Facebook Comments Box

Wednesday, December 25, 2013

MKURUGENZI WA KCMC AACHIA NGAZI

Mkurugenzi wa Hospitali ya KCMC ameachia ngazi. Hii imefuatia uamuzi wake alio utoa kwenye kikao cha bodi ya wakurugenzi wa msamaria mwema.
Dk Ntabaye ameomba bodi ya wakurugenzi wa msamaria mwema wasimuongeze mkataba mwingine tena.
Inasemekana mkurugenzi huyo ameacha manung'uniko na malalamiko mengi hospitali hapo pamoja na kushusha ari ya kazi kwa wafanyakazi wa hospitali hiyo.
Nafasi ya ukurugenzi kwa sasa imekaimiwa na Pro ulomi.


KOCHA WA SIMBA AFARIKI DUNIA

James Kisaka enzi za uhai wake.
Aliyekuwa kocha wa makipa wa Klabu ya Simba, James Kisaka amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Burhan, Dar es Salaam. Kisaka aliyewahi kuwa kipa wa timu hiyo miaka ya nyuma, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kichwa, macho na miguu kwa muda mrefu.
MUNGU AIPUMZISHE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI. AMINA
CHANZO: GPL


Tuesday, December 24, 2013

PICHA: WAZIRI MWAKYEMBE AFANYA UKAGUZI WA NAULI ZA MABASI LEO




Waziri wa Uchukuzi,Dr Harisoni Mwakembe afanya ukakuguzi wa tiketi ilikubaini mabasi yaliyo toza gharama kubwa za nauli zakusafiria katika kipindi cha Xmass na mwaka mpya,badhi ya mabasi yalikamatwa nakuamuliwa kurudisha nauli zilizozidi abiria wao.zoezi hilo limefanyika majira ya alfajiri katika eneo la Visiga mkoani pwani na kila basi lilozidisha nauli lilitozwa faini ya shilingi laki mbili na nusu. 



WANNE WAKAMATWA NA HEROIN ARUSHA


GEDSC DIGITAL CAMERAKamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari bunduki aina ya SMG iliyokamatwa wilayani Ngorongoro hivi karibuni huku mkono wake wa kulia akiwa ameshika kifurushi chenye madawa ya kulevya aina ya Heroin yaliyokamatwa jana wilayani Arumeru. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
 
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
 
Kuelekea katika kusherehekea Sikukuu ya Krimas, Jeshi la Polisi Mkoani hapa limeendelea kupambana na wahalifu wa madawa ya kulevya ambapo safari hii limefanikiwa kuwakamata watu wanne wakiwa na madawa ya kulevya aina ya Heroin. Tukio hilo limetokea jana tarehe 23.12.2014 muda wa saa 12:30 jioni maeneo ya Elikyurei wilayani Arumeru.
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi wa Mkoani hapa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas amesema kwamba tukio hilo limefanikiwa baada ya kupata taarifa toka kwa raia wema ambapo askari wa Jeshi hilo walikwenda katika eneo husika na kuwakuta watuhumiwa hao wakiwa ndani ya chumba cha mtuhumiwa mmojawapo huku wakiwa wanaendelea kufunga kete za madawa hayo na tayari walikuwa wamefunga kete 25.
 
Kamanda Sabas aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Seifu Bakari (28) na Hamid Makame wote ni wakazi wa Elikyurei wilayani Arumeru pamoja na wenzao ambao ni Evance Gidion (29) Mkazi wa Ngarenaro na Abraham Hamis (23) Mkazi wa Kaloleni jijini hapa.
 
Kamanda Sabas alisema kwamba madawa hayo yenye uzito wa gramu 100 yanakadiriwa kuwa na thamani ya Tsh 10 Mil. Mpaka hivi Jeshi hilo linaendelea kuwahoji watuhumiwa hao ili kufahamu undani zaidi na watafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.
 
Kufuatia tukio hilo na mengine ya nyuma Kamanda Sabas alizidi kuwashukuru wananchi wa Mkoa huu kwa jinsi wanavyoonyesha ushirikiano kwa jeshi hilo juu ya kufichua vitendo vya uhalifu na wahalifu na kuahidi kuendeleza falsafa ya Polisi Jamii ambayo inaleta mafanikio makubwa katika suala zima la kuimarisha amani na utulivu Mkoani hapa.



SHILOLE NDANI YA UBALOZI WA TANZANIA UINGEREZA

Mheshimiwa Kallaghe akiongea na mwanamuiki wa kitanzania Shilole




TAARIFA KWA UMMA KUTOKA TFF

Rais wa TFF, Jamal Malinzi


Monday, December 23, 2013

BAADA YA KIPIGO: YANGA WAMTIMUA KOCHA WAO

KOCHA Ernie Brandts hana chake tena Yanga na ndani ya siku mbili, uongozi wa klabu hiyo utatangaza kumtimua.
Taarifa za uhakika ambazo blog hii imezipata kutoka ndani ya Yanga, zimeeleza Brandts ameshafukuzwa kazi.
“Kweli Brandts ameonekana hafai na wakubwa walikaa jana kikao mara tu baada ya mechi ya Simba na Yanga, wamefikia hatua ya kumuachisha kazi.
“Mimi ninavyojua tayari mawasiliano na makocha kadhaa yameanza na Brandts atapewa muda kidogo tu ili akusanye virago vyake na kurejea kwao Uholanzi,” kilieleza chanzo cha uhakika.
Lakini viongozi wa Yanga walikuwa wagumu kulizungumzia suala hilo, ingawa mtu mwingine wa karibu na uongozi wa Yanga, alisema huenda leo Yanga wakatangaza.
“Wanaweza kutangaza kesho (leo), nimeelezwa kuwa wamefikia uamuzi huo na kuna bosi mmoja atatangaza leo au kesho,” alisema na kuongeza: “Kama mtaandika wanaweza wasitangaze.”
Brandts amejikuta katika wakati mgumu baada ya kikosi chake kulambwa na Simba kwa mabao 3-1 katika mechi ya Nani Mtani Jembe iliyopigwa juzi jijini Dar.
Inaelezwa baada ya mechi hiyo, kocha huyo aliyeipa Yanga ubingwa msimu uliopita, alishindwa kuwaridhisha mabosi wake baada ya kuulizwa sababu za kufungwa.
Mbali na Brandts, inadaiwa kuwa uongozi wa timu hiyo una mpango wa kutimua benchi zima la timu hiyo, akiwemo Kocha Msaidizi, Fred Felix Minziro.
Kocha wa sasa wa Mbeya City, Juma Mwambusi, ndiye anapewa nafasi kubwa ya kuchukua nafasi ya Minziro kwenye kikosi hicho cha Jangwani.
Yanga inatarajia kwenda kuweka kambi na inaelezwa zitakuwa nchi kati ya Hispania, Uturuki au Ureno na taarifa zinasema kuwa inataka kwenda na benchi zima la ufundi.


Na katika tofuti ya Yanga wameeleza muda huu kuwa kocha huyo amepewa notisi ya siku thelathini ya kusitisha mkataba wake kuanzia tarehe 22 mwezi huu..


Saturday, December 21, 2013

WAKIWA NA ASILIMIA ZAIDI YA MIA ZA USHINDI YANGA YATANDIKWA 3 KWA 1 NA MAHASIMU WAO BILA YA HURUMA



Timu ya Simba ya Msimbazi Dar es Salaam leo wameonesha kwamba wao sio wa kuchezea japo hawakupewa kabisa nafasi ya ushindi na mashabiki walio wengi. 

Simba ailionesha kuwa leo watapoteza mawazo ya mashabiki walio wengi wa Yanga pale ilipojipatia bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao kutoka Burundi ambae anaongoza kwa ufungaji wa mabao katika ligi kuu ya Vodacom Amis Tambwe.

 Tambwe baadae akaipatia timu yake bao la pili kwa mkwaju wa Penati baada ya Mshambuliaji wao mwenye chenga za maudhi Ramadhan Abdallah Singano 'MESI' kuangushwa ndani ya eneo la hatari na beki wa Yanga David Charles Luhende na mwamuzi kuamuru ipigwe penati.

Simba walipata bao la tatu kutoka kwa mchezaji wao mpya Awadh Juma baada ya kufanikiwa kumpokonya mpira kipa wa Yanga Juma Kaseja Juma aliyetaka kuurudisha mpira ndani ya box ili audake ndipo ukamgonga na mfungaji kuuwahi na kuuweka nyavuni.

Yanga walijipatia bao la kufutia machozi kupitia kwa Emanuel Okwi kwa kichwa baada ya kuwazidi ujajnja mabeki wa timu ya simba ambao leo wamestahili pongezi kubwa kwa kuwa imara tangu mwanzo.


ZITTO KABWE APOKELEWA KAMA RAISI MKOANI KIGOMA ALIPO WASILI LEO ASUBUHI TAZAMA PICHA






Zitto Kabwe akiwa katika gari la wazi mara baada ya kutua kigoma asubui ya leo ambapo amepata mapokezi ya kishindo.
 



KIBONZO: KIPANYA NA WATAFUNA NCHI



HEBU JIONEE JINSI WANAOBEBA MADAWA YA KULEVYA WANAVYO PASULIWA ILI KUYATOA

Dawa za Kulevya hazifai hakuna asiyefahamu jambo hili lakini unakuta baadhi ya watu wanayaweka maisha yao rehani na kukubali kuwa 'Punda' na kubeba mizigo hii haifai waache mara moja wote wenye tabia hii ni hatari kwa maisha yao.



Picha ya X-ray inavyoonesha tumboni madawa yaliovyo kwa mtu aliyebeba.

Athari inayoweza kupatikana yakiwa mwilini kama unavyoweza kujionea hapo juu.


Operesheni ikifanyika tayari kuyaondoa madawa hayo yaliyo sababisha kijana huyu kufariki.


Utumbo umetolewa tayari ili kuanza kuyatoa madawa hayo.


Kama uonavyo weza kujionea dawa hizo zikiwa ndani ya utumbo mpana.
Dawa zikianza kutolewa pamoja na kushafishwa kama unavyoona katika picha.




Kabla mtu hajazimeza zinakuwa hivi, sasa hebu fikiria mtu anameza kete hadi 5000 hii ni balaa kubwa sana.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU