Monday, January 6, 2014
Sunday, January 5, 2014
SHOTI YA UMEME YATHIRI NYUMBA ZAIDI YA MIA: MOTO MPAKA SASA BADO HAUJAZIMWA
YANGA YAWAHENYESHA WAZUNGU

MAPINDUZI CUP: SIMBA WAVUTWA SHATI NA KCC

Kwa ujumla timu zote ziulionekana kucheza kwa umakini mkubwa hasa katika safu za ulinzi ikiwa ni ishara ya kuepuka kupoteza mchezo na kubakiza matumaini ya kufuzu kwa robo fainali. ambapo hadi mapumziko timu zote zilikuwa zimepiga mikwaju miwili tu iliyolenga lango la mpinzani.
Kipindi cha pili Simba ilionekana kuimarika zaidi hasa baada ya kuingia kwa Said Ndemla kuchukua nafasi ya Amri Kiemba na pia Betram Mwombeki aliyechukua nafasi ya Amissi Tambwe, ambaye alionekana kukosa ujanja wa kuipenya ngome ya waganda kwa kudhibiwa vilivyo. Kwa ujumla Simba walipiga mikwaju mingi zaidi iliyolenga lango kwani walipata mikwaju 6 wakati KCC walipiga mitatu
Simba Nusura waandike bao katika mwa kipindi chapili pale Ndemla alipopiga mkwaju mkali ambao hata hivyo uliokolewa na mlinda lango na ukawa kona butu.
KCC wangeweza kuandika goli la kusawazisha katika dakika za mwisho kabisa za mchezo kamasi uhodari wa mlinda lango Ivo Mapunda kuuucheza mpira uliokuwa ukielekea langoni na kufanya timu zote mbili zifune alama moja na kufikisha alama nne.
KCC iko kilelelni mwa kundi B ikiipiku Simba kwa wingi wa magoli ya kufunga wakati AFC na KMKM zinashika nafasi ya tatau na ya nne kwani zote zina alama moja kila moja. Michezo ya mwisho keshokutwa ndiyo itaamua ni tiu ipi iende robo fainali wakati Simba itakapocheza na KMKM na na KCC wakiikabili AFC Leopards
Kesho Jumamosi kuna michezo mine. Kwenye uwanja wa Gombani Pemba watoza ushuru wa Uganda, URA watapepetana na timu mseto ya Pemba (Clove Stars) kuanzia saa 8 mchana na baadaye saa 10 Mbeya CITY watakipiga na timu ya Chuoni.
Wakati hayo yakiwa Pemba, Unguja kwenye uwanja wa Amaan saa 10 jioni Ashanti United wataonyeshana kazi na timu mseto ya unguja (Spice Stars) na sa 2 usiku mabingwa watetezi Azam watawakabili Tusker ya Kenya.
TETESI: MABERE MARANDO ARUDISHA KADI YA CHADEMA
Friday, January 3, 2014
BENKI KUU YA TANZANIA YATOA SARAFU YENYE THAMANI YA SHILINGI 50,000 YA PAMOJA
BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa sarafu maalumu ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye thamani ya sh 50,000.
Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, alisema kuwa sarafu hiyo iliyotengenezwa kwa madini ya fedha kwa asilimia 92.50, imetolewa kwa ajili ya kumbukumbu tu na haitaingizwa katika mzunguko wala kutumika kwa kulipia malipo ya aina yoyote.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki ya BoT ilimnukuu Profesa Ndulu akisema sarafu hiyo imetolewa kwa idadi ya vipande 3,000 kwa ajili ya tukio hilo na kuwahimiza wananchi kuinunua kwa ajili ya kumbukumbu hiyo.
Kwa mujibu wa Gavana, kutolewa kwa sarafu hiyo kunakwenda sambamba na utaratibu wa Benki Kuu kutoa sarafu maalumu za aina hiyo kama sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya matukio mbalimbali muhimu ya kitaifa na kimataifa.
“Kwa kawaida, baada ya muda, thamani ya sarafu kama hizi huongezeka na kuwa na faida zaidi kwa wanaozimiliki,” alisema Profesa Ndulu.
Gavana Ndulu alieleza sarafu hizo zitapatikana Januari 5 kwa bei ya sh 50,000 katika matawi ya benki za biashara zitakazokuwa zimepata sarafu hizo kutoka Makao Makuu ya Benki Kuu, Dar es Salaam na matawi ya Benki Kuu yaliyoko Zanzibar, Arusha, Mbeya na Mwanza.
“Benki za biashara zinaweza pia zikasambaza sarafu hizi kupitia matawi yake,” alisema gavana na kuongeza taarifa za usambazaji zitatolewa na benki hizo.
Katika sarafu hiyo, upande wa mbele unaonesha sura ya hayati Sheikh Abeid Aman Karume na maandishi yanayosomeka: ‘Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi’.
Upande mwingine wa sarafu unaonesha nembo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, maandishi yanayosomeka: “Miaka Hamsini ya Mapinduzi”, thamani ya sarafu na miaka 1964-2014.
ANGALIA ALICHO POST BERBATOV KUHUSU ARSENAL
Maswali mengi yalitokea jana baada ya mwanasoka Dimitar berbatov kupost katika ukuta wake wa facebook kuhusu Arsenal alipost habari ambayo ilikuwa ikiuliza kuwa kama yeye anaweza kuisaidia timu hiyo ya Arsenal kuchukua ubingwa.
Hata hivyo post hiyo haikuweza kudumu kwa zaidi ya dakika 20 kwani aliifuta katika ukurasa wake huo.
Vyombo vingi vya habari vimekuwa vikitaja kuwa mshambuliaji huyo mkali ameshamalizana na Arsenal na sasa imebaki mkataba kusainiwa tu.
Kochawa Arsenal aliamua kutafuta mshambuliaji baada ya washambuliaji wake wawili kuumia Giroud na Bendtner. Baadhi ya washambuliaji anao wataka ni pamoja na Lewandowski na Benzema
Picha chini ni post ya Dimitar Berbatov katika ukurasa wake maalum wa facebook.
Thursday, January 2, 2014
PICHA: MESSI ALIPOPANDA MLIMA KILIMANJARO
Kama ulikuwa hauna habari basi habari ndio hii mshambiliaji wa barcelona alie majeruhi sasa Messi alipanda hadi kwenye kilele cha mlima kilimanjaro hivi karibuni.