Facebook Comments Box

Friday, October 11, 2013

PICHA: AJALI MBAYA KABUKU TANGA

Lori la Mizigo likiwa limeacha njia jana, baada ya kugongana na basi katika eneo la Kabuku mkoani Tanga na kuyahusisha magari matatu katika ajali hiyo. (Picha na Francis Dande) 

Askari wa usalama barabarani wakiwa katika eneo la tukio.
 

Baadhi ya watu wakishuhudia ajali iliyoya kutanisha malori mawili pamoja na basi la abiria lenye namba za usajili T 158 BXG, iliyotokea jana katika eneo la Kabuku, mkoani Tanga




MISHAHARA YA WANASOKA WA TANZANIA

Utafiti wa Mwanaspoti katika klabu zote 14 zinazoshiriki Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara umeonyesha kuwa klabu tatu; Azam, Yanga na Simba ndizo zinazolipa wachezaji wake mishahara mikubwa zaidi nchini.

Katika wachezaji 13 wanaolipwa zaidi ya shilingi milioni mbili kwa mwezi, Azam imetoa wachezaji watano sawa na Yanga huku Simba ikitamba na wachezaji watatu.

Kundi la kwanza, wanaolipwa mshahara wa milioni 4/= kwa mwezi ni:
Kipre Tchetche (Azam), Kipre Balou (Azam), Aggrey Morris (Azam), John Bocco (Azam) Brian Umony (Azam) na Haruna Niyonzima (Yanga).

Kundi la pili, wanaolipwa mshahara wa shilingi milioni 3.6/= kwa mwezi yupo Mbuyu Twite wa (Yanga).

Kundi la tatu la wanaolipwa mshahara wa milioni 3.3/= kwa mwezi wapo Abeil Dhaira na Joseph Owino  (wote wa Simba)

Kundi la nne linalipwa 2.5/= kwa mwezi lina Mrisho Ngassa wa Yanga.

Kundi la tano la wachezaji ambao wanalipwa milioni mbili kwa mwezi ni:
Didier Kavumbagu (Yanga)
Hamisi Kiiza (Yanga)
Amri Kiemba (Simba)

Uchunguzi wa Mwanaspoti, umethibitisha kuwa mshahara wa chini kwa wachezaji wa Azam ni shilingi milioni moja wakati Simba na Yanga ina kundi la wachezaji wanaolipwa kima cha chini cha shilingi laki tatu kwa mwezi.

Mishahara ya wachezaji haikatwi kodi yoyote.



Thursday, October 10, 2013

HII NI MOJA YA MOVIE KALI KUTOKEA HAPA BONGO





PICHA ZA MOVIE YA WEMA NA DIAMOND

Mi busu nayo imo si movie


mahaba teletele ili movie ilete uhalisia
Movie inaitwa Temptation ikiwa imemshirikisha Wema na mpenzi wake wa zamni Naseeb maarufu kama Diamond. Kwenye picha wawili hao wakiwa katika sehemu yabuchukuaji wa vipande vya sinema hiyo.



Wednesday, October 9, 2013

HILI NDIO GARI LA MTOTO WA BAKHRESA LENYE THAMANI YA MILIONI 805

                             Gari aina ya Brabus ambayo inayomilikiwa na mmiliki wa klabu ya Manchester City ya England, imeonekana leo Dar es Salaam, lakini ni mali ya Yussuf Bakhresa, mtoto wa bilionea Mtanzania, Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa. Vyanzo vimesema Yussuf alitoa oda maalum kutengenezewa gari hili na thamani yake jumla si chini ya dola za Kimarekani 500,000 sawa na shiingi milioni 805 za kibongo.

Hii hapa mali ya Yussuf Bakhresa

Huyu jamaa ndiye anayeendesha gari la hili la mtoto wa Bakhresa

Angalia alivyotulia ndani ya mzigo wa dola 500,000

Ni oda maalum kwa ajili ya Yussuf Bakhresa 



Mwingine mwenye gari kama hii Dar es Salaam nani? 

Kutoka Manchester hadi Dar es Salaam


SOURCE: BIN ZUBEIRY

HIZI NDIO KAULI ZA WANASHERIA WANAO MPINGA TUNDU LISSU KUHUSU KATIBA MPYA

Baadhi ya wanasheria wameunga mkono utaratibu wa  Rais kutia saini Muswada wa  Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2013, uliopitishwa hivi karibuni na Bunge kwa hoja kwamba umepitia   mchakato sahihi na halali wa Kikatiba.

Wanasheria hao wakaeleza kumshangaa mwanasheria mwenzao na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), kwa ushauri wake alioutangaza kwa umma, kumtaka Rais asisaini muswada huo, kwamba ushauri huo ni wa 
kisiasa zaidi, usio na tija kwa uongozi wala unaofuata utaratibu na sheria.

Wamenukuliwa wakizungumza na mwandishi kwa nyakati tofauti jana, wakisema kuwa muswada huo kama ilivyo miswada mingine ya sheria, una nafasi ya kusainiwa na yakiwepo marekebisho, unarudishwa bungeni kujadiliwa na kurekebishwa.

Wakili wa kujitegemea, John Mapinduzi alisema: "Lazima muswada huo usainiwe ndipo urudishwe bungeni kwa marekebisho, Lissu ni mwanasiasa tu anapotosha umma… sasa utarudishwaje bungeni wakati ulishapita?" Alihoji Mapinduzi.

Mwanasheria mwingine wa kujitegemea, Jerome Msemwa alisema kusainiwa muswada huo ni njia sahihi na inafanyika mara nyingi (??) na kama kuna marekebisho, yanafanyika baadaye: "Wabunge kama Lissu waliamua kutoka wenyewe bungeni wakati muswada unajadiliwa… hakuna aliyewafukuza, sasa iweje leo watake usisainiwe? Haina maana leo hii kumshauri Rais kutosaini. Ushauri wa Lissu, kisheria hauna maana yoyote, hawezi kumshauri Rais leo asisaini wakati anafahamu kuwa hata baada ya kusainiwa, kuna nafasi ya kurudishwa bungeni na kujadiliwa kwa marekebisho yoyote," alisema Msemwa.

Msemwa alisema Rais asiposaini muswada huo na kuurudisha bungeni, maana yake vikao vya wabunge vilivyokaa Dodoma  kujadili muswada huo, vilipoteza muda na fedha za wananchi bure.  --- via HabariLeo


MISHAHARA YA WAZIRI MKUU, MAWAZIRI NA RAIS WATAJWA

Picture
Zitto Kabwe: "Siku ya Nne ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi imetupeleka Wilaya ya Sikonge Mkoa wa Tabora. Nikiwa na Wenyeviti wa chama wa mikoa ya Kigoma, Katavi na Tabora pia Mwenyekiti wa Kanda ya Magharibi Ndg. Mambo tumefanya mikutano 4."
Mishahara ya Viongozi wa Umma lazima iwe wazi kwa umma. Sheria za Mishahara ziweke wazi kabisa kuwa mishahara hii itakuwa wazi na itakatwa kodi. Juzi Mpanda nimewaambia wananchi Mshahara wa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa mwezi. Nikiwa Igunga mnamo tarehe 13 Oktoba tutawaambia wananchi mshahara wa Rais na Makamu wa Rais. Iwapo Rais wa marekani mshahara wake na mapato yake ni wazi na unakatwa kodi, iweje Rais wa nchi ndogo kama Tanzania. Wameifungia Mwananchi kwa kutaja viwango vya mishahara ya watumishi wa Umma. Wamfungie Mbunge kama wanaweza. --- Zitto Kabwe.
Akizungumza katika mkutano wake mjini Mpanda jana wilayani Sikonge wakati akihutubia mikutano ya hadhara katika ziara ya Kanda ya Magharibi kwa ajili ya ujenzi wa chama, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe  ameutaja mshahara wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  kuwa ni jumla ya shilingi milioni 26 pasipo
kukatwa kodi. Akichanganua alisema Pinda anapokea sh. mil. 11.2 kama mbunge, sh mil. 8 kwa nafasi ya Waziri na kiasi kinachosalia  kufikia sh mil. 26 kwa nafasi ya Waziri Mkuu.

Alisema sababu hiyo ya mishahara mikubwa isiyokatwa kodi ndiyo huwafanya viongozi wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa wakali pale vyombo vya habari vinapotaka kuwafahamisha wananchi namna watumishi wao wanavyojilipa.

“Nimeanza na mshahara wa Waziri Mkuu pia siku zijazo nitataja na wa Rais, kwa kuwa amesaini makubaliano na Serikali ya Marekani kuendesha nchi kwa uwazi, na moja ya uwazi ni kwa muajiri kujua kiasi anachomlipa mwajiriwa wake,” alisema Zitto.

Hatua ya Zitto imekuja baada ya kuwapo mvutano mkubwa kuhusiana na kile kinachodaiwa ‘usiri’ wa mishahara ya watumishi wa umma, wakati ni haki ya walipa kodi kujua kile wanachowalipa walioomba kuwaongoza. (nukuu kutoka TanzaniaDaima)


ANGALIA DIAMOND ALICHOSEMA KUHUSU KURUDIANA KWAKE NA WEMA


Diamond akimkiss Penny kuonesha mapenzi yao
Katika siku za hivi karibuni katika magazeti mbali mbali ya hapa Bongo pamoja na mitandaoni kumekuwa na habari inayosema kuwa Naseeb Abdulmalik "Diamond" amerudiana na aliyekuwa mpenzi wake ambaye aliachana nae kutokana na mwana dada huyo Wema  Sepetu kukosa uaminifu katika mapenzi yao.
 
Taarifa zaidi zilisema kuwa Wema na Diamond walikutana Dubai wakati Diamond akienda Indonessia na Wema akielekea Hong kong na kula bata sana tu na kuashiria kuwa wamerudiana.
 
Lakini Diamond ameeleza kwenye Blog yake This is Diamond habari yote kama ifuatavyo:-
 
"Kumekuwa na Uvumi na Habari nyingi sana 
Mitandaoni na Kwenye Media tofauti... kwamba mimi na Mwanadada Wema Sepetu tuna mahusiano ya Kimapenzi, kitu
 ambacho Sikweli na taarifa hizo ni za uongo.. uvumi huu ulianza kisa tu yeye kucomment kwenye Account yangu ya Instagram?..
 
Hebu tujifunze kubadilika, inamaana watu mkiwa hamko kimahusiano ya Mapenzi basi msizungumze ama Kushiriki kwa chochote? Futeni huo uzamani na Mbadilike, inamaana
 
Mnapenda kuona watu wanauadui... nimuda wa kufanya kazi ili Kulipa sifa na heshima Taifa la Tanzania na si kuwekeana chuki zisizo na faida.." alisema Diamond.
Diamond akiwa na Penny



Tuesday, October 8, 2013

HII NDIO TATHMINI YA MAPATO UWANJA WA TAIFA YANGA WANAONGOZA

uwanja wa taifa
Ripoti Watazamaji na Mapato katika uwanja wa Taifa kwa mechi zinazozihusu timu mbili za Yanga na Simba inaonekana kuwa si nzuri tangu mzunguko wa kwanza wa Ligi kuu Tanzania bara kuanza, tovuti ya kandanda imebaini.

Kutokana na ripoti ambayo hutumwa kila baada ya mechi kutoka TFF, tovuti ya kandanda imetengeneza ripoti kuangalia mechi zinazohusu timu ya Yanga na Simba sc zote za Dar es salaam wakati wakitumia uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Mashabiki wa Yanga.

Mechi ambayo ilivutia watazamaji wengi ilikuwa ni ile ya Yanga dhidi ya Coastal Union ambayo ilichezwa tarehe28, Agosti. Jumla ya Mashabiki 26,137 waliingia na kutengeneza Milioni152, katika uwanja ambao unachukua watazamaji elfu 60, ikiwa ni mechi ambayo inashika nafasi ya pili mpaka muda huu kwa mapato, ya kwanza ikiwa ya ngao ya jamii kati ya Yanga na Azam FC, Agosti 18, ambayo iliingiza milioni 208 kutoka kwa mashabiki 26,084.

Simba vs Mgambo FC

Mechi kati ya Simba vs Mgambo ndio inayoshika mkia kwa sasa kwa idadi ya watazamaji ambao walikuwa ni 10,241 na kuuingiza milioni 54 tu.
Jumla ya Bilioni 1.2 zimetengenezwa mpaka sasa kwa mechi hizi, Yanga ikiwa imetengeneza zaidi, kiasi cha milioni 791 na watazamaji wengi zaidi. Hivyo haina Ubishi Yanga ni bidhaa bora zaidi sokoni mpaka sasa.
 

Swali la kujiuliza, Kwanini mapato na watu wanapungua? Je ni sababu baadhi ya mechi kuanza kuonyeshwa katika Luninga? au muingiliano wa Ratiba ya EPL na ligi Maarufu Duniani?

Tunavyoona:

Ni muda muafaka wa kufanya mechi zote kuwa na mvuto wa kuwapeleka watazamaji uwanjani, miundombinu bora, na Matangazo..ambayo tunaamini ni jukumu la Idara ya masoko na biashara ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mechi za Simba na Yanga ni muhimu kwao kuwaingizia mapato na timu zinazocheza nazo, kwakuwa huwa nusu kwa nusu. Ni vema kuwekeza katika kuhamasisha mashabiki kwenda uwanjani na kuangalia mpira na kuongeza mapato zaidi ya haki za televisheni.

*Maelezo yametengenezwa kwa msaada wa ripoti kutoka TFF.

CHANZO: KANDANDA


Monday, October 7, 2013

VIJANA WAKUTWA MSITUNI WAKIFANYA MAZOEZI MAKALI

Kamanda Zellothe Stephen akionesha CD za mafunzo ya kijeshi zilizokuwa zinatumiwa na kundi hilo.

Na Abdallah Bakari, Mtwara — POLISI mkoani Mtwara inawashikilia watu 11 kwa tuhuma za kupata mafunzo ya kijeshi msituni kwa kutumia CDs za al-Shabaab.
Tukio hilo la aina yake limetokea katika mlima Makolionga wilaya ya Nanyumbu mkoani hapa ambapo pia CDs zenye mafunzo mbalimbali ya kijeshi 25 zimekamatwa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Zelothe Stephen ameuambia “mtandao wa Kusini Leo” kuwa watuhumiwa hao
walikamatwa wiki moja iliyopita baada ya jeshi lake kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema: “CD hizo zilikuwa zinatoa mafunzo ya Al-Shabaab ya kuchinja watu, Mauaji wa Osama Bin Laden, Zindukeni Zanzibar, Kuandaa Majeshi, Mauaji wa Idd Amin na Mogadishu Sniper,” alisema Stephen.
Alisema watuhumiwa wote ni wakazi wa wilaya ya Nanyumbu mkoani hapa na kwamba walikuwa wakiongoza na Mohamed Makande 39, mkazi wa kijiji cha Sengenya ambaye pia anashikiliwa na jeshi hilo.
Aliwataja wengine waliokamatwa kuwani Hassan Omary (39) mkazi wa kijiji cha Nanyulu, Rashid Ismail (27). Abdallah Y. Hamisi (32), Salum Wadi (38), Fadhili Rajabu (20), Abbas Muhidini (32), Ismail Chande (18), Said Mawazo, Issa Abeid (21), na Ramadhani Issa (26) wote wakazi wa kijiji cha Likokona.
Kuhusu vitu watuhumiwa walivyokamatwa navyo, Kamanda Zelothe alisema, “Tumekamata mapanga mawili, Deki ya DVD, Solar, Visu, Tochi, Betri, Simu za kiganjani 5, Vyombo mbalimbali vya kulia chakula, Baiskeli tatu, Vitabu mbalimbali wa dini ya Kiislam, Unga wa mahindi kilo 50, Mahidi kilo 150 na virago vya kulalia. Vingine ni mfuko wa kijani unaosadikiwa ni wa kijeshi wenye nembo ya nanga ya meli yenye mistari kulia na kushoto na nyoka katikati.”
Alisema jeshi lake licha ya kuwafikisha watuhumiwa mahakamani, linaendelea na uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na Polisi Makao Makuu kwa lengo la kufanikisha kuunasa mtandao mzima.


IRINGA FOOTBALL FOR HOPE CENTRE WATENGENEZA KITUO NA UWANJA WA KISASA

Mkurugenzi wa Shirika la Vijana, Walemavu na Watoto (IDYDC) mkoani Iringa, Jonnie Nkoma akimweleza Katibu Mkuiu wa TFF, Angetile Osia juu ya kituo kipya cha Iringa Football for Hope Centre kitakachozinduliwa wiki hii ili kukuza vipaji vya watoto na Vijana mkoani humo. Kushoto ni Mwanachama wa Tabata Veteran, Ipyana Mwakasege. (picha: Mpoki Bukuku)

Kituo cha kisasa cha vijana cha Iringa Football for Hope Centre kinatarajiwa kufunguliwa mwishoni mwa wiki hii mjini Iringa ikiwa ni sehemu shamrashamra za uzimwaji wa Mwenge wa Uhuru.
Akizungumza mjini Iringa juzi Katibu Mkuiu wa TFF, Angetile Osiah alisema kituo hicho kilichojengwa na Shirika la Vijana, Walemavu na Watoto (IDYDC) la mkoani Iringa kimefadhiriwa na shirikisho la soka la Kimataifa (FIFA) ili ukuza vipaji vya mpira na kutoa elimu na ushauri nasaha: "Mradi huu haupitii moja kwa moja katika vyama vyetu vya michezo bali katika
taasisi zinazotoa eklimu za kijamii na kufundisha soka," alisema Angetile.
Alipongeza shirika la IDYDC kwa kukamilisha mradi huo na kusema kitendo hicho kitafanya FIFA kutoa fedha zaidi kwa ajili ya miradi kama hiyo nchini: "FIFA watafurahi kuiona fedha walizotoa zinatumika ipasavyo kitu ambacho kitawafanya wawe radhi kutoa misaada zaidi na hii itasaidia kukuza soka letu."
Mkurugenzi wa IDYDC, Jonnie Nkoma alimweleza Katibu Mkuu wa TFF kwamba kwa sasa ujenzi wa kitu hicho uko katika hatua za mwishoni kukamilika na kwamaba kitaanza kuhudumia timu za watoto na vijana zaidi ya 120 kitakapofunguliwa.
Nkoma alisema kituo hicho kitakuwa kinatumika usiku na mchana kwani wanafunzi na watoto watakuwa wakipata mafunzo nyakati za jioni wakati vina na watoto wa mitaani watatumia usiku kwa ajili ya mazoezi ya kukuza vipaji vyao: "Mbali na michezo vijana watakuwa wanapata mafunzo ya afya ya uzazi na ugonjwa waUkimwi na pia watapata nafasi ya kujua afya zao kwa kupima UKIMWI bure papa hapa kituoni.
Mbali na uwanja, kituo hicho pia kina ofisi, vyumba vya kutoa elimu na ushauri nasaha, upimaji wa VVU, chumba cha kompyuta na darasa.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU