Facebook Comments Box

Saturday, July 12, 2014

AJALI ENEO LA UBUNGO MATAA MUDA HUU

Gari la mchanga lililokuwa likitokea maeneo ya kimara limemshinda dereva wakati wa kukata kona kutoka barabara ya Morogoro kuingia barabara ya Mandela hapa eneo la Ubungo. Hakuna mtu aliye fariki bali ni majeraha machache kwa dereva.




Friday, July 11, 2014

DIAMOND PLATNUMZ APOKELEWA KWA SHANGWE NA BASHASHA AKITOKEA MAREKANI

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya hapa Tanzania maarufu kama Bongo Fleva Naseeb Abdulmalik a.k.a Diamond Platnumz aliwasili jana tarehe 10/07/2014 akitokea Marekani alikokwenda kwa ajili ya kushiriki katika tuzo za BET ambazo hufanyika kila mwaka.

Diamond alikua katika kategori ya Best African Act ambayo ilichukuliwa na Davido kutoka Nigeria na yeye kuishia kupata cheti cha ushiriki ambapo kwake sio vibaya maana anaamini huo ni mwanzo mzuri kwake wa kuelekea katika mafanikio.


Baada ya kuwasili Diamond aliwashukuru wote waliofika kumpokea na kusema kuwa safari yake ilikuwa nzuri na amejifunza mambo mengi sana pia amekutana na watu wengi na tutarajie mengi mazuri katika muziki wetu.

Na kwa upande mwingine alitoa shukran za dhati kabisa kwa watanzania kuipokea vema video yake mpya ya mdogomdogo, ambayo inafanya vema kwenye vituo vya luninga hapa nchini kwa sasa.


Tuesday, July 8, 2014

BOMU LALIPUKA ARUSHA NA KUUWA NA KUJERUHI

Taarifa zilizotufikia za kusikitisha zinasema kwamba kumetokea mauwaji katika mgahawa wa Wama ulioko Gymkhana jijini Arusha (Pichani chini). Tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku wa kuamkia leo na kusababisha watu zaidi ya 8 kujeruhiwa vibaya, idadi ya waliopoteza maisha bado haijajulikana, majeruhi wote wamepelekwa katika hospitali ya Seliani jijini Arusha.




Thursday, July 3, 2014

MTOTO AFUNGIWA KWENYE BANDA LA MBUZI KWA MIAKA 10

Mwenyekiti wa Umoja wa Watu wenye Ulemavu Kenya, David Sankok akionyesha hali halisi ya maisha ya mtoto huyo kabla ya kuokolewa. Picha na Ndaya Mgoyo Juni 21 ilikuwa ni siku ya kawaida kwa Mama Nancy mkazi wa Narok nchini Kenya, lakini ilifichua siri nzito ya mtoto aliyefichwa kwa miaka kumi katika banda la mbuzi.Akiwa katika shughuli zake za nyumbani, mara akatokea mtoto mdogo wa jirani yake aitwaye Jane. 
     
Binti huyo akaanza kucheza na wenzake kwa dakika kadhaa na mara akaacha michezo na kuanza kukimbia kuelekea nyumbani kwao.Wenzake wakamuuliza “mbona unakimbia wakati bado tunacheza”. Akajibu, “nakwenda kwenye banda la mifugo kumpa chakula Ben. Muda umekimbia na hakuna mtu nyumbani”.Kwa kauli hiyo, mwanamke huyo alitaka kujua iwapo Ben anaishi kwenye nyumba ya jirani yake kwani ni miaka 10 imepita tangu amtie machoni.“Ben yupo na anaishi kwenye banda la mifugo. Huwa anahudumiwa na mama, lakini kwa sasa mama hayupo na baba amekwenda kazini. Mimi nina jukumu la kumpa chakula,” alijibu Jane.

Mama huyo akapata shauku ya kumtembelea mtoto huyo kuona kinachoendelea kwa jirani zake, Lo! anachokiona haamini macho yake; Mtoto Ben amefungwa kwa kamba kwenye kigodoro chembamba akiwa hajiwezi kwa njaa. Hivyo ndivyo alivyoibuliwa mtoto Ben baada ya kukaa katika banda la mbuzi kwa muda wa miaka 10 bila majirani kufahamu. 

Ben, ambaye kwa sasa ana miaka   miaka 14 alizaliwa akiwa kiziwi, bubu   na ulemavu. Aibu ya kuzaa mtoto kama huyo ndiyo ilifanya wazazi wake wamfungie kwenye zizi la wanyama kwa muda wa miaka 10 na wakihakikisha  hakuna jirani wala ndugu wa karibu anayefahamu juu ya tukio hilo. Historia ya mtoto huyo Kwa mujibu wa baba mlezi Mr Jeremiah Mbusia,  ambaye ni askari katika Wizara ya Mali Asili, Narok Kenya, mtoto  huyo siyo wake wa
kuzaa bali alifika katika nyumba hiyo miaka 12 iliyopita akiwa na mama yake wakati huo mtoto huyo alikuwa na miaka minne.

 Alilelewa katika nyumba hiyo kwa miaka miwili na ndipo wazazi wake, yaani baba yake wa kambo na mama yake mzazi wakaamua kumuweka katika kibanda kidogo nje ya nyumba yao  na hutumiwa
kama zizi la mbuzi na kondoo. Maisha ndani ya  zizi Akiwa kwenye zizi mtoto huyo aliwekewa godoro ukutani na mkono wake mmoja ulifungwa kwa kamba ukutani. Ilikuwa ni vigumu kuvumilia harufu kali kutoka katika zizi hilo kwani kulikuwa na mchanganyiko wa kinyesi na mikojo ya binadamu na wanyama.

Wadogo zake Ben walisema kuwa wazazi wao huwa wanamsafisha mtoto huyo wakati wowote wanaotaka na kuwa anaweza kushinda na kinyesi au kulala nacho. “Ni mara chache kukuta akisafishwa   mara mbili kwa siku. Kwa kawaida husafishwa mara moja tu na wakati mwingine hasafishwi kabisa,” alisema mtoto huyo. 

Kwa nini ilikuwa rahisi kujulikana? Ugunduzi wa mtoto huyo ulitokana na ukweli kwamba mama yake aliamua kuondoka nyumbani na kuacha familia nzima kutokana na ugomvi na mume wake. Mama huyo alikuwa akifanya siri ya kulinda mtoto huyo asijulikane hapo nyumbani na alipoondoka watoto wenzake ndiyo walikuwa na jukumu la kumlisha mwezao. Kauli ya baba mlezi Kwa kujibu wa baba wa kambo, mama wa mtoto huyo alikuwa hamtaki mwanaye kwani aliamini kwamba kuishi naye ni kuongeza mikosi.

 Baada ya kuishi pamoja walijikuta wakiwa wamezaa watoto watatu na mama huyo aliona kuwa watoto hao ndio walikuwa muhimu katika maisha yake kuliko Ben, ambaye alimzaa na mwanaume mwingine kabla ya kuolewa katika ndoa rasmi. “Mama yake alikuwa hampendi na hata wazo la kumweka katika banda lilitoka kwake. Aliamini kuwa kukaa naye ndani kama watoto wa kawaida ilikuwa ni usumbufu na akitoa visingizio kwamba akikaa ndani anaweza kuvunja vitu na kuwa anaweza kushika vitu vya hatari kama vile moto,” alijitetea baba mlezi wa Ben. 

“Tulikosana na mama watoto kwa ugomvi wa kawaida tu katika familia, hiyo ilikuwa ni miezi minne iliyopita, ajabu ni kwamba amenikimbia na kuniachia familia akiwamo mtoto mlemavu.”

“Nashindwa kumlea vizuri kwa kuwa natakiwa kwenda katika mihangaiko yangu ndiyo maana wadogo zake walikuwa wakimhudumia wakati sipo.” Imefahamika kuwa mwanamke huyo amekimbilia kwao eneo la Rimuru, Kenya ambapo ni kwa wazazi wake na akiwaambia jamaa zake wa karibu kuwa hawezi kurudi katika nyumba ya mume wake kwani hawapatani. 

Kauli za majirani Majirani wanasema walikuwa wakifahamu kuwa nyumbani kwa jirani yao kuna mtoto mwenye ulemavu wa akili lakini hawakumwona kwa muda mrefu. 

“Tulikuwa tukifahamu kwamba kuna mtoto mlemavu wa akili lakini katika kipindi cha miaka 10 iliyopita hatukumwona. Tulidhani wamemhamishia sehemu nyingine. Ilikuwani vigumu kusikia sauti
kwa kuwa mtoto mwenyewe ni bubu na kiziwi,” alisema jirani mmoja. Kumuokoa Ben Baada ya majirani kupata taarifa za kuwepo kwa mtoto huyo, walimuita mwandishi wa habari mmoja ili kushuhudia hali halisi.

Mwandishi huyo alitoa taarifa polisi na pia kwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Kenya, Dk David Ole Sankok na kwa pamoja walivamia katika nyumba hiyo iliyopo Fanaka Estate, Narok na kumwokoa mtoto huyo katika mateso.

 Baada ya kumtoa kwenye kibanda hicho waligundua kuwa hali ya mtoto huyo haikuwa nzuri kwani alikuwa amepooza upande mmoja wa kushoto kutokana na kulala kwa muda mrefu, viungo vyake vilikuwa vimejikunja kutokana na kukosa lishe kwa siku nyingi na nywele zake zilibadilika rangi kutokana na kutokaa kwenye mwanga wa jua kwa muda mrefu. “Alikuwa akitoa harufu kali, ilikuwa ni vigumu hata kumsogelea, lakini kwa kuwa tulikuwa tumedhamiria kumwokoa ilibidi tufanye hivyo,” akasema Dk Ole Sankok. “Tulimkuta katika mateso makubwa sana, eneo alilokuwa amelala lilikuwa na kunguni, chawa na viroboto wengi,” anasema.

Anaongeza kuwa wadudu hao walipokuwa wakimsogelea kinywani
alikuwa akiwatafuna na kuwameza kwani alikuwa na njaa muda wote.“Nilipoona hali hiyo nilijaribu kuondoa viroboto waliokuwa karibu na mdomo wake, kwa kuwa alikuwa amewazoea sana na aliona ni kama kitoweo chake alitoa sauti ya ukali kuashiria kwamba nisiwatoe, nilipojaribu kuwatoa kwa nguvu alitaka kuniuma kwa meno,” alisema daktari huyo. 

Wazazi wa kijana huyo walikuwa hawaaniki godoro nje kwani
hawakua na jingine la kumtandikia pia walihofia majirani huenda wangehoji. Huduma ya kwanza Baada ya kugunduliwa, Ben alipelekwa katika Hospitali ya Mji wa Narok kwa ajili ya matibabu. Alipewa huduma za haraka ikiwa ni pamoja na huduma za kurudisha afya mwilini kwa vyakula vya protini na vitamini.

 Vilevile alikuwa akianikwa juani mara kwa mara kwa lengo la kumrudishai vitamini. Kwa kuwa mgongo wa mtoto huyo ulianza kutoa vidonda alipewa matibabu ya vidonda. “Mtoto huyo alikuwa amepungua mwili kwa kiasi kikubwa  ilikuwa unaweza kumbeba kama mtoto mdogo. Hata   rangi yake ya ngozi ilibadilika,” alisema Dk Sankok, ambaye pia anaendesha kliniki binafsi katika mji wa Narok. “Licha ya kuwa na umri wa miaka 14 alikuwa na kilo 15 pekee,” aliongeza.

Sankok aliwahakikishia watu waliomzunguka mtoto huyo kwamba
atamfikisha katika kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa akili na viungo na atampa mazoezi ya kutosha kuhakikisha anarudi
katika hali ya kawaida.

“Unajua kuna wazazi ambao wana kawaida ya kuwaficha watoto
wao kwa sababu wana matatizo ya viungo ama   ya akili. Hilo siyo
jambo zuri hata kidogo, watoto kama hao ni binadamu wa kawaida
na wanatakiwa kulelewa kwa misingi yote ya kibinadamu,” anasema.

Anasema kama mzazi anaona hawezi kumhudumia mtoto kama
huyo ni bora amfikishe katika vituo vya kulea watu wa aina hiyo
kuliko kumficha ndani na kumpa mateso makubwa.
Chanzo: Mwananchi


AZAM WASAJILI MSHAMBULIAJI WA HAITI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Haiti, aliyecheza Kombe la Mabara mwaka jana nchini Brazil, Leonel Saint-Preux ametua Azam FC kwa ajili ya kujiunga nayo kwa msimu ujao.

Kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon amesema amekuwa na mchezaji huyo kwa siku mbili na atahitaji muda zaidi kumuona kabla ya kuamua kumsajili au la. Mshambuliaji huyo aliyezaliwa Machi 12, mwaka 1985 in Cap-Haitien mara ya mwisho alichezea klabu ya FELDA United F.C. ya Ligi Kuu ya Malaysia.

Preux alianzia Zenith ya kwao,ambako alikuwa mfungaji mzuri katika Ligi ya nchini humo. Saint-Preux alisaini Minnesota Thunder ya Daraja la Kwanza Marekani Aprili 15, mwaka 2009, kabla ya kuhamia Hanoi ya Vietnam.

Machi 2010 alisiani mkataba wa awali na Aztex, lakini akatemwa baada ya kufeli vipimo vya afya. Kimataifa Saint-Preux, alianzia kuchezea timu za vijana za Haiti wa umri tofauti. Alikuwemo kwenye kikosi cha Haiti kilichofuzu michezo ya Olimpiki mwaka 2008 mjini Beijing, akifunga bao la kukumbukwa kutoka umbali wa mita 40 timu yake ikishinda 2-1 dhidi ya Canada.

Alianza kuchezea timu ya wakubwa ya Hati mwaka 2007. Alifunga
bao lake la kwanza timu ya taifa ya Haiti Novemba 19, mwaka 2008 katika sare ya 1-1 Surinam. Haiti ilifungwa 10-0 na Hispania kwenye michuano.
Hii ndio mechi ambayo Haiti ilitandikwa goli 10 kwa 0 mshambuliaji huyu wa azam anaonekana akikabwa na beki ya Hispania ambayo imeonesha udhaifu mkubwa kwenye kombe la dunia linalo endelea Brazil hivi sasa. Katika mechi hiyo mshambuliaji huyu mpya wa azam hakuweza kumsaidia timu yake kabisa.
CHANZO: BIN ZUEIRY


Wednesday, July 2, 2014

MAJAMBAZI WASHAMBULIA BASI LA MAGEREZA

Chini ni picha ambazo  ni tukio lilotokea hivi punde maeneo ya mikocheni ilipo TMJ hospitali wanaposema kuwa majambazi walikuwa wakishambulia gari lililo mbele ya basi la magereza. Wakadhani kwenye basi lile kutakuwa na askari mwenye silaha wakalishambulia na basi hilo la magereza.

Basi lilikuwa lilotokea mahakama ya kawe ambapo hupelekwa kesi ndogo ndogo. Majambazi hao wamemuumiza askari mmoja wa kike na hakuna mahabusu alie toroka. 





Sunday, June 29, 2014

TUKIO LILILOMSABABISHIA LUIS SHUAREZ AFUNGIWE MICHEZO TISA NA FAINI HILI HAPA

Accident? Luis Suarez told FIFA he did not deliberately bite Giorgio Chiellini but fell on top of him Shuarez akifanya yake

Big miss: FIFA have been formally informed of Uruguay's appeal against Suarez's ban
Time: The Uruguay football federation will now have a further seven days to prepare paperwork for the appeal
Painful: Suarez fell to the ground and held his teeth straight after the encounter with centre back ChielliniSuarez na Chiellini wakiwa chini baada ya tukio.
Evidence: Chiellini looked outraged as he showed the referee the apparent point of impact on his shoulderChiellini akionesha sehemu aliyopigwa jino na Luis Shuarez.


BRAZIL YAFANIKIWA KUINGIA ROBO FAINALI KWA KUITOA TIMU NGUMU YA CHILE HUKU COLOMBIA NAYO IKIIFUNGISHA VIRAGO URUGWAI.


Kikosi cha Brazil kimefanikiwa kuingia katika hatua ya robo fainali baada ya kuiondoa timu ngumu ya Chile kwa mikwaju ya penati 3-2. awali timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 na hata zilipoongezwa dakika 30 bado mchezo huo ulikuwa na matokeo hayo hayo ndipo wakaingia kwenye mikwaju ya penati na ndipo Brazil wakaibuka kidedea.
Wild emotion: Brazil's players celebrate their dramatic 3-2 penalty shootout against Chile in the last 16
Wachezaji wa Brazil kama wanavyoonekana wakishangilia ushindi wao baada ya kuitoa timu ngumu ya Chile kwa mikwaju ya penati 3-2.

Conflicting emotions: David Luiz celebrates Brazil's win in front of a backdrop of a crestfallen Chile
David Luiz akishangila nyuma ya wachezaji wa Chile wakati wao wakiwa wameshika viuno hawaamini yaliyotokea.
Broken: Alexis Sanchez feeling the pain after missing in the shootout
Alexis Sanchez akiwa na maumivu ya kukosa penat kama anavyoonekana amejilaza chini.

Embrace: Brazil heroes Julio Cesar and David Luiz getting emotional in their celebrations
Luiz na Cesar wakikumbatiana kwa furaha


Embrace: Neymar struggles to hold back his emotions as he hugs his boss Luiz Felipe Scolari
Neymar na Scolari wakikumbatiana kwa furaha iliyopita kifani

Dejection: Chilean players slump to the floor after their heartbreaking defeat
Chile hawaamini kabisa kilichotokea

Emotive: A Chilean couple cry whilst Brazilian fans celebrate around them

Contrast: Chile players forlorn whilst Brazil's stars celebrate

Lost: Arturo Vidal looks on dejected after his side's dramatic defeat

Crucial moment: Gonzalo Jara (left) watches on as his penalty strikes the post and eliminates Chile
Gonzalo Jara akitazama Penati yakeinavyokwenda kugonga mwamba na kutoka nje na ndiyo penati iliyowatoa Chile kwenye mashindano

Distraught: Heartbroken Chile applaud their devastated fans inside the Estadio Mineirao after losing to Brazil

Safe hands: Julio Cesar saved two penalties for Brazil to help them reach the World Cup quarter-finals

Hero: Cesar (centre) was hoisted high by Brazil's players in amongst the wild celebrations in Belo Horizonte

In it to win it: Midfielder Paulinho (centre) rallies the Brazil squad before the shootout against Chile
Paulinho akiwapa wenzake mbinu za kupata ushindi kwenye mikwaju ya penati. 

Colombia nayo imeifungasha virago Urugway kwa kichapo cha 2-0 na kutinga robo fainali.
Contact: Rodriguez connects with the ball brilliantly on the volley after letting it drop from his chestRodriguez akiunganisha mpira ambao aliutuliza kifuani kabla ya kuachia fataki na kuandika bao la kwanza kwa nchi yake ya Colombia.
Volley: Diego Godin tries in vain to stop Rodriguez's rocket as it flies towards goal Diego Godin na wenzake wa Urugway wakijaribu kumziwia muuwaji wao jana katika mechi kati ya Colombia na Urugway Rodriguez's.
Helpless: Fernando Muslera can do nothing to stop Rodriguez's goal-bound strikeFernando Muslera akishindwa kabisa kuuziwia mpira ambao ulikuwa unaingia nyavuni na kuiandikia Colombia bao la kwanza kama unavyo jionea hapo pichani.
Ecstatic: Rodriguez peels away after seeing the ball bounce down and into the net after hitting the crossbar  Rodriguez akiipatia Colombia bao la pili

Chanzo:Daily Mail



Saturday, June 28, 2014

MWEZI WA RAMADHAAN NI MWEZI AMBAO QURA'N ILISHUKA:TUCHUME THAWABU HIZI

Mwezi Wa Ramadhaan Imeteremshwa Qur-aan - Jichumie Fadhila Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan
    Nasiha Za Minasaba Mbalimbali
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) 
(( شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ))
((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi)) [Al-Baqarah: 184]
Ndugu Muislamu, jitahidi ufanye ibada hii adhimu usome na kuhifadhi Qur-aan kwa wingi kabisa kwani thawabu na fadhila zake ni nyingi na adhimu mno kama tunavyozinukuu humu. Pia jitahidi uweze kuhitimisha (kumaliza kuisoma) japo mara moja Qur-aan nzima kabla ya mwezi wa Ramadhaan kwisha. 
Zifautazo Ni Fadhila Mbali mbali Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan:
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)   
(( الَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ يَتْلُونَهُ حَقَّ تِلاَوَتِهِ أُوْلَئِكَ يُؤْمِنُونَ بِهِ))
((Wale tuliowapa Kitabu, wakakisoma kama ipasavyo kusomwa, hao ndio kweli wanakiamini)) [Al-Baqarah:121]
KUFANYA BIASHARA NA ALLAAH YENYE FAIDA TELE NA ISIYOANGUKA
Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)
   
(( إِنَّ الَّذِينَ يَتْلُونَ كِتَابَ اللَّهِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَأَنفَقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً يَرْجُونَ تِجَارَةً لَّن تَبُورَ )) (( لِيُوَفِّيَهُمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ إِنَّهُ غَفُورٌ شَكُورٌ))
((Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na wakasimamisha Swalah, na wakatoa kwa siri na kwa dhaahiri katika Tulivyowaruzuku, hao hutaraji biashara isiyododa (isiyoanguka))) ((Ili Yeye Awalipe ujira wao kwa ukamilifu, na Awazidishie kutokana na fadhila zake. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe Mwenye shukrani)) [Faatwir: 29-30]
MTU BORA KABISA NI MWENYE KUJIFUNZA NA KUIFUNDISHA
عن عثمانَ بن عفانَ رضي الله عنه أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلّم قالَ  )) خَيرُكُم مَنْ تعَلَّمَ القُرآنَ وعَلَّمَه))   صحيح البخاريِّ
Imetoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhiya Allahu 'anhu)   kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema ((Mbora wenu ni yule mwenye kujifunza Qur-aan kisha akaifundisha)) [Al-Bukhariy]
THAWABU MARA MBILI KWA MWENYE KUISOMA KWA MASHAKA
(Mwenye ulimi mzito au tabu ya kufahamu kwa haraka, lakini inambidi Muislamu ajitahidi kujifunza kuisoma sawa sawa)
عن عائشة رضي الله عنها أنَّ النبي صلى الله عليه وسلّم قال  الماهرُ بالقرآن مع السَّفرةِ الكرامِ البررة،  والذي يقرأ القرآنَ ويتتعتعُ فيه وهو عليه شاقٌّ له أجرانِ)) البخاري ومسلم
Imetoka kwa 'Aisha (Radhiya Allahu 'anha)   kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema, ((Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur-aan atakuwa pamoja na Malaika  Waandishi wa Allaah watukufu wacha Mungu, na yule ambaye anaisoma Qur-aan kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa  atapata ujira mara mbili))  [Al-Bukhaariy na Muslim]  
WATU WA QUR-AAN NI WATU BORA KWA ALLAAH (SUBHAANAHU WA TA'ALA)
  عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: (( إِنَّ لِلَّهِ أَهْلِينَ مِنْ النَّاسِ)) قَالُوا يَا رَسُولَ اللَّهِ مَنْ هُمْ قَالَ:  ((هُمْ أَهْلُ الْقُرْآنِ أَهْلُ اللَّهِ وَخَاصَّتُهُ)) أحمد و إبن ماجه
Imetoka kwa Anas (RadhiyaAllaahu  'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema ((Allaah Anao watu Wake wa karibu katika watu)).  Wakamuuliza, ewe Mjumbe  wa Allaah, nani hao? Akasema: (( Hhao ni watu walioiandama Qur-aan na ni  watu waliokuwa bora kabisa wa Allaah))  [Ahmad, na Ibn Maajah]   
          TOFAUTI YA ANAYEISOMA NA ASIYEISOMA QUR-AAN
عن أبي موسى الأشْعَريِّ رضي الله عنه أنَّ النَّبي صلى الله عليه وسلّم قالَ ((مثلُ المؤمنِ الَّذِي يقرأ القرآنَ مَثَلُ الأتْرُجَّةِ ريحُها طيبٌ وطعمُها طيّبٌ، ومثَلُ المؤمِن  الَّذِي لاَ يقرَأ القرآنَ كمثلِ التمرة لا ريحَ لها وطعمُها حلوٌ )) البخاري ومسلم
Kutoka kwa Abu Musa Al-Ash'ariy (Radhiya Allahu 'anhu)   kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema ((Mfano wa Muumini ambaye anayesoma Qur-aan ni kama tunda la Utrujjah harufu yake nzuri na ladha yake nzuri.  Na mfano wa Muumini asiyesoma Qur-aan mfano wake kama tende zisizokuwa na harufu lakini zina ladha tamu)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
THAWABU KWA KILA HERUFI MOJA
عن عبدالله بن مسعودٍ رضي الله عنه أن النبيَّ صلى الله عليه وسلّم قال: (( من قَرأ حرفاً من كتاب الله فَلَهُ به حَسَنَةٌ، والحسنَةُ بعشْر أمْثالها، لا أقُول الم حرفٌ  ولكن ألفٌ حرفٌ ولاَمٌ حرفٌ وميمٌ حرفٌ))  رواه الترمذي.
Imetoka kwa 'Abdullahi Bin Mas'uud (Radhiya Allahu 'anhu kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema, ((Atakayesoma herufi moja katika kitabu cha Allaah atapata hasanah (jema) moja, na kila hasanah moja ni sawa na thawabu kumi, wala sisemi 'Alif-Laam-Miym' ni herufi moja, bali Alif ni herufi moja na Laam ni herufi moja na Miym ni herufi moja))  At-Tirimidhiy
KIOMBEZI SIKU YA QIYAAMAH
عن أبي أمَامةَ رضي الله عنه أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلّم قال:   ((اقْرَؤوا القُرآنَ فإنه يأتي يومَ القيامةِ شفيعاً لأصحابهِ)) مسلم
Imetoka kwa Abu Umaamah (Radhiya Allahu 'anhu)    kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema ((Someni Qur-aan kwani itakuja siku ya Qiyaamah ikimuombea   mwenye kuisoma)) Muslim
QUR-AAN HUMNYANYUA MTU NA HUMDHALILISHA MWINGINE
قال عمر رضي الله عنه : أما إن نبيكم صلى الله عليه وسلم قد قال: (( إن الله يرفع بهذا الكتاب أقواماً ويضع  به آخرين ))  صحيح مسلم 
Imetoka kwa 'Umar (Radhiya Allahu 'anhu) ambaye amesema, Mtume wenu amesema   ((Allaah Atawanyanyua baadhi ya watu kwa kitabu hiki (Qur-aan) na Atawadhalilisha wengine kwa kitabu hiki))  [Muslim] 
QUR-AAN HUMPANDISHA MTU DARAJA YA PEPO
عن عبد الله بن عمرو رضي الله عنهما قال : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم (( يقال لصاحب القران اقرأ و ارتق ورتل كما كنت ترتل في الدنيا فإن منزلتك عند آخر آية تقرؤها )) .  (صحيح الجامع
Imetoka kwa 'Abdullah bin 'Umar (Radhiya Allahu 'anhuma) kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema ((Huambiwa rafiki wa Qur-aan (Aliyeiandama Qur-aan) soma na panda (juu katika daraja za Pepo)  na uisome kwa 'Tartiyl' (utaratibu na utungo) kama ulivyokuwa ukiisoma (kwa Tartiyl) ulipokuwa duniani, kwani makazi yako ni pale utakapofika katika aya ya mwisho utakayoisoma)) [Sahiyh Al-Jaami'i]
MWENYE KUHIFADHI QUR-AAN HUTANGULIA KABURINI (KWA AJILI YA MWANGA ANAOJAALIWA NAO)
عن جابر رضي الله عنه كان رسول الله صلى الله عليه وسلم يجمع بين الرجلين  من قتلى أحد في ثوب واحد ثم يقول : أيهم أكثر أخذاً للقرآن ؟ فإذا أشير إلى  أحدهما قدمه في اللحد .  (صحيح البخاري)
Imetoka kwa Jaabir (Radhiya Allahu 'anhu)  kwamba alikuwa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwakusanya watu wawili waliokufa katika vita vya Uhud katika nguo moja kisha anauliza, ((Nani katika hao mwenye Qur-aan zaidi? Anapojulishwa mmoja kati ya hao, humtanguliza kaburini))  [Al-Bukhaariy]
KUTEREMKA MALAIKA KWA UTULIVU NA RAHMA KWA WANAOSOMA QUR-AAN
عن أبى هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال ((ما اجتمع قوم في  بيت من بيوت الله يتلون كتاب الله ويتدارسونه فيما بينهم إلا نزلت عليهم السكينة وغشيتهم الرحمة وحفتهم الملائكة وذكرهم الله فيمن عنده)) . صحيح مسلم      
Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allahu 'anhu)   kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema ((Hawakusanyiki pamoja watu katika miongoni mwa nyumba za Allaah wakisoma kitabu cha Allaah, na wanafundishana baina yao, ila huwateremkia utulivu na hufunikwa na rahma na Malaika huwazunguka na Allaah Anawataja mbele ya aliokuwa nao)) [Muslim]
KUHIFADHI NA KUJIFUNZA MAANA YAKE NI BORA KULIKO MAPAMBO YA DUNIA
عن عقبة بن عامر رضي الله عنه قال: خرج رسول الله صلى الله عليه وسلم ونحن في الصفة فقال((أيغدو أحدكم  كل يوم إلى بطحان العقيق, فيأتي منه بناقتين كوماوين في غير إثم ولا قطيعة رحم? فقلنا يا رسول الله نحب ذلك قال : أفلا يغدو أحدكم إلى المسجد فيتعلم أو يقرأ آيتين من كتاب الله عز وجل خير له من ناقتين, وثلاث خير له من ثلاث , وأربع خير له من أربع , ومن أعدادهن من الإبل)) رواه مسلم وغيره
Imetoka kwa 'Uqbah bin 'Aamir  (Radhiya Allahu 'anhu)  ambaye amesema, Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alitujia wakati tulikuwa katika Suffah akauliza, kuna yeyote miongoni mwenu anayetaka kwenda  soko la But-haan-Al-'Aqiyq na akapata humo ngamia wawili (wa thamani kabisa wa kike) bila ya kutenda dhambi au kukata undugu? Tukajibu kwamba sote tunapenda kufanya na kupata hivyo. Kisha akasema, basi aende mmoja wenu msikitini akajifunze au asome aya mbili katika kitabu cha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) basi akifanya hivyo ni bora kuliko ngamia (wa thamani kabisa wa kike).  Na aya tatu ni bora kuliko ngamia watatu, na aya nne ni bora kuliko ngamia wanne, na mfano wa hivyo hivyo wa aya kwa ngamia )) [Muslim]
MWENYE KUHIFADHI QUR-AAN HUVALISHWA TAJI SIKU YA QIYAAMAH
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم ((يجيء القرآن يوم القيامة فيقول: يا رب حله,  فيلبس تاج الكرامة ثم يقول: يا رب زده, فيلبس حلة الكرامة, ثم يقول: يا رب ارض عنه فيرضى عنه فيقول: اقرأ وارق ويزاد بكل آية حسنة))  رواه الترمذي والحاكم وصححه الألباني
Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allahu 'anhu)   ambaye amesema, Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema, ((Qur-aan itakuja siku ya Qiyaamah na itasema, Ewe Mola, Mpambe (Mwenye kuhifadhi Qur-aan) kisha atavalishwa taji, kisha (Qu'raan) itasema Ewe Mola, muongezee, kisha huyo mtu atavishwa nguo ya heshima, kisha itasema (Qur-aan) Ewe Mola Ridhika naye, Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ataridhika naye. Kisha ataambiwa, soma na panda, atapokea thawabu zaidi za mema kwa kila aya (atakayosoma) )) At-Tirmidhy na Al-Haakim na kaisahihisha Albaniy
Allaahumma Tujaalie Tuwe Wenye Kuiandama Qur-aan Ili Utulipe Fadhila hizi Ya Rabb


Friday, June 27, 2014

ANDREY COUTINHO WA BRAZIL AWASILI NCHINI KUICHEZEA YANGA

 Huyu ndio
Huyu ndio kiungo machachari kutoka brazili aliesajiliwa na Yanga Africans Sports Club ametua leo Jijini Dar
Msemaji wa Yanga Baraka Kizuguto akipiga picha na mbrazili Cuotinho wa Yamga



CUF WAKIJIANDAA NA MKUTANO MKUU ASUBUHI HII

Wanachama wa Chama cha wananchi CUF wakiwa katika hekaheka za kuingia katika mkutano mkuu ambao unafanyika Blue Pearl Hotel asubuhi hii  
 



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU