Facebook Comments Box

Thursday, June 13, 2013

SOMA NA DOWNLOAD HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA ALIYO IWASILISHA LEO BUNGENI KUHUSU MAKADIRIO YA BAJETI YA SEREKALI



MSANII LANGA KILEO AFARIKI DUNIA LEO

Photo: Msanii Langa Kileo (Maarufu kama Langa) amefariki dunia leo hii.

Langa alipelekwa hospitali akiwa hajitambui. Anadaiwa kuwa alikumbwa na Malaria kali sana, Hali iliyopelekea kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili jana.

Endelea kupata updates za kilichotokea na kinachotokea hapa -> http://j.mp/196omf9 




Langa Kileo (msanii wa Hip Hop Tanzania, pichani) amefariki dunia leo hii. Langa alipelekwa hospitali akiwa hajitambui. Anadaiwa kuwa alikumbwa na Malaria kali sana, Hali iliyopelekea kukimbizwa Hospitali ya Muhimbili jana. Uchunguzi wa chanzo cha kifo chake bado unaendelea. Msanii Langa aliwahi kutamba na kikundi cha Wakilisha pamoja na witness na sara ni miongoni mwa wasanii wakongwe wa bongo flava nchini Tanzania. Mungu amrehemu.
Baba wa marehemu Mzee Kileo amesema kuwa mtoto wake Langa kwenye picha amefariki dunia leo majira ya saa 10 katika hospitali ya Taifa Muhimbili.Taarifa kamili na mipango ya mazishi zitatolewa pale vikao vya familia vitakapofanywa.Pia baba yake alisema msiba huu umetokea wakati mama yake Langa hayupo Tanzania,alisema kwa sasa mama yake Langa yupo Marekani lakini baada ya kupewa taarifa hizo tayari ameshakata tiketi ya kurudi Tanzania na ataanza safari kesho.Msiba uko nyumbani kwao maeneo ya Mikocheni
Aminiel Aligaesha ambae ni Afisa Uhusiano wa hospitali ya Taifa Muhimbili amethibitisha kwamba msanii Langa amefariki dunia June 13 2013 saa kumi na moja jioni baada ya kufikishwa hospitalini hapo toka juzi jioni ambapo kutokana na sababu za kimaadili kwenye tiba, Muhimbili hospitali hawawezi kusema rapper huyu alikua anaumwa nini bali ndugu ndio wenye mamlaka ya kufanya hivyo.
Kwenye maelezo aliyoyatoa kwa millardayo.com Aminiel amesema Marehemu Langa alipokelewa kwenye idara ya wagonjwa wa magonjwa ya dharura usiku wa kuamkia jana na kupatiwa huduma ambapo leo June 13 2013 ndio alihamishiwa kwenye chumba cha wagonjwa Mahututi na baadae kufariki dunia.



WIMBO MPYA: LADY JAY DEE - YAHAYA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgZRc-6zgweWLXEnexB_JYoOpMZFkCbgUznz_4T69HIJTXITcCp25vwaNTEWgt1qnVQ65D7KALXR3_Ht7EodV1TChjp7M03AGxT3LhL1qxnLBqHiz29Kf2i5oenQYDB1mL7KohrCbZNyOE/s640/jay+dee.jpg 





VIDEO: ORIJINO KOMEDI WAKIELEZEA MKATABA WAO MPYA




VIDEO YA VANESSA MDEE - CLOSER




MWANA FA AKIZUNGUMZIA MKWARUZANO WAKE NA LADY JAY DEE





Wednesday, June 12, 2013

HII NDIO VIDEO YA MCHUNGAJI ALIENASWA AKIMTOMASA MUUMINI WAKE

clip_image002KATIKA  hali ya kushangaza , mchungaji mmoja huko nchini Nigeria amejikuta akiaibika baada ya video yake aliyokuwa  akimtomasa  mwanamke  wakati wa  maombi  kuvuja na kusambaa kitika mitandao mbali mbali ya kijamii.
Video hiyo ilirekodiwa kwa kutumia kamera zilizokuwa zimetegeshwa kitika ofisi ya mchungaji huyo bila yeye kujua.

Tazama video ya mchungaji huyo hapa
 

AMPIGA MUMEWE BAADA YA KUKUTA AKIANGALIA TV KABLA YA KUMALIZA KAZI ZA NYUMBANI

MWANAMUME mmoja katika mtaa wa Mwanzo, Eldoret anauguza majeraha baada ya kupigwa na mkewe kufuatia mzozo uliotokana na yeye kupatikana akitazama runinga kabla ya kumaliza kazi ya nyumbani.

Kwa mujibu wa majirani mkewe mwanamume huyo, alirejea nyumbani jioni kutoka kazini mnamo Jumatatu na kumkuta akitazama televisheni. Mara moja, alimrukia na kumpiga vibaya.

Mwanaume huyo aliokolewa na majirani waliofika kuitika kilio chake na kumkuta akigaragara sebuleni kutokana na maumivu. Walimpeleka katika zahanati ya kibinafsi alikotibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani.

Majirani walisema wawili hao wamekuwa wakigombana mara kwa mara baada ya mwanamume huyo
kufutwa kazi miezi michache iliyopita.

Wakazi wa Mwanzo sasa wanalitaka Shirika la Maendeleo ya Wanaume kuingilia kati na kuokoa wanaume ambao wanadai wanadhulumiwa na kuchapwa na wake zao kila siku. Wanasema visa hivyo vimeongezeka mtaani humo. Aidha, wanataka wanaume hao wapewe ushauri wa kisheria kuwasaidia kutafuta usaidizi.

Mmoja wa wakazi, Justus Mwaniki, alisema wanaume wengi wanapigwa na wake zao kwa kuonekana kama mzigo nyumbani hasa wanapokosa kazi: “Sisi huwatunza wake zetu, na kukidhi mahitaji hao hata wakiwa hawana kazi na huleta nyumbani mapato yetu kwa matumizi ya familia. Mbona wadhulumu wanaume ambao hawana kazi?” alishangaa.

Majuzi, kiongozi wa Maendeleo ya Wanaume Nderitu Njoka alijipata taabani baada ya kukaripiwa na mwanamke mwenye nyumba kaunti ya Kiambu alipokuwa ameenda kumwoka mwanamume aliyedai alikuwa akizuiliwa na kudhulumiwa nyumbani.


KIBONZO: KUSIGANA KWA MAONI YA CUF TANGANYIKA NA CUF ZANZIBAR

Picture


CCM YAPATA UGENI KUTOKA PALESTINA


Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akimlaki Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, alipowasili asubuhi hii, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara ya Kichama, hapa nchini. Pamoja naye ni Wajumbe wa NEC wa PLO,
Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, alipowasili asubuhi hii, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julisu Nyerere, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara ya Kichama, hapa nchini. Pamoja naye ni Wajumbe wa NEC wa PLO, Jehad Zneed na Saleh Raafat (Kushoto). Wapili kulia ni Balozi wa Palestina hapa nchini  Dk. Nasri Abujasir.
Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, akizingumza Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Ukombozi wa Palestina (PLO), Tayaseer Khalid ambaye pia ni mjube wa Halmashauri Kuu ya Chama hicho, kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Kiongozi huyo anatarajiwa kuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuanzia saa 3.30 asubuhi hii, kwenye hoteli ya Protea Courtyard, jijini Dar es Salaam


WIMBO MPYA WA CHRISTIAN BELLA




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU