Facebook Comments Box

Saturday, January 19, 2013

ANGALIA REAL SOCIEDAD ILIPO IPA KICHAPO BARCELONA LEO




BIFU LA SINTAH NA RAYUU: HAYA NDIO MANENO MAZITO WALIOTUPIANA


Ikisemekana bifu hilo lilianza baada ya Sintah kumuandika vibaya Rayuu katika mtandao wake kama inavyoonekana hapo juu
Baada ya maneno hayo ndio ikamlazimu Rayuu nae kujibu maneno hayo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook



SAEED KUBENEA KUGOMBEA UBUNGE 2015

Mwandishi wa habari wa gazeti la Mwanahalisi Saed Kubenea, inasemekana amejipanga kugombea Ubunge Jimbo la Kibaha Mjini kupitia CHADEMA mwaka 2015. kwa hivi sasa Jimbo hilo linaongozwa na Silvestry Koka [CCM].
Saeed Kubenea ameshauriwa na Dr Slaa agombee ubunge na CHADEMA itampa sapoti katika hilo na amemuhakikishia kuwa atashinda


KAMATI YA UCHAGUZI YA TFF YA AHIRISHA UCHAGUZI


UCHAGUZI WA VIONGOZI TAFCA WAAHIRISHWA 

Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeahirisha uchaguzi wa Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) uliokuwa ufanyike leo (Januari 19 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Uchaguzi umeahirishwa kwa vile ulitaka kufanyika bila kuzingatia Katiba ya TAFCA Ibara ya 32(1) na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF Ibara ya 10(6) na 26(2), hivyo Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeahirisha uchaguzi huo kwa vile nafasi zilizoombwa kugombewa na idadi ya waombaji uongozi haikidhi matakwa ya Katiba ya TAFCA.
Pia taratibu za kikanuni ikiwa ni pamoja na kuwaarifu waombaji uongozi ambao hawakukidhi matakwa ya Katiba ya TAFCA hazikukamilika kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Licha ya upungufu huo, TAFCA haikuwasilisha taarifa za mchakato mzima kama ilivyoombwa na TFF. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeiagiza Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA kuandaa uchaguzi mpya utakaokidhi matakwa ya Kamati ya TAFCA baada ya Uchaguzi Mkuu wa TFF.
TFF inaishauri TAFCA kutumia fursa ya Mkutano Mkuu wa leo (Januari 19 mwaka huu) kujadili mustakabali wa TAFCA kwa kuwa chama hicho kimeshindwa mara mbili kupata idadi ya wagombea wanaokidhi akidi ya Kamati ya Utendaji.
Pia TAFCA haijawahi kufanya mikutano ya Kamati ya Utendaji na Mkutano Mkuu kwa karibu miaka minne.
Boniface Wambura

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

HII NDIO YANGA BWANA - HIVI NDIVYO ILIVYOWATANDIKA WASAUZI TAIFA LEO

 Didier Kavumbagu (kushoto) akijaribu kumtoka beki wa Black Leopards, wakati wa Mchezo huo, uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete.
jj
 Kikosi cha Yanga.
 Kikosi cha Black Leopards.
 Mchezaji wa Yanga, Kabange Twite (kushoto) akimiliki mpira huku akidhibitiwa na beki wa Black Leopards, Nkosiabo Xakane, wakati wa mchezo huo.
Mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete. (PICHA NA SUFIANI MAFOTO)


SIMBA YACHEZEA KICHAPO CHA 3 KWA 1

 Mabingwa wa soka Tanzania Bara,Simba wameshindwa kutamba mbele ya Wenyeji wao mara baada ya kufungwa mabao 3-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya Taifa ya Jeshi la Oman. mechi hiyo ilichezwa Ijumaa jioni kwenye uwanja wa Qaboos Complex jijini Muscat.
bao la simba lilifungwa katika kipindi cha pili na Haruna Moshi 'Boban' huku Mwenyekiti wa Simba,Ismail Aden Rage akiwa jukwaani pamoja na viongozi wengine wa simba, Rahma Al Kharoos na Musleh Rawahi pamoja na Kocha Talib Hilal wakiishuhudia Simba ikizama mbele ya wanajeshi hao

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjlRCm9tsdl0GuqK8TLbE1shCvEZJgJ5ZlH_m5XkhR1hTThltEl1Xt8bq8XcTQF75XYFCL6no8X9TueY_JkNVtYjykqNT-6pBUZ_PX-fKmeb_-wQHsscSKl5YQpRPaAvlNjUKfcBaSRVcQ/s1600/rAGE.JPGMwenyekiti wa Simba na Mfadhili wa safari ya Simba Rahma Al Kharoos akiangalia timu ya Simba ikipokea kichapo

TRA,,TUME YA UCHAGUZI NA JUMUIYA YA SERIKALI ZA MITAA (ALAT) WATOA MAONI YA KATIBA MPYA





 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi akiwasilisha maoni ya Jumuiya hiyo kuhusu Katiba Mpya kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba jijini Dar es Salaam Ijumaa, jan 18, 2013. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani.

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Ally saleh akiongea katika mkutano na Uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) uliokutana na Tume kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya  katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiqMBipiZ6xuBIr7S_HqKfhWiuqiFBoed3IEs9XBug6QoRugraXDI0Az5Ds1eGNQSGepfRtK37-qqZr9CU1TXRs9ua0wUX1VMSfErSIKhDoA3xD8p-04w6K9UDnSz8lIPc8OzlqnwMu59Q/s1600/CRC-TRA+Jaji+Warioba+na+Viongozi+wa+TRA.jpg
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Harry Kitillya (mwenye tai nyekundu) akiongea na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba mara baada ya Mamlaka hiyo kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya kwa Tume katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjd_pJBymQJ4i5jeCDYb62zhaA8NubxDoPSA2TSdrA9lKa6fWm3PMmw8CVwFlBK22h8TYtK3O0_l2A54dSMrmWFnP0-F0hJaKzK9VrmQoUslqkyipIyydYZhjKBPPvWqxr7lAvVuT40p2s/s1600/CRC-TRA+Picha+ya+pamoja.jpg

 Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Joseph Warioba (wa sita kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) waliongozwa na Mwenyekiti wa Bodiu ya TRA Bw. Bernard Mchomvu (wa nne kutoka kushoto) mara baada ya Mamlaka hiyo kuwasilisha maoni yake kuhusu Katiba Mpya jijini Dar es Salaam.



Friday, January 18, 2013

THEO WALCOTT AONGEZA MKATABA WA MIAKA MITATU NA NUSU ARSENAL

Baada ya malumbano ya muda mrefu mchezaji Theo walcott ameamua kukubali kuongeza mkataba na Arsenal kwa muda wa miaka mitatu na nusu. Katika mkataba huo mchezaji huyo atakuwa akilipwa Paund 100,000 kwa wiki ambazo ni zaidi ya milioni miambili hamsini za tanzania. Mchezaji huyo alikataa kuongeza mkataba wa miaka mitano ambao ungempa paund 70,000 kwa mwezi. Mbali na mihele yote hiyo mchazaji huyo amepewa na bonasi ya paundi milioni 3 kwa ajili ya kuongeza mkataba huo. Imeichukua Arsenal mwezi mzima wa malumbano na mchezaji huyo kupata saini yake.

Baada ya kupata saini ya mchezaji huyo kocha wa Arsena alisema "We are all delighted that Theo has signed a new contract. He joined us as a 16-year-old and since then has developed very well to become an extremely important player for both Arsenal Football Club and England." akiwa anaelezea furaha yake na klabu kwa ujumla kwa mchezaji muhimu ambae alijiunga kilabuni hapo akiwa na miaka 16 mpaka sasa amekuwa muhimu kwa kilabu na timu ya taifa ya uingereza

Nae Theo alisema "I am very happy to have signed a new contract here at Arsenal. Thanks to everyone for their continued support, especially the manager, everyone at the club and most importantly the fans. I have made it clear from the start that I wanted to stay at Arsenal so I am pleased we have agreed a deal that everyone is happy with. What’s important now is for the team to realise its potential and win trophies.” Akionesha furaha yake baada ya kuweka saini na kuonesha nia ya kutafuta makombe katika kilabu hicho kilichopatwa na ukame wa makombe

SIMBA WAFANYA BONGE LA SHOW LA BONGO FLEVA WAKATI WA TAFRIJA YAO

Hapa wakimwaga burudani najua unaijua ile staili ya wazee wa Bongo Fleva "Piga keleleeeeeeeeeee"

Kwa show nzuri ilibidi mama aende kuwatunza.


Mdhamini wa safari ya Simba Rahma jana aliwaalika Simba nyumbani kwake eneo la Al Kheri jijini Muscat, Oman jana usiku kwa ajili ya chakula cha usiku.
Walikula pamoja na baadaye bendi maalum kutoka Tanzania iliwapigia muziki na wakaserebuka pamoja huku Rahma akimwaga noti kama maji.

Katika hafla hiyo, Rahma alikabidhiwa jezi ya Simba na Musleh Rawah ambaye ni mmoja wa wadau wa Msimbazi na jezi ya timu ya taifa ya Oman na kocha wa makipa wa timu hiyo, Haroun Amur.



GHARAMA ZA KUPIGA SIMU ZASHUSHWA


Picture
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kampuni za mitandao ya simu Tanzania wakisikiliza maoni mbalimbali, Dar es Salaam jana, kuhusu utozaji wa viwango sawa kwa upigaji simu kwa mitandao yote nchini ifikapo Mwezi Machi mwaka huu. (Picha: Charles Lucas/MAJIRA)
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kampuni za mitandao ya simu Tanzania wakisikiliza maoni mbalimbali, Dar es Salaam jana, kuhusu utozaji wa viwango sawa kwa upigaji simu kwa mitandao yote nchini ifikapo Mwezi Machi mwaka huu. (Picha: Charles Lucas/MAJIRA) Mapendekezo ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kampuni za simu kushusha gharama hizo kwa dakika kuanzia Machi mosi mwaka huu ili kumpunguzia gharama ya kupiga simu kwa mteja wa kampuni moja ya simu ya mkononi kwenda kwa mteja wa kampuni nyingine yamekubaliwa kwa kiasi kikubwa. Wakizungumza Dar es Salaam jana katika mkutano wa kukusanya maoni ya wadau na watumiaji wa simu za mkononi ulioandaliwa na TCRA, Kampuni za Airtel Tanzania, Tigo Tanzania na Vodacom Tanzania zilidai punguzo hilo litawapotezea mapato na kuvuruga nia yao ya kuendelea kuwekeza. Mwakilishi wa Airtel Tanzania, Mwanasheria Clara Mramba, alisema wao wanakubali punguzo hilo lakini gharama zishuke kwa hatua kutoka mwaka mmoja hadi mwingine kwa kuanzia Sh 84 Machi hadi Sh 29.26 mwaka 2017. Alidai kuwa kushuka kwa kiwango hicho kikubwa cha Sh 34.92 Machi, kunaweza kuharibu uwekezaji wao: Tunataka ianze kushuka kutoka shilingi 112 hadi shilingi 85 kwa mwaka huu, shilingi 63 kwa mwaka unaofuata, shilingi 47 kwa mwaka unaofuata, shilingi 34.5 kwa mwaka unaofuata na shilingi 26.96 kwa mwaka unaofuata. Mkisema mshushe gharama hizo kutoka shilingi 112 hadi shilingi 35 ambazo ni sawa na asilimia 69 mtapunguza kasi ya uwekezaji wetu kwa sababu sekta ya mawasiliano inahitaji uwekezaji mkubwa. Mwakilishi wa Vodacom Tanzania, Mwanasheria Walarick Ngitu, alisema kama gharama hizo zitashuka kwa kiasi hicho watashindwa kufunga minara ya mawasiliano katika maeneo ya vijijini. Alipendekeza punguzo lianze kwa asilimia 35 na mwakani asilimia 20 na kwenda taratibu hadi mwaka 2017 jambo litakalosaidia sekta hiyo ikue huku gharama ikipungua taratibu: Watu wengi wa vijijini wanapigiwa zaidi simu kuliko wao kupiga, kwa hiyo mkishusha gharama hizo ni wazi minara ya mawasiliano haitafungwa vijijini kwa sababu kampuni itakuwa haipati faida na itawekeza zaidi mijini, tunaomba bei hizo zisishuke kwa uharaka wa namna hiyo. Mwakilishi wa Tigo Tanzania, Revocatus Nkata, alisema endapo gharama hizo zitashuka zitawasumbua kulipa kodi ya Serikali kwa sababu mapato yao yatapungua. Alitaka punguzo lianzie Sh 80 na soko lisiingiliwe kwa kuwa tayari limekomaa ili liendelee na ushindani: Uwekezaji wetu tunaotaka kuufanya lazima utapungua kama gharama hizi zitapungua, pia ni dhahiri tutapata tabu ya kulipa kodi serikalini. Si hivyo tu, bali soko la mawasiliano sasa hivi limekomaa hivyo halihitaji kuingiliwa, bora liachwe na kampuni ziendelee kufanya biashara. Kampuni za Sasatel, Sixtelecom, Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), BOL na Zantel na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia zimekubali gharama hizo kushuka. Mwakilishi wa Sasatel, Godfrey Murisi, alisema punguzo hilo litawafaidisha wateja na watakuwa waaminifu kutokana na huduma wanazozipata. Mwakilishi wa Sixtelecom, Said Abdala, alisema Tanzania ndio nchi pekee ambayo ina gharama kubwa katika muingiliano wa simu na ikishuka italeta ushindani katika soko. Mwakilishi wa TTCL, Mrisho Shaaban, alisema mtumiaji wa simu hatakiwi kubebeshwa gharama zisizo za lazima na agizo hilo lilitakiwa kuanza mapema kabla ya Machi, mwaka huu. Mwakilishi wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Samson John, alisema gharama hizo zitakaposhuka zitampa mtumiaji unafuu wa kupiga simu na itaondoa ukiritimba katika soko: Gharama zikishuka maana yake mtumiaji atafaidika na kampuni nyingine mpya zitapata nafasi ya kutoa huduma za mawasiliano sokoni, sisi tunataka sekta ya mawasiliano ikizidi kutanuka na ukiritimba wa baadhi ya kampuni uondoke. Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Samson Mwela alisema wamekubaliana na mapendekezo hayo, kwa kuwa sekta hiyo inaendeshwa kwa ushindani ambao unalindwa, hivyo ni lazima mtumiaji apate haki zake. Alisema kupungua kwa gharama hizo, kutawapunguzia watumiaji mzigo wa simu ikiwa ni pamoja na kudhibiti simu bandia zinazotumiwa na wengi na kuongeza unafuu wa matumizi ya simu mpaka vijijini. Stanley Mwabulambo wa Baraza la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA-CCC), alibainisha kuwa waliunga mkono kwa kuwa mpango wa kibiashara wa kampuni hizo hutegemea gharama za muunganisho. Alizitaka kampuni hizo kuwa bunifu katika ushindani huku akitaka punguzo hilo lionekane kwa mteja na TCRA ihakikishe punguzo hilo haliongezwi upande mwingine. Mkuu wa Idara ya Ushawishi na Utetezi wa Ushindani kutoka Tume ya Ushindani (FCC), Shadrack Nkelebe alisema mapendekezo hayo yataongeza ushindani kwa kuruhusu wateja kuwa na chaguo na kampuni moja. Waziri wa zamani wa Ujenzi na Uchukuzi, Nalaila Kiula aliunga mkono mapendekezo hayo na kuitaka TCRA kuzitazama zaidi kampuni za simu kwa manufaa ya wateja kutokana na huduma wanazotoza gharama kubwa. Akifunga mkutano huo wa mwisho, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TCRA, Jaji mstaafu, Buxton Chipeta, alisema maoni yaliyotolewa yatafanyiwa kazi: Mawazo yote yaliyotolewa yatafanyiwa kazi na tutakuja na jibu moja kabla agizo halijaanza kutekelezwa, nia yetu kubwa tunataka mtumiaji wa simu asiumizwe na mtoa huduma za mawasiliano naye asiumie. Mkurugenzi wa Ofisi za Kanda wa TCRA, Victor Nkya alisema jana kwamba katika mapendekezo yao gharama hiyo inatakiwa kushuka kuanzia Machi kutoka Sh 112 ya sasa mpaka Sh 34.92. Mwakani inatarajiwa kuwa Sh 32.4; mwaka 2015 Sh 30.58; mwaka 2016 Sh 28.57 na mwaka 2017 Sh 26.96. Kutokana na mapendekezo hayo ambayo yalitokana na utafiti uliobaini kuwa gharama hizo nchini ni kubwa, wadau na kampuni zilizohudhuria kongamano la wadau la kujadili bei hizo, walikubali. TCRA ilitoa mapendekezo hayo baada ya kupata ripoti ya Kampuni Mwelekezi Mshauri kutoka Uingereza iliyofanya utafiti kwa kuangalia mapato na faida za kampuni za simu nchini.


2013 AFRICA CUP OF NATIONS (AFCON) MATCHES TIMETABLE/FIXTURES



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU