (Boniface, anayekuwa Kocha Msaidizi) ni kocha wa maana pamoja na Juma Pondamali (Kocha wa Makipa) wanaijua Yanga vilivyo, tuna uhakika kwamba tukishakutana tukipitia orodha ya mwisho na kuchagua wa kutua nchini, tusifanye makosa.”
Hata hivyo kiongozi huyo mwenye ushawishi mkubwa ndani ya Yanga hakuwa na idadi kamili ya makocha walioomba kazi hiyo inayoachwa wazi na Ernest Brandts ambaye amepewa notisi.
Bin Kleb alisema hawezi kusema idadi kwa sasa kwa vile wamekuwa wakipokea barua pepe za maombi hayo kila baada ya muda mfupi.
MKWASA AANZA KWA MIKWARA
Boniface Mkwasa ameiangalia timu hiyo na kutamka kuwa wachezaji wake hawana uwezo wa kucheza dakika 90, hivyo ataanza mazoezi ya aina nne kuwandaa kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mkwasa ametoa kauli hiyo mara baada ya mazoezi ya siku ya kwanza kumalizika jana Ijumaa baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili kuifundisha timu hiyo akirithi mikoba ya Fred Minziro aliyekuwa msaidizi wa Brandts.
Akizungumza na Mwanaspoti, Mkwasa alisema kuwa timu hiyo inahitaji mabadiliko ya haraka katika kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kutokana upungufu aliouona ambao ni;
Moja; Pumzi. Hilo ndilo la kwanza linalohitajika ambalo ameliona kwa wachezaji kushindwa kumudu kucheza dakika 90 jambo ambalo ni baya kwa timu inayojiandaa na michuano ya kimataifa.
Katika kuhakikisha analifanyia kazi hilo, tayari ameuomba uongozi kutafuta uwanja mkubwa kushinda ule wanaoutumia hivi sasa wa Bora uliopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam. Wanahamishia mazoezi yao Uwanja wa Tanganyika Packers ambao una eneo kubwa kwa lengo la kuwaongezea pumzi wachezaji hao.

Pili; Kasi. Ameona timu hiyo inacheza soka la taratibu ambalo yeye halitaki, anataka kuona timu inacheza kwa kasi ili kuwachosha wapinzani wao ndani ya uwanja.
Tatu; Pasi. Nalo ni tatizo kwani anasema wachezaji wanapiga pasi hovyo. Anasema ili timu icheze soka safi, lazima wapige pasi zitakazowafikia wenzao ndani ya uwanja na siyo kuwapelekea adui na kuanza kupata tabu ya kukaba.
Nne; Kumiliki mipira. Hilo nalo ni tatizo ingawa amesema ni karibu kwa timu zote zinazoshiriki ligi, hivyo amepanga kulimaliza tatizo hilo kwa Yanga.
“Ninajua ni ngumu kumaliza matatizo hayo katika muda huu mfupi wakati timu inajiandaa na ligi, lakini ninaamini nitalipunguza, jambo kubwa nahitaji ushirikiano kutoka kwa wachezaji, ninaomba viongozi kuhakikisha wanasimamia nidhamu ya wachezaji, pale wanaomba ruhusa na kupewa basi warudi kwa wakati,” alisema.
MAZOEZI MARA MBILI
Mkwasa amebadilisha muda wa mazoezi ambapo kuanzia keshokutwa Jumatatu yatakuwa yakifanyika jioni tu na kadiri siku zinavyokwenda mazoezi ya timu hiyo yatakuwa yakifanyika mara mbili kwa siku yaani asubuhi na jioni.
Mkwasa alikaa kikao kirefu na wachezaji juzi Alhamisi jioni klabuni na aliiambia Mwanaspoti kuwa kikao hicho kilikuwa kwa ajili ya kuwafahamu wachezaji kabla ya kuanza kazi rasmi jana Ijumaa.
“Lengo langu lilikuwa kufahamiana na kupanga mikakati, mimi si mgeni Yanga, naamini ushirikiano kutoka kwa wachezaji na viongozi utasaidia timu kupata mafanikio kwenye Ligi Kuu na michuano ya kimataifa,” alisema Mkwasa.
Habari za ndani zinasema Yanga itasafiri kwenda nchi mojawapo kati Hispania, Uturuki au Ureno na inadaiwa timu inatakiwa kuondoka kati ya Januari 9 na 10.
Viongozi wanafuatilia maandalizi ya safari hiyo ili ifanyike katika muda huo.  

CHANZO: MWANASPOTI


MAPINDUZI CUP: SIMBA WAVUTWA SHATI NA KCC



Wekundu wa Msimbazi Simba wameshindwa kuwatambia KCC ya Uganda baada ya kutoshana nguvu kwa kutoka sare ya bila kufungana katika mchezo wa kundi B kuwania Kombe la Mapinduzi uliochezwa uwanja wa Amaan usiku huu.
Kwa ujumla timu zote ziulionekana kucheza kwa umakini mkubwa hasa katika safu za ulinzi ikiwa ni ishara ya kuepuka kupoteza mchezo na kubakiza matumaini ya kufuzu kwa robo fainali. ambapo hadi mapumziko timu zote zilikuwa zimepiga mikwaju miwili tu iliyolenga lango la mpinzani.

Kipindi cha pili Simba ilionekana kuimarika zaidi hasa baada ya kuingia kwa Said Ndemla kuchukua nafasi ya Amri Kiemba na pia Betram Mwombeki aliyechukua nafasi ya Amissi Tambwe, ambaye alionekana kukosa ujanja wa kuipenya ngome ya waganda kwa kudhibiwa vilivyo. Kwa ujumla Simba walipiga mikwaju mingi zaidi iliyolenga lango kwani walipata mikwaju 6 wakati KCC walipiga mitatu

Simba Nusura waandike bao katika mwa kipindi chapili pale Ndemla alipopiga mkwaju mkali ambao hata hivyo uliokolewa na mlinda lango na ukawa kona butu.

KCC wangeweza kuandika goli la kusawazisha katika dakika za mwisho kabisa za mchezo kamasi uhodari wa mlinda lango Ivo Mapunda kuuucheza mpira uliokuwa ukielekea langoni na kufanya timu zote mbili zifune alama moja na kufikisha alama nne.

KCC iko kilelelni mwa kundi B ikiipiku Simba kwa wingi wa magoli ya kufunga wakati AFC na KMKM zinashika nafasi ya tatau na ya nne kwani zote zina alama moja kila moja. Michezo ya mwisho keshokutwa ndiyo itaamua ni tiu ipi iende robo fainali wakati Simba itakapocheza na KMKM na na KCC wakiikabili AFC Leopards

Kesho Jumamosi kuna michezo mine. Kwenye uwanja wa Gombani Pemba watoza ushuru wa Uganda, URA watapepetana na timu mseto ya Pemba (Clove Stars) kuanzia saa 8 mchana na baadaye saa 10 Mbeya CITY watakipiga na timu ya Chuoni.

Wakati hayo yakiwa Pemba, Unguja kwenye uwanja wa Amaan saa 10 jioni Ashanti United wataonyeshana kazi na timu mseto ya unguja (Spice Stars) na sa 2 usiku mabingwa watetezi Azam watawakabili Tusker ya Kenya.


TETESI: MABERE MARANDO ARUDISHA KADI YA CHADEMA

Mwanasheria Mabere Marando
Habari zilizo tufikia ambazo bado hazijathibitishwa zinasema Mwansheria Mabere Marando amerudisha kadi ya CHADEMA kwa madai ya kuwa cham hicho kimekuwa hakitendi haki


Friday, January 3, 2014

BENKI KUU YA TANZANIA YATOA SARAFU YENYE THAMANI YA SHILINGI 50,000 YA PAMOJA

PROFESA BENNO NDULU - GAVANA WA BENKI KUU YA TANZANIA

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa sarafu maalumu ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye thamani ya sh 50,000.

Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, alisema kuwa sarafu hiyo iliyotengenezwa kwa madini ya fedha kwa asilimia 92.50, imetolewa kwa ajili ya kumbukumbu tu na haitaingizwa katika mzunguko wala kutumika kwa kulipia malipo ya aina yoyote.




Sarafu hii imetolewa maalumu kama maadhimisho ya miaka 50 ya mapinduzi ya Zanzibar, haitatumika kwa manunuzi.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki ya BoT ilimnukuu Profesa Ndulu akisema sarafu hiyo imetolewa kwa idadi ya vipande 3,000 kwa ajili ya tukio hilo na kuwahimiza wananchi kuinunua kwa ajili ya kumbukumbu hiyo.


Kwa mujibu wa Gavana, kutolewa kwa sarafu hiyo kunakwenda sambamba na utaratibu wa Benki Kuu kutoa sarafu maalumu za aina hiyo kama sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya matukio mbalimbali muhimu ya kitaifa na kimataifa.


Kwa kawaida, baada ya muda, thamani ya sarafu kama hizi huongezeka na kuwa na faida zaidi kwa wanaozimiliki,” alisema Profesa Ndulu.

Gavana Ndulu alieleza sarafu hizo zitapatikana Januari 5 kwa bei ya sh 50,000 katika matawi ya benki za biashara zitakazokuwa zimepata sarafu hizo kutoka Makao Makuu ya Benki Kuu, Dar es Salaam na matawi ya Benki Kuu yaliyoko Zanzibar, Arusha, Mbeya na Mwanza.

Benki za biashara zinaweza pia zikasambaza sarafu hizi kupitia matawi yake,” alisema gavana na kuongeza taarifa za usambazaji zitatolewa na benki hizo.

Katika sarafu hiyo, upande wa mbele unaonesha sura ya hayati Sheikh Abeid Aman Karume na maandishi yanayosomeka: ‘Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi’. 

Upande mwingine wa sarafu unaonesha nembo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, maandishi yanayosomeka: “Miaka Hamsini ya Mapinduzi”, thamani ya sarafu na miaka 1964-2014.


ANGALIA ALICHO POST BERBATOV KUHUSU ARSENAL

Maswali mengi yalitokea jana baada ya mwanasoka Dimitar berbatov kupost katika ukuta wake wa facebook kuhusu Arsenal alipost habari ambayo ilikuwa ikiuliza kuwa kama yeye anaweza kuisaidia timu hiyo ya Arsenal kuchukua ubingwa.

Hata hivyo post hiyo haikuweza kudumu kwa zaidi ya dakika 20 kwani aliifuta katika ukurasa wake huo.

Vyombo vingi vya habari vimekuwa vikitaja kuwa mshambuliaji huyo mkali ameshamalizana na Arsenal na sasa imebaki mkataba kusainiwa tu.

Kochawa Arsenal aliamua kutafuta mshambuliaji baada ya washambuliaji wake wawili kuumia Giroud na Bendtner. Baadhi ya washambuliaji anao wataka ni pamoja na Lewandowski na Benzema

Picha chini ni post ya Dimitar Berbatov katika ukurasa wake maalum wa facebook.



Thursday, January 2, 2014

PICHA: MESSI ALIPOPANDA MLIMA KILIMANJARO

Kama ulikuwa hauna habari basi habari ndio hii mshambiliaji wa barcelona alie majeruhi sasa Messi alipanda hadi kwenye kilele cha mlima kilimanjaro hivi karibuni.



MSIMAMO WA LIGI YA UINGEREZA BAADA YA MECHI ZA JANA



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU