KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Benedict XVI ametangaza kuachia madaraka ya kuongoza kanisa ifikapo mwishoni mwa mwezi huu, uamuzi ambao ni wa kwanza tangu karne ya 15 kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Habari la AFP.
Katika taarifa yake, Papa amesema amefikia uamuzi huo ambapo sasa ana umri wa miaka 85.
Msemaji wa Papa, Federico Lombardi amesema kiongozi huyo wa juu kabisa wa Kanisa Katoliki duniani, ataachia ofisi rasmi tarehe 28 Februari, mwaka huu saa mbili kamili asubuhi.
Wachambuzi mbalimbali wa masuala ya Vatican wanasema safari hii, kuna uwezekano mikoba ya Baba Mtakatifu Benedict XVI ikarithiwa na Kardinali kutoka Afrika.
Kardinali Peter Turkson wa Ghana ametajwa kama mrithi-mtarajiwa wa nafasi hii nyeti ndani ya Kanisa Katoliki, linalokadiriwa kuwa na waumini zaidi ya bilioni moja dunia nzima.
Mwingine ni Kardinali Francis Arinze; mzaliwa wa Nigeria ambaye alichukua nafasi ya Benedict XVIkama Kardinali-Askofu wa Velletri-Segni alipoteuliwa kuwa Papa miaka nane iliyopita.
Monday, February 11, 2013
MAPIGANO MAKUBWA GEITA KATI YA WAISLAM NA WAKRISTO
Chanzo chetu kinaarifu mpaka sasa msikiti umesha chomwa moto na polisi bado hawajafika kwa kuhofia uchache wao kwa hiyo wameagiza polisi kutoka Mkoa wa Mwanza waje kuwasaidia kutuliza ghasia hizo.
Silaha zinazotumika ni silaha za jadi watu wanazunguka mtaani wanakukamata wanakuuliza jina ukitaja jina tofauti na imani yao unapigwa kiasi cha kutosha tu
Kwa mujibu wa Taarifa hizo tayari idadi ya watu 10 wamejeruhiwa kwa kukatwa mapanga ambapo mmoja hali yake inaelezwa kuwa mbaya na amekimbizwa ktika hospitali ya wilaya ya geita,tayari polisi wa kikosi maalum cha kutuliza ghasia FFU kikiongozwa na Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai mkoani Geita wamewasili eneo la tukio.
Wakristo hao walifanya mkutano wa hadhara jana na kusema kuanzia leo hawatakubali kula nyama iliyochinjwa na waislam. Na kutenga eneo lao maalumu la kuchinji nyama zao
CHAMA CHA KUTETEA HAKI ZA WANAUME
KATIBU WA UHAMASISHAJI WA TAMRA TAIFA BWANA HATIBU MGEJA AKIWA NA MWEKA HAZINA WA TAMRA TAIFA BWANA JUMA KOMBO
TANZANIA MEN’S RIGHTS ASSOCIATION
Equal treatments for all
UTANGULIZI
TAMRA ni Asasi ya kiraia iliyoanzishwa na wanaume wa Tanzania kwa lengo
la kutoa msaada wa Kisheria pamoja na Elimu ya Haki na Wajibu katika
mahusiano ya kindoa kati ya mwanamke na mwanaume.
Kuanzishwa kwa asasi hii
kumekuja katika kipindi hiki baada ya tafiti mbalimbali kuonyesha kuwa
wapo wanaume wengi wanaofanyiwa vitendo vya ukatili katika masuala ya
ndoa kwa kunyimwa haki zao za kindoa kutupiwa virago pindi mwanamke
anapoamua kumchoka mwanamme kufuatana na kukosa kipato, kupungukiwa
nguvu za kiume na mambo kama hayo , jambo ambalo limeonekana kuwa ni
chanzo cha migogoro katika ndoa inayosababisha ongezeko la watoto
wanaoishi bila wazazi wa pande zote mbili yaani [ Baba na Mama] huku
hali hii ikiigharimu jamii na wanandoa kupigana na kusababisha majeraha
na mauaji katika jamii.
Si hivyo tu Mwanamme wa
Tanzania amekuwa ni mvumilivu kwa vile amekuwa akitendewa mambo yote
haya bila kuwa na chombo cha kukemea vitendo hivi jambo lililotoa
ushawishi kwa waanzilishi wa chama hiki kupata uchungu na hatimaye
kuamua kuanzisha Asasi hii.
Muda mrefu mwanaume wa
Tanzania hakupata wapi pa kwenda kupata msaada wa kisheria, imefika
wakati wanaume kuwa na chama cha kuwatetea dhidi ya unyanyasaji kutoka
kwa wake zao katika nyanja mbali mbali ikiwemo mambo ya ndoa,urithi wa
mali kwa wagane, pamoja na ulezi wa watoto.
TAMRA kinaenda mbali katika kuelimisha wanaume juu ya haki zao za msingi
pamoja na kuwaelimisha juu ya wajibu wao kama baba katika kuitunza
familia yake,kuondoa mfumo dume na mfumo jike, kupiga vita unyanyasaji
kwa mke na watoto,urithi wa mali kwa wajane na wagane pamoja na kulea
watoto kabla na baada ya kufariki kwa wanandoa.
Jina la asasi: Asasi hii itajulikana kuwa ni Chama cha kutetea haki za
wanaume Tanzania/Tanzania Men’s Rights Association kwa kifupi TAMRA
(1) Kuanzishwa kwa TAMRA:
Asasi ya TAMRA ilianzishwa 01/05/2012
(2) Makao Makuu.
Makao makuu ya TAMRA
yatakuwa katika Mtaa wa Mpakani ‘A”Kijito Nyama Jijini Dar Es Salaam
kituo cha Afrika sana Nyumba Block namba 45.
vile vile kutakuwa na ofisi ndogo ya Makao Makuu Jijini MWANZA
(3) Anuani ya Chama ni. Chama Cha Kutetea Haki za Wanaume Tanzania.
S.L.P 60065
Dar Es Salaam - Tanzania
Simu: Mwenyekiti TAMRA TAIFA +255 784 203 556
Katibu Mkuu TAMRA TAIFA +255 787 565 533
Blog: yetu ni www.tamratanzania.blogspot. com
TAFSIRI
“TAMRA” itamaanisha ni TANZANIA MEN’S RIGHTS ASSOCIATION.
KUTAKUWA NA VIONGOZI WAFUATAO WA TAMRA
· Kutakuwa na Mwenyekiti wa TAMRA Taifa.
· Katibu mkuu wa TAMRA Taifa.
· Mweka Hazina wa TAMRA Taifa.
· Katibu wa Uhamasishaji wa TAMRA Taifa.
· Wajumbe wa Bodi ya TAMRA
KAZI ZA TAMRA.
TAMRA itakuwa na kazi zifuafuatazo:
(1) Kutetea wanaume dhidi ya unyanyaswaji katika ndoa.
(2) Kutoa elimu juu haki za Wanamme
(3) Kuwaelimisha wanamme kuondokana na mfumo dume/jike.
(4) Kuelimisha
wanaume kuhusu haki na usawa kati ya mwanamme na mwanamke katika kutoa
maamuzi kwa mambo mbalimbali ya kifamilia, kisiasa na kiuchumi.
(5) Umiliki wa mali katika familia.
(6) Haki ya kushiriki na kufurahia ndoa.
(7) Kuelimisha jamii juu ya Haki ya kumiliki mali kwa pamoja kabla na baada ya kifo cha mmoja wa wanandoa.
(8) Kuelimisha
wanandoa kuhusu Haki na wajibu wa kuheshimiwa na kupendwa kwa
kila mwanandoa kama ilivyo katika maandiko matakatifu bila kuathiri
itikadi za dini.
(9) Kuhakikisha
kwamba TAMRA inashirikiana na taasisi za kutetea haki za wanawake ili
kuondoa imani potofu dhidi ya mwanamme ili kujenga mahusiano mazuri
katika familia badala ya kuchochea uhasama kwa kumkandamiza mwanamme
kuwa ndiyo chanzo cha migogoro ndani ya familia.
10.kuhakikisha kuwa kuna
usawa na uhuru wa kujieleza pindi mashauri ya ndoa yanapopelekwa katika
vituo vya Polisi kwa uchunguzi na hatimaye hatua ya kupelekwa katika
vyombo vya maamuzi.
11.Kuhakikisha kuwa wapo
Mawakili wa kutosha panapotokea mashauri katika Mahakama watakaotetea
Haki za Wanaume ili kuhakikisha Haki inatendeka
MALENGO YA TAMRA.
TAMRA itakuwa na malengo kama ifuatavyo:-
(1) Kupigania Haki za mwanaume katika masuala mbalimbali ikiwamemo kulinda na kudumisha ndoa.
(2) Kulinda Haki ya mwanaume ngazi ya familia ,kitaifa na kimataifa.
(3) Kuelimisha waathirika wa unyanyasaji
(4) Kutoa msaada wa kisheria Bure kwa kutumia mawakili wa TAMRA.
(5) Kutoa
elimu ya Afya na malezi ya mtoto wa kiume ili akue katika maadili
yanayozingatia haki sawa kwa wote kuondoa dhana ya mfumo dume.
(6) Kutoa elimu juu ya magonjwa mbalimbali yakiwemo magonjwa yasiyokuwa na tiba ikiwamo Ukimwi (HIV/AIDS).
(7) Kutoa elimu na mafunzo kwa wanamme ili kuwafundisha ujasiria mali kuondoa utegemezi .
(8) Kufanya upatanishi na usuluhishi kwa wanandoa kwa kuzingatia mila,Desturi,Dini pamoja na sheria za Nchi.
(9) Kutoa elimu kwa wanaume kukubali mabadiliko ya mwili kufuatana na umri kuwa mkubwa kati ya mwanamme na mwanamke.
10 Kulinda Haki za kila raia bila kujali itikadi za dini, rangi, kabila jinsia na taifa.
11 Kutoa Elimu ya uraia.
11 Kushirikiana
na serikali na taasisi mbalimbali za kimataifa katika maadhimisho
ya siku ya mwanamme Duniani ikiwemo kuandaa sherehe hizo kitaifa
kufuatana na kalenda ya kimataifa kila mwaka.
12 Kutoa
misaada kwa makundi ya wasiojiweza yatima, wazee,wagonjwa ,wakimbizi
majeruhi wa ajari, majanga kama njaa,mafuriko, shule au kujenga majengo
ya kutoa huduma za afya na elimu kulinda na kutunza mazingira kuangalia
chaguzi ndani na nje ya Tanzania.
Sunday, February 10, 2013
NIGERIA WACHUKUA UBINGWA WA AFCON 2013
![]() |
Obi akimpongeza Sunday Mba |
NIGERIA imetwaa ubingwa wa Afrika usiku huu, baada ya kuifunga Burkina Faso bao 1-0 katika fainali kali iliyopigwa kwenye Uwanja wa FNB(Soccer City), Johannesburg, Afrika Kusini.
Shujaa wa Nigeria usiku wa leo alikuwa ni Sunday Mba aliyefunga bao hilo pekee la ushindi dakika ya 40, baada ya kutokea purukushani kwenye lango la Burkina Faso'
Hilo linakuwa taji la tatu la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Nigeria kihistoria, baada ya awali kutwaa taji hilo mwaka 1980 na 1994.
Zaidi ya hapo, Nigeria walishika nafasi ya tatu mwaka 2002, 2004, 2006 na 2010.
MTIBWA WAPIGWA NNE KWA MMOJA NA AZAM
Kutoka katika ukurasa wa facebook wa timu ya Azam inatueleza kuwa leo imeweza kuwa twisha magoli ya kutosha timu ya Mtibwa Sugar katika mechi iliyochezwa manungu morogoro.
BARAZA LA MITIHANI LAIKANA PAGE YA FACEBOOK INAYOTUMIA JINA LAKE
Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) limesema
matokeo ya kidato cha nne bado hayajakamilika na kuwa habari zilizozagaa
wiki hii kuwa yapo tayari si za kweli.
Hata hivyo Baraza hilo limebainisha kuwa licha ya kutokamilika, matokeo hayo yanakaribia kutoka kwa mujibu wa ratiba za baraza hilo ambapo hutakiwa kutoa matokeo hayo mwezi Februari.
Akizungumza na mwandishi jana, Ofisa Habari na Mawasiliano wa NECTA, John Nchimbi alisema uvumi wa kwamba matokeo hayo yako tayari ulitokana na kuzushwa kupitia mtandao wa kijamii (Facebook).
Alifafanua kwamba habari kuwa matokeo hayo yameanza kutoka kisirisiri kabla hayajatangazwa rasmi na kwamba hatua hiyo inalenga kuyachakachua, siyo taarifa sahihi.
Aliwataka wananchi kuwa makini na uvumi huo kwa vile endapo matokeo hayo yatakuwa tayari yatatangazwa na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo na pia kuwekwa kwenye tovuti ya Baraza pamoja na wananchi kuweza kuyapata kupitia simu zao za mkononi.
Hata hivyo Baraza hilo limebainisha kuwa licha ya kutokamilika, matokeo hayo yanakaribia kutoka kwa mujibu wa ratiba za baraza hilo ambapo hutakiwa kutoa matokeo hayo mwezi Februari.
Akizungumza na mwandishi jana, Ofisa Habari na Mawasiliano wa NECTA, John Nchimbi alisema uvumi wa kwamba matokeo hayo yako tayari ulitokana na kuzushwa kupitia mtandao wa kijamii (Facebook).
Alifafanua kwamba habari kuwa matokeo hayo yameanza kutoka kisirisiri kabla hayajatangazwa rasmi na kwamba hatua hiyo inalenga kuyachakachua, siyo taarifa sahihi.
Aliwataka wananchi kuwa makini na uvumi huo kwa vile endapo matokeo hayo yatakuwa tayari yatatangazwa na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo na pia kuwekwa kwenye tovuti ya Baraza pamoja na wananchi kuweza kuyapata kupitia simu zao za mkononi.
Uvumi huu umetokana na mtu asiyejulikana kufungua akaunti ya facebook yenye jina la Baraza na kuanza kuweka taarifa hizo zisizo sahihi. Napenda kuwajulisha wananchi kuwa Baraza letu halina mtandao kama huo hivyo taarifa hizo si sahihi.
Nchimbi
alibainisha kuwa matokeo hayo si siri hivyo yakiwa tayari Katibu
Mtendaji atayatangaza kupitia vyombo vya habari na baadaye yataanza
kusambazwa kwa kutumia mtandao.
Aliwataka wananchi kuwa makini ili wasitapeliwe na wanaojifanya kuwa wanaweza kupata matokeo ya mwanafunzi kabla hayajatangazwa rasmi kwa vile suala hilo haliwezekani.
Aliwataka wananchi kuwa makini ili wasitapeliwe na wanaojifanya kuwa wanaweza kupata matokeo ya mwanafunzi kabla hayajatangazwa rasmi kwa vile suala hilo haliwezekani.
MSUYA ALAZWA KWENYE HOSPITALI YA KIFALME UINGEREZA

Rais Jakaya Kikwete akimjulia hali Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa David
Msuya Hospitalini, kwa sasa amepelekwa Uingereza kwa matibabu zaidi
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Cleopa David Msuya aliyepelekwa nchini
Uingereza hivi karibuni kwa matibabu, anatibiwa katika hospitali ya
kifahari inayomilikiwa na familia ya Malkia Elizabeth wa Uingereza.
Msuya anatibiwa katika Hospitali ya ‘The King
Edward the V11’s Sister Agnes’ ambayo ni binafsi inayoongoza kwa huduma
bora na gharama nchini humo, ambayo mlezi wake mkuu ni Malkia Elizabeth
wa Uingereza.
Waziri Msuya aliyekuwa amelazwa katika Hospitali
ya Muhimbili kitengo cha Mifupa (MOI), alipelekwa nchini Uingereza
Februari saba kwa ndege maalumu ya kukodi. Hata hivyo, gharama za kukodi
ndege iliyomsafirisha Msuya kwenda Uingereza hazijajulikana, wala
aliyemlipia.
Mwananchi Jumapili liliwasiliana kwa simu na
hospitali hiyo ya The King Edward the V11’s Sister Agnes na kuzungumza
na idara ya mapokezi, ambayo baada ya kupewa jina la waziri huyo kwa
herufi moja moja, walimuunganisha mwandishi kwa simu hadi katika kitengo
cha kuhudumia wagonjwa.
Simu ya pili ilipokelewa na msichana aliyehoji
maswali kadhaa ambapo baada ya kuridhishwa na majibu ya mwandishi,
alimuunganisha moja kwa moja na Msuya katika chumba alicholazwa .
Hata hivyo, baada ya kupokea simu ya mwandishi wa
habari hizi, Waziri Mkuu huyo mstaafu hakuzungumzia lolote kuhusu hali
yake ya kiafya, bali alimhoji mwandishi, akitaka kujua alikopata
mawasiliano ya hospitali aliyolazwa.
“Habari yako, nani anazungumza?,?? Msuya aliuliza.
Baada ya mwandishi kujitambulisha, Msuya alisema: “Nani aliyekupa
‘contact’ zangu za huku?.” Kisha akakata simu.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein
Mwinyi alipohojiwa kuhusu gharama za matibabu ya viongozi nje ya nchi
alisema kuwa zinalipwa na Serikali.
“Mawaziri wakuu wastaafu na waliopo madarakani
wote ni wafanyakazi wa Serikali, hivyo gharama za matibabu yao zinalipwa
na Serikali,” alisema Mwinyi na kuongeza:
“Hata hivyo Serikali hulipa gharama hizo kwa
anayetibiwa nje iwapo kuna sababu ya kufanya hivyo, hii siyo kwa
viongozi tu, bali kwa Mtanzania yoyote mwenye mahitaji.”
Ofisa Uhusiano wa Kitengo cha MOI , Almas Jumaa
alisema kuwa Msuya alipewa ruhusa katika hospitali hiyo tangu Februari
Nne, baada ya kupata nafuu. Hospitali ya Mfalme Edward wa Saba iliyopo
katika Mtaa wa Beaumont, katika Jiji la Westmister, ilianzishwa mwaka
1899.
Mtoto wa mfalme wa Wales, ambaye baadaye alikuwa
Mfalme, Edward wa V11, kimada wake Agness Keyser, pamoja na dada wa
Agness, aliyeitwa Fanny, walianzisha huduma za matibabu kwa ajili ya
maofisa wa jeshi.
CHADEMA WAFUKUZA WENGINE MOROGORO
Ndugu Amani Mwaipaja

Chama cha Demokrasia na maendeleo chadema mkoa wa morogoro kimemfukuza uanachama aliyekuwa mgombea Ubunge wa jimbo la morogoro mjini na mwanasheria wa chama hicho mkoa wa morogoro Amani Mwaipaja wakimtuhuni kutumika kukivuruga chama hicho wakati huu wa vuguvugu la Kuimarisha vyama vya siasa kuelekea uchaguzi wa viongozi wa serikaliza mitaa na vijiji mwaka 2014 na uchaguzi mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani mwaka 2015.
Subscribe to:
Posts (Atom)