Wednesday, July 31, 2013
Tuesday, July 30, 2013
TAMASHA LA SIMBA LAPELEKWA MBELE: TP MAZEMBE HAWATAKUJA KUSHIRIKI TAMASHA HILO
TAMASHA
la kuazimisha siku ya Simba SC linaweza kusogezwa mbele kwa simu mbili,
kupisha sikukuu ya Eid El Fitri hivyo kufanyika Agosti 10, badala ya
Agosti 8, kama ilivyo kawaida yake.
Aidha, mpango wa Simba SC kucheza na mabingwa wa Afrika mara nne, Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umeshindikana kutokana na timu hiyo ya Lubumbashi kutingwa na michuano ya Kombe la Shirikisho.
Na
kwa sababu hiyo, timu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo, Dar es Salaam
sasa itacheza na SC Villa ya Uganda katika tamasha hilo, Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam.
Simba ilitumai kucheza na Mazembe yenye wachezaji wake wa zamani wawili, Mbwana Samatta na Patrick Ochan ambao iliwauzua klabu hiyo miaka miwili iliyopita, lakini ratiba ya michuano ya CAF imeharibu mambo.
Katika maendeleo mengine, wachezaji wa Simba SC waliokuwa na kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wanatarajiwa kujiunga na wenzao kambini, Bamba Beach, Kigamboni kuanzia leo jioni.
Wachezaji waliokuwa Stars ni viungo Amri Kiemba na Haroun Chanongo. Kiemba alicheza dakika zote 90 na kufunga la Stars ikilala 3-1 Uwanja wa Mandela, Namboole na kutolewa jumla ya mabao 4-1, baada ya awali kufungwa 1-0 Dar es Salaam wiki mbili zilizopita, wakati Chanongo aliingia uwanjani dakika ya 78 kumpokea John Bocco ‘Adebayor’ wa Azam FC.
SOURSE: BIN ZUBEIRY
Aidha, mpango wa Simba SC kucheza na mabingwa wa Afrika mara nne, Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umeshindikana kutokana na timu hiyo ya Lubumbashi kutingwa na michuano ya Kombe la Shirikisho.
![]() |
| Kikosi cha simba kilichopita kikiwa na wachezaji wazuri kama Mrisho Ngassa, Juma Kaseja, Haruna Moshi na Mwinyi kazimoto |
Simba ilitumai kucheza na Mazembe yenye wachezaji wake wa zamani wawili, Mbwana Samatta na Patrick Ochan ambao iliwauzua klabu hiyo miaka miwili iliyopita, lakini ratiba ya michuano ya CAF imeharibu mambo.
Katika maendeleo mengine, wachezaji wa Simba SC waliokuwa na kikosi cha timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars wanatarajiwa kujiunga na wenzao kambini, Bamba Beach, Kigamboni kuanzia leo jioni.
Wachezaji waliokuwa Stars ni viungo Amri Kiemba na Haroun Chanongo. Kiemba alicheza dakika zote 90 na kufunga la Stars ikilala 3-1 Uwanja wa Mandela, Namboole na kutolewa jumla ya mabao 4-1, baada ya awali kufungwa 1-0 Dar es Salaam wiki mbili zilizopita, wakati Chanongo aliingia uwanjani dakika ya 78 kumpokea John Bocco ‘Adebayor’ wa Azam FC.
SOURSE: BIN ZUBEIRY
UJUMBE ALIOPEWA SHEIKH PONDA NA VIONGOZI WA UAMSHO ALIPOWATEMBELEA GEREZANI
![]() |
| Sheikh Ponda Issa Ponda |
Na Bakari Mwakangwale,
An-Nuur — VIONGOZI wa Jumuiyaya UAMSHO Zanzibar wamesema kwamba pamoja
na kuzuiwa kwao Gerezani, hawana shaka kuwa ipo siku hakiitasimama na
hatimaye kupatikana Taifa Uhuru la Zanzibari.
Kauli hiyo wameitoa mbele ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi zaKiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, muda mfupi baada ya kukutanana viongozi hao Ijumaa ya wiki iliyopita katika Gereza la Kiinuamiguu, lililopo Mtaa wa Kilimani Zanzibar.
Sheikh Ponda, alifika gerezani hapo akiwa katika muendelezo wa ziara zake anazofanya nchini na kuongea na Waislamu, baada ya kumalizika kwa kesi yake na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje.
Akiongea na Mwandishi wa habari hizi katika ofisi za Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), Kinondoni, Jijini Dares Salaam, mapema wik ihii alisema alifanikiwa kuonana na viongozi wa UAMSHO na kuongea nao kwa muda wa dakika 45.
Alisema, Masheikh hao waliopo gerezani kwa muda wa miezi tisa sasa, wapo imara kiimani ambao walitumia fursa hiyo kumpa salamu kwa Wazanzibari huku naye akiwapa salamu kutoka kwa Waislamu wa Bara. “Hawana hofu pamoja na kushikili wa na Dola kwa muda wote huo, kwani wanachoamini wao kuwa wapo katika haki, na uimara wao unakuja kutokana na kuijua vizuri historia ya kupigania haki kuwa hata Mitume
Kauli hiyo wameitoa mbele ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi zaKiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, muda mfupi baada ya kukutanana viongozi hao Ijumaa ya wiki iliyopita katika Gereza la Kiinuamiguu, lililopo Mtaa wa Kilimani Zanzibar.
Sheikh Ponda, alifika gerezani hapo akiwa katika muendelezo wa ziara zake anazofanya nchini na kuongea na Waislamu, baada ya kumalizika kwa kesi yake na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje.
Akiongea na Mwandishi wa habari hizi katika ofisi za Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), Kinondoni, Jijini Dares Salaam, mapema wik ihii alisema alifanikiwa kuonana na viongozi wa UAMSHO na kuongea nao kwa muda wa dakika 45.
Alisema, Masheikh hao waliopo gerezani kwa muda wa miezi tisa sasa, wapo imara kiimani ambao walitumia fursa hiyo kumpa salamu kwa Wazanzibari huku naye akiwapa salamu kutoka kwa Waislamu wa Bara. “Hawana hofu pamoja na kushikili wa na Dola kwa muda wote huo, kwani wanachoamini wao kuwa wapo katika haki, na uimara wao unakuja kutokana na kuijua vizuri historia ya kupigania haki kuwa hata Mitume
wa Mwenyezi
Mungu, walipo tangaza haki, walipata misukosuko na kupigwa vita na
watawala.” Alisema Shkh. Ponda, Akielezea hali za Viongozi hao wa
UAMSHO.
Ponda, alisema kuwa Masheikh hao, MselemAli, Azan Khalid, Musa Juma pamoja nae Amir Farid Had, kwa kwa ujumla akiyatafakari maongezi yao anaona ni wazi kuwa msimamo wao ni kutorudi nyuma katika kupigania haki na zaidi alidai walimuambia hawana shaka kuwa ipo siku haki itasimama na batili itaondoka Visiwani humo. Alisema, Masheikh hao, walimtaka awafikishie ujumbe Wazanzibar katika mikutano yake kuwa wasiache kuzungumzia haki zao za msingi wanazodai kwani kwa kufanya hivyo ndiyo kuitendea haki Zanzibar.
“Katika fursa hii mliyoipata ya kuwahutubia Wazanzibar na hatimae Watanganyika, waambien imsimamo wetu bado ni uleule wa kutetea Taifa Uhuru la Zanzibari na bila shaka pia huo utakuwa ni Uhuru kwa Watanganyika pia,” alisema Sheikh Ponda, akimnukuu Amir Farid Had.
Sheikh Ponda alisema viongozi hao walimuagiza kutumia vema fursa ya mikutano yake Visiwani humo na hatimae Bara kwa kuinua hamasa za Waislamu huku wakimtaka kuwaelekeza kutumia vema mafunzo na misimamo waliyoitoa juu ya Taifa huru la Zanzibar.
“Darsa zetu bila shaka zimejenga imani na akida, vilevile zinatosha kuwa semina za kujitambua.
Lakini pia tulijenga hamasa kubwa na utayari wakutetea haki hadharani. Kama Waislamu hawatakiwi kurudi nyuma wasinyamaze hata kidogo”, alisema Sheikh Ponda, akidai kuwa huo ni ujumbe kutoka kwa Sheikh Mselem Ali.
Awali Sheikh Ponda, kwa upande wake aliwapa viongozi hao salamu na hisia za Waislamu wa Bara kufuatia ziara zake katika mikoa kadhaa ya Tanzania Bara zilizoandaliwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu mara baada ya kutoka Gerezani.
“Waislamu wa Bara wanatambua msimamo wenu wa kupigania haki, pia wanaamini kukamatwa kwenu ni ukweli wa methali isemayo ‘kiza kinapozidi kuwa kinene ndivyo kupambazuka kunavyokaribia’ hivyo wako pamoja nanyi.” Alisema SheikhPonda, akirejea kauli yake mbele ya viongozi wa UAMSHO Gerezani.
Katika ziara yake hiyo Visiwani humo, Sheikh Ponda, pia alipata fursa ya kuwahutubia maelfu ya Wazanzibar katika mihadhara sita iliyoandaliwa na Jumuiya ya UAMSHO katika maeneo mbalimbali ya Unguja.
Akiwahutubia maelfu ya waumini waliohudhuria katika muhadhara uliofanyika Mkoa wa Mjini Maghribi Masjid Sahaba Daraja Bovu, Sheikh Ponda, aliwataka Waislamu wa Zanzibar kuchukua hadhari ya njama zinazopikwa kuvunja udugu wao kwa lengo la kuwagawa. Kwa mujibu wa Sheikh Ponda, alisema maelfu ya Waislamu waliokutana katika Msikiti wa harakati maarufu kwa jina la Msikiti wa Mbuyuni, walisema wanatafakari hatma ya viongozi wao wanaoshikiliwa na Dola kwa zaidi ya miezi tisa sasa.
“Msimamo kama huo ulitolewa tena katika mkusanyiko mkubwa uliofanyika siku iliyofuata (Ijumaa iliyopita) mara tu baada swala ya Ijumaa katika Msikiti wa kwa Mpendae kwa Kificho.
Kuonesha hisia zenu kama hivi bila shaka mnajenga nguvu kubwa ya pamoja na wakati utakapofika watawatoa tu viongozi wenu”. Alisema Sheikh Ponda, akiwahutubia waumini wa Nungwi.
Aidha Shkh Ponda, aliwataka waumini wa Nungwi kujiimarisha kwa miradi ya maendeleo kwa kutumia vizuri hazina kubwa ya ardhi waliyonayo ambayo imekuwa ikivamiwa kwa kasi kubwa na wawekezaji wa mahoteli ya kitalii, ambao kwa asilimia tisini wanaharibu utamaduni wa Mzanzibar.
Sheikh Ponda, alisema Jumuiya ya UAMSHO, inatarajia kufanya muhadhara mkubwa siku ya Ijumaa katika Msikiti wa Mbuyuni, lengo likiwa ni kufanyama jumuisho ya mihadhara iliyofanyika akiwa hukowiki iliyopita.
--
Rejea ya habari: An-Nuur no. 1081
Ponda, alisema kuwa Masheikh hao, MselemAli, Azan Khalid, Musa Juma pamoja nae Amir Farid Had, kwa kwa ujumla akiyatafakari maongezi yao anaona ni wazi kuwa msimamo wao ni kutorudi nyuma katika kupigania haki na zaidi alidai walimuambia hawana shaka kuwa ipo siku haki itasimama na batili itaondoka Visiwani humo. Alisema, Masheikh hao, walimtaka awafikishie ujumbe Wazanzibar katika mikutano yake kuwa wasiache kuzungumzia haki zao za msingi wanazodai kwani kwa kufanya hivyo ndiyo kuitendea haki Zanzibar.
“Katika fursa hii mliyoipata ya kuwahutubia Wazanzibar na hatimae Watanganyika, waambien imsimamo wetu bado ni uleule wa kutetea Taifa Uhuru la Zanzibari na bila shaka pia huo utakuwa ni Uhuru kwa Watanganyika pia,” alisema Sheikh Ponda, akimnukuu Amir Farid Had.
Sheikh Ponda alisema viongozi hao walimuagiza kutumia vema fursa ya mikutano yake Visiwani humo na hatimae Bara kwa kuinua hamasa za Waislamu huku wakimtaka kuwaelekeza kutumia vema mafunzo na misimamo waliyoitoa juu ya Taifa huru la Zanzibar.
“Darsa zetu bila shaka zimejenga imani na akida, vilevile zinatosha kuwa semina za kujitambua.
Lakini pia tulijenga hamasa kubwa na utayari wakutetea haki hadharani. Kama Waislamu hawatakiwi kurudi nyuma wasinyamaze hata kidogo”, alisema Sheikh Ponda, akidai kuwa huo ni ujumbe kutoka kwa Sheikh Mselem Ali.
Awali Sheikh Ponda, kwa upande wake aliwapa viongozi hao salamu na hisia za Waislamu wa Bara kufuatia ziara zake katika mikoa kadhaa ya Tanzania Bara zilizoandaliwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu mara baada ya kutoka Gerezani.
“Waislamu wa Bara wanatambua msimamo wenu wa kupigania haki, pia wanaamini kukamatwa kwenu ni ukweli wa methali isemayo ‘kiza kinapozidi kuwa kinene ndivyo kupambazuka kunavyokaribia’ hivyo wako pamoja nanyi.” Alisema SheikhPonda, akirejea kauli yake mbele ya viongozi wa UAMSHO Gerezani.
Katika ziara yake hiyo Visiwani humo, Sheikh Ponda, pia alipata fursa ya kuwahutubia maelfu ya Wazanzibar katika mihadhara sita iliyoandaliwa na Jumuiya ya UAMSHO katika maeneo mbalimbali ya Unguja.
Akiwahutubia maelfu ya waumini waliohudhuria katika muhadhara uliofanyika Mkoa wa Mjini Maghribi Masjid Sahaba Daraja Bovu, Sheikh Ponda, aliwataka Waislamu wa Zanzibar kuchukua hadhari ya njama zinazopikwa kuvunja udugu wao kwa lengo la kuwagawa. Kwa mujibu wa Sheikh Ponda, alisema maelfu ya Waislamu waliokutana katika Msikiti wa harakati maarufu kwa jina la Msikiti wa Mbuyuni, walisema wanatafakari hatma ya viongozi wao wanaoshikiliwa na Dola kwa zaidi ya miezi tisa sasa.
“Msimamo kama huo ulitolewa tena katika mkusanyiko mkubwa uliofanyika siku iliyofuata (Ijumaa iliyopita) mara tu baada swala ya Ijumaa katika Msikiti wa kwa Mpendae kwa Kificho.
Kuonesha hisia zenu kama hivi bila shaka mnajenga nguvu kubwa ya pamoja na wakati utakapofika watawatoa tu viongozi wenu”. Alisema Sheikh Ponda, akiwahutubia waumini wa Nungwi.
Aidha Shkh Ponda, aliwataka waumini wa Nungwi kujiimarisha kwa miradi ya maendeleo kwa kutumia vizuri hazina kubwa ya ardhi waliyonayo ambayo imekuwa ikivamiwa kwa kasi kubwa na wawekezaji wa mahoteli ya kitalii, ambao kwa asilimia tisini wanaharibu utamaduni wa Mzanzibar.
Sheikh Ponda, alisema Jumuiya ya UAMSHO, inatarajia kufanya muhadhara mkubwa siku ya Ijumaa katika Msikiti wa Mbuyuni, lengo likiwa ni kufanyama jumuisho ya mihadhara iliyofanyika akiwa hukowiki iliyopita.
--
Rejea ya habari: An-Nuur no. 1081
Monday, July 29, 2013
NITAJIUZULU NIKIBAINIKA NAUZA MADAWA YA KULEVYA - IDD AZZAN
Idd Azzan amekaririwa katika habari iliyoandikwa na mwandishi Bakari Kimwanga, na kuchapoishwa kwenye gazeti la MTANZANIA jana akisema kuwa hatua ya kuhusishwa na biashara haramu ya dawa za kulevya ni kutotenda haki mbele ya jamii hasa wapiga kura wake na Taifa kwa ujumla. Akasema mtu aliyendika barua ya tuhuma dhidi yake amedhamiria kumshushia heshima na huenda ana jambo limejificha.
Alisema kutokana na hali hiyo, anashindwa kuchukua hatua yoyote ya kufanya zaidi ya kuliandikia barua Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi dhidi ya barua hiyo kuweza kubaini ukweli wa jambo hilo.
Ni kweli nimeiona hiyo barua katika mtandao, inayodaiwa imeandikwa na kijana ambaye amekamatwa Hong Kong nchini China. Lakini ninajiuliza kama kweli yeye ni raia mwema, katika hili kwa nini hakutaka kutaja jina lake kwenye barua hiyo?
Hata nilipoisoma nimebaini kuwa huyo mtu ametumika na huenda kabisa hayupo nje ya nchi, kwani
katika maelezo yake anataja jina la Balozi Philip Marmo kuwa amemsaidia hali ya kuwa hivi karibuni Rais Kikwete alimteua Balozi mpya Abdulrahman Shimbo na Marmo kuwa Balozi wa Shirikisho la Ujerumani.
Kingine naona alijaribu kuandika uongo kuweza kuaminisha jamii, kwani hata hilo jila la balozi mwanzo limetajwa jina la Bernard na kukatwa kwa wino. Ninapenda kulieleza Taifa kuwa naomba vyombo vya usalama vifanye uchunguzi wa jambo hili na nikibainika ninauza dawa za kulevya nipo tayari kujiuzulu ubunge wangu.
Kubwa haki itendeke katika kufanya uchunguzi wa jambo hili, ila ni lazima jamii na Watanzania kwa ujumla tusikubali kwa makusudi watu waichafue nchi yetu kwa chuki na fitna tu.
Sijawahi kuuza dawa za kulevya na hata katika familia yangu hakuna mtu anayefanya biashara hiyo haramu. Kila mmoja anajua kuwa Idd nilikuwa Diwani wa Kata ya Magomeni, huku kazi yangu kubwa ikiwa ni biashara ya magari na daladala ambayo ninaendelea nayo hadi sasa mbali ya ubunge kama nilivyopewa heshima na wapiga kura wangu wa Kinondoni.
Alipoulizwa
kuwa ni hatua gani ikibainika hakuna ukweli wa jambo hilo baada ya
vyombo vya usalama kufanya uchunguzi, Azzan alisema: “Ni ngumu kusema
hatua gani nitachukua ikibainika hakuna ukweli, lakini nataka kusema
kama yule aliyeandika barua hii angetaja jina lake ni wazi baada ya
uchunguzi ningeweza kuomba ushauri kwa mwanasheria wangu hatua za
kuchukua, lakini kwa kuwa hakutaja jina ni ngumu kuweza kuamua.”
Source: WAVUTI
DIAMOND ANUNUA MTAA DAR ES SALAAM
WAKATI Wema Isaac Sepetu akiongeza idadi ya magari kwa kununua mkoko wa maana, zilipendwa wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amemziba mdomo baada ya kununua eneo kubwa ambalo ndani yake kuna nyumba tatu, jirani na anapoishi Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006, Ijumaa Wikienda lina maelezo kamili.
Diamond.
Akizungumza na gazeti, hili muda mfupi baada ya kukamilisha kila
kitu kuhusiana na ununuzi wa eneo hilo ambalo kwa mujibu wake anatarajia
kujenga jengo lenye ghorofa nne na nyumba za kawaida tatu, Diamond
alisema kuwa anajitahidi kuongeza idadi ya mijengo anayomiliki kwa kuwa
ndicho kitu cha thamani kuliko magari.
Wema.
Katika hali iliyotafsiriwa kuwa ni kumtunishia msuli Wema, jamaa
alitupia maneno: “Mimi siyo kama hao wanaokimbilia kununua magari ya
kifahari ili mradi waonekane wako juu kifedha.Eneo alilonunua Diamond anayemiliki nyumba zaidi ya tano Dar lipo mtaa wa nne kutoka anapoishi Wema.
YANGA WAKATAA AZAM TV KUONESHA MECHI ZAO
| mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji (katikati) akiongea na waanidishi wa habari, Makamu mwenyekiti Clement Sanga (kushoto) na mjumbe wa kamati ya utendaji Mark Anthony (kulia) |
Uongozi wa klabu ya Yanga
leo umefanya mkutano na waandishi wa habari juu ya urushwaji wa michezo
yake ya Ligi Kuu katika kituo cha luninga cha Azam ambacho kimeingia
makubaliano na kamati ya Ligi Kuu kuonyeshwa michezo yote ya ligi kwa
kipindi cha miaka miatatu (3).
Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa klabu ya
Yanga Yusuf Manji amesema uamuzi wa kamati ya ligi kuingia mkataba na
kituo cha Azam Tv bila ya kuwashirikisha wahusika wenyewe ambao ni
vilabu vishiriki haukuwa sawa.
Sisi kama klabu ya
Yanga tulikaa kikao cha kamati ya utendaji na kuona taratibu za kupewa
haki ya matangazo kwa kampuni ya Azam haikua sawa, sisi viongozi wa
kalbu ya Yanga hatukushirikishwa katika mchakato huo hivyo tukaona ni
vema tuje kwa vyombo vya habari tuulezee umma juu ya maazimio ya kamati
ya utendaji.
Ifuatayo ni taarifa kamili kwa vyombo vya habari:
YAH: URUSHWAJI KATIKA TELEVISHENI MICHEZO YA YANGA.
Hivi
karibuni, Tanzania Football Federation (TFF) iliunda Tanzania Premier
League chini ya Bodi yampitoBodi ya TPL ambayo ni msimamizi mpaka hapo
Bodi itakayokuwa imechaguliwa kidemokrasia. Bodi hii imeamua peke yake
kuingia katika mkataba wa miaka 3 (mitatu) na kampuni inayoitwa Azam
Television (ambayo ina mapromota wale wale wanaomiliki Azam Football
Club). Makubaliano ambayo Bodi ya TPL inatarajia kuingia na Azam
Television, Kamati ya Utendaji ya YANGA inalipinga kwa nguvu zote katika
misingi ifuatayo:
1. BODI YA TPL
1.1 Bodi
iliyoko sasa hivi ni ya mpito ambayo ilitakiwa kutenguliwa na Bodi
iliyochaguliwa kidemokrasia kwa kupitia uchaguzi wa tarehe ……….. mwaka
huu na haitakiwi kuingia katika mikataba a miaka mingi wakati inakaribia
kuondoka katika ofisi.
1.2 Bodi ya TPL iliyoko sasa hivi haikuchaguliwa kidemokrasia.
1.3 Bodi ya TPL iliyoko sasa hivi haina mjumbe hata mmoja aliyeteuliwa kutoka YANGA.
2. UTARATIBU WA DUNIA NZIMA
2.1 Haijawahi
kutokea katika ligi ya mpira wa miguu ya kisasa kulazimishwa kwa Klabu
inayoshindana katika ligi kuachia haki zake za urushwaji wa michezo
zichukuliwe na chombo cha habari cha Klabu ya upinzani.
2.2 Mfumo
(undertaking) ambao TPL inataka kuanzisha kwa njia ya kulazimisha
mkataba kwa YANGA iachie urushwaji wa michezo yake ya soka yarushwe na
Azam TV unatishia sana uwepo wa msingi wa ushindani katika soka ya
Tanzania.
2.3 Makubalianokati
ya TPL na Azam Television kuhusu utaratibu wa malipo yanasemakwamba
Klabu ya YANGA na Klabu zingine zitakazoshiriki katika Ligi Kuu ya
Tanzania watapata mgao sawa wa mapato ya urushwaji wa michezo hii,
ambayo YANGA inapinga kwa sababu kama inavyofanyika duniani kote kwenye
ligi zilizofanikiwa (angalau) kutofautisha mgawanyo wa mapato kati ya
timu kufuatana na matokeo ya mwisho wa ligi.
2.4 Kamati
ya Utendaji ya YANGA siyo tu haikubaliani na mgawanyo sawa wa mapato
ambao hautofautishi kati ya timu ya kwanza katika ligi na timu ya mwisho
katika ligi, lakini pia ukosefu wa viwango (premiums) vitakavyolipwa:
2.4.1 Vilabu vya mpira vyenye ufuasi wa washabiki wengi;
2.4.2 Vilabu vya mpira vinavyoendeshwa na Wanachama;
2.4.3 Vilabu vya mpira visivyopata ruzuku kutoka Serikalini n.k.
3. MIGOGORO YA MASLAHI
3.1 Makamu
Mwenyekiti wa Bodi ya Mpito ya TPL ni Mkurugenzi mwandamizi wa
Makampuni ya Azam na kwa hivyo mazungumzo ya siri kati ya Bodi ya TPL
na Azam ni ya kutiliwa mashaka.
3.2 Makampuni
ya Azam yana yanashindana kibiashara na makapuni mengi yakiwemo ya
utengenezaji wa vinywaji baridi na imeonyesha huko awali inaweka
“matakwa maalum” muhimu zaidi kuliko mprira wa miguu, kama vile Azam
F.C. hawashiriki katika Kombe la Tusker na kwa hiyo YANGA inakuwa na
msimamo kwamba kwa Azam Television kupewa leseni ya kurusha matangazo ya
mpira wa miguu inatishia biashara za washiriki wa sasa na wa baadaye wa
YANGA.
3.3 Azam
na YANGA wana uadui wa kimichezo. Kumbuka, wakati MRISHO NGASSA
alipotaka kwenda YANGA, Azam F.C. walimkopesha kwa nguvu kwa Klabu ya
Simba! Kwa hiyo YANGA itahatarika kwa matangazo yenye upendeleo kama
Azam Television itarusha hewani michezo yake n.k.
4. KUTOKUWA NA UWAZI
4.1 Mkataba
wa utangazaji wa miaka mingi unaotaka kuingiwa kati ya TPL na ambao
badohaujarushwa Television ya Azam haukushindanishwa na vyombo vingi vya
habari, na vyombo ambayo wako tayari kwenye soka havikujulishwa kuhusu
fursa hii au walizuiliwa kufikisha mapendekezo yao ya maombi ya haki za
kurusha matangazo katika Ligi Kuu (Tanzania Premier League).
4.2 Ukosefu
wa uwazi wa TPL unanonyesha kuwa MoU iliyokusudiwa kuwekewa saini na
TPL haikufikishwa YANGA kwa ajili ya mapitio ya kisheria, licha ya YANGA
kufanya ombi hilo kwaTPL.
5. MAZINGATIO YA KIBIASHARA
5.1 Mamlaka
ya kuamua mzozo wowote wa mkataba wa leseni ya utangazaji wa Ligi Kuu
(Tanzania Premier Leagu) itakuwa ni Mahakama ya kisheria na siyo FIFA.
TPL inasingizia kwamba leseni ya matangazo ambayo inakusudia kufanya
kuwa ni maagizo ya FIFA na kwa hiyo YANGA inapaswa kuukubali "lock,
stock and barrel."
5.2 TPL
inaelezea kimakosa makubaliano ya leseni ya urushaji wa mchezo ya
mpira inayotarajia kuingia na Television ya Azam kama "makubaliano ya
udhamini" (“sponsorship agreement”) ambayo siyo sahihi, kwa sababu
urushaji wa michezo ya mpira wa miguu ni biashara inayotokana na maslahi
ya uhusiano na hivyo
wahusika wote ni lazima wazingatie maslahi yao ya kifedha.
Kwa
mfano, moja ya vyanzo muhimu vya mapato ya YANGA ni mapato ya kiingilio
ya mlangoni yatokanayo na michezo ya mpira wa miguu ambayo urushwaji wa
michezo hii itapunguza mapato haya. Kwa wastani michezo ya YANGA Dar
es Salaam huingiza makusanyo ya mlangoni shilingi milioni 50 kwa kila
mchezo na hata kushuka kidogo kwa 25% katika mahudhurio ya mechi za
YANGA zinafikia mara mbili ya mapendekezo ya mapato takribani Sh milioni
8.3 kwa mwezi kupokelewa na YANGA kutoka mradi wa kibiashara kati ya
TPL na Azam Television. Kwa kuzingatia haya, kwamba hata siku za nyuma
kama kulikutokea fursa ya kurusha mchuano wa mpira unapochezwa, wadau
wote (Timu za mpira wa miguu, TFF na Mtangazaji) walikuwa wanaafikiana
kwanza kwa pamoja kuhusu mapato na mgawanyo wake.
Kamati
ya Utendaji ya YANGA ina maoni kwamba makubaliano yoyote ya kibiashara
yanayoihusu ni lazima iyalinde maslahi kifendha ya Klabu yake ambapo
makubaliano ya TPL / Azam Television hayaangalii na kwa hiyo, Kamati ya
Utendaji ya YANGA haitaki mchezo wake urushwe hewani na Azam Television.
Msisitizo
wa TPL kuwa lazima Azam Television irushe hewani michezo ya YANGA
linasikitisha. Kamati ya Utendaji ya YANGA haina tatizo na Vilabu
vingine vya mpira wa miguu zikiruhusu michezo yao kurushwa na Azam
Television ila haifurahii kuwa TPL inalazimisha YANGA kuonyesha mchezo
wake wa Vodacom Premier League katika Azam Television.
......................
(YUSUF MANJI)
MWENYEKITI
YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB
29 JULAI, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)

