Facebook Comments Box

Wednesday, June 18, 2014

TANZANIA YAKOPESHWA BILIONI 24.1 KUSAIDIA BAJETI



Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum (kushoto) akibadilishana
hati ya mkataba wa mkopo uliotolewa na Serikali ya Japani kwa Tanzania, hafla
hiyo ilifanyika leo mjini Dodoma. Kulia ni Balozi wa Japan Nchini Tanzania
Masaki Okada.


Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum (wa kushoto) akiongea na
waandishi wa habari pamoja na Maafisa kutoka Wizara ya Fedha (hawapo pichani)
wakati wa kutiliana saini mkataba wa mkopo uliotolewa na Serikali ya Japani kwa
Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika leo mjini Dodoma. Kulia ni Balozi wa Japan
Nchini Tanzania Masaki Okada
Balozi wa Japan Nchini Tanzania Masaki Okada akiongea na
waandishi wa habari pamoja na Maafisa kutoka Wizara ya Fedha (hawapo pichani)
wakati wa kutiliana saini mkataba wa mkopo uliotolewa na Serikali ya Japani kwa
Tanzania katika hafla ilifanyika leo mjini Dodoma.

Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japani
(JICA) nchini Yasunori Onioshi akiahidi shirika lake kuendelea kushirikiana na
Serilkali ya Tanzania katika masuala mbalimbali yamaendeleo nchini, leo mjini
Dodoma.
Baadhi ya waandishi wa habari pamoja, Maafisa kutoka Wizara
ya Fedha na Ubalozi wa Japani wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Fedha  Saada Mkuya Salum wakati wa kutiliana saini
mkataba wa mkopo uliotolewa na Serikali ya Japani kwa Tanzania katika hafla
ilifanyika leo mjini Dodoma.

(Picha na habari na Ingiahedi Mduma na Eleuteri Mangi-Wizara
ya Fedha)

Wakati wizara ya fedha ikiendelea na majadiliano ya Bajeti
ya Serikali mjini Dodoma, Serikali ya Japan imetoa kiasi cha Yen za Kijapani
bilioni 1.5 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 24.1 za kitanzania kutoka
Serikali ya Japani kwa ajili ya shughuli za maendeleo hapa  nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo ya kutiliana saini , Waziri
Mkuya aliishukuru Serikali ya Japani kwa kuwa na  ushirikiano mzuri na Tanzania.

“Mkopo huu utachangia bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha
wa 2014/2015, na fedha hizo zitaelekezwa katika sekta ya Maji, Elimu na Afya”
alisema Waziri Mkuya.

Aidha, Mkuya aliendelea kusema kuwa, “tunatoa shukurani kwa
Serikali ya Japani kwa misaada mbalimbali ambayo imekuwa ikiitoa ambayo imeleta
mafanikio makubwa nchini ambapo hivi sasa tumeona umaskini unapungua na kipato
kinaongezeka kwa wananchi kwa mujibu wa taarifa ya Sensa ya watu na makazi ya
2012”. Akijibu swali kuhusu fedha hizo za mikopo kuchelewa kufika, Waziri Mkuya
alisema kuwa changamoto kubwa ambayo Serikali imekuwa ikiipata ni kutokana na
taratibu  za sera za nchi husika ambapo
kila nchi wana sera zao.

Kwa upande wake Balozi wa Japan Nchini Tanzania Masaki Okada
alisema kuwa msaada huo unahusiana na ushirikiano wa pamoja na Benki ya Dunia
katika mkopo wa kumi na moja wa kusaidia kupunguza umaskini ambao umekuwa
ukitolewa tangu mwaka 2001.

Mikopo hiyo imekuwa ikitolewa kwa masharti ya mkataba wa
mkopo nafuu wa riba ya asilimia 0.01 kwa Serikali  hapa nchini. Balozi Okada alisema kuwa nchi
yake imekuwa ikitoa mikopo mabalimbali ili kusaidia Serikali ya Tanzania katika
kupunguza umaskini ambapo misaada hiyo imekuwa ikitumika kufuatana na GBS hapa
Tanzanaia kwa kutoa fedha moja kwa moja ambazo zinalenga kuharakisha juhudi za
kupunguza umasikini hususani MKUKUTA.

Naye Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la
Japani (JICA) nchini Yasunori Onioshi alisema kuwa shirika lake litaendelea
kushirikiana na Serilkali ya Tanzania katika kusaidia bajeti yake kwani
Tanzania inakua kwa haraka na mahitaji yake yanaendelea kuongezeka kila mara.Makampuni
ya Kijapani yanayofanya kazi na Serikali ya Tanzania ni pamoja na Kampuni ya
Sigara (TCC) inayomilikiwa na Kampuni ya Kimataifa ya Tumbaku ya Kijapani,
Panasonic Energy Tanzania na JICA.

Hali ya hewa ya Dodoma ni baridi na majadiliano kuhusu
Bajeti ya Serikali yameanza na yanaendelea.

Imetolewa na:

Msemaji Mkuu

Wizara ya Fedha

Tuesday, June 17, 2014

SHAMBULIZI JINGINE MPEKETONI KENYA

Shambulizi lengine limetokea katika eneo la Mpeketoni karibu na
Lamu , pwani ya Kenya na kusababisha vifo vya watu 10.
Shambulizi la leo limetokea siku moja tu baada ya Al Shabaab kukiri
kufanya mashambulizi yaliyowaua watu 50 Jumatatu.
Polisi wanasema kuwa washambuliaji hao walivamia kijiji kimoja
usiku kucha.
Kundi la Al Shabaab lilikiri kufanya mashambulizi hayo na kuambia
shirika la habari la Reuters kuwa operesheni yao ya mashambulizi
itaendelea nchini Kenya.
Takriban watu 50 waliuawa katika mashambulizi yaliyofanyika usiku
wa kuamkia Jumatatu huku washambuliaji wakishambulia hoteli na
kituo cha polisi pamoja na kuteketeza magari.

 CHANZO: BBC


Monday, June 16, 2014

UCHUNGUZI: SIMU YA MKONONI ZINAATHIRI MBEGU ZA KIUME

Baadhi ya watu wanahisi kuwa uchunguzi zaidi unahitajika
Uchunguzi wa utafiti kutoka chuo kikuu cha Exeter nchini
Uingereza, unaonyesha kuwa kiwango cha mbegu za uzazi za
wanaume huathiriwa kwa kuweka simu za mkononi kwenye mifuko
ya suruali.
Hata hivyo ,mwana sayansi wa maswala ya uzazi na
shahawa,alisema kuwa ushahidi huo bado haukuwa na uhakika
wowote hivyo basi simu yake bado inaendelea kukaa mfukoni
mwake.
Uchunguzi huo uliochapishwa katika jarida la 'Environment
International' ulilaumu mnunurisho wa kielectromagnetiki kuwa
chanzo kikuu.
Lilichanganua tafiti kumi tofauti kuonyesha ubora wa shahawa
ikihusisha wanaume 1,492.Hii ilijumuisha kupimwa kwa shahawa
zilizowekwa wazi kwa mnunurisho wa simu za rununu, kwa
maabara na udadisi wa wanaume katika cliniki za uzazi
Kiongozi wa uchunguzi huo Dkt.Fiona Mathews aliambia BBC kuwa
kutokana na uchunguzi huo,moja tu ndio ulionyesha uhusiano kati
ya utumizi wa simu na kudidimia kwa ubora wa shahawa.
"Nafikiri kwa mwanamume wa makamu hakuna haja ya kuingiwa na
hofu,iwapo unajua una uwezekano wa kuwa na shida ya kizazi basi
itakuwa jambo la busara kutoweka simu mfukoni ,pia kugeuza
mtindo wako wa kula."
Mbegu za uzazi za wanaume zinasemekana kuathirika kutokana na simu za mkononi
'Uchunguzi zaidi'
Alikubali kukosolewa na wana sayansi wengine huku akiunga mkono kuwa kuna umuhimu wa kufanya uchunguzi zaidi.
Dkt,Mathews alimaliza kwa kusema"hili ni jambo la kusisimua lakini hatusemi kwa uhakika kuwa kila anayebeba simu mfukoni atakuwa na shida ya kizazi."
Dkt.Allan Pacey kutoka chuo kikuu cha Sheffield anasema kuwa wazo hilo la kudidimia kwa shahawa na kuharibu "DNA"linatokana na "radio frequency" na mnunurisho wa kielectromagnetiki zinazopatikana kwenye simu na pengine joto aidha moja kwa moja kutoka kwenye simu au mnunurisho.
Dkt huyo anayefanya uchunguzi wa shahawa bado hajashawishika akisema ushahidi huo hauna msingi na ataendelea kuweka simu mfukoni.
Aliambia BBC,"kumekuwa na shauku kwa mda kama kuweka rununu mfukoni kunaweza changia kudidimia kwa ubora wa shahawa na nguvu za kiume kivyovyote.
"Kumekuwa na habari zisizokuwa na msingi lakini kwa maoni yangu uchunguzi uliofanywa hadi kufika sasa haujakuwa wa kutosha kwa sababu wachunguzi aidha hawakuhifadhi shahawa vile inavyofaa ama wamedadisi matumizi ya simu kati ya wanaume bila kuzingatia mambo mengine kama mitindo yao ya maisha.
"Tunayohitaji ni uchunguzi kufanywa ambapo utumizi wa simu unazingatiwa vile vile tabia zinazoathiri maisha yao.
Hadi pale tutakapo tafakari hayo,nitaendelea kuweka simu yangu katika mfuko wa mkono wa kulia wa suruale yangu!"

CHANZO: BBC


MUHADHARA MKUBWA LEO MAGHARIBI: UTAKUWA LIVE TV IMAAN NA RADIO IMAAN

Assalaam Alaykum warahmatullah wabarakatuh. .

Tangazo la Muhadhara.

Eneo: Masjid Haqq Morogoro.
Baada ya maghreb na kisha saa 9pm patakuwa na Kipindi maalum Cha Fatawa (maswali na majibu) Live Radio na Tv Imaan.

Mtoa Mada: Shekh Issa Almubali3 شيخ عيسى المبلع (kutoka Saudi Arabia).Ni mmoja katika wanafunzi wa mashekh wakubwa kama Ibn othaymeen, Ibn Baaz, Albaniy, Na Jibreen. (ALLAH AWAREHEM)

Tunaomba kila mmoja amwambie mwenzie.


SOMA MAGAZETI YA LEO TAREHE 16,JULY 2014



Saturday, June 14, 2014

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI 14 JUNE 2014



RAIS WA KENYA IPELEKA HARAMBEE STARS BRAZIL

Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta akitoa hotuba yake katika Ikulu ya Nairobi wakati wa hafla ya kuiaga timu ya Taifa ya Kenya Harambee Stars aliyoipa ofa ya kwenda ziara ya mafunzo kwenye Kombe la Dunia nchini Brazil

Rais Kenyatta akiongea na wachezaji wa Harambee Stars



Rais Kenyatta akigawa tiketi kwa wachezaji huku akishuhudiwa na mkewe Margaret Kenyatta na Seneta wa Nairobi Mike Sonko (kushoto)


Rais Kenyatta, mkewe Mama Margaret Kenyatta na Seneta wa Nairobi Mike Sonko wakipozi Ikulu ya Nairobi na Harambee Stars wakati wa hafla hiyo fupi ya kukabidhi tiketi za ndege za kuendea Brazil kuona kombe la dunia

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameizawadi kwa kuifadhili timu ya taifa ya soka Harambe Stars ziara ya kwenda Brazil kutazama michuano ya kombe la dunia 
Hafla ya kuikabidhi rasmi ufadhili huo timu hiyo, ilifanyika katika ikulu ya Rais Ijumaa ambapo wachezaji kumi na moja wa timu hiyo walikabidhiwa tiketi za ndege kwenda Brazil. 
Kitendo cha Rais bila shaka ni jambo la kutaka kuwatia motisha wachezaji wa timu ya taifa ambao hivi karibuni waliicharaza Djibouti mabao mawili kwa moja katika duru ya kwanza ya michuano ya kuwania kombe la taifa bingwa Afrika baadaye mwakani.
Mmoja wa wachezaji hao alifurahi sana na kusema kuwa hatua ya Rais Kenyatta kwao imetimiza ndoto yao. Rais atagharamia tiketi za timu hiyo kutazama michuano, malazi na usafiri ingawa haijulikani ni mechi zipi watakazotazama. 
Hatua ya Rais Kenyatta imewashangaza watu wengi sana nchini Kenya kwa kuwa timu ya taifa ya Kenya haikuwahi kufuzu kushiriki michuano hiyo, sasa wengi wanahoji hatua yake itasaidia nini?
Soka ya Kenya imekuwa ikikumbwa na changamoto si haba, usimamizi duni na wachezaji kukosa motisha ya kufanya vyema kwa ajili ya usimamizi huo mbaya. 
Kenyatta na mkewe mama wa kwanza wa taifa Margaret Kenyatta wamewafadhili vijana hao kwa kima cha dola elfu arobaini. 
Akitoa ufadhili huo Kenyatta amesema lengo lake hasa ni kuwapa matumaini na motisha ya kuweza kuinua mchezo wa soka nchini Kenya.
Pia ni kama ishara ya kuthamini wachezaji hao ambao hivi karibuni walishinda kombe la Cecafa. 
Kenyatta mwenyewe hatakwenda na kikosi hicho bali amewaasa vijana hao kuwa mabalozi wema wa Kenya nchini Brazil. Ufadhili huu unakuja miezi sita baada ya Kenyatta kukubali kumlipa mshahara wa kocha wa timu hiyo kwa miakja miotano ijayo. 
Kenya haijawahi kufuzu kwa michuano ya kombe la dunia lakini ziara hii kwa vijana wa Harambee Stars itawafungua macho huku wakiwa na azma ya kufuzu kwa michuano ya taifa bingwa Afrika mwaka 2015 baada ya kufuzu kwa duru ya pili na kujiandaa kuchuana na Lesotho tarehe 18 Julai.
CHANZO:BBC


NYUMBA YA BALOZI WA MSUMBIJI TANZANIA YAUNGUA

Habari zilizotufikia ni kwamba nyumba ya balozi wa Msumbiji iliyoko maeneno ya Masaki imewaka moto. Habari zinaendelea kutupasha kwamba fire walifika lakini maji yalikuwa kidogo.


UHOLANZI WAIPA UISPANIA KIPIGO CHA MBWA MWIZI.

Van persie akishangilia kwa kugonganisha mikono na kocha wake
Magoli mawili  yaliyofungwa na Van persie na mawili yaliyofungwa na roben na moja la vrij yaliyosha kabisa kuisambaratisha uhispania japo wao ndio walikuwa wakwanza kupata goli kwa njia ya penati.
Timu ya uhispania ndio ilitabiriwa na wengi kuonesha mpira mzuri na kuchukua kombe ila kwa jana wengi wanasema huu ndio mwisho wa utawala wake kisoka na wanaipa nafasi kubwa uholanzi.
 
Van persie akifunga goli kwa kichwa cha kuchumpa watu wanakifananisha na ndege kubwa za mizigo na watu ikiwa inaruka



BOMU LAUA MTU MMOJA KWENYE DAURA ZANZIBAR

Hii ni picha ya mtu anaesadikiwa kufa baada ya kitu kinachosadikiwa kuwa bomu kurushwa zanzibar.eneo la darajani kulikokuwa kunafanyika daura ya masheikh wa Afrika mashariki. Inasemekana huyu aliekufa ni mwanafunzi wa sheikh Quasim Mafuta Qaasim wa tanga na sheikh mwenyewe kaumia mkono na mguu kulikuwa na sheikh mwingine kutoka kenya ambae hakupata madhara yoyote. Tunamtakia apone mapema. Na marehemu Allah amuhifadhi.
Inna lilayh wa inna ilayhi rajiuun 


Friday, June 13, 2014

PICHA: AJALI ILIYOTOKEA MOROCO MCHANA WA LEO

 
Baadhi ya Watu wakitazama ajali ya magari mawili kama yaonekanavyo pichani,iliyotokea mapema leo eneo la Moroco-Posta jijini Dar,katika ajali hiyo ambayo chanzo chake hakikufahamika mara moja,mtu mmoja alijeruhiwa na hakuna aliyepoteza maisha.



Mama ambaye jina lake halikufahamika mara moja moja aliyekuwa kwenye gari lenye usajili wa namba T679 CKC,akipewa huduma ya kwanza mara baada ya kupoteza fahamu



Moja ya gari ambalo pia lilipata ajali mara baada ya kuacha barabara na kuvamia mtaro kama lionekanavyo pichani



Moja ya gari ambalo pia lilipata ajali mara baada ya kuacha barabara na kuvamia mtaro kama lionekanavyo pichani,huku abiria wake mmoja akiwa amepoteza fahamu,kama aonekavyo kwa mbali



Majeruhi akipewa huduma ya kwanza na mmoja wa akina mama aliyekuwa akifanya usafi kando kando ya barabara mapema leo asubuhi,katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza maisha.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU