Facebook Comments Box

Thursday, November 8, 2012

HATIMAYE DIRECTOR WA FILAMU YA KUMKASHIFU MTUME AHUKUMIWA

.
The man behind an anti-Muslim film that led to violence in the Middle East has been sentenced to one year in prison.
Mark Basseley Youssef, 55, was sentenced on Wednesday for violating probation stemming from a 2010 bank fraud conviction.
US District Court Judge Christina Snyder handed down the sentence after Youssef admitted four of eight alleged violations including obtaining a fraudulent California driver’s licence.
Youssef served most of a 21-month prison term in the bank fraud case. Federal authorities wanted Youssef to serve two years for the violations.
After he was released from prison, Youssef was barred from using computers or the Internet for five years without approval from his probation officer.
None of the violations had to do with the content of “Innocence of Muslims,” a film that depicts Mohammad as a religious fraud, pedophile and a womaniser.
The movie sparked violence in Libya and other parts of the Middle East, killing dozens. Enraged Muslims had demanded severe punishment for him, with a Pakistani cabinet minister even offering $100,000 to anyone who kills him.
Federal authorities have said they believe Youssef is responsible for the film, but they have not said whether he was the person who posted it online.
He also was not supposed to use any name other than his true legal name without the prior written approval of his probation officer.
At least three names have been associated with Youssef since the film trailer surfaced – Sam Bacile, Nakoula Basseley Nakoula and Youssef. Bacile was the name attached to the YouTube account that posted the video.
Court documents show Youssef legally changed his name from Nakoula in 2002, though when he was tried, he identified himself as Nakoula. He wanted the name change because he believed Nakoula sounded like a girl’s name, according to court documents.

Tuesday, November 6, 2012

HII NDIO SIRI NDANI YA SIMBA



Kipa wa Simba,Juma Kaseja.

KOCHA MKUU wa Simba, Milovan Cirkovic ameapa kuendelea kumtumia kipa Juma Kaseja mechi zote huku bosi wa makipa, James Kisaka naye akiweka wazi hali ya mambo na kilichotokea Simba ikaondoka kileleni mwa Ligi Kuu Bara.

Milovan ametamka hivi: "Sijui kitu gani tumekutana nacho maana tunarekebisha makosa kwenye mazoezi wakiingia uwanjani kwenye mechi wanarudia tena, nashindwa kuelewa."

Lakini Kocha wa Makipa, Kisaka amesema bao alilofungwa, Juma Kaseja na Hussein Javu wa Mtibwa Sugar na timu yake kulala mabao 2-0 juzi Jumapili ni makosa yake na sasa kazi aliyonayo ni kurudisha imani kwa mashabiki wake ingawa amesisitiza hajashuka kiwango na kuwataka mashabiki wakumbuke fadhila.

Milovan amesema ataendelea kumtumia kwenye kikosi chake kwa sababu anaamini ndiye kipa bora zaidi ya wote. Kisaka amesema kutokana na uzoefu wake na idadi ya mabao 10, Kaseja aliyofungwa katika mechi za Ligi Kuu Bara ni uzembe wa mabeki na makosa ya kawaida.

"Wanaposema, Kaseja ameshuka kiwango siyo kweli kwa sababu aina ya mabao aliyofungwa si makosa yake ni safu nzima ya ulinzi. Kwanza Simba ilikuwa na tatizo la beki, mabao yaliyofungwa yalikuwa yanasababishwa na beki. Pili, kumekuwa na makosa ya kutoelewana kwa safu nzima ya ulinzi," alisema Kisaka.

"Lakini hili la pili tulilofungwa na Mtibwa linaweza kuwa ni makosa yake kwa sababu alienda kucheza mpira kwa kupiga chenga na adui akatumia udhaifu mwanya huo kumnyang'anya na kufunga.

"Unajua mashabiki wamekuwa wakisubiri kuona ubaya tu wazungumze na hawakumbuki fadhila ambazo Kaseja alizifanya kwa kipindi chote cha ushindi. Kaseja alifanya juhudi binafsi tukashinda beki ilikuwa haieleweki lakini hilo hawajui na kuangalia kosa hili la leo na kumpa wakati mgumu kufanya kazi ya ziada ili kurudisha imani kwa mashabiki wake.

"Naamini, Kaseja ndiye kipa bora zaidi ya wote kikosini ndiyo maana nampa nafasi ya kudaka mechi zote, makosa yanatokea ni hali ya kawaida hata hivyo nitaendelea kumtumia kwenye mechi zangu," aliongeza Milovan.
Hata hivyo, Kaseja aliyekuwa katika wakati mgumu na huzuni, aligoma kuzungumza lolote.

Matokeo hayo ambayo yaliipa Yanga mwanya wa kuongoza ligi yalimtoa machozi Kaseja haswa baada ya mashabiki kuonyesha kutokuwa na imani naye na kumuimbia nyimbo za kumdhihaki.

Hali halisi
Kwa mujibu wa duru za ndani ya Simba, uwezekano wa Milovan kukaa benchi la ufundi kwenye mzunguko wa pili wa ligi ni mdogo kwa kuwa hajatimiza malengo ambayo uongozi ulimtaka kushinda mechi zote nne dhidi Azam, Polisi Morogoro, Mtibwa na Toto African.

Aliishinda Azam mabao 3-1, akatoa suluhu na Polisi kabla ya kufungwa mabao 2-0 na Mtibwa juzi Jumapili na Jumapili ana kibarua cha Toto jijini Dar es Salaam.

Msimu uliopita Moses Basena alitimuliwa Simba baada ya kumaliza mzunguko wa kwanza akiwa na pointi 28 wakati Milovan akishinda mechi ya mwisho atamaliza na 26.

Habari zinapasha kuwa viongozi wa juu wa Simba jana Jumatatu walijadiliana hali ya mambo ingawa hawakutaka kutoa ufafanuzi wowote.

Hali ya kutoaminiana na pia kutopendana kwa baadhi ya wachezaji, chokochoko za ndani ya uongozi imedaiwa kuwa ni chanzo cha matokeo hayo ingawa wachambuzi wa mambo wanaeleza sare za Simba ni kutokana na uchakavu wa viwanja na morali ndogo ya timu.

Simba imetoka suluhu mechi mbili za Tanga dhidi ya Coastal Union na JKT Mgambo, kabla ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu dhaifu na inayochukia kushinda mechi ya Polisi Morogoro na juzi juzi huko huko Morogoro ikapigwa mabao 2-0 na Mtibwa.

Habari za ndani zinadai baadhi ya wachezaji wamekuwa wakiogopana kwa imani za kishirikina na wengine hawaongei kabisa wala kupeana pasi uwanjani.

Habari zinadai pia hata kucheza mechi nyingi kwa Kaseja peke yake hakuwafurahishi baadhi ya wachezaji ambao wanadai amechoka ndiyo maana inafika wakati anafungwa magoli laini ambayo Wilbert Mweta asingefungwa.

Suala la Kaseja limeonekana gumu kwani viongozi pamoja na makocha wanamkubali mno na wala hawana mpango wa kumweka benchi licha ya kelele za wanachama.

Jingine kubwa ni kwamba baadhi ya wachezaji wanadai kocha Milovan anaingiliwa na baadhi ya viongozi ambao wanamlalamikia kwa kutotoa nafasi kwa wachezaji wengi vijana na badala yake kuendelea kung'ang'ania walewale.


KATIBU WA MUFTI ZANZIBAR AMWAGIWA TINDIKALI

Watu mbalimbali wakiaangalia Katibu wa mufti Zanzibar Fadhili Soraga akipelekwa Hospitali baada ya kumwagiwa Tindikali na watu wasiojulika. Katibu alikuwa akifanya mazoezi kwenye viwanja vya mwanakwerekwe

Hapa akipelekwa kwenye chumba cha huduma ya kwanza hospitali ya mwanakwerekwe

Hapa akipandishwa kwenye gari ili awahishwe Muhimbili Hospital dar es Salaam


MUUWAJI WA KAMANDA BAROW ALIHUDHURIA MAZISHI YAKE

POLISI mjini Mwanza imebaini kuwa mmoja wa watuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, alikwenda kuaga mwili wa Kamanda huyo katika uwanja wa Nyamagana sambamba na wananchi wengine. Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Lily Matola jana alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Abdallah Petro ‘Ndayi’ (32) mkazi wa Mjimwema mjini hapa ambaye anashikiliwa Polisi. Kwa mujibu wa Kamanda Matola, Petro mbali na kutajwa kuhusika na mauaji hayo, pia anadaiwa kuwa na rekodi ya kufungwa miaka 30 jela katika gereza la Butimba kwa unyang’anyi wa kutumia silaha mwaka 2006. Alitoka gerezani mwaka 2010 baada ya kukata rufaa Mahakama Kuu ya Tanzania. Petro pia imebainika pia kuwa ni mdogo wa mtuhumiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Muganyizi Peter. Vielelezo vyakamatwa Kamanda Matola alisema mbali na kuwa na uhusiano huo, Petro na mtuhumiwa mwingine, Abdurahim Ismail Athuman ‘Dula’ (28) mkazi wa Mkudi Ghana, pia mjini hapa, baada ya kukamatwa kwa nyakati tofauti Mjimwema na Kilimahewa mwishoni mwa wiki, waliwapeleka polisi mahali walikoficha baadhi ya mali za marehemu. Mali wanazodaiwa kuonesha polisi ni pamoja na redio ya mawasiliano ya Polisi na funguo za gari alilotumia kamanda Barlow siku ya tukio la mauaji yake. Kamanda Matola alisema watuhumiwa waliwapeleka polisi katika shimo la majitaka kwenye maeneo ya Nyanshana, jijini Mwanza walipokuwa wameficha vitu hivyo. Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Joseph Konyo alisema watuhumiwa baada ya kutimiza uhalifu, walitenganisha redio hiyo ya mawasiliano ili isipatikane. “Damu ya mtu haipotei bure, hayo yote ni pamoja na Mungu mwenyewe, kwani sisi peke yetu hatuwezi, wananchi mmetusaidia sana,” alisema Kamanda Konyo. Baada ya kuonesha polisi vitu hivyo ambavyo sasa vimechukuliwa kama vielelezo katika kesi ya mauaji ya Barlow, Kamanda Matola alisema watuhumiwa hao walipekuliwa na kukutwa pia na kadi tatu za simu za Vodacom na Airtel, simu ya mkononi, viatu vya ngozi na begi dogo. Pia walikutwa na kofia mbili za kijeshi aina ya bereti; moja ikiwa ya Polisi na nyingine ya kampuni ya binafsi ya ulinzi, sare za kampuni ya ulinzi, mtarimbo, bisibisi, mapanga, televisheni mbili, sub-hoofer na deki. Alisema walipohojiwa, walidai wamekuwa wakihifadhiwa na Ryoba Matiku ‘Mama Nyangi’ katika eneo la Nyakabungo Miembeni ambako mipango yote ya uhalifu imekuwa ikisukwa. Mama huyo anashikiliwa pia kwa mahojiano.

HATIMAYE SERIKALI YASEMA TPI WALITENGENEZA ARV FEKI

LICHA ya wamiliki wa kiwanda cha Tanzania Pharmaceutical Industries Limited (TPI) kukana kutengeneza na kusambaza dawa bandia za kupunguza makali ya UKIMWI, serikali imethibitisha kuwa kiwanda hicho ndicho kilitengeneza dawa hizo aina ya TT-VIR 30 yenye toleo Na OC.01.85. Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, akisema kuwa serikali itawachukuliwa hatua za kisheria wote waliohusika katika suala hilo. Alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa suala hilo hatari linapatiwa ufumbuzi wa kudumu na kuzuia lisitokee tena, kabla ya kuchukua hatua hizo za kisheria uchunguzi unafanywa kupitia vyombo vya usalama. Dk. Rashid alikiri kuingia katika mzunguko kwa dawa hizo bandia lakini akawatoa hofu wagonjwa wote wanaotumia (ARV’s) kuwa dawa zinazopatikana kwenye vituo vya kutolea huduma hiyo kwa sasa ni salama na zenye viwango vinavyotakiwa. “Tunatoa wito kwamba waendelee kutumia dawa hizo kama wanavyoshauriwa na madaktari… kupitia Wizara ya Afya, serikali imehakikisha uwepo wa dawa za kutosha na kupunguza makali ya ukimwi katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya,” alisema. Dk. Rashid alifafanua kuwa Wizara ya Afya hununua dawa hizo kupitia Bohari ya Dawa (MSD), ambayo imepewa jukumu la kununua, kuzitunza na kusambaza katika vituo vya kutolea huduma za afya. Alisema kwa hapa nchini kuna kiwanda kimoja tu cha TPI kinachotengeneza dawa hizo na kwamba zile za bandia zilibainika mwanzoni mwa Agosti mwaka huu katika ukaguzi wa kawaida wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) katika Hospitali ya Tarime. Alisema baada ya ukaguzi na uchunguzi kwenye vituo vyote vya huduma za afya katika mkoa wa Mara na nchi nzima ilibainika kuwa dawa yenye jina la biashara TT-VIR 30 toleo namba 0C.01.85 ni bandia. Alisema pia ilibainika kuwa nyaraka zilizokutwa katika Bohari ya Dawa (MSD) zinaonyesha kuwa TPI iliiuzia MSD dawa hiyo bandia toleo namba 0C.01.85. Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa uchunguzi ulibaini kuwa dawa hiyo bandia ilikuwa na dawa zenye rangi tatu tofauti, njano, nyeupe na vidonge vya rangi mbili tofauti za pinki na nyeupe. Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo wa Afya, dawa zilizokuwa na rangi ya njano, zilikuwa na kiambata cha Efaverenz badala ya viambata aina ya Nevirapine, Lamivudine na Stavudine vinavyopaswa kuwemo. Aidha vidonge vyenye rangi nyeupe na vile vyenye rangi ya pinki na nyeupe vilikuwa na viambata vinavyotakiwa kuwepo yaani Nevirapine, Lamivudine na Stavudine kama ilivyokuwa kwenye lebo. Akielezea kuhusu hatua zilizochukuliwa na serikali baada ya matokeo hayo ya uchunguzi alisema ni pamoja na kusimamisha mara moja matumizi ya dawa hizo aina ya TT-VIR 30 toleo Na 0C.01.85. Hatua nyingine ni pamoja na kusitisha uzalishaji wa dawa zote katika kiwanda cha TPI Ltd hadi uchunguzi wa suala hilo utakapokamilika ikiwa ni pamoja na kujiridhisha tena ubora wa dawa inazozalisha. Alisema pia vigogo wa MSD akiwamo mkurugenzi wake walisimamishwa na kwamba wizara imeunda timu ya wataalamu kwa lengo la kufuatilia mwendelezo wa tiba na matunzo kwa wagonjwa wa UKIMWI.

Sunday, November 4, 2012

YANGA NA AZAM KATIKA PICHA

Kiiza akijaribu bila mafanikio kufunga

Aggrey Morris akiruka juu ya Paul Ngalema kupiga mpira kichwa

Mbuyu Twite akimuacha chini Salum Abubakar

Kiiza akimtoka Hajjji Nuhu

Haruna Niyonzima 

Chuji akijadiliana na Niyonzima kabla ya kupigwa kwa mpira wa adhabu

Kiiza alivyomuenzi Mafisango

Mwadini akidaka mpira hewani 

Simon Msuva anateleza

Mwadini akiruka kupangua mpira

Msuva

Hatari kwenye lango la Yanga

Jabir Aziz akimdhibiti Chuji

Kiiza anapasua katikati ya Ibrahim Shikanda kulia na Sure Boy kushoto 

Nadir Haroub 'Cannavaro' akimdhibiti John Bocco

Hatari kwenye lango la Yanga

Stewart Hall alitia huruma

Frank Domayo kulia akipambana na Aggrey Morris

Niyonzima akipiga shuti mbele ya Shikanda

Twite anapasua

Sure Boy akimtoka Twite

Sure Boy na Twite

Chuji akipiga kisu mbele ya Sure Boy

Msuva anatafuta njia

Shughuli

Yanga wakipiga ndiki kabla ya mechi

Kikosi cha Azam leo

Kiiza anamtoka Erasto Nyoni

Kikosi cha Yanga leo

Hatari kwenye lango la Azam

Hatari kwenye lango la Yanga

Msuva akiwasalimia wenzake benchi baada ya kupumzishwa

Niyonzima kushoto, Nyoni kulia

Kiiza na Hajji Nuhu


Kiiza baada ya kufunga bao la pili


Kavumbangu wa pili kutoka kushoto, akishangilia bao lake na wenzake

Kavumbangu wa kwanza kushoto


LIVE SCORE : FT YANGA 2 - 0 AZAM, MTIBWA 2 - 0 SIMBA


Kutoka Taifa: Mpira umeisha Yanga wanatoka kifua mbele kwa Goli kwa sifuri

Kutoka Morogoro:  Mpira umeisha Mtibwa Inatoka kifua mbele kwa 2 kwa sifuri

Kutoka Morogoro: Gooooool Mtibwa wanapata goli la pili hapa. Nilisema huyu Javu ana historia ya kufunga katika uwanja huu. Ndio maana mara zote tunaandika mtibwa wanaongoza kwa goli la kwanza na hili ni la pili

Kutoka Mtibwa: Dk 88 Mtibwa bado wapo mbele kwa goli la kwanza

Kutoka Morogoro: Mwinyi kazimoto anaachia shuti kali linapanguliwa na kipa na kuwa kona. Simba wanalisakama lango la mtibwa

Kutoka Morogoro: Husein Javu anaingia kuchukua nafasi ya Muhamed Mkopi. Huyu Javu ana historia nzuri ya kufunga katika uwanja huu

Kutoka Morogoro: Dk 79 Okwi anawakosakosa mtibwa na inakuwa kona. Husein Sharrif anapewa kadi ya njano kwa kupoteza muda. askari wameongezwa uwanjani

 Kutoka Taifa: Gooooooool Yanga wanaongeza goli la pili. Ni Hamis Kiiza "diego" anafunga goli safi sana hapa. Alivua jezi hapa kiiza anapewa kadi ya njano

Kutoka Taifa: Abdi Kassim anachukua nafasi ya Hamis Mcha.

Kutoka Taifa: Msuva anaenda nje anaingia Luhende.Yanga wanakosa goli baada ya Kavumbagu kuchelewa krosi ya Niyonzima

Kutoka Taifa: Dk 51 Erasto Nyoni anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumkanyaga Niyonzima wa Yanga.

Kutoka Taifa: Dk 48 Bocco anashindwa kuuwahi mpira aliopigiwa na Khamis Mcha lakini Chuji anautoa na kuwa kona. Azam inapata kona ambayo inakolewa na mabeki wa Yanga.

Kutoka Taifa: Kipindi cha pili kinaanza hapa uwanja wa taifa kati ya Yanga na Azam

Kutoka Morogoro: Babu Ally anapewa kadi ya njano kwa kumfanyia madhambi emanuel Okwi. Na Mrisho Ngassa anaingia kuchukua nafasi ya Akuffor. Chollo anaingia nafasi ya Ochieng

Kutoka Morogoro: Mpira umeanza Jamal anatoka na anaingia Issa


Kutoka Morogoro: Washabiki wa Simba wamtupia chupa mwamuzi wa pambano hili, vile vile wamewarushia vilevile chupa wachezaji wao. mmoja wa washabiki hao wa simba amekamatwa na polisi. Ulinzi zaidi unahitajika katika mechi hii maana inaonekana washabiki wa simba hawana uvumilivu.

Taifa; Dk 45 HALF TIME..... AZAM 0-1 YANGA

 Kutoka Morogoro: Mtibwa wanapata kona tatu mfululizo, lakini, Kaseja anadaka, dakika ya 42 sasa

 Taifa: Dk 39 Yanga na Azam zinashambuliana kwa zamu na mpira unachezwa katikati sana.

Kutoka Morogoro: Mtibwa inaongoza kwa bao moja dhidi ya Simba, mfungaji Mohamed Mkopi. MTBWA 1-0 SIMBA


Taifa:  Dk 32 Azam inapata kona baada ya Mbuyu Twite kuutoa mpira nje
Khamis Mcha anapiga kona lakini Bocco anautoa mpira nje.
Dakika ya 28, Akuffor, anashindwa kutumia makosa ya mlinzi wa Mtibwa ambaye alipiga pasi fupi kwa mwenzake na kuiwahi. Lakini, akiwa ndani ya sita anashindwa kuamua kufunga au kutoa pasi, na kupiga pasi mkaa iliyonaswa na mlinzi wa Mtibwa. Dakika ya 30 sasa.
Kutoka Taifa: Dk 28 Bocco anapiga shuti kali langoni kwa Yanga lakini kipa Ally Mustapha anadaka
 Dk 26 Athuman Idd Chuji anamchezea faulo Michael Bolou.
Kutoka Morogoro: Kwa dakika 20 za mwanzo, mechi bado imebalansi hakuna mashambulizi ya maana sana ambayo timu zinayaandaa. Kila timu inacheza kama haitafuti ushindi. Mara mbili, mshambuliaji, Said Mkopi wa Mtibwa amejaribu kumtoka Amir Maftah, lakini hakufanya cha maana. Emmanuel Okwi anajitahidi kuwakimbiza mabeki wa Mtibwa Sugar, lakini bado hapati, sapoti ya karibu kutoka Sunzu na Akuffor. Mtibwa, wamepiga kona nne hadi sasa, wakati,Simba, wamepata kona moja tu. Kiujumla, mchezo bado umepooza hadi sasa.
 
 Kutoka taifa: Dk 18 Niyonzima wa Yanga,anakosa bao la wazi kwa kupiga nje mpira aliopokea kutoka kwa Oscar Joshua.
Dk 15 Erasto Nyoni wa Azam anamchezea rafu Msuva 
Dk 14 Simon Msuva wa Yanga anakosa bao la wazi baada ya kushindwa kuuwahi mpira uliopigwa na Haruna Niyonzima.
Dk 13 Mpira unachezwa kwa kasi sana na timu zote zinatawala kiungo
 
 Kutoka Morogoro - Kwa dakika hizi kumi za mwanzo, timu zote zinaonekana kucheza kwa kuogopana zaidi. Mtibwa, walianza kufika katika lango la Simba, kupitia kwa Shaaban Nditti. Walinzi wa Simba, Keita na Ochieng, wakamthibiti. Bado hakuna soka la kuvutia na la mipango, japo, Mtibwa, wanaonekana kucheza kitimu hadi sasa. Simba, wanapata kona ya kwanza, lakini haina madhara, dakika ya 12 
Dk 9 GOOO...... Didier Kavumbagu anaifungia Yanga bao la kwanza baada ya kutokea piga nikupige katika lango la Azam. AZAM 0-1 YANGA
Kutoka taifa: DK 3 Hamis Kiiza anakosa bao la wazi kwa upande wa Yanga.
 Kutoka taifa: Mpira ndio umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya
Azam Fc Vs Young Africans
Morogoro - Mpira umeanza hapa Morogoro - Simba wakianza kwa kasi.
Leo tunaendeza utamaduni wetu wa kuwaletea matukio muhimu yanayoendelea kwenye viwanja tofauti vya ligi kuu ya Tanzania bara - kwa siku ya leo tunawaletea matukio ya mechi mbili kubwa kati ya Azam na Yanga, na Simba dhidi ya Mtibwa.
Kutoka Morogoro - Hiki ndio kikosi cha kwanza cha Simba kinachoanza: Kaseja, Kapombe, Maftah, Keita, Ochieng, Mkude, Kiemba, Kazimoto, Sunzu, Okwi, Akuffor
Hiki ndio kikosi cha Yanga ambacho tumefanikiwa kukipata. 
1.Ally Mustapha 'Barthez'
2.Mbuyu Twite
3.Oscar Joshua
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6.Athuman Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Didier Kavumbagu
10.Hamis Kiiza
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Yaw Berko
2.Juma Abdul
3.David Luhende
4.Nurdin Bakari
5.Nizar Khalfani
6.Jeryson Tegete
7.Said Bahanunzi


MAALIM SEIF AZUNGUMZA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad ameelezea kuchukizwa kwake na vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani vilivyotokea hivi karibuni visiwani Zanzibar.

Amesema vitendo hivyo vimeigharimu Zanzibar katika Nyanja mbali mbali zikiwemo za kiuchumi, kisiasa na kijamii, sambamba na kuitia doa katika jamii ya kimataifa.

Akihutubia mkutano wa hadhara wa chama hicho katika viwanja vya demokrasia Kibandamaiti mjini Zanzibar, Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amevilaumu vyombo vya dola kwa kutochukuwa hatua zinazostahiki katika kudhibiti vitendo hivyo.

Amesema hatua zilizochukuliwa katika kurejesha amani baada ya kutokea kwa vurugu hizo hazikuwa muafaka, kwani zimekuwa zikiwadhalilisha na kuwanyanyasa wananchi wasiokuwa na hatia pamoja na kuhujumu mali zao.

Amesema yeye binafsi amechukizwa na kitendo cha kuuliwa kwa askari polisi katika eneo la Bububu, Koplo Said Abrahmani lakini bado serikali na vyombo vya dola vina jukumu la kulinda haki za raia kwa kuwasaka wanaohusika na tukio hilo, na sio kuwanyanyasa raia wasiokuwa na hatia.

“Nazungumza haya kwa unyonge sana leo, sikufikiria kuwa vitendo hivi vingetokea Zanzibar katika wakati huu tunaotekeleza maridhiano ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa”, alieleza Maalim Seif na kuongeza: “Sipendi kuisema serikali yangu na Rais wangu hadharani, lakini inanibidi niseme ‘Rais wangu Dkt Shein unatuangusha’ kwa kuwa wewe ndiye mwenye jukumu kubwa zaidi la kulinda amani ya nchi hii” alieleza.

Ametahadharisha kuwa huenda vitendo hivyo vimepangwa kuvuruga umoja wa Wazanzibari ambao umeiletea sifa kubwa Zanzibar, na kuwataka wananchi kutokubali kuingizwa katika mtego utakaopelekea kuvunjika kwa umoja na mshikamano uliopo miongoni mwa wananchi.

Katibu Mkuu huyo wa CUF alienda mbali zaidi kwa kudai kuwa vikundi vinavyolalamikiwa kufanya vurugu vikiwemo vya ‘Ubaya ubaya, Mbwa mwitu na Janjawid vilikuwepo kabla ya tukio hilo na kwamba vimetokana na kundi kubwa la vijana la JANJAWID lililoahidiwa kupewa ajira na Serikali.

Katika hatua nyengine Maalim Seif ameitaka Tume ya mabadiliko ya katiba kufanya kazi kwa uadilifu na kuheshimu mawazo ya wananchi wanayoyatoa bila ya kuonyesha upendeleo kwa baadhi ya watu au makundi fulani.

“Tume hii inaonekana kuanza kuwa na ‘bias’ kwa baadhi ya watu na makundi fulani, lakini tunamwambia Jaji Warioba tume yake iheshimu mawazo ya wananchi”, alitanabahisha.

Katika risala ya wanachama wa chama hicho kwa wilaya sita za Unguja iliyosomwa na Katibu Mtendaji wa vijana CUF taifa Khalifa Abdallah walitahadharisha juu ya uwezekano wa kuwepo kwa ajenda ya siri ya kuvuruga Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Amesisitiza kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa bado inahitajika katika kupata ukombozi wa kweli wa Zanzibar, sambamba na kuendeleza umoja na mshikamano wa Wazanzibari.

Naye Kaimu wa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bw. Salim Bimani amewasisitiza wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao juu ya mabadiliko ya katiba, na kuiomba Tume inayohusika na ukusanyaji wa maoni kuwapa fursa wananchi kutoa maoni yao kwa uwazi.

“Wananchi msikubali kuchokozeka, nendeni mkatoe maoni kwani hii ni fursa pekee ya kupata katiba tuitakayo” alisisitiza Bimani.




SHABAN KADO APATA AJALI

 Mchezaji wa simba Uhuru Selemani aandika katika wall yake ya Facebook kuwa mchezaji wa Mtibwa Sugar Golikipa Shaaban Kado amepata ajali Chalinze. Hii labda ndio inayofanya leo asiwepo uwanjani. Blog hii inafuatilia na habari kamili itakupa baada ya muda.
Ndugu zangu mliopo chalinze naomba mfatilie hapo hospitali kado kapata ajari nasim yake haipatikan pls naomba mfatilie atakae kuwa nataarifa aniinbox namba yake sory jaman


LORD EYES APATA DHAMANA

.
Stori za uhakika nilizozipata muda mfupi uliopita ni kwamba mkali wa Hiphop kutoka A Town ambae alikua anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za wizi wa vifaa vya gari la Ommy Dimpoz, Isack Waziri (Lord Eyes) hivi sasa yuko nje kwa dhamana.
Ametoka nje kwa dhamana toka ijumaa ya novemba 2 2012.
Oktoba 23 2012 Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni Charles Kenyela alikaririwa na millardayo.com akisema “Watuhumiwa hawa wawili Kurushinde na Lord Eyes tunawashikilia kwa tuhuma zipatazo 30, yani matukio mbalimbali 30 pengine yanaweza yakaongezeka ambayo yameripotiwa kutokea katika maeneo mbalimbali kama vile Mlimani City, Kijitonyama, ufukwe wa bahari kama Coco beach, kwenye kumbi mbalimbali za starehe na pia  kwenye maeneo ambayo kunakua na harusi, sehemu ambazo kunakua na magari mengi watu hawa ndio huwa wanaitumia hiyo nafasi kufanya uhalifu, tunawashikilia kwa makosa ya wizi”
.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU