Tuesday, January 29, 2013
MAFURIKO YALETA BALAA MORO JIONI YA LEO
Mvua
kubwa iliyonyesha morogoro jioni ya leo imesababisha mafuriko katika
mtaa wa morogoro.Mvua hiyo iliyoanza kunyesha kuanzia saa tisa alasiri
imenyesha takribani kwa masaaa mawili imesababisha mafuriko katika
barabara ya msamvu kuingia katikati ya mji hali iliyosababisha msongamano
mkubwa wa magari.
Maji yakiwa yamejaa eneo la mtawala baada ya mvua kubwa kunyesha jioni hii mkoani morogoro
Mafuriko
hayo yaliingia katika makazi ya watu na hapa ni mashine za kukoboa
mpunga wakiwa wamesimamisha kazi zao baada ya maji kuingia ndani.
VILIO VYATAWALA BAADA YA LULU KUACHIWA LEO KWA DHAMANA
Lulu
na mama yake mzazi wakilia baada ya kukutana nje ya Mahakama, Lulu
amechiwa huru na Mahakama leo january 29 2013 mchana, pembeni ni
mwigizaji Dr. Cheni ambae amekua karibu na familia ya Lulu kwa muda
mrefu sana.
Ama kwa hakika nnje ya mahaka pamegeuka kilio mara muigizaji elizabeth
michael kuachiwa kwa dhamana leo tarehe 29 lulu amepewa dhama kutokana
na kesi inayomkabili ya kumuuwa bila kukusudia aliyekuwa star wa bongo
movie marehemu steven kanumba.
Mara baada ya lulu kumuona mama yake wamejikuta wakiangua kilio hadi
watu wakaribu wakawa wanashangaa.kazi ilikuwa kwa muigizaji dk cheni
ambaye kiukweli katika watu wakupongezwa katika hili anachukuwa nafasi
ya kwanza kwa binadamu ,cheni amekuwa mstari wa mbele kumsimamia lulu
hadi amepata dhamana.
Lulu akiingia kwenye gari huku akisaidiwa na Dk cheni kwa nyuma yake |
Mama yake lulu aliwahi kukaririwa akisema kwa sasa anamuona cheni ni
zaidi ya binadamu wa kawaida kwani bila yeye hajui kama ataweza
kumuokowa mwanae mama huyo amejikuta akilia kwa furaha baada ya kumuona
tena mwanae huyo.
Dk chen amezungumza na thesuperstarstz na kutuambia anashukuru mungu
kwakumpa moyo wa ujasiri wa kumsaidia binti huyo kwani wengi walimsusa
lakini tukumbuke mungu ndiye mlipaji wa yote hatupaswi kumuhukumu mtu
kwani hata mahakama bado haijamuhukumu lulu sasa sikuona sababu ya
baadhi ya wasanii kujitenga na lulu na ndio maana nikajitolea kumsaidia
hadi nijue mwisho wake.
Lulu akilia kwa furaha na kushindwa hata kuongea chochote alipokuwa anahojiwa jambo lililofanya cheni amuongelee |
Cheni ambaye ni mmoja kati ya wadhamini waliotoa milioni 20 za
kitanzania cheni amekuwa masaada mkubwa sana kwa lulu jambO ambalo
limefanya lulu kumuona cheni ni zaidi ya baba yake kwa sasa na ndio
maana mara nyingi hata kabla ya tukio la lulu na kanumba kutokea bado
lulu alikuwa anamuita cheni baba japo haikujulikana kwanini na cheni
katika familia ya kina lulu anaheshimika sana na ndio maana haikuwa
rahisi kwake kutojitolea kwa hilo.
WAZIRI MKUU AENDESHA KIKAO CHA KUTAFUTA SULUHU MTWARA
Waziri
Mkuu Mhe. Mizengo Pinda yupo Mkoani Mtwara akikutana na makundi ya wadau
mbalimbali wa mkoa huo ili kusikia kutoka kwao mawazo, michango na
dukuduku zao kuhusu mradi wa gesi asilia.
Imeripotiwa kuwa Waziri Mkuu angekutana na wanahabari baadaye leo saa 9 alasiri ili kutoa mjumuisho wa maongezi yake...
Imeripotiwa kuwa Waziri Mkuu angekutana na wanahabari baadaye leo saa 9 alasiri ili kutoa mjumuisho wa maongezi yake...
Taarifa
mpya zitawekwa hapa punde zitakazopatikana. Kwa sasa, tafadhali sikiliza
rekodi ya kipindi cha Amka na PRIDE FM radio, kilichozungumzia
muhtasari wa yaliyojiri katika kikao cha jana kati ya Waziri Mkuu na
Wadau.
TAARIFA MPYA ZA ZIARA YA WAZIRI MKUU
Waziri
Mkuu alikuwa akutane na Waandishi leo saa tisa alasiri. Kutokana na
kikao kirefu cha madiwani wa Manispaa ya Mtwara/Mikindani na Mtwara
vijijini pamoja na kikao cha wafanyabiashara, majumuisho ya ziara ya
Mtwara atayatolea ufafanuzi kesho.
Dondoo muhimu:
Dondoo muhimu:
- Kwa ufupi wajumbe wengi wamekataa bomba la gesi lisiende Dar
- Wamemkataa Mkuu wa Mkoa na kumtaka Waziri Mkuu aondoke naye
- Wajumbe (Madiwani ) kumpinga kwa kauli moja Hawa Ghasia kwa kile kilichosemwa kutumia mamlaka kutoa kauli za uongo kuhusu Mtwara Vijijini kuunga mkono suala la gesi iende Dar madiwani waMtwara vijijini. Wamesema hawakushirikishwa.
- Mzozo wa viwanja baina ya Madiwani na Mkuu wa Wilaya
- Waziri Mkuu ametumia mbinu ya kisiasa kuwashawishi Wadau kuwa bomba liende Dar
- Wajumbe wameondoka kwa shingo upande kwa kukubali kutokubaliana na Waziri Mkuu
- Kikao kinafanyika chini ya ulinzi Mkali wa FFU, JWTZ na UwT (Usalama wa Taifa)
- Hawa Ghasia arudishwa Uwanja wa Ndege, JKNIA asije Mtwara kwani anaweza kuchafua hali ya hewa
- Polisi wanadai Meya anataka kuwachonganisha na jamii/wananchi kutokana na kauli yake ya kusema wao ndio chanzo cha vurugu
Subscribe to:
Posts (Atom)