Thursday, June 13, 2013
MSANII LANGA KILEO AFARIKI DUNIA LEO
Langa
Kileo (msanii wa Hip Hop Tanzania, pichani) amefariki dunia leo hii. Langa
alipelekwa hospitali akiwa hajitambui. Anadaiwa kuwa alikumbwa na Malaria kali
sana, Hali iliyopelekea kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili jana. Uchunguzi wa
chanzo cha kifo chake bado unaendelea. Msanii Langa aliwahi kutamba na kikundi
cha Wakilisha pamoja na witness na sara ni miongoni mwa wasanii wakongwe wa
bongo flava nchini Tanzania. Mungu amrehemu.
Baba
wa marehemu Mzee Kileo amesema kuwa mtoto wake Langa kwenye picha amefariki
dunia leo majira ya saa 10 katika hospitali ya Taifa Muhimbili.Taarifa kamili
na mipango ya mazishi zitatolewa pale vikao vya familia vitakapofanywa.Pia baba
yake alisema msiba huu umetokea wakati mama yake Langa hayupo Tanzania,alisema
kwa sasa mama yake Langa yupo Marekani lakini baada ya kupewa taarifa hizo
tayari ameshakata tiketi ya kurudi Tanzania na ataanza safari kesho.Msiba uko
nyumbani kwao maeneo ya Mikocheni
Aminiel
Aligaesha ambae ni Afisa Uhusiano wa hospitali ya Taifa Muhimbili amethibitisha
kwamba msanii Langa amefariki dunia June 13 2013 saa kumi na moja jioni baada
ya kufikishwa hospitalini hapo toka juzi jioni ambapo kutokana na sababu za
kimaadili kwenye tiba, Muhimbili hospitali hawawezi kusema rapper huyu alikua
anaumwa nini bali ndugu ndio wenye mamlaka ya kufanya hivyo.
Kwenye
maelezo aliyoyatoa kwa millardayo.com Aminiel amesema Marehemu Langa
alipokelewa kwenye idara ya wagonjwa wa magonjwa ya dharura usiku wa kuamkia
jana na kupatiwa huduma ambapo leo June 13 2013 ndio alihamishiwa kwenye chumba
cha wagonjwa Mahututi na baadae kufariki dunia.
Wednesday, June 12, 2013
HII NDIO VIDEO YA MCHUNGAJI ALIENASWA AKIMTOMASA MUUMINI WAKE
Video hiyo ilirekodiwa kwa kutumia kamera zilizokuwa zimetegeshwa kitika ofisi ya mchungaji huyo bila yeye kujua.
Tazama video ya mchungaji huyo hapa
AMPIGA MUMEWE BAADA YA KUKUTA AKIANGALIA TV KABLA YA KUMALIZA KAZI ZA NYUMBANI
MWANAMUME mmoja katika
mtaa wa Mwanzo, Eldoret anauguza majeraha baada ya kupigwa na mkewe
kufuatia mzozo uliotokana na yeye kupatikana akitazama runinga kabla ya
kumaliza kazi ya nyumbani.
Kwa mujibu wa majirani mkewe mwanamume huyo, alirejea nyumbani jioni kutoka kazini mnamo Jumatatu na kumkuta akitazama televisheni. Mara moja, alimrukia na kumpiga vibaya.
Mwanaume huyo aliokolewa na majirani waliofika kuitika kilio chake na kumkuta akigaragara sebuleni kutokana na maumivu. Walimpeleka katika zahanati ya kibinafsi alikotibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani.
Majirani walisema wawili hao wamekuwa wakigombana mara kwa mara baada ya mwanamume huyo
Kwa mujibu wa majirani mkewe mwanamume huyo, alirejea nyumbani jioni kutoka kazini mnamo Jumatatu na kumkuta akitazama televisheni. Mara moja, alimrukia na kumpiga vibaya.
Mwanaume huyo aliokolewa na majirani waliofika kuitika kilio chake na kumkuta akigaragara sebuleni kutokana na maumivu. Walimpeleka katika zahanati ya kibinafsi alikotibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani.
Majirani walisema wawili hao wamekuwa wakigombana mara kwa mara baada ya mwanamume huyo
kufutwa kazi miezi michache iliyopita.
Wakazi wa Mwanzo sasa wanalitaka Shirika la Maendeleo ya Wanaume kuingilia kati na kuokoa wanaume ambao wanadai wanadhulumiwa na kuchapwa na wake zao kila siku. Wanasema visa hivyo vimeongezeka mtaani humo. Aidha, wanataka wanaume hao wapewe ushauri wa kisheria kuwasaidia kutafuta usaidizi.
Mmoja wa wakazi, Justus Mwaniki, alisema wanaume wengi wanapigwa na wake zao kwa kuonekana kama mzigo nyumbani hasa wanapokosa kazi: “Sisi huwatunza wake zetu, na kukidhi mahitaji hao hata wakiwa hawana kazi na huleta nyumbani mapato yetu kwa matumizi ya familia. Mbona wadhulumu wanaume ambao hawana kazi?” alishangaa.
Majuzi, kiongozi wa Maendeleo ya Wanaume Nderitu Njoka alijipata taabani baada ya kukaripiwa na mwanamke mwenye nyumba kaunti ya Kiambu alipokuwa ameenda kumwoka mwanamume aliyedai alikuwa akizuiliwa na kudhulumiwa nyumbani.
Wakazi wa Mwanzo sasa wanalitaka Shirika la Maendeleo ya Wanaume kuingilia kati na kuokoa wanaume ambao wanadai wanadhulumiwa na kuchapwa na wake zao kila siku. Wanasema visa hivyo vimeongezeka mtaani humo. Aidha, wanataka wanaume hao wapewe ushauri wa kisheria kuwasaidia kutafuta usaidizi.
Mmoja wa wakazi, Justus Mwaniki, alisema wanaume wengi wanapigwa na wake zao kwa kuonekana kama mzigo nyumbani hasa wanapokosa kazi: “Sisi huwatunza wake zetu, na kukidhi mahitaji hao hata wakiwa hawana kazi na huleta nyumbani mapato yetu kwa matumizi ya familia. Mbona wadhulumu wanaume ambao hawana kazi?” alishangaa.
Majuzi, kiongozi wa Maendeleo ya Wanaume Nderitu Njoka alijipata taabani baada ya kukaripiwa na mwanamke mwenye nyumba kaunti ya Kiambu alipokuwa ameenda kumwoka mwanamume aliyedai alikuwa akizuiliwa na kudhulumiwa nyumbani.
CCM YAPATA UGENI KUTOKA PALESTINA

Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akimlaki Makamu Mwenyekiti
wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni
mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, alipowasili asubuhi hii, Uwanja
wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa ajili
ya ziara ya Kichama, hapa nchini. Pamoja naye ni Wajumbe wa NEC wa PLO,


Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akiwa na Makamu Mwenyekiti
wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni
mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, alipowasili asubuhi hii, Uwanja
wa Ndege wa Kimataifa wa Julisu Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa ajili
ya ziara ya Kichama, hapa nchini. Pamoja naye ni Wajumbe wa NEC wa PLO,
Jehad Zneed na Saleh Raafat (Kushoto). Wapili kulia ni Balozi wa
Palestina hapa nchini Dk. Nasri Abujasir.

Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akizingumza Makamu
Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid
ambaye pia ni mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, kwenye Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Kiongozi
huyo anatarajiwa kuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman
Kinana kuanzia saa 3.30 asubuhi hii, kwenye hoteli ya Protea Courtyard,
jijini Dar es Salaam
Subscribe to:
Posts (Atom)
