Facebook Comments Box

Wednesday, May 29, 2013

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AENDELEA NA ZIARA YAKE CHINA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Rais wa China Xi jinping alipofika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Serikali wa Jamhuri hiyo
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwatambulisha Viongozi katika ujumbe aliofuatana nao kwa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Xi jinping, walipofika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Serikali wa Jamhuri hiyo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwatambulisha Viongozi katika ujumbe aliofuatana nao kwa Rais wa Jamhuri ya watu wa China Xi jinping, walipofika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Serikali wa Jamhuri hiyo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa nne kushoto)akiwa na ujumbe wake katika mazungumzo na Rais wa China Xi Jinping,(wane kulia) katika Ikulu ya Mjini Beijing Nchini China.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Makamo wa Rais wa China Li Yuanchao,katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwa katika  mazungumzo na  Makamo wa Rais wa China Li Yuanchao,katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia)akiwa katika  mazungumzo na Makamo wa Rais wa China Li Yuanchao,(kulia)katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,pamoja na ujumbe aliofuatana nao.
 Mke wa Rais wa Zanzibar mama Mwanamwema Shein akisalimiana na mke wa makamo wa Rais wa China Mama Li Yuanchao katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,pamoja na ujumbe aliofuatana nao.
  Mke wa Rais wa Zanzibar mama Mwanamwema Shein akisalimiana na  makamo wa Rais wa China Mama Li Yuanchao katika makaazi yake Mjini Beijing nchini China akiwa katika ziara ya mualiko wa Kiserikali wa Nchi hiyo,pamoja na ujumbe aliofuatana nao.




JIDE AAHIRISHA SHOO YAKE YA MIAKA 13 KUTOKANA NA KIFO CHA MSANII MWENZAKE ALBERT MANGWEA 'NGWEA'

Mwana Dada Komando katika mziki wa Bongo na mkongwe wa siku nyingi JUDITH WAMBURA 'Lady Jay Dee' Bint Machozi, Mamaa Somefood hayo yote ni majina yake si unajua tena sanaa, amesitisha onesho lake la kutimiza miaka 13 tangu aanze kufanya burudani lililokuwa lifanyike siku ya Ijumaa hii ya tar 31/05/2013 ndani ya Mjengo wake wa Nyumbani Lounge kutokana na Kifo cha Msanii mwenzake katika Bongo Fleva ambaye amepatwa na Msiba nje ya nchi huko Bondeni kwa MADIBA alikokwenda kutoa Show.
 
Jide amesema hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha Super Mix kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha East Africa Radio kwa masikitiko makubwa sana, na amesema show hiyo haitafanyika kama ilivyokuwa imepangwa na badala yake mpaka tarehe nyingine itakapo pangwa tena.


Tuesday, May 28, 2013

KIBADEN AANZA KASI RASMI SIMBA LEO

IMEWEKWA MEI 28, 2013 SAA 4:00 ASUBUHI
Kocha mpya wa Simba SC, Alhaj Abdallah Athumani Seif 'King Kibaden' au Chifu Mputa kulia akiwa na Wasaidizi wake, Jamhuri Mussa Kihwelo 'Julio' (katikati) na Suleiman Abdallah Matola 'Veron' kushoto kwenye Uwanja wa Kinesi, Urafiki, Dar es Salaam asubuhi ya leo wakati kabla ya kuanza usaili wa wachezaji waliojitokeza kuomba kusajiliwa katika timu hiyo. Kibaden ameanza rasmi kazi leo na atasaini mkataba kesho.


Wazee wa Kijiwe; Jamhuri kulia na Matola kushoto wakiwa nje ya Uwanja wakiangalia vijana waliojitokeza kuomba kusajiliwa Simba SC wakati wanacheza kuonyesha vipaji vyao


Mchezaji wa kiungo aliyewahi kuchezea timu ya taifa ya vijana chini ya Jamhuhi  Kihwelo, Samuel Ngassa naye amejitokeza kuomba nafasi Simba SC


Matola akimpa taarifa muhimu Kibadeni, anayeandika


Kibadeni kulia na Matola aliyeipa mgongo kamera ya BIN ZUBEIRY 


Tabasamu mwanana; Kibadeni akifurahia kazi mpya Simba SC


Katibu wa Simba SC, Evodius Mtawala kulia na Meneja wa timu za vijana za Simba SC, Patrick Rweyemamu kushoto


Mungu nisaidie Kibadeni anione; Mmoja wa vijana waliojitokeza kujaribu bahati zao Simba SC akisali kabla ya kuanza kwa usaili


Sala inaendelea


Anamalizia sala


Anafunga sala
SOURSE:BIN ZUBEIRY


MUIGIZAJI DR CHENI ALISHWA SUMU



Katika hali ya kushangaza na isiyo eleweka mwigizaji Mahsein Awadhi maarufu kama Dr. Cheni amekumbwa na balaa la kulishwa chakula chenye sumu weekend iliyopita alipokuwa kwenye sherehe moja ya harusi jijini Dar es Salaam alipohudhuria kama MC au mshereheshaji wa harusi hiyo.
Akiongea na bongo movies leo asubuhi, Dr. cheni alisema kuwa baada ya kumaliza kula chakula ambacho alipakuliwa na mmoja wa wahudumu wa sherehe hiyo alianza kujisikia vibaya na kuishiwa nguvu na aliamua kutoka nje kujaribu kupata hewa akidhani ladba ni joto la ukumbini ila hali ilizidi kuwa mbaya na aliamua kutafuta maziwa akihisi labda inaweza kuwa vidonda vya tumbo ndipo alipoanza kutapika na baadae kukumbizwa hospitalini na ndipo alipogungulika kuwa amelishwa chakula chenye sumu.
Tulipomuuliza labda sababu gani anahisi zinaweza kuwa zimepelekea watu hao kutaka kumdhuru alisema kuwa, mpaka sasa hajaweza kupata jibu kamili ila anaamini watu waliofanya hivyo wanamfahamu na wana nia mbaya sana kwake na sio watu wema.
Dr. Cheni alisema kuwa kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na moja ya watu walikuwa wa kwanza kufika hospitalini baada ya yeye kupatwa na majanga hayo ni mwigizaji Elizabeth Michael (LULU) ambaye kwa sasa yupo karibu sana na Dr. Cheni aliyekuwa mstari wa mbele katika kushughulikia mpaka kufanikisha suala la dhamana ya kesi iliyokuwa inamkabili mwanadada huyo.


HUYU NDIO ALIOKAMATWA AKIUZA UUME WA BINAADAMU


Jeshi la polisi nchini malawi wanamshikilia kijana mmoja baada ya kumkuta akiuza sehemu ya siri ya mwanaume.
Kijana huyo mwenye miaka 24 alikamatwa baada ya wananchi kutoa ripoti kituo cha polisi kuwa kunamzee kalala relini huku akiwa anatokwa damu nyingi 
 Polisi walifika eneo la tukio na kumkuta mzee huyo akiwa hoi na kuamua kumkimbiza hosipitali.

Baada ya kufikishwa hosipitali, madaktari  gundua kuwa mzee huyo alikuwa amejeruhiwa kwa kukatwa sehemu zake za siri...

Madaktari hao walilipoti kwa maofisa hao wa polisi na ndipo msako mkali ulipo pita katika wilaya ya Lakeshore mjini Salima na polisi hao kufanikiwa kumtia mbaroni kijana huyo baada ya kumkuta  akiwa katika gesti bubu akijaribu kuuza uume huo kwa dola za kimarekani 360.
  Mtuhumiwa Samuel Banda
Polisi walisema mtuhumiwa Samuel Banda alikamatwa na kiungo hicho ambacho alikuwa amekifunga katika karatasi nyeupe.

Mtuhumiwa alikiri kuwa huwa anauza viungo mbalimbali vya binadamu kwa wafanya biashara maarufu nchini humo ambao wanaamini wakivipata viungo hivyo huwasaidia katika biashara zao na huwaongezea utajiri.
 


Sunday, May 26, 2013

UAMSHO WAKUSANYA ZAIDI YA SAINI 60,000 ZA KUHOJI MUUNGANO WA TANZANIA


Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kislamu (JUMIKI) imekusanya zaidi ya majina elfu 60 na saini zao kwa ajili ya kudai kura ya maoni ya kukataa au kuukubali Muungano. Akitoa taarifa ya Jumuiya hiyo kwa wandishi wa habari huko hoteli ya Mazson, Naibu Amir wa Uamsho, Sheikh Haji Ali amesema jumuiya hiyo inaamini Muungano uliopo umefanywa bila ya ridhaa ya wananchi. Amesema hivi sasa umefika wakati kwa Wanzanzibari kudai kura ya maoni na mustakabali wa Zanzibar. Aidha, Sheikh Ali amesema Uamsho itaendelea na shughuli zake za kuelimisha, kutetea na kudai Zanzibar yenye mamlaka kamili Kitaifa na Kimataifa bila ya kuvunja sheria na taratibu za nchi. Amesema baadhi ya viongozi kwa utashi wao wa kisiasa wamejaribu kuzuia mihadhara ya Jumuiya hiyo, lakini hatua hiyo imefanyika nje ya sheria kwa vile Jumuiya hiyo imesajiliwa kisheria. Wakati huo huo, jumuiya hiyo imekanusha taarifa zainazoenezwa na vyombo vya habari na wanasiasa kuihusha na vurugu na vitendo vya uvunjifu wa amani ikiwemo uchomaji wa makanisa, maskani na mauaji.



PICHA MBALIMBALI ZA BOMU LILILOLIPUKA MAKAMBAKO JANA



 

Wanafunzi Wanne wa shule ya sekondari NABOTI iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Makambako wamejeruhiwa na Mlipuko wa Mabaki ya Bomu huku mmoja akipata Mshtuko wa Moyo kutokana na Mlipuko huo Baada ya Wanafunzi Takribani saba wa Kidato cha Kwanza kwenda kuyaokota Mabaki hayo kwenye Mlima uliopo Jirani na maeneo ya Jeshi.

Saturday, May 25, 2013

LIVE MATCH CENTRE: BAYERN MUNICH VS DORTMUND KWA PICHA ZINAZOTEMBEA NA PICHA ZA KAWAIDA

BAYERN MUNICH NDIO BINGWA WA UEFA 2012/2013
Screenshot2013-05-25at1
Screenshot2013-05-25at1

Alskdjf_original
Robben's akifunga goli zuri
Goal3_original
Gundogan's akifunga penati
Dante_original
Faulo iliyoleta penati
Goal2_original
Goli la Bayern katika muonekana mzuri

Goal1_original
Robben akimpa pasi Mandzukic alieutia mpira kimiani

.
Screenshot2013-05-25at12
Screenshot2013-05-25at12

Robben_original
Shuti la Robben's lilizuiliwa na sura ya  Weidenfeller's.
Save_original 
Kipa wa Dortmund Roman Weidenfeller. akaonesha maajabu kwa kuokoa mchomo huu

Lewandoski_original
Shuti la Lewandowski's lilizuiliwa na golikipa Manuel Neuer.

Screenshot2013-05-25at11
Will ana Jaden Smith nao wamehudhuria mchezo huu



VIDEO: ANGALIA RAIS ALIVYOKAMATWA AKIIBA PENI




VIDEO: LIVE PERFORMANCE YA NEY WA MITEGO NA DIAMOND







 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU