Facebook Comments Box

Thursday, November 8, 2012

AZAM YASIMAMISHA WACHEZAJI BAADA YA KIPIGO CHA SIMBA

Azam imeonekana kuingia katika mgogoro na wachezaji wake mahiri kwa madai kuwa walipewa pesa ili kuihujumu timu yao ili ifungwe na simba. Timu hiyo ilifungwa 3 kwa 1 na simba. Wachezaji walio simamishwa ili kupisha uchunguzi ni 1. Erasto Nyoni 2. Said Moradi 3. Deograatius Munishi a.k.a Dida

MAHAKAMA KUU YATOA UAMUZI KESI YA LEMA

IMG-20121108-WA0007
IMG-20121108-WA0006
Baadhi ya wananchi, wapenzi wa Chadema wakimlaki Mh Lema mara baada ya kuwasili katika viwanja vya mahakama.
IMG-20121108-WA0004
Jopo la Majaji likiwa tayari kuanza kazi
IMG-20121108-WA0003Kutoka kushoto, Henry Kileo, Nuru Ndosi na Mh Godbless Lema
IMG-20121108-WA0002Henry Kileo akiwa ndani ya ukumbi wa Mahakama Kuu, Dar es Salaam
IMG-20121108-WA0005Katibu wa Chadema Kanda ya Kinondoni, Henry Kileo (kushoto) akibadilishana mawazo na mdau wa Chadema mara baada ya kuwasili viwanja vya Mahakama Kuu
IMG-20121108-WA0008
IMG-20121108-WA0009
Wananchi na viongozi wakiingia kuandikisha chumba cha mapokezi katika Ofisi ya Chadema Kinondoni, Dar es Salaam.
IMG-20121108-WA0010Picha tatu za mwisho, baada ya shauri kuamuliwa, Mh Lema akiwashukuru wananchi waliojitokeza katika ya ofisi ya Chadema  Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Pingamizi lililowekwa na upande wa wajibu rufani kupitia Wakili wao Alute Mughwai  ili rufaa ya Lema kupinga kuvuliwa ubunge isisikilizwe limetupiliwa mbali na Mahakama ya Rufaa baada ya kuridhika kwamba kosoro zilizolalamikiwa zilikuwa kwa upande wa Mahakama.
Pia kifungu kilichomhukumu Lema kina makosa hivyo kesi itatajwa tena baada ya siku 14 kwa ajili ya kuendelea kusikiliza hoja za walio kata rufaa.



Wadaiwa kwenye shauri hilo ni wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, waliofungua shauri lililotengua ubunge wa Lema wakidai kuwa wakati wa kampeni alimdhalilisha mgombea wa CCM, Dk. Batilda Burian kwa kutumia lugha za matu
Lema anawakilishwa na Wakili Method Kimomogoro, anayesaidiana na Tindu Lissu.


HATIMAYE DIRECTOR WA FILAMU YA KUMKASHIFU MTUME AHUKUMIWA

.
The man behind an anti-Muslim film that led to violence in the Middle East has been sentenced to one year in prison.
Mark Basseley Youssef, 55, was sentenced on Wednesday for violating probation stemming from a 2010 bank fraud conviction.
US District Court Judge Christina Snyder handed down the sentence after Youssef admitted four of eight alleged violations including obtaining a fraudulent California driver’s licence.
Youssef served most of a 21-month prison term in the bank fraud case. Federal authorities wanted Youssef to serve two years for the violations.
After he was released from prison, Youssef was barred from using computers or the Internet for five years without approval from his probation officer.
None of the violations had to do with the content of “Innocence of Muslims,” a film that depicts Mohammad as a religious fraud, pedophile and a womaniser.
The movie sparked violence in Libya and other parts of the Middle East, killing dozens. Enraged Muslims had demanded severe punishment for him, with a Pakistani cabinet minister even offering $100,000 to anyone who kills him.
Federal authorities have said they believe Youssef is responsible for the film, but they have not said whether he was the person who posted it online.
He also was not supposed to use any name other than his true legal name without the prior written approval of his probation officer.
At least three names have been associated with Youssef since the film trailer surfaced – Sam Bacile, Nakoula Basseley Nakoula and Youssef. Bacile was the name attached to the YouTube account that posted the video.
Court documents show Youssef legally changed his name from Nakoula in 2002, though when he was tried, he identified himself as Nakoula. He wanted the name change because he believed Nakoula sounded like a girl’s name, according to court documents.

Tuesday, November 6, 2012

HII NDIO SIRI NDANI YA SIMBA



Kipa wa Simba,Juma Kaseja.

KOCHA MKUU wa Simba, Milovan Cirkovic ameapa kuendelea kumtumia kipa Juma Kaseja mechi zote huku bosi wa makipa, James Kisaka naye akiweka wazi hali ya mambo na kilichotokea Simba ikaondoka kileleni mwa Ligi Kuu Bara.

Milovan ametamka hivi: "Sijui kitu gani tumekutana nacho maana tunarekebisha makosa kwenye mazoezi wakiingia uwanjani kwenye mechi wanarudia tena, nashindwa kuelewa."

Lakini Kocha wa Makipa, Kisaka amesema bao alilofungwa, Juma Kaseja na Hussein Javu wa Mtibwa Sugar na timu yake kulala mabao 2-0 juzi Jumapili ni makosa yake na sasa kazi aliyonayo ni kurudisha imani kwa mashabiki wake ingawa amesisitiza hajashuka kiwango na kuwataka mashabiki wakumbuke fadhila.

Milovan amesema ataendelea kumtumia kwenye kikosi chake kwa sababu anaamini ndiye kipa bora zaidi ya wote. Kisaka amesema kutokana na uzoefu wake na idadi ya mabao 10, Kaseja aliyofungwa katika mechi za Ligi Kuu Bara ni uzembe wa mabeki na makosa ya kawaida.

"Wanaposema, Kaseja ameshuka kiwango siyo kweli kwa sababu aina ya mabao aliyofungwa si makosa yake ni safu nzima ya ulinzi. Kwanza Simba ilikuwa na tatizo la beki, mabao yaliyofungwa yalikuwa yanasababishwa na beki. Pili, kumekuwa na makosa ya kutoelewana kwa safu nzima ya ulinzi," alisema Kisaka.

"Lakini hili la pili tulilofungwa na Mtibwa linaweza kuwa ni makosa yake kwa sababu alienda kucheza mpira kwa kupiga chenga na adui akatumia udhaifu mwanya huo kumnyang'anya na kufunga.

"Unajua mashabiki wamekuwa wakisubiri kuona ubaya tu wazungumze na hawakumbuki fadhila ambazo Kaseja alizifanya kwa kipindi chote cha ushindi. Kaseja alifanya juhudi binafsi tukashinda beki ilikuwa haieleweki lakini hilo hawajui na kuangalia kosa hili la leo na kumpa wakati mgumu kufanya kazi ya ziada ili kurudisha imani kwa mashabiki wake.

"Naamini, Kaseja ndiye kipa bora zaidi ya wote kikosini ndiyo maana nampa nafasi ya kudaka mechi zote, makosa yanatokea ni hali ya kawaida hata hivyo nitaendelea kumtumia kwenye mechi zangu," aliongeza Milovan.
Hata hivyo, Kaseja aliyekuwa katika wakati mgumu na huzuni, aligoma kuzungumza lolote.

Matokeo hayo ambayo yaliipa Yanga mwanya wa kuongoza ligi yalimtoa machozi Kaseja haswa baada ya mashabiki kuonyesha kutokuwa na imani naye na kumuimbia nyimbo za kumdhihaki.

Hali halisi
Kwa mujibu wa duru za ndani ya Simba, uwezekano wa Milovan kukaa benchi la ufundi kwenye mzunguko wa pili wa ligi ni mdogo kwa kuwa hajatimiza malengo ambayo uongozi ulimtaka kushinda mechi zote nne dhidi Azam, Polisi Morogoro, Mtibwa na Toto African.

Aliishinda Azam mabao 3-1, akatoa suluhu na Polisi kabla ya kufungwa mabao 2-0 na Mtibwa juzi Jumapili na Jumapili ana kibarua cha Toto jijini Dar es Salaam.

Msimu uliopita Moses Basena alitimuliwa Simba baada ya kumaliza mzunguko wa kwanza akiwa na pointi 28 wakati Milovan akishinda mechi ya mwisho atamaliza na 26.

Habari zinapasha kuwa viongozi wa juu wa Simba jana Jumatatu walijadiliana hali ya mambo ingawa hawakutaka kutoa ufafanuzi wowote.

Hali ya kutoaminiana na pia kutopendana kwa baadhi ya wachezaji, chokochoko za ndani ya uongozi imedaiwa kuwa ni chanzo cha matokeo hayo ingawa wachambuzi wa mambo wanaeleza sare za Simba ni kutokana na uchakavu wa viwanja na morali ndogo ya timu.

Simba imetoka suluhu mechi mbili za Tanga dhidi ya Coastal Union na JKT Mgambo, kabla ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu dhaifu na inayochukia kushinda mechi ya Polisi Morogoro na juzi juzi huko huko Morogoro ikapigwa mabao 2-0 na Mtibwa.

Habari za ndani zinadai baadhi ya wachezaji wamekuwa wakiogopana kwa imani za kishirikina na wengine hawaongei kabisa wala kupeana pasi uwanjani.

Habari zinadai pia hata kucheza mechi nyingi kwa Kaseja peke yake hakuwafurahishi baadhi ya wachezaji ambao wanadai amechoka ndiyo maana inafika wakati anafungwa magoli laini ambayo Wilbert Mweta asingefungwa.

Suala la Kaseja limeonekana gumu kwani viongozi pamoja na makocha wanamkubali mno na wala hawana mpango wa kumweka benchi licha ya kelele za wanachama.

Jingine kubwa ni kwamba baadhi ya wachezaji wanadai kocha Milovan anaingiliwa na baadhi ya viongozi ambao wanamlalamikia kwa kutotoa nafasi kwa wachezaji wengi vijana na badala yake kuendelea kung'ang'ania walewale.


KATIBU WA MUFTI ZANZIBAR AMWAGIWA TINDIKALI

Watu mbalimbali wakiaangalia Katibu wa mufti Zanzibar Fadhili Soraga akipelekwa Hospitali baada ya kumwagiwa Tindikali na watu wasiojulika. Katibu alikuwa akifanya mazoezi kwenye viwanja vya mwanakwerekwe

Hapa akipelekwa kwenye chumba cha huduma ya kwanza hospitali ya mwanakwerekwe

Hapa akipandishwa kwenye gari ili awahishwe Muhimbili Hospital dar es Salaam


MUUWAJI WA KAMANDA BAROW ALIHUDHURIA MAZISHI YAKE

POLISI mjini Mwanza imebaini kuwa mmoja wa watuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, alikwenda kuaga mwili wa Kamanda huyo katika uwanja wa Nyamagana sambamba na wananchi wengine. Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Lily Matola jana alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Abdallah Petro ‘Ndayi’ (32) mkazi wa Mjimwema mjini hapa ambaye anashikiliwa Polisi. Kwa mujibu wa Kamanda Matola, Petro mbali na kutajwa kuhusika na mauaji hayo, pia anadaiwa kuwa na rekodi ya kufungwa miaka 30 jela katika gereza la Butimba kwa unyang’anyi wa kutumia silaha mwaka 2006. Alitoka gerezani mwaka 2010 baada ya kukata rufaa Mahakama Kuu ya Tanzania. Petro pia imebainika pia kuwa ni mdogo wa mtuhumiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Muganyizi Peter. Vielelezo vyakamatwa Kamanda Matola alisema mbali na kuwa na uhusiano huo, Petro na mtuhumiwa mwingine, Abdurahim Ismail Athuman ‘Dula’ (28) mkazi wa Mkudi Ghana, pia mjini hapa, baada ya kukamatwa kwa nyakati tofauti Mjimwema na Kilimahewa mwishoni mwa wiki, waliwapeleka polisi mahali walikoficha baadhi ya mali za marehemu. Mali wanazodaiwa kuonesha polisi ni pamoja na redio ya mawasiliano ya Polisi na funguo za gari alilotumia kamanda Barlow siku ya tukio la mauaji yake. Kamanda Matola alisema watuhumiwa waliwapeleka polisi katika shimo la majitaka kwenye maeneo ya Nyanshana, jijini Mwanza walipokuwa wameficha vitu hivyo. Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Joseph Konyo alisema watuhumiwa baada ya kutimiza uhalifu, walitenganisha redio hiyo ya mawasiliano ili isipatikane. “Damu ya mtu haipotei bure, hayo yote ni pamoja na Mungu mwenyewe, kwani sisi peke yetu hatuwezi, wananchi mmetusaidia sana,” alisema Kamanda Konyo. Baada ya kuonesha polisi vitu hivyo ambavyo sasa vimechukuliwa kama vielelezo katika kesi ya mauaji ya Barlow, Kamanda Matola alisema watuhumiwa hao walipekuliwa na kukutwa pia na kadi tatu za simu za Vodacom na Airtel, simu ya mkononi, viatu vya ngozi na begi dogo. Pia walikutwa na kofia mbili za kijeshi aina ya bereti; moja ikiwa ya Polisi na nyingine ya kampuni ya binafsi ya ulinzi, sare za kampuni ya ulinzi, mtarimbo, bisibisi, mapanga, televisheni mbili, sub-hoofer na deki. Alisema walipohojiwa, walidai wamekuwa wakihifadhiwa na Ryoba Matiku ‘Mama Nyangi’ katika eneo la Nyakabungo Miembeni ambako mipango yote ya uhalifu imekuwa ikisukwa. Mama huyo anashikiliwa pia kwa mahojiano.

HATIMAYE SERIKALI YASEMA TPI WALITENGENEZA ARV FEKI

LICHA ya wamiliki wa kiwanda cha Tanzania Pharmaceutical Industries Limited (TPI) kukana kutengeneza na kusambaza dawa bandia za kupunguza makali ya UKIMWI, serikali imethibitisha kuwa kiwanda hicho ndicho kilitengeneza dawa hizo aina ya TT-VIR 30 yenye toleo Na OC.01.85. Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid, akisema kuwa serikali itawachukuliwa hatua za kisheria wote waliohusika katika suala hilo. Alisema kuwa katika kuhakikisha kuwa suala hilo hatari linapatiwa ufumbuzi wa kudumu na kuzuia lisitokee tena, kabla ya kuchukua hatua hizo za kisheria uchunguzi unafanywa kupitia vyombo vya usalama. Dk. Rashid alikiri kuingia katika mzunguko kwa dawa hizo bandia lakini akawatoa hofu wagonjwa wote wanaotumia (ARV’s) kuwa dawa zinazopatikana kwenye vituo vya kutolea huduma hiyo kwa sasa ni salama na zenye viwango vinavyotakiwa. “Tunatoa wito kwamba waendelee kutumia dawa hizo kama wanavyoshauriwa na madaktari… kupitia Wizara ya Afya, serikali imehakikisha uwepo wa dawa za kutosha na kupunguza makali ya ukimwi katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya,” alisema. Dk. Rashid alifafanua kuwa Wizara ya Afya hununua dawa hizo kupitia Bohari ya Dawa (MSD), ambayo imepewa jukumu la kununua, kuzitunza na kusambaza katika vituo vya kutolea huduma za afya. Alisema kwa hapa nchini kuna kiwanda kimoja tu cha TPI kinachotengeneza dawa hizo na kwamba zile za bandia zilibainika mwanzoni mwa Agosti mwaka huu katika ukaguzi wa kawaida wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) katika Hospitali ya Tarime. Alisema baada ya ukaguzi na uchunguzi kwenye vituo vyote vya huduma za afya katika mkoa wa Mara na nchi nzima ilibainika kuwa dawa yenye jina la biashara TT-VIR 30 toleo namba 0C.01.85 ni bandia. Alisema pia ilibainika kuwa nyaraka zilizokutwa katika Bohari ya Dawa (MSD) zinaonyesha kuwa TPI iliiuzia MSD dawa hiyo bandia toleo namba 0C.01.85. Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa uchunguzi ulibaini kuwa dawa hiyo bandia ilikuwa na dawa zenye rangi tatu tofauti, njano, nyeupe na vidonge vya rangi mbili tofauti za pinki na nyeupe. Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo wa Afya, dawa zilizokuwa na rangi ya njano, zilikuwa na kiambata cha Efaverenz badala ya viambata aina ya Nevirapine, Lamivudine na Stavudine vinavyopaswa kuwemo. Aidha vidonge vyenye rangi nyeupe na vile vyenye rangi ya pinki na nyeupe vilikuwa na viambata vinavyotakiwa kuwepo yaani Nevirapine, Lamivudine na Stavudine kama ilivyokuwa kwenye lebo. Akielezea kuhusu hatua zilizochukuliwa na serikali baada ya matokeo hayo ya uchunguzi alisema ni pamoja na kusimamisha mara moja matumizi ya dawa hizo aina ya TT-VIR 30 toleo Na 0C.01.85. Hatua nyingine ni pamoja na kusitisha uzalishaji wa dawa zote katika kiwanda cha TPI Ltd hadi uchunguzi wa suala hilo utakapokamilika ikiwa ni pamoja na kujiridhisha tena ubora wa dawa inazozalisha. Alisema pia vigogo wa MSD akiwamo mkurugenzi wake walisimamishwa na kwamba wizara imeunda timu ya wataalamu kwa lengo la kufuatilia mwendelezo wa tiba na matunzo kwa wagonjwa wa UKIMWI.

Sunday, November 4, 2012

YANGA NA AZAM KATIKA PICHA

Kiiza akijaribu bila mafanikio kufunga

Aggrey Morris akiruka juu ya Paul Ngalema kupiga mpira kichwa

Mbuyu Twite akimuacha chini Salum Abubakar

Kiiza akimtoka Hajjji Nuhu

Haruna Niyonzima 

Chuji akijadiliana na Niyonzima kabla ya kupigwa kwa mpira wa adhabu

Kiiza alivyomuenzi Mafisango

Mwadini akidaka mpira hewani 

Simon Msuva anateleza

Mwadini akiruka kupangua mpira

Msuva

Hatari kwenye lango la Yanga

Jabir Aziz akimdhibiti Chuji

Kiiza anapasua katikati ya Ibrahim Shikanda kulia na Sure Boy kushoto 

Nadir Haroub 'Cannavaro' akimdhibiti John Bocco

Hatari kwenye lango la Yanga

Stewart Hall alitia huruma

Frank Domayo kulia akipambana na Aggrey Morris

Niyonzima akipiga shuti mbele ya Shikanda

Twite anapasua

Sure Boy akimtoka Twite

Sure Boy na Twite

Chuji akipiga kisu mbele ya Sure Boy

Msuva anatafuta njia

Shughuli

Yanga wakipiga ndiki kabla ya mechi

Kikosi cha Azam leo

Kiiza anamtoka Erasto Nyoni

Kikosi cha Yanga leo

Hatari kwenye lango la Azam

Hatari kwenye lango la Yanga

Msuva akiwasalimia wenzake benchi baada ya kupumzishwa

Niyonzima kushoto, Nyoni kulia

Kiiza na Hajji Nuhu


Kiiza baada ya kufunga bao la pili


Kavumbangu wa pili kutoka kushoto, akishangilia bao lake na wenzake

Kavumbangu wa kwanza kushoto


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU