Facebook Comments Box

Tuesday, May 28, 2013

KIBADEN AANZA KASI RASMI SIMBA LEO

IMEWEKWA MEI 28, 2013 SAA 4:00 ASUBUHI
Kocha mpya wa Simba SC, Alhaj Abdallah Athumani Seif 'King Kibaden' au Chifu Mputa kulia akiwa na Wasaidizi wake, Jamhuri Mussa Kihwelo 'Julio' (katikati) na Suleiman Abdallah Matola 'Veron' kushoto kwenye Uwanja wa Kinesi, Urafiki, Dar es Salaam asubuhi ya leo wakati kabla ya kuanza usaili wa wachezaji waliojitokeza kuomba kusajiliwa katika timu hiyo. Kibaden ameanza rasmi kazi leo na atasaini mkataba kesho.


Wazee wa Kijiwe; Jamhuri kulia na Matola kushoto wakiwa nje ya Uwanja wakiangalia vijana waliojitokeza kuomba kusajiliwa Simba SC wakati wanacheza kuonyesha vipaji vyao


Mchezaji wa kiungo aliyewahi kuchezea timu ya taifa ya vijana chini ya Jamhuhi  Kihwelo, Samuel Ngassa naye amejitokeza kuomba nafasi Simba SC


Matola akimpa taarifa muhimu Kibadeni, anayeandika


Kibadeni kulia na Matola aliyeipa mgongo kamera ya BIN ZUBEIRY 


Tabasamu mwanana; Kibadeni akifurahia kazi mpya Simba SC


Katibu wa Simba SC, Evodius Mtawala kulia na Meneja wa timu za vijana za Simba SC, Patrick Rweyemamu kushoto


Mungu nisaidie Kibadeni anione; Mmoja wa vijana waliojitokeza kujaribu bahati zao Simba SC akisali kabla ya kuanza kwa usaili


Sala inaendelea


Anamalizia sala


Anafunga sala
SOURSE:BIN ZUBEIRY


MUIGIZAJI DR CHENI ALISHWA SUMU



Katika hali ya kushangaza na isiyo eleweka mwigizaji Mahsein Awadhi maarufu kama Dr. Cheni amekumbwa na balaa la kulishwa chakula chenye sumu weekend iliyopita alipokuwa kwenye sherehe moja ya harusi jijini Dar es Salaam alipohudhuria kama MC au mshereheshaji wa harusi hiyo.
Akiongea na bongo movies leo asubuhi, Dr. cheni alisema kuwa baada ya kumaliza kula chakula ambacho alipakuliwa na mmoja wa wahudumu wa sherehe hiyo alianza kujisikia vibaya na kuishiwa nguvu na aliamua kutoka nje kujaribu kupata hewa akidhani ladba ni joto la ukumbini ila hali ilizidi kuwa mbaya na aliamua kutafuta maziwa akihisi labda inaweza kuwa vidonda vya tumbo ndipo alipoanza kutapika na baadae kukumbizwa hospitalini na ndipo alipogungulika kuwa amelishwa chakula chenye sumu.
Tulipomuuliza labda sababu gani anahisi zinaweza kuwa zimepelekea watu hao kutaka kumdhuru alisema kuwa, mpaka sasa hajaweza kupata jibu kamili ila anaamini watu waliofanya hivyo wanamfahamu na wana nia mbaya sana kwake na sio watu wema.
Dr. Cheni alisema kuwa kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na moja ya watu walikuwa wa kwanza kufika hospitalini baada ya yeye kupatwa na majanga hayo ni mwigizaji Elizabeth Michael (LULU) ambaye kwa sasa yupo karibu sana na Dr. Cheni aliyekuwa mstari wa mbele katika kushughulikia mpaka kufanikisha suala la dhamana ya kesi iliyokuwa inamkabili mwanadada huyo.


HUYU NDIO ALIOKAMATWA AKIUZA UUME WA BINAADAMU


Jeshi la polisi nchini malawi wanamshikilia kijana mmoja baada ya kumkuta akiuza sehemu ya siri ya mwanaume.
Kijana huyo mwenye miaka 24 alikamatwa baada ya wananchi kutoa ripoti kituo cha polisi kuwa kunamzee kalala relini huku akiwa anatokwa damu nyingi 
 Polisi walifika eneo la tukio na kumkuta mzee huyo akiwa hoi na kuamua kumkimbiza hosipitali.

Baada ya kufikishwa hosipitali, madaktari  gundua kuwa mzee huyo alikuwa amejeruhiwa kwa kukatwa sehemu zake za siri...

Madaktari hao walilipoti kwa maofisa hao wa polisi na ndipo msako mkali ulipo pita katika wilaya ya Lakeshore mjini Salima na polisi hao kufanikiwa kumtia mbaroni kijana huyo baada ya kumkuta  akiwa katika gesti bubu akijaribu kuuza uume huo kwa dola za kimarekani 360.
  Mtuhumiwa Samuel Banda
Polisi walisema mtuhumiwa Samuel Banda alikamatwa na kiungo hicho ambacho alikuwa amekifunga katika karatasi nyeupe.

Mtuhumiwa alikiri kuwa huwa anauza viungo mbalimbali vya binadamu kwa wafanya biashara maarufu nchini humo ambao wanaamini wakivipata viungo hivyo huwasaidia katika biashara zao na huwaongezea utajiri.
 


Sunday, May 26, 2013

UAMSHO WAKUSANYA ZAIDI YA SAINI 60,000 ZA KUHOJI MUUNGANO WA TANZANIA


Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kislamu (JUMIKI) imekusanya zaidi ya majina elfu 60 na saini zao kwa ajili ya kudai kura ya maoni ya kukataa au kuukubali Muungano. Akitoa taarifa ya Jumuiya hiyo kwa wandishi wa habari huko hoteli ya Mazson, Naibu Amir wa Uamsho, Sheikh Haji Ali amesema jumuiya hiyo inaamini Muungano uliopo umefanywa bila ya ridhaa ya wananchi. Amesema hivi sasa umefika wakati kwa Wanzanzibari kudai kura ya maoni na mustakabali wa Zanzibar. Aidha, Sheikh Ali amesema Uamsho itaendelea na shughuli zake za kuelimisha, kutetea na kudai Zanzibar yenye mamlaka kamili Kitaifa na Kimataifa bila ya kuvunja sheria na taratibu za nchi. Amesema baadhi ya viongozi kwa utashi wao wa kisiasa wamejaribu kuzuia mihadhara ya Jumuiya hiyo, lakini hatua hiyo imefanyika nje ya sheria kwa vile Jumuiya hiyo imesajiliwa kisheria. Wakati huo huo, jumuiya hiyo imekanusha taarifa zainazoenezwa na vyombo vya habari na wanasiasa kuihusha na vurugu na vitendo vya uvunjifu wa amani ikiwemo uchomaji wa makanisa, maskani na mauaji.



PICHA MBALIMBALI ZA BOMU LILILOLIPUKA MAKAMBAKO JANA



 

Wanafunzi Wanne wa shule ya sekondari NABOTI iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Makambako wamejeruhiwa na Mlipuko wa Mabaki ya Bomu huku mmoja akipata Mshtuko wa Moyo kutokana na Mlipuko huo Baada ya Wanafunzi Takribani saba wa Kidato cha Kwanza kwenda kuyaokota Mabaki hayo kwenye Mlima uliopo Jirani na maeneo ya Jeshi.

Saturday, May 25, 2013

LIVE MATCH CENTRE: BAYERN MUNICH VS DORTMUND KWA PICHA ZINAZOTEMBEA NA PICHA ZA KAWAIDA

BAYERN MUNICH NDIO BINGWA WA UEFA 2012/2013
Screenshot2013-05-25at1
Screenshot2013-05-25at1

Alskdjf_original
Robben's akifunga goli zuri
Goal3_original
Gundogan's akifunga penati
Dante_original
Faulo iliyoleta penati
Goal2_original
Goli la Bayern katika muonekana mzuri

Goal1_original
Robben akimpa pasi Mandzukic alieutia mpira kimiani

.
Screenshot2013-05-25at12
Screenshot2013-05-25at12

Robben_original
Shuti la Robben's lilizuiliwa na sura ya  Weidenfeller's.
Save_original 
Kipa wa Dortmund Roman Weidenfeller. akaonesha maajabu kwa kuokoa mchomo huu

Lewandoski_original
Shuti la Lewandowski's lilizuiliwa na golikipa Manuel Neuer.

Screenshot2013-05-25at11
Will ana Jaden Smith nao wamehudhuria mchezo huu



VIDEO: ANGALIA RAIS ALIVYOKAMATWA AKIIBA PENI




VIDEO: LIVE PERFORMANCE YA NEY WA MITEGO NA DIAMOND







HAWA NDIO WACHEZAJI WATATU WALIOSAJILIWA NA SIMBA JANA

SIMBA SC usiku wa jana imesaini wachezaji watatu wapya kwa mpigo, akiwemo mshambuliaji hatari wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Zahor Iddi Pazi ambaye msimu uliopita alikuwa anatakiwa na Yanga SC akatimkia Azam FC.
Zahoro Pazi
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema leo kwamba, mbali na Zahor anayechezea JKT Ruvu kwa mkopo akitokea Azam FC, wengine waliosajiliwa ni kipa Andrew Ntala kutoka Kagera Sugar na beki Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ kutoka Mtibwa Sugar.
Poppe, ambaye ni Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) alisema wachezaji wote wamesaini mikataba ya miaka miwili kila mmoja.
“Bado tunaendelea na usajili wetu kwa umakini na kimya kimya. Nataka nirudie kusema kwamba, sera ya Simba SC si kusajili kutoka Yanga SC. Bali wao Yanga ndio wanasajili kwetu. 
Nashangaa jana Katibu wao (Lawrence Mwalusako) ametamba ameniziba mimi mdomo baada ya kumsaini Haruna Niyonzima,”.
“Yule ni mchezaji wao, na sisi hatujawahi kutoa tamko la kumtaka yule mchezaji. Kama alikuwa anawatia presha ili wampe fedha nyingi kwa kuwahadaa Simba wanamtaka, amefanikiwa, ila sisi hakuwa kabisa katika mipango yetu,”alisema Poppe.
Poppe amesema Simba SC wanasajili kisayansi na si kama wapinzani wao hao, Yanga SC ambao wanaingia hasara ya fedha nyingi na wanacheza pata potea.
“Sisi tulimsajili Mbuyu Twite kama yeye tu, lakini wao wakaingilia akawapa sharti wamsajili na ndugu yake (Kabange Twite), wakaingia mkenge wakasajili mtu ambaye wamemlipa fedha nyingi, lakini hawajamtumia na hakuwa chaguo lao,”.
Issa Rashid akipambana na Simon Msuva wa Yanga
“Sasa sisi hatuna ulimbukeni wa aina ile katika kusajili, tunafanya mambo yetu kisayansi, na ndiyo maana wachezaji tunaosajili wanakuwa lulu na baadaye tunawauza nje kwa fedha nyingi tunapata faida kubwa, angalia Patrick Ochan, Emanuel Okwi na Mbwana Samatta. “Biashara nzuri sana. Hatukutumia hata Sh. Milioni 100 katika usajili wao, wameingiza karibu Milioni 700, Yanga wanaweza?”alihoji Poppe.
Poppe alisema pamoja na kusaini watatu hao wapya, Simba SC imewapa mikataba wachezaji wake kadhaa chipukizi waliopandishwa kutoka kikosi cha pili, akiwemo Haruna Chanongo ambaye alikuwa kwenye rada za Yanga pia.
Kusajiliwa kwa watatu hao wapya, kunafanya idadi ya wachezaji wapya waliosajiliwa Simba SC kufika wanne, baada ya Twaha Shekuwe ‘Messi’ wa Coastal Union kuwa mchezaji wa kwanza mpya kusajiliwa katika timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao.
Lakini Simba SC, tayari imempoteza mchezaji mmoja, Mrisho Ngassa ambaye amesajiliwa na watani wa jadi, Yanga SC.

SOURSE: BIN ZUBEIRY

PICHA: SHABIKI WA YANGA ANAELIA YANGA IKIFUNGWA AKIONESHA TIKETI YAKE YA KUANGALIA FAINALI YA UEFA LEO USIKU

#UEFA Shabiki Steven wa Yanga nae katisha!! atachekia mechi Golden Tulip leo usiku, nitatoa zawadi ya vocha kwa watu watano wa mwanzo watakaopatia kwa kuniandikia hapa, anza sasa hivi mtu wangu
Yule shabiki wa Yanga maarufu kama mzee wa uungwana akifurahi na tiketi yake ya kuangalia mechi ya Uefa leo kwenye hoteli ya Golden Tulip


JOSE MORINHO AKUBALI MKATABA WA MIAKA MINNE CHELSEA

Mitando mbalimbali maarufu ya Uingereza imeripoti kuwa Kocha JOSE MOURINHO atakwenda uingereza tarehe 2 mwezi wa 6 kwa ajili ya kutia saini mkataba wa miaka minne ambao utakuwa na thamani ya Paundi 250,000 kwa wiki.

Tajiri wa Chelsea amemuhakikishia kuwa hizo fedha zinazokaribia paundi milioni 50 zipo kwa ajili ya mkataba huo. Hilo litamfanya haraka baada ya mechi ya Real Madrid na Osasunaambayo ndio mechi ya mwisho kwa Real Madrid msimu huu kutompotezea muda kocha huyo maana baada ya mechi hiyo atapanda ndege na kwenda uingereza kwa ajili ya mkataba huo. Katika safari hiyo ataongozana na kocha wa viungo Rui Faria na kocha wa magolikipa Salvino Louro.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU