Saturday, May 25, 2013
HAWA NDIO WACHEZAJI WATATU WALIOSAJILIWA NA SIMBA JANA
![]() |
| Zahoro Pazi |
Poppe, ambaye ni Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) alisema wachezaji wote wamesaini mikataba ya miaka miwili kila mmoja. “Bado tunaendelea na usajili wetu kwa umakini na kimya kimya. Nataka nirudie kusema kwamba, sera ya Simba SC si kusajili kutoka Yanga SC. Bali wao Yanga ndio wanasajili kwetu.
Nashangaa jana Katibu wao (Lawrence Mwalusako) ametamba ameniziba mimi mdomo baada ya kumsaini Haruna Niyonzima,”.
“Yule ni mchezaji wao, na sisi hatujawahi kutoa tamko la kumtaka yule mchezaji. Kama alikuwa anawatia presha ili wampe fedha nyingi kwa kuwahadaa Simba wanamtaka, amefanikiwa, ila sisi hakuwa kabisa katika mipango yetu,”alisema Poppe.
Poppe amesema Simba SC wanasajili kisayansi na si kama wapinzani wao hao, Yanga SC ambao wanaingia hasara ya fedha nyingi na wanacheza pata potea.
“Sisi tulimsajili Mbuyu Twite kama yeye tu, lakini wao wakaingilia akawapa sharti wamsajili na ndugu yake (Kabange Twite), wakaingia mkenge wakasajili mtu ambaye wamemlipa fedha nyingi, lakini hawajamtumia na hakuwa chaguo lao,”.
![]() |
| Issa Rashid akipambana na Simon Msuva wa Yanga |
Poppe alisema pamoja na kusaini watatu hao wapya, Simba SC imewapa mikataba wachezaji wake kadhaa chipukizi waliopandishwa kutoka kikosi cha pili, akiwemo Haruna Chanongo ambaye alikuwa kwenye rada za Yanga pia.
Kusajiliwa kwa watatu hao wapya, kunafanya idadi ya wachezaji wapya waliosajiliwa Simba SC kufika wanne, baada ya Twaha Shekuwe ‘Messi’ wa Coastal Union kuwa mchezaji wa kwanza mpya kusajiliwa katika timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao.
Lakini Simba SC, tayari imempoteza mchezaji mmoja, Mrisho Ngassa ambaye amesajiliwa na watani wa jadi, Yanga SC.
SOURSE: BIN ZUBEIRY
PICHA: SHABIKI WA YANGA ANAELIA YANGA IKIFUNGWA AKIONESHA TIKETI YAKE YA KUANGALIA FAINALI YA UEFA LEO USIKU
| Yule shabiki wa Yanga maarufu kama mzee wa uungwana akifurahi na tiketi yake ya kuangalia mechi ya Uefa leo kwenye hoteli ya Golden Tulip |
JOSE MORINHO AKUBALI MKATABA WA MIAKA MINNE CHELSEA
Mitando mbalimbali maarufu ya Uingereza imeripoti kuwa Kocha JOSE MOURINHO atakwenda uingereza tarehe 2 mwezi wa 6 kwa ajili ya kutia saini mkataba wa miaka minne ambao utakuwa na thamani ya Paundi 250,000 kwa wiki. Tajiri wa Chelsea amemuhakikishia kuwa hizo fedha zinazokaribia paundi milioni 50 zipo kwa ajili ya mkataba huo. Hilo litamfanya haraka baada ya mechi ya Real Madrid na Osasunaambayo ndio mechi ya mwisho kwa Real Madrid msimu huu kutompotezea muda kocha huyo maana baada ya mechi hiyo atapanda ndege na kwenda uingereza kwa ajili ya mkataba huo. Katika safari hiyo ataongozana na kocha wa viungo Rui Faria na kocha wa magolikipa Salvino Louro.
Friday, May 24, 2013
BREAKING NEWS: AMRI KIEMBA ASAINI YANGA
WAKATI Haruna Niyonziam
akiwa amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Yanga, habari zilizotufikia
hivi punde zinasema kiungo wa Simba, Amri Kiemba amesajiliwa na Yanga tayari
kwa kuitumikia timu hiyo kwa msimu ujao.
Akizungumza na mtandao
huu, mtu mmoja kutoka kamati ya usajili ya Yanga, amesema Kiemba amesajiliwa kwa
mkataba wa miaka miwili ili kuongoza nguvu katika safu ya usajili ya Yanga.
Mtandao huu unaahidi kuwasiliana
na Kiemba muda mfupi atakapotoka mazoezini katika kambi ya Taifa Stars
kujiandaa na mechi ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2014.
Atakapotoka mazoezini mtandao
huu utawasiliana naye kiungo huyo ili aweze kueleza ukweli juu ya usajili wake
kwa Yanga.
Kiemba aliwahi
kuichezea Yanga miaka ya nyuma kabla ya kutimka katika timu hiyo.
SOURSE: SHAFFIH DAUDA
M23 KUIVAMIA TANZANIA; WANANCHI WA KAGERA WATAHADHARISHWA

Serikali ya Mkoa wa Kagera imewatahadharisha wananchi wake kuepukana na wageni wasiowafahamu kwenye maeneo yao kutokana na tishio la kikosi chaM 23 cha nchini Congo DRC kinachotishia kuivamia Tanzania...
Kumekuwa na mapigano makali kati ya waasi waM23 na vikosi vya serikali nchini Congo ambako jeshi letu lipo huko...
Waasi hao wametishia kuivamia Tanzania muda wowote ili kulipiza kisasi.Miongoni mwa mipaka ambayo iko wazi ni Kagera, na hii ndo sababu iliyopelekea serikali ya Mkoa huo kutoa tahadhari kwa wananchi wake na watanzania kwa ujumla....
HATIMAYE NIYONZIMA ASAINI YANGA MIAKA MIWILI
HATIMAYE
kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Hakizimana Fadhili Niyonzima
amesaini mkataba wa miaka miwili zaidi kuendelea kuichezea Yanga SC na
klabu hiyo asubuhi ya leo imetangaza rasmi kuongeza mkataba na mchezaji
huyo wa zamani wa APR na Rayon za kwao.
Kulikuwa kuna mvutano mkubwa kati ya Yanga SC na Haruna juu ya mkataba mpya na kiungo huyo ilikuwa aondoke kesho kurejea kwao, bila kusaini mkataba mpya.
Hata hivyo, kutokana na kuwapo kwa taarifa kwamba Simba SC imemtengea dau la Sh. Milioni 70 na Azam FC pia inamtaka kwa dau nono zaidi, Yanga imekubali kila alichoomba Haruna katika mkataba mpya na wamemalizana.
Kulikuwa kuna mvutano mkubwa kati ya Yanga SC na Haruna juu ya mkataba mpya na kiungo huyo ilikuwa aondoke kesho kurejea kwao, bila kusaini mkataba mpya.
Hata hivyo, kutokana na kuwapo kwa taarifa kwamba Simba SC imemtengea dau la Sh. Milioni 70 na Azam FC pia inamtaka kwa dau nono zaidi, Yanga imekubali kila alichoomba Haruna katika mkataba mpya na wamemalizana.
Akiongea na waandishi wa habari makao ya klabu ya Yanga, katibu mkuu
Lawrence Mwalusako amesema wameamua kumuongezea mkataba mchezaji huyo
kufuatia kuuhitaji mchango wake kwani katika kipindi chake cha miaka
miwili ameonyesha kiwango cha hali ya juu na kutoa mchango mkubwa.
Mwalusako amesema kumekua yakiongelewa mengi juu ya mchezaji wetu Niyonzima, baadhi ya vyombo vya habari vimekua vikitoa taarifa za kupotosha juu yake ukweli leo umedhihirika kwamba Niyonzima ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kuitumikia kwa miaka miwili.
Haruna Niyonzima alijiunga na Yanga kwa mara ya kwanza Julai 2011 akitokea katika timu ya APR nchini Rwanda ambapo katika miaka yake miwili aliyoichezea timu ya Yanga amefanikiwa kuisadia kupata makombe mawili ya ubingwa wa Ligi Kuu 2012-2013 na Kombe la Kagame 2011-2012.
Naye Niyonzima amesema anawashukuru wanachama, washabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga kwa kuwa naye muda wote, Yanga ni nyumbani kwangu kwani najisikia furaha kuichezea timu hii na malengo yangu ni kuisadia ili iweze kufanya vizuri katika upatashindano ya kimataifa.
Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu ya Yanga Abdallah BinKleb amesema palikua na propaganda nyingi juu ya Niyonzima, lakini ukweli ndio huu Niyonzima ataendelea kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili.
"Tunautambua mchango wake alioutoa kwa miaka mwili kwani ameweza kutupatia vikombe viwili vya Ligi Kuu ya Vodacom na Kombe la Kagame hivyo tumemuongezea mkataba wa miaka miwili tena ili aendelee kutoa mchango wake na kuisadia timu katika michezo ya kimataifa" alisema BinKleb
SOURSE: BIN ZUBEIRYMwalusako amesema kumekua yakiongelewa mengi juu ya mchezaji wetu Niyonzima, baadhi ya vyombo vya habari vimekua vikitoa taarifa za kupotosha juu yake ukweli leo umedhihirika kwamba Niyonzima ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kuitumikia kwa miaka miwili.
Haruna Niyonzima alijiunga na Yanga kwa mara ya kwanza Julai 2011 akitokea katika timu ya APR nchini Rwanda ambapo katika miaka yake miwili aliyoichezea timu ya Yanga amefanikiwa kuisadia kupata makombe mawili ya ubingwa wa Ligi Kuu 2012-2013 na Kombe la Kagame 2011-2012.
Naye Niyonzima amesema anawashukuru wanachama, washabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga kwa kuwa naye muda wote, Yanga ni nyumbani kwangu kwani najisikia furaha kuichezea timu hii na malengo yangu ni kuisadia ili iweze kufanya vizuri katika upatashindano ya kimataifa.
Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu ya Yanga Abdallah BinKleb amesema palikua na propaganda nyingi juu ya Niyonzima, lakini ukweli ndio huu Niyonzima ataendelea kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili.
"Tunautambua mchango wake alioutoa kwa miaka mwili kwani ameweza kutupatia vikombe viwili vya Ligi Kuu ya Vodacom na Kombe la Kagame hivyo tumemuongezea mkataba wa miaka miwili tena ili aendelee kutoa mchango wake na kuisadia timu katika michezo ya kimataifa" alisema BinKleb
Thursday, May 23, 2013
MAJAMBAZI WAMELIVAMIA HILI GARI NA KUPORA PESA LEO

Matundu matatu ya risasi katika kioo cha gari lililovamiwa na majambazi.
![]() |
| Wanausalama barabarani wakichukua taarifa eneo la tukio. |
Majambazi
yaliyokuwa na silaha aina ya SMG yakiwa na pikipiki aina ya Bajaj Boxer
yamevamia gari ndogo aina ya VITZ N a kuwajeruhi watu wawili wenye
asili ya asia na kupora kiasi cha fedha ambacho bado thamani yake
haijafahamika mara moja.
SHEHA AMWAGIWA TINDIKALI ZANZIBAR
\
Sheha
Mohammed Omary Said aliyemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana akiwa
katika hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja akipatiwa matibabu, Sheikh
Mohammed amepata maumivu makali sehemu za kifuwa na jicho kuumia
Kamanda
wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mukhadam Khamis,amesema chombo
kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la tukio
na kwamba polisi imekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili kugundua
aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole.
Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua.
Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua.
Sheha
Mohammed Kidevu akiwa katika wodi ya Hospitali kuu ya Rufaa Mnazi Mmoja
akipata matibabu ya majaraha ya kitu kinachosadikiwa kwa Tindi
Kali,akipata matibabu hayo katika hospitali hiyo.
BUNGE LA AHIRISHWA TENA LEO
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Anna Makinda
ameliahirisha tena bunge leo asubuhi ili kupisha kamati ya uongozi ya
Bunge iendelee kukutana ili kutoa maamuzi na tamko kuhusu vurugu za
Mtwara zilizojotokeza jana na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia na
uharibifu mbalimbali kutokea ikiwemo kuchomwa moto nyumba za viongozi wa
serikali,chama cha mapinduzi na nyumba ya mwandishi wa habari wa TBC.

Subscribe to:
Posts (Atom)






