Facebook Comments Box

Thursday, September 26, 2013

POLISI WAZUIA BINTI WA MIAKA 14 KUFUNGA NDOA NA BWANA WA MIAKA 35 GOMS


NDOA iliyokuwa tayari kufungwa  kati ya Hamis Ngaumba (35), mkazi wa Bangulo, Ulongoni, Gongo la Mboto, Dar na binti wa miaka 14 anayetajwa kwa jina moja la Zubeda, imesambaratishwa na polisi wa Kituo cha Polisi cha Sitaki-Shari, Dar kutokana na umri wa bi harusi kuwa mdogo.

Binti wa miaka 14, Zubeda akiwa tayari kufunga ndoa na Hamis (35).
Kizaazaa hicho cha aina yake kilichovuta hisia za wengi kilitokea saa 10:00 jioni, Jumapili iliyopita.

Mapema siku ya tukio, msamaria mwema ambaye hakupendezwa na kitendo hicho alitoa taarifa kwa mapaparazi ambao nao waliwataarifu polisi wa Kituo cha Polisi Sitaki-Shari na kupewa maafande kutoka dawati linaloshughulikia unyanyasaji wa kijinsia na kuambatana nao hadi eneo la tukio.

Kabla ya kufika eneo la tukio kwanza ilikuwa ni kwa mjumbe wa eneo hilo Shina Namba 10, Erasto Nyakiege ambaye alikiri kusikia taarifa hizo za mtoto kufungishwa ndoa lakini alizipata muda mfupi kabla polisi na waandishi hao kufika eneo hilo.
Hamis Ngaumba (35) aliyetaka kumuoa binti wa miaka 14.

Mapaparazi, Polisi na Mjumbe huyo waliambatana hadi kwenye nyumba ambayo ilikuwa na shamra shamra za ndoa hiyo na kumkuta shehe akijiandaa kufungisha huku waalikwa wakiwa wameshakaa mkao wa kula pilau.

Mshtuko mkubwa ulitokea eneo la sherehe baada ya watu kuwaona askari, wengine walikimbia kama wanafukuzwa na simba. Bi harusi yeye alikimbilia chumbani huku bwana harusi akijichanganya katikati ya wageni waalikwa lakini polisi walimweka ‘mtukati’.

Akizungumza baada ya kunaswa, Shehe Bakari alisema ndiyo kwanza alikuwa anajiandaa kwa zoezi la kuwafungisha ndoa wawili hao lakini kama angebaini kuwa mtoto huyo ana miaka isiyokidhi vigezo.

Zubeda alisema cha kushangaza siku moja aliwaona wazazi wa kijana huyo wakipeleka barua ya posa na mahari na kumkabidhi mjomba na bibi yake kwani baba yake mzazi anaishi Shinyanga na mama anaishi Tabora, tangu akiwa mdogo anaishi na bibi yake huyo.

“Mimi natamani sana kusoma lakini sina uwezo kwani niliishia darasa la tatu baada ya wazazi wangu kushindwa kunisomesha ndipo bibi akaja kunichukua ndiyo maana suala la kuolewa limenitokea tu bila mwenyewe kupenda. Ilikuwa kama utani lakini wakapokea mahari,” alisema Zubeda huku akilia kwa uchungu.



BAADA YA KUONA WATAMKOSA MCHEZAJI KWA MSIMU MZIMA HATIMAYE YANGA WAMLIPIA NGASSA DENI LAKE KWA SIMBA

Mrisho Khalfan Ngassa akiwa katika Jezi tofauti za timu alizowahi kuchezea ambazo ni Simba, Azam na Yanga zote za Dar es Salaam.

Kikao cha mchana wa leo baina ya uongozi wa klabu ya Yanga ya Dar es Salaam na mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa kimefikia mwafaka kuhusu deni la mchezaji huyo kwa klabu ya Simba SC, Sh. Milioni 45, imefahamika.

Yanga SC italipa fedha hizo na Ngassa ataendelea kucheza katika klabu hiyo akiachana na mpango wa kwenda Oman, anakotakiwa na klabu moja ya huko, ambayo iko tayari kutoa kiasi cha Sh. Milioni 100, ambazo zingelipa deni la Wekundu wa Msimbazi na nyingine kulipwa Yanga ambao wana Mkataba naye kwa sasa.

Hata hivyo, haijajulikana Ngassa atailipaje fedha hizo Yanga, baada ya awali kuwapo kwa habari juu ya namna mbili, kwanza kukatwa mshahara na nyingine kuongezewa Mkataba.



PICHA: MWANAMKE WA KICHINA AMETOKA SALAMA KATIKA AJALI HII MBAYA

Mwanamke mmoja wa kichina amepona katika ajali mbaya zaidi kutokea. Mwanamke huyo alikuwa akiendesha gari yake pembeni ya gari kubwa lililobeba kontena la rangi ya machungwa ghafla kontena likadondokea gari lake na kulikandamiza kwa karibia nusu ya gari lote ikiwemo sehemu ya dereva kama picha hapo juu inavyo onekana. Baada ya waokoaji kufika na kunyanyua kontena walishitushwa na sauti za kuomba msaada. Walifanikiwa kumtoa na kumkuta mama huyo akiwa hata michubuko kama picha hapo chini zinavyo onekana katika tukio la kumuokoa.
 kontena likinyanuliwa

mwana mama wa kichina akitolewa kwenye gari alilopata ajali

 Mama huyo wa kichina akionekana salama baada ya kunyanyua kontena
akitolewa ndani ya gari baada ya waokoaji kukata sehemu ya gari




BABU WA LOLIONDO - SAMUNGE AITABIRIA MAKUBWA TANZANIA


Mchungaji Ambilikile Mwasapile "Babu wa Loliondo"
 
 Mchungaji Ambilikile Mwaisapile wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonyesha kuwa Tanzania itakuwa kioo cha Afrika na baadaye kioo cha dunia.

Ametoa kauli hiyo siku ya (Jumanne, Septemba 24, 2013) mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia akiwa njiani kurejea mjini Arusha.

Mchungaji Mstaafu Mwaisapile maarufu kama 'Babu wa Samunge' alisema kuna mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye Biblia lakini hayakutokea Israeli na sasa yatafanyika hapa Samunge. “Mungu ametupenda sana, yanakuja mambo makubwa na wala hayako mbali. Kama mimi ni mzee na nitayaona, kwa hiyo mtarajie kuwa hayako mbali kutokea,” alisema huku akishangiliwa.

Alisema katika mafunuo aliyopewa na Mungu ameonyeshwa kwamba watu wengi zaidi watafurika kijijini Samunge kuliko ilivyokuwa hapo awali. Alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali kwa misaada iliyotoa wakati wa ‘kugawa kikombe’ ikiwemo mahema, maji na ulinzi.

Akitoa ombi maalum kwa niaba ya vijana mbele ya Waziri Mkuu, Bw. Elias Kalumbwa alisema wanaomba kuchimbiwa bwawa ili waweze kujiajiri kupitia kilimo cha mbogamboga na matunda.

Bw. Kalumbwa ambaye amesomea masuala ya wanyamapori alisema eneo la kuchimba bwawa lipo katika mto wa msimu unaopita kijijini hapo. “Eneo la kuchimba bwawa lipo katika mto wetu, vijana tunaweza kujiajiri endapo tutapata bwawa ili tufanye kilimo cha umwagiliaji maji,” alisema huku akishangiliwa.

Naye Bibi Martha Sereri (70) alimweleza Waziri Mkuu kwamba wanaomba jimbo la Ngorongoro ligawanywe kwa sababu ni kubwa sana kiasi kwamba inamuwia vigumu mbunge wao kufika maeneo yote. Aliomba pia wapatiwe walimu wa sayansi na hisabati kwa ajili ya shule 10 za sekondari zilizopo kwenye tarafa yao.



DAKITARI BANDIA ALIYEKAMATWA KCMC AFIKISHWA MAHAKAMANI MOSHI LEO



Daktari Feki Bw. Alex Sumni Massawe akipelekwa Mahakamani.

Mtu mmoja anayedaiwa kuwa ni daktari bandia aliyekamatwa akijiandaa kufanya upasuaji katika hospitali ya Rufaa ya Kcmc, leo atapandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi mjini Moshikusomewa shitaka lake kwa mara ya kwanza.

Mtuhumiwa huyo aliyetambulika kwa Jina la Alex Sumni Massawe alinaswa septemba 05, 2013 majira ya saa tano asubuhi ikidaiwa alitaka kumfanyia upasuaji mgonjwa aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa ngozi.

Mama mzazi wa kijana aliyetaka kufanyiwa upasuaji huo Bi Pamvelina Shirima alikutana na Daktari huyo katika Baa maarufu iliyopo eneo la Dar Street na kumtoza Shilingi 200,000/= akidai zitatumika kuharakisha mwanae afanyiwe vipimo vya upasuaji huo.



LIVERPOOL YACHAPWA KAMOJA NA MAN U NA KUTOLEWA KOMBE LA LIGI


Macho yote yalikuwa kwa Luis Suarez baada ya kurejea Liverpool kufuatia kumaliza adhabu yake ya mechi 10, lakini Javier Hernandez akaiteka shoo kwa bao lake pekee lililoipeleka Manchester United Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One.
 
Na wakati mshambuliaji huyo wa Uruguay alizomewa na mashabiki Uwanja wa Old Trafford, alikuwa ni Chicharito aliyepoza maumivu ya David Moyes kufuatia kipigo cha mabao 4-1 kutoka kwa wapinzani, Manchester City katika Ligi Kuu Jumapili.Liverpool ilitawala sehemu kubwa ya mchezo na Daniel Sturridge alipoteza nafasi kadhaa za kufunga.
 
Wayne Rooney, ambaye ndiye mchezaji bora zaidi kwa United hivi sasa, alipiga kona nzuri baada ya mapumziko na Hernandez akaunganisha nyavuni.
 
Sasa Man United watamenyana na Norwich nyumbani baada ya kuwatoa Liverpool kwa bao moja hilo la Chicharito.

Kikosi cha Manchester United kilikuwa: De Gea, Rafael Da Silva, Smalling, Evans, Buttner, Jones, Giggs, Nani, Rooney, Kagawa na Hernandez. 

Liverpool: Mignolet, Toure, Skrtel, Sakho, Jose Enrique, Gerrard, Lucas, Henderson, Suarez na Moses, Sturridge.  
Roar: Javier Hernandez celebrates after handing Manchester United the lead at Old Trafford
Javier Hernandez akishangilia baada ya kufunga bao pekee la Manchester United Uwanja wa Old TraffordCheck the technique: Hernandez leaps into the air as Wayne Rooney's corner found him free in the penalty area
 Hernandez akienda hewani kuunganisha kona ya Wayne Rooney
That's better: David Moyes celebrates Hernandez's goal after the misery of Sunday's derby defeat
David Moyes akishangilia bao la HernandezLook who's back: Luis Suarez looked happy to be in the Liverpool side again as he warmed up for the match
Luis Suarez akionekana mwenye furaha kuwa kikosini Liverpool tenaExchanging pleasantries: Suarez shakes hands with Wayne Rooney before the match
Suarez akipeana mkono na Wayne Rooney kabla ya mechiSaved: The Uruguay striker nearly got in on goal in the first half but was shut out by United keeper David De Gea
Suarez alikaribia kufunga kipindi cha kwanza, lakini kipa wa United, David De Gea akaokoaIn the action: Suarez gets a header in as United left back Alex Buttner watches on
Suarez akipiga kichwa huku beki wa kushoto wa United, Alex Buttner akimuangaliaOuch: United defender Phil Jones fouls Suarez with a crunching tackle
Beki wa United, Phil Jones akimchezea rafu SuarezNot enjoying the match, Roy? United legend Keane was in the stands watching the action
Gwiji wa United, Roy Keane alikuwa jukwaani akiangalia mechiFull blooded: Rooney shows his commitment in the tackle with Mamadou Sakho
Rooney akipambana na Mamadou Sakho


ARSENAL KUMENYANA NA CHELSEA BAADA YA KUITOA WESTBROM KWA PENATI 4-3

 
Klabu ya Arsenal iliendeleza wimbi la ushindi kwa kuitoa kwa matuta West Brom Uwanja wa The Hawthorns na kuingia Raundi ya Nne ya michuano hiyo. Eisfeld aliifungia Arsenal dakika ya 61 kabla ya Berahino kusawazisha dakika ya 71.
 
Arsenal itamenyana na wapinzani wao katika Jiji la London, Chelsea katika Raundi ya Nne ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One Cup baada ya kuitoa West Brom kwa penalti 4-3 Uwanja wa Hawthorns.
 
Mechi hiyo iliisha kwa sare ya 1-1 usiku wa jana ndipo ilipoamuriwa zipigwe penati ambapo Washindi walipata penati zao 4 na walikosa moja wakati Westbrom wao walikosa penati mbili.
 
Keeping his cool: Nacho Monreal stepped up to convert the winning penalty for Arsenal
 Nacho Monreal akiifungia Arsenal penalti ya ushindi
Cue celebrations: Monreal's Arsenal team-mates rushed to congratulate the Spaniard after his strike
Monreal na wachezaji wenzake wa Arsenalwakishangilia
Nice work: Arsene Wenger talks to the returning Nicklas Bendtner before his penalty Arsene Wenger akizungumza na Nicklas Bendtner kabla ya kupiga penalti yake
Cool: Arsenal's Thomas Eisfeld netted the opener for the visitors after the hour mark
Thomas Eisfeld akiifungia bao la kwanza Arsenal
Incoming: Nicklas Bendtner collides with the post in the first half at The Hawthorns
Nicklas Bendtner alikuwa mwiba usiku wa jana The Hawthorns
New look: The Denmark striker donned a beard and a David Beckham-esque haircut
Mdenmark Nicklas Bendtner amekuja kwa staili ya nywele za David Beckham
Congratulations: Bendtner and Eisfeld are mobbed by team-mates after Arsenal opened the scoring
Bendtner na Eisfeld wakipongezwa na wachezaji wenzao


HII NDIO TIMU BORA YA WIKI YA LIGI KUU YA UINGEREZA


Timu bora ya wiki ya Ligi Kuu ya Uingereza.
Ligi Kuu ya Uingereza iliendelea wikiendi iliyopita kwa timu kupata matokeo tofauti ya soka ambayo ni Ushindi,Sare na Kufungwa.Wakati huo huo kuna wachezaji waliong’aa katika timu zao.
Kifuatacho ni kikosi bora cha wiki:
Golikipa/Mlinda Mlangoo ni D.Marshall(Cardiff City)
Mabeki ni L.Bacuna(Aston Villa),V.Kompany(Man City), D.Lovren(Southampton)  na      L.Baines(Everton)
Viungo ni M.Amalfitano(West Brom) ,Oscar(Chelsea), M.Ozil(Arsenal) na S.Nasri(Man City).
Washambuliaji ni S.Aguero(Man City) na L. Remy(Newcastle).



Wednesday, September 25, 2013

TIMU YA WASICHANA YA AIRTEL RISING STARS YAPONGEZWA NA SERIKALI KWA KUTWAA UBINGWA

Wachezaji waliozawadiwa kwa kungara katika michuano ya Airtel Rising stars wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Mkurugenzi wa maendeleo ya michezo nchini Leonard Thadeo (mwisho kulia) na katibu mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Angetile Osiah(mwisho kushoto).

Mkurugenzi wa maendeleo wa michezo nchini bw Leonard Thadeo ameipongeza timu ya wasichana ya Tanzania baada ya kutwaa ubingwa wa vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars yaliomalizika juzi nchini Nigeria.

Tanzania waliibuka mabingwa baada ya kuwafunga Kenya katika fainali, pia amewapongeza wavulana baada ya kufikia hatua ya nusu fainali. Mabingwa wamezawadiwa kombe pamoja na kitita cha dola za marekani 10,000.

Katika pongezi zake pia amewapongeza wafungaji kwa upande wa wasichna ni Shelda Boniface na mvulana ni Athanas Mdamu na pia amempongeza mchezaji bora kutoka timu ya wasichana ambae ni Tatu Iddi .

Katika mashindano haya Tanzania imetoa rekodi tatu , mfungaji bora kwa upande wa wasichana magoli matano, mfungaji bora wa kiume magoli manne , mchezaji bora kwa upande wa wasichana na pia wachezaji watatu upande wa wavulana wamefunga magoli matatu katika mechi moja (hat-trik) na kuondoka na mpira kila mmoja.

Kabla ya kukabidhiwa kombe na mabingwa hao , Mkurugenzi wa maendeleo ya michezo nchini bw Leonard Thadeo amesema kuwa serikali kupitia wizara ya michezo itaendelea kusaidi mpira wa vijana wenye umri mdogo ili kuifikisha mbali Tanzania katika medani ya soka.

Akiongea kwa niaba ya msafara wa timu kocha Rogacian Kaijage amesema kua mashindano yalikua magumu ila wamefanikiwa kuchukua ubingwa , amewapongeza vijana wake , kocha mwenzie wa timu ya wavulana Abel Mtweve na pia ameishukuru Serikali , Airtel , TFF, pamoja na DRFA 
Kocha wa timu ya wasichana ya Airtel Rising stars Rogatician Kaijage akiongea wakati wa halfa ya kuwapongeza wachezaji wa timu ya Airtel Rising stars. 

Naodha wa timu ya wasicha ya Airtel Rising Stars chini ya umri wa miaka 17 Stumai Abdalah akimkabidhi kombe la ubingwa Mkurugenzi wa maendeleo ya michezo nchini Leonard Thadeo.
Kaptain ya timu ya wasichana Stumai Akikabidhi cheti cha kushinda kwa Mkurugenzi wa maendeleo ya michezo nchini Leonard Thadeo.
Mchezaji wa timu ya wasichana Neema Paul pamoja na Mkurugenzi wa maendeleo ya michezo nchini Leonard Thadeo wakionyesha mfano wa hundi ya dolla 10,000 iliyokabithiwa kwa timu ya washichana na Airtel baada ya kuibuka washindi wa michuano ya Airtel Rising stars Afrika. 
Chanzo: Michuzi


PRES UHURU KENYATTA DECLARES END OF WASTGATE MALL SIEGE


President Uhuru Kenyatta of Kenya has announced that a siege of Nairobi's Westgate shopping mall was over."We have ashamed and defeated our attackers, that part of our task is completed," President Uhuru Kenyatta said in a televised address to the nation: "Our losses are immense," he added.
He said that 61 civilians and 6 members of the security forces died during the operation, of the injured civilians, 62 were operated on and are still receiving treatments in various hospitali.He said that 5 terrorist have been killed and 11 gunmen are in custody.
He called three days of national mourning starting tomorrow. President Kenyatta said they can not confirm at the moment the reports that American and British nationals are among the attackers, noting that forensics experts are working to establish their nationalities."These cowards will meet justice," Kenyatta avowed.



TAARIFA: UKWELI KUHUSU AJALI YA SHEIKH NURDIN KISHKI

                    Sheikh Nurdin Kishki
UKWELI KUHUSU AJALI YA SH. NURDIN KISHKI.
Katika Surat Hujurat (49:6) Allaah anasema "Enyi mliyoamini! Akikujieni mpotovu na habari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutokujua, na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyoyatenda".
Leo majira ya asubuhi Sh. Nurdin alipokuwa akielekea katika moja ya shule anazozisimamia iitwayo AL-HIKMA BOYS HIGH SCHOOL iliyopo Mikwambe - Kigamboni (Dar es salaam), gari aliyokuwa amepanda iligongana na gari nyingine. Lakini alhamdulillah Sh. Nurdin hakuumia sana.
Baadae aliwahishwa hospitali na vipimo vinaonyesha kuwa hakuumia sana kama inavyozushwa kwenye mitandao hivi sasa.
Sh. Nurdin Kishki anaendelea vizuri na wala msije mkadanganyika na taarifa itakayokuwa tofauti na hii.
Tunamuomba Allaah amkinge Sheikh wetu Sh. Nurdin Kishki pamoja na Masheikh wengine na kila aina ya mabalaa!
'Amin'


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU