Facebook Comments Box

Saturday, May 11, 2013

PICHA ZA BONANZA LA VYUO VIKUU VYA MKOA WA KILIMANJARO


Mabingwa wa Netball VETA MOSHI wakiwa katika goli la Mwenge University


Mvua zilizonyesha kabla zilileta dosari na kuchelewesha mechi za Basketball





Mabingwa Kcmc kabla ya Fainali ya Mpira wa Kikapu


Vikombe vya washindi vilivyo tolewa


Washindi wa mpira wa Kikapu KCMC wakiwa na kikombe chao

Fred Maiko Leizer akiwa na kikombe cha mshindi wa kwanza
Waandaaji wa mashindano wakitoa maelezo kabla ya Fainali ya KCMC na Baptist


Kikundi cha kucheza mziki cha TIGO kikitoa burudani

Kikundi cha sarakasi cha TIGO kikitoa burudani baada ya mashindano kuisha




MSIKILIZE MRISHO MPOTO AKIMSEMA LADY JAY DEE HADHARANI

Msanii Mrisho Mpoto ambaye pia ametoa mada katika semina iliyo andaliwa na Clouds Media ambapo alimchamba Lady Jay Dee hadharani. Msikilize hapo chini
 




JESHI LA POLISI LAKANUSHA KANISA KUPIGWA BOMU

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dar es Salaam limetoa taarifa baada ya kuwepo uvumi kuwa Kanisa la KKKT usharika wa Kunduchi Beach, lililopo Kunduchi, Dar es Salaam limelishambuliwa kwa kupuliwa kwa bomu na kurushiana risasi.

Kamanda wa Polisi Suleiman Kova amesema ukweli ni kuwa hakuna ulipuaji bomu uliofanyika katika Kanisa la KKKT Kunduchi Beach ISIPOKUWA kikosi cha Polisi kilichokuwa kinapambana na wahalifu waliokuwa karibu na Kanisa hilo kililazimika kurusha bomu la machozi ili kupambana na kuwatia mbaroni wahalifu hao.

Kova ameongeza kwa kusema waumini waliokuwepo Kanisani walishituka kwa kudhani kuwa wamevamiwa, lakini baadaye walipofahamu kinachoendelea walijitokea ili kusaidia, "Wakati askari wetu wanapambana na majambazi hayo- waumini wa kanisa hilo wamejitokeza kuwasaidia askari wetu. Naomba unisaidie kukanusha. Siyo kweli, nitazungumza na vyombo vingine vya habari kuweka sawa," amesema Kova.

---
Taarifa hii imekukuliwa kutoka ITV na Radio One Stereo.
Tusubiri taarifa iliyoahidiwa kutolewa ili kuondoa tashwishi.


NAIBU WAZIRI AINGILIA KATI UGOMVI WA JIDE NA RUGE


IKIWA ni siku moja tu tangu Naibu Waziri wa Habari  Michezo Vijana na Utamaduni Amos Makala kutangaza hadharani kulivalia njuga suala la mzozo kati ya Mkurugenzi wa wa Kampuni ya Clouds Media Group Ruge Mutahaba  na msanii nyota wa kike wa Bongo Fleva Judith ‘Wambura Lady Jaydee’  Ruge ametoa ya moyoni.
Tanzania Daima ambayo ilimpigia simu Ruge na kumuuliza ana lipi la kusema baada ya Makala kutamka kwamba atawaita wawili hao na kuzungumza nao sambamba na kuleta suluhu.
“Mimi kana nilivyosema katika tamko langu wiki iliyopita kwamba niko tayari tuitwe na watu watusikilize  pande zote mbili  hasa mlalamikaji na ukweli uweze kuwa wazi zaidi kwa sababu hadi sasa Lady Jaydee amekuwa akisema mambo mengi kiasi kwamba hata nashindwa kumuelewa”
Na siyo Waziri Makalla tu pia ikiwezekana hata kama kuna watu wengine wanataka kujitokeza ili kutuweka katika kiti moto watuulize maswali na kila mmoja wetu aote majibu mbele ya hao watu mimi niko radhi kufanya hivyo” anasema Ruge.
Wakati huohuo Ruge ameongeza kwamba  tayari ameshafuata taratibu za kisheria ikiwa ni pamoja na kumfungulia jalada la malalamiko ya kutukanwa na Lady Jaydee na taarifa hiyo amepelekewa  msanii huyo akiitwa katika vyombo vya sheria.
Lakini ninaweza kusema jambo hili linaweza kuzungumzika nje ya vyombo vya sheria kwani sisi tunaliona ni jambo dogo na la mzaha lakini lina athari kubwa katika jamii inayotuzunguka  anasema Ruge.
Mwanzoni mwa mwezi huu Lady Jaydee aliamua kuibuka na kuituhumu Clouds Media Group  kwa kutumia mitandao ya kijamii kama facebook, twitter nab log yake kwamba wana muhujumu kimuziki , kuzuia matangazo ya mgahawa wake wa Nyumbani Lounge   na kipaji chake kwa ujumba tuhuma ambazo Ruge na Clouds wanazikanusha vikali.
Mwandishi wa habari hii alijaribu kumtafuta Lady Jaydee azungumzie kuhusu kauli ya Waziri kwa kupitia simu ya mumewake Gadner Habash simu iliita bila kupokelewa.


SEMINA YA 'TWEN ZETU' YA CLOUDS MEDIA GROUP ILIVYOFANYIKA DODOMA



Mbunge wa Kigoma Kaskazini CHADEMA Ndugu Zitto Kabwe akizungumza na wasanii mabalimbali wakati akitoa mada katika semina ya kampeni maalum ya “Twen Zetu” iliyofanyika kwenye ukumbi wa African Dream mjini Dodoma leo , Kampeni hiyo inazungumzia na kuhamasisha vijana kuwa wabunifu na kutumia fursa zilizopo ili kujikwamua kimaisha lakini pia kuleta maendeleo kwa wasanii wenyewe na taifa kwa ujumla Watu mbalimbali wametoa mada katika semina hiyo ambao ni Patrick Ngowi, Zeno Ngowi Msanii Mrisho Mpoto na Ndugu Zitto Kabwe mwenyewe.
MRISHO MPOTO AKITOA MADA KATIKA SEMINA HIYO DODOMA HII LEO


Mkurugenzi wa Maendeleo na Utafiti Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba akizungumza katika semina hiyo . Mkubwa Fella kutoka TMK akizungumza katika semina hiyoDJ Elly katikati Godzilla kushoto na Izo Busness wakiwa katika semina hiyo.Benny Kinyaiya akizungumza katika semina hiyo kulia ni Babu Tale na kushoto ni Said Bonge.Millad Ayo akizungumza Anold Kayanda akitoa mawazo yake.Ibrahim Masoud na washiriki wengine wakiwa katika semina hiyoDj fetty Afande sele akiwa na wenzie, kulia ni Shilole.
Khamis Mandi B12 akichangia Mada Gerlad Hando Shafii Dauda na Loveness Love 'Diva' wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika semina hiyo


Friday, May 10, 2013

TAARIFA MPYA YA WIZARA YA ELIMU KUHUSU MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mnamo tarehe 03 Mei, 2013 Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Wiliam Lukuvi (Mb) ilitoa Kauli ya Serikali Bungeni Kuhusu Taarifa ya Awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Sababu za kushuka kwa ufaulu wa Mtihani wa Kidato cha Nne Mwaka 2012.

Kauli ya Serikali ilielekeza kuwa matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012 yafutwe na yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011 ili Wanafunzi hao wawe katika mazingira yanayofanana na ya wenzao wa miaka iliyopita kwa kuwa mfumo uliotumika mwaka 2012 katika kupanga matokeo na madaraja ni tofauti na ule uliotumika mwaka 2011 na miaka iliyotangulia.

Kwa kuzingatia mapendekezo ya Tume na Maelekezo ya Baraza la Mawaziri, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kwar mamlaka aliyonayo chini ya Sheria ya Baraza la Mitihani Tanzania, kifungu cha 20, sura 107 ameliagiza Baraza la Mitihani la Taifa kupitia upya Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012.

Aidha, imeagizwa kwamba matokeo hayo yaandaliwe kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011. Serikali haikuagiza kufanyika upya kwa mitihani hiyo na wala haikuagiza kusahihishwa upya. Hivyo, Serikali inapenda kuwahakikishia wananchi kwamba hapatakuwa na zoezi la kurudia usahihishaji wa mtihani huo kwa sababu hakuna dosari zilizobainishwa kwenye usahihishaji wa mitihani hiyo.

Alama za watahiniwa ambazo zimehakikiwa zipo tayari, kitakachofanyika ni kwa Baraza la Mitihani kutumia alama hizo kuchakata matokeo upya kwa kutumia viwango vya ufaulu vilivyotumika mwaka 2011. Utaratibu ambao umekuwa ukitumika tangu mwaka 1973 wakati Baraza lilipoanzishwa, ni wa kuweka viwango vya ufaulu kila mwaka kwa kuzingatia ufaulu wa somo husika na ufaulu katika mwaka uliotangulia.

Kutokana na maelezo hayo, ni dhahiri kuwa zoezi la kupitia upya matokeo ya Kidato cha Nne 2012 litachukua muda mfupi na matokeo yatatangazwa hivi karibuni.

Selestine Gesimba

KAIMU KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
10/05/2013


HII NDIO BARUA YA FIFA ILIYOMLETEA MATATIZO SHAFFIH DAUDA

Mtandao wa shaffihdauda umeripoti kwa kuiweka barua halisi ya FIFA kwa TFF. Kitu ambacho TFF wamemjia juu Shaffih Dauda na kumpa siku saba aeleze ameipata wapi barua hii ya kiofisi.

MGOMO WA DALADALA WAITIKISA IRINGA LEO

Huko mjini Iringa, daladala za Manispaa hiyo zimegoma kufanya biashara leo kutokana na  kile  wamiliki na madereva  wanachodai ni kuchoshwa na manyanyaso ya Afisa mpya wa SUMATRA wa mkoa wa Iringa.

Francis Godwin katika blog yake anasema kiini cha mgomo huo ni kinatokana na kuchukizwa na uamuzi  wa SUMATRA mkoa wa Iringa kufuta stendi ya Posta pamoja na kuzuia daladala kukaa kwa muda katika eneo la stendi ya daladala ya Miyomboni maeneo ambayo walikuwa wakikaa siku zote, hivyo, madereva  hao wamesema hawatafanya kazi hadi hapo SUMATRA Iringa itakapofuta maagizo yake hayo.
Picture
Picture
Picture



KIBONZO: ANGALIA WACHEZAJI WA MAN U WAKIMLILIA FERGUSON NA BABA WA MWAKA

Kibonzo cha picha kinaco onesha wachezaji waMan U wakimlilia SAF
Huyu amepewa tuzo ya ubaba wa mwaka


Thursday, May 9, 2013

DAVIS MOYES NDIO KOCHA MPYA WA MANCHESTER UNITED KWA MIAKA 6 IJAYO


Hatimaye Manchester United imethibitisha DAVID MOYES ndio atakuwa kocha mpya wa kumrithi Sir Alex Ferguson kwa mkataba wa miaka 6.

Alex Ferguson jana alitangaza kustaafu kuifundisha timu hiyo aliyodumu nayo kwa takribani miaka 27 na akiwa anamtaja mrithi wake wake Fergie alisema: "Wakati tunajadili mtu wa kunirithi wote tulikubaliana kuhusu David Moyes.
"David ni mtu makini mwenye miiko ya kazi. Nimekuwa nikipenda ufanyaji wa kazi yake kwa muda mrefu na niliwahi kumshawishi mwaka 1998 ajiunge nami kuwa msaidizi wangu hapa. Akiwa kijana mdogo na akiwa ndio anaanza maisha yake ya ukocha na tangu wakati huo amekuwa akifanya kazi nzuri na klabu ya Everton.


"Hakuna swali kwamba ana kila ubora ambao tulikuwa tunautegemea kwa meneja mpya wa klabu hii.”- alisema Ferguson.

SOURSE: SHAFFIH DAUDA

PICHA ZA HUKUMU YA SHEIKH PONDA


Kama kawaida walikuwepo pia!

Akiwa na furaha baada ya hukumu yake kumalizika leo katika mahakama ya kisutu jijini dar es salaam
Akiteta jambo na baadhi ya watu!
Akihojiwa na mmoja wa waandishi wa habari!
Mhadhiri Maarufu wa Kiisilamu Sheikh Habibu Mazinge  (suti nyeusi) akimlaki Sheikh Ponda mara baada ya kuachiliwa huru.

Ponda akizungumza na waandishi wa habari.
"Kuna utaratibu umeandaliwa na jumuiya na taasisi za kiisilamu Tanzania tutawaita tutazungumza kwa pamoja lakini kikubwa ninachoweza kusema kwamba tumeshuhudia uonevu na dhulma tunayofanyiwa waislam nanyie ni mashuhuda hapa leo." Alisema.
Tutatoa tamko!
Kuna mengi yamejitokeza na wale waliokuwa wakiogopa sasa wamepata somo!

Safari ikaanza!


Akapewa ulinzi tena!

Akaingia kwenye gari!

Msafara ukavamiwa na wafuasi baada ya dereva wa gari lake kulisimamisha awasalimie wafuasi hao jambo ambalo polisi walikuwa hawalitaki na kuzua mabishano mazito kwenye mataa ya Maktaba Squire. 

Wafuasi wakajimwaga barabarani!

Takbirrrrrrrrrr!Allahu Akibarrrr!

Wafuasi wakivamia gari kumsalimia baada ya dereva wagari hilo kulisimamisha huku polisi wakimvamia aliondoe gari hilo haraka.
Walifukuza msafara huo hadi pale ulipotokomea!

Wananchi bado wakiwa na hamu ya kumuona mdai haki na kiongozi wao

Mpaka wamuone kiongozi wao
Msafara uliendelea kukimbizwa hadi walipotokomea mbali kwa spidi ya kubwa
Waumini wa dini ya Kiisilamu ambao walijitokeza kusikiliza hukumu ya kesi ya Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49, wakimbeba juu juu mmoja ya muumini mwenzao ambae alishtakiwa pamoja mara baada ya kushinda kesi hiyo kwenye mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
HATIMAYE katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiisilamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda na wafuasiwake 49 leo wameachiliwa huru na mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kufuatia kushinda mashtaka yote yaliyokuwa yakiwakibili. Hata hivyo Sheikh Ponda amehukumiwa kifungo cha nnje mwaka mmoja kutokana na utetezi wake kuonyesha kulikuwa na nia yakutenda kosa hilo.
Mara baada ya kutolewa hukumu hiyo mahakamani hapo pali ibuka shangwe za furaha kutoka kwa mamia ya wafuasi wake waliokuwa wamejazana karibu na eneo la Mahakama hiyo.
Pamoja na maelezo yote aliyoeleza Jaji aliyesoma hukumu hiyo alifafanua mambo mbalimbali kuhusu kiwanja kinachodaiwa na waisilamu hao.
1.Mahakama hiyo haina uwezo wakuzungumzia mmiliki halali wa kiwanja kutokana na masuala ya migogoro ya aridhi kuwa na mahakama yake ingawa imegundua kuna tatizo umiliki.
2.Upande wa Serikali hakuwa na hoja ya kisheria wala ushahidi wa kutosha wakuwatia hatiani watuhumiwa.
3. Hati ya Mashataka ilikuwa na mapungufu mengi ya kisheria.
4.Hakimu awaonyesha njia yakudai mali hiyo waisilamu kutokana na kile alichodai mali ya wakfu huwa haiuzwi wala haibadilishwi matumizi yaliyokusudiwa.
5.Upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha kwamba watuhumiwa waliopo mbele ya mahakama ni wafuasi wa sheikh Ponda. Awasihi Waisilamu kufuata taratibu za kisheria ili kuipata mali hiyo halali itumike kwa madhumuni yaliyokusudiwa.


Baada ya hukumu wafuasi wa sheikh Ponda wakitoka kwenye mahakama ya Kisutu.

Tumewashinda!




Furaha!
Machozi yalitiririka, Jazba na ahawali zikapanda!


Safari ya kuelekea Mtambani Kinondoni Ikaanza.
Hoyoooooooooo!




Mmoja wa ndugu wa mtuhumiwa akilia baada ya kumkumbatia ndugu yake kutokana na kushinda kesi hiyo.
"Pole ndio safari ya kusaka haki" Ndugu alisikika kabla ya kulia.


Waliopo kwenye majengo ya karibu wakatoka nnje kushuhudia!




Polisi wakiwa wamejipanga kwa tahadhari kwa lolote litakalotokea.


Waandishi nao walifanya mahojiano na baadhi ya washtakiwa na ndugu wa washtakiwa hao.
Ulinzi wa Ponda wakati wa kuondoka mahakamani hapo baada ya kuachiliwa.
Msafara wa ulinzi ukiondoka Kisutu!






 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU