Facebook Comments Box

Saturday, May 18, 2013

MPAMBANO WA YANGA NA SIMBA KATIKA PICHA


Haruna Shamte akipambana na Simon Msuva wa Yanga.
   
Nahodha wa Yanga Nadir Haroub akinyanyua ubingwa wa ligi kuu ya VODACOM msimu wa 2012/2013
   


kikosi cha Simba kilichoanza hii leo.
  
Makocha wa Yanga Ernest Brandts pamoja na Felix Minziro wakijadiliana jambo.
   




Sir Juma Nature pia alikuwepo kutoa burudani.
   




  Hili ndo lilikuwa bao la kwanza la Yanga lilifungwa na Didier Kavumbagu kwa kichwa.

Mrisho Ngassa akiwa amevalishwa jezi ya YANGA kwa mara nyingine tena huku akiwa amefurahi kweli kweli.
  



Mwamuzi wa mchezo wa leo Saanya akiwa chini mara baada ya kuumia.
   

ATHUMAN IDD "CHUJI" ACHAGULIWA MCHEZAJI BORA

Athuman Idd Chuji


Kiungo mkongwe wa Athumani Idd ‘Chuji’ ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa mechi ya watani.

Chuji aliyecheza namba sita katika mechi ya watani leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar amekuwa mchezaji bora wa mechi hiyo.

aliouonyesha  uwezo mkubwa SuperSport imemtanza Chuji kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.


Chuji aliwathibiti washambuliaji wa Simba na ndiye alikuwa akianzisha mashambulizi karibu yote ya Yanga.

Chuji alipiga zaidi ya pasi nne ndefu ambazo zilifika, pia alikuwa akimchezesha kiungo Haruna Niyonzima ambaye pia alimtumia kama sehemu ya kuhifadhi mipira anapokwama.


VIDEO: USHAHIDI WA WANAJESHI WA ISRAELI KUINGIA SYRIA NA KUPIGA




KIBONZO: NANI KUIBUKA MBABE KATI YA YANGA NA SIMBA



Photo



ELIMU YA MSINGI KUWA MIAKA 10

The Minister for Education and Vocational Training, Dr Shukuru KawambwaWAZIRI KAWAMBWA.WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI WAKIWA DARASANI.
RASIMU ya Sera ya Elimu na Mafunzo nchini inapendekeza kuunganisha elimu ya msingi na sekondari ya kawaida ya sasa ili kuunda elimu-msingi itakayotolewa kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2018, imefahamika. 
Rasimu ya kwanza ya Sera hiyo imeshakamilika na sasa wadau mbalimbali wanatoa mapendekezo yao kuiboresha, kabla ya kupelekwa bungeni ili kutungiwa sheria.
Aidha, mikakati hiyo itakayotekelezwa ni kuhuisha muundo na utaratibu mpya wa elimu na mafunzo kwa kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa miaka mitatu na mitano anapitia elimu ya awali kwa kipindi kisichop
ungua mwaka mmoja kabla ya kujiunga na elimu-msingi.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alithibitisha kwa gazeti hili wiki hii mjini hapa kuhusu kukamilika kwa rasimu ya kwanza ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2013.
“Ni kweli Sera hiyo imekamilika baada ya kuandaliwa kwa miaka mitatu. Imepita kwa wadau mbalimbali, mashuleni, vyuoni na katika taasisi mbalimbali nchini ambao wametoa maoni yao. 
“Jumapili (kesho) tunatarajia kuwa waheshimiwa wabunge nao watapata fursa ya kuijadili na kutoa maoni yao katika semina iliyoandaliwa maalumu kwao,” alisema Mulugo katika Viwanja vya Bunge.
Alisema baada ya maoni hao ya wabunge, watapeleka Rasimu hiyo kwa mamlaka husika kwa ajili ya andiko la mwisho kabla ya kupelekwa katika Bunge lijalo ili itungwe sheria kuhusu Sera ya Elimu na Mafunzo.
Hata hivyo, semina hiyo huenda isifanyike kesho kutokana na kuingiliana na ratiba nyingine, kwani wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) watakuwa na mkutano na Mwenyekiti wao wa Taifa, Rais Jakaya Kikwete, kwenye Ukumbi wa White House mjini hapa.
Wiki moja iliyopita, wakati akiongoza kikao, Spika wa Bunge, Anne Makinda aliwaambia wabunge kuwa makabrasha waliyokuwa wakipewa na wahudumu ni kuhusu Sera ya Elimu na hivyo waende wakayasome, kwani kuna siku wataijadili.
Kwa mujibu wa rasimu, mambo mengine yanayotarajiwa kutekelezwa na Sera ni kuhuisha mitaala ya sasa ya elimu ili ikidhi muundo mpya wa elimu na mafunzo, kuhuisha sheria na taratibu mbalimbali za utoaji elimu ili ziendane na muundo mpya wa elimu-msingi.
Kuimarisha mfumo wa usimamizi, ithibati na udhibiti wa utoaji wa elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali ili kukidhi malengo na muundo mpya wa elimu-msingi.
Nyingine ni kuongeza ubora wa miundombinu katika shule za sasa za msingi ili kukidhi mahitaji na malengo ya elimu-msingi ikiwa ni pamoja na kuongeza madarasa ya elimu-msingi katika kila shule ya msingi ya sasa, kujenga maabara za sayansi na maktaba katika kila shule ya elimu-msingi.
“Kutenga rasilimali fedha za kutosha kwa ajili ya nyenzo, vifaa na zana za kufundishia na kujifunzia, vitabu vya kiada na ziada, maandiko, machapisho ya maktaba pamoja na vifaa vya maabara,” ilieleza rasimi hiyo ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. 
Kuimarisha matumizi ya lugha za Kiswahili na Kiingereza katika ngazi ya elimu – msingi kama lugha za kujifunzia na kuwasiliana.
Kuweka utaratibu utakaohakikisha kuwa wanafunzi wanaomaliza elimu na mafunzo ngazi husika kwa ufanisi na wale wanaokatisha masomo au mafunzo yao kwa sababu mbalimbali, wanaendelea na kuhitimu masomo au mafunzo yao katika mfumo rasmi wa elimu na mafunzo. 
Jambo jingine litakalotekelezwa ni kutoa elimu kwa umma kuhusu madhumuni, malengo na matarajio ya Sera mpya ya Elimu na Mafunzo.
Rasimu ilieleza kuwa mambo chanja yanayotarajiwa kupatikana baada ya mkakati kutekelezwa ni kuwepo kwa elimu ya awali ya lazima kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja kabla ya kujiunga na elimu msingi, kuwepo kwa elimu msingi ya miaka 10 kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne cha sasa kwa watoto wote wenye rika la kwenda shule.
Matokeo mengine ni kuwepo kwa mfumo nyumbufu, miundo na taratibu za kujiendeleza katika mikondo anuai ya kitaalamu na kitaaluma, kuwepo kwa elimu na mafunzo yenye viwango, ubora na sifa zinazotambulika kitaifa, kikanda na kimataifa.
“Kuwepo kwa fursa mbalimbali za elimu na mafunzo zinazokidhi mahitaji ya wananchi na ya nchi kiuchumi, kijamii, kisayansi na kiteknolojia.
“Kuwepo kwa ugharimiaji endelevu wa elimu na mafunzo na kuwepo kwa mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia masuala mtambuka,” ilifafanua Rasimu ya Sera ya Elimu na Mafunzo.
Kuhusu elimu ya awali, ilieleza kuwa mkakati ni kuweka vigezo, viwango na taratibu ili elimu ya awali iwe ya lazima na itolewe katika kila shule ya elimu – msingi, na kuwa sheria, miongozo na taratibu kuhusu elimu hiyo lazima kuwekwa na kutekelezwa ifikapo mwaka 2018.
Katika elimu msingi, ni kuwa ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne, na kutolewa kwa miaka 10 na umri wa kuanza darasa la kwanza kuwa kati ya miaka minne hadi sita kulingana na uwezo wa mtoto kumudu masomo katika ngazi husika.
Shabaha katika eneo hili ni sheria na miongozo kuhusu elimu-msingi kuwekwa na kutekelezwa ifikapo mwaka 2016, mpango wa utekelezaji wa utoaji wa elimu-msingi kuwepo ifikapo mwaka 2018 na elimu-msingi kutolewa ifikapo 2018.
Kwa mujibu wa dibaji ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, Sera mpya imeandaliwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau ikitilia maanani mafanikio yaliyoletwa na Sera zilizotangulia na kulifanya Taifa kupiga hatua katika nyanja za elimu na mafunzo.
“Sera kuu zilikuwa ni Sera ya Elimu na Mafunzo 1995, Sera ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo 1996 na Sera ya Taifa ya Elimu ya Juu 1999 ambazo zilitekelewa sambamba na sera nyingine ambazo zinaigusa sekta ya elimu na mafunzo kama vile Sera ya Sayansi na Teknolojia 1996, Sera ya Habari na Utangazaji 2003, Sera ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na ya Binafsi 2009 pamoja na nyingine za aina hiyo,” alisema Dk Kawambwa.

AMA KWELI KUISHI KWINGI KUONA MENGI JIONEE MERCEDES S-CLASS INAYO JIENDESHA YENYEWE HAIHITAJI DEREVA






The backrests recline to 45 degrees, the heated seats have an energising massage function and even the armrests can be heated or cooled. But it’s not all about relaxation.
You get working desks in the back, plus two DVD screens which can be linked to the web for connectivity, along with a mega-music system, all of which can be operated from an app on your phone.
There’s even a climate control with air balance and an active perfuming system with four different smells to waft around the cabin!
Also, 115 years after cars were first fitted with electric headlamps, the S-Class is the first car since to have virtually NO lightbulbs — although its 500 LEDs mean it won’t leave you in the dark.
Smooths out potholes ... Mercedes S-Class
The new S-Class is very much the Airbus of motoring.
It’s a trailblazing, advanced trendsetter for business high-fliers when they are on the ground.
Over the years the car has been the best-selling luxury limo.
Alongside its high-spec standards it has always been at the forefront of technology, a winning recipe which has made it the favourite wheels of executives and politicians.

Gari hili Tayari lipo sokoni UK na Inakadiriwa kuuzwa kati ya £65,000 na £170,000.


Friday, May 17, 2013

PICHA: ALEX SONG NA GERARD PIQUE WAKIPIGANA HADHARANI

Astonishing: Gerard Pique (right) and Alex Song seem to be fighting on top of the Barcelona bus
Gerard Pique (kulia) na Alex Song wakiwa wanapigana juu ya basi la Barcelona

Shocked: Victor Valdes (left) and Alexis Sanchez (far left) watch as the pair grapple
Victor Valdes (kushoto) and Alexis Sanchez (kushoto) wakiwatazama
Astonishing: Gerard Pique (right) and Alex Song seem to be fighting on top of the Barcelona bus
Song akionesha ubabe
Astonishing: Gerard Pique (right) and Alex Song seem to be fighting on top of the Barcelona bus
Song akiwa tayari kurusha ngumi

Defence: Pique
Song akionekana na hasira akimfokea Pique
Happy? Other Barcelona stars turn to watch as Song and Pique continue to tussle
Caught flush: Song seems to land a slap on Pique's cheek during the scuffle
Hapa Song akimpa kibao


Caught flush: Song seems to land a slap on Pique's cheek during the scuffle
Hapa ndundi zikianza
Caught flush: Song seems to land a slap on Pique's cheek during the scuffle
Konde likamtoka Song
Huu ugomvi unaweza ukawa umetokana na bia nyingi zilizokuwepo kwenye gari hilo. Wanasiasa wa Catalonia wamelaumu kitendo hicho na kusema ni mfano mbaya kwa vijana
Stepping in: Carles Puyol (back) holds onto Pique's shirt as Valdes holds him by the arm
Carles Puyol akimkunja shati pique

Heated? Puyol and Valdes talk between themselves as the scuffle diffuses Puyol na Valdes katikati wakijaribu kuamulia ugomvi  

Happy? Song (left) poses alongside Sanchez (centre) and Eric Abidal (right) Song (kushoto) alongside Sanchez (katikati) and Eric Abidal (kulia)



MWANDISHI CHARLES MULLINDA AJITOA KWENYE JUKWAA LA WAHARIRI


8 c1dd8
Charles Mullinda


Mhariri Mtanzania Jumatano
Kaimu Mwenyekiti
Jukwaa la Wahariri
YAH: KUJITOA KWENYE JUKWAA


Napenda kukufahamisha kuwa nimeamua kujitoa kwenye Jukwaa la Wahariri kwa sababu siridhiki na mwenendo wa Jukwaa hilo.Nimeamua kujitoa kwa sababu sijaridhishwa na uamuzi uliofikiwa wa kuingilia uhuru wa habari na kufumbia macho baadhi ya mambo ambayo ninaamini hayapaswi kufumbiwa macho.
Uamuzi wangu huu pia unatokana na jinsi jukwaa linavyotumia nguvu kubwa kuficha ukweli unao wahusisha
baadhi ya wahariri ambao gazeti hili lilibaini kuwa walikuwa na mawasiliano yenye utata na aliyekuwa mtuhumiwa wa ugaidi, Joseph Ludovick. Aidha siridhishwi na jinsi baadhi ya wahariri wanavyoshambuliwa na wahariri wenzao katika magazeti yao pasipo Jukwaa kuchukua hatua huku kwa upande mwingine likitumia nguvu kubwa na pesa nyingi kuwalinda baadhi ya wahariri ambao nyendo zao zinatia mashaka.

Kikao cha kwanza na TEF na kilichofanyika leo kimedhihirisha pasipo mashaka kuwa TEF iliamua kuwa na ajenda maalumu ya kumshughulikia Mullinda kwa kuwa tu nilionyesha mawasiliano ya Deodatus Balile na Ansbert Ngurumo dhidi ya Ludovick kama ambavyo gazeti la Tanzania Daima lilivyoonyesha mawasiliano ya Dennis Msaki na Ludovick.
Ripoti ya timu iliyoundwa kuchunguza ukweli wa habari iliyoandikwa na gazeti la Mtanzania Jumatano ina upungufu mkubwa wa kimantiki ambao hata kwenye kikao niliuonyesha lakini haukusikilizwa.Ushahidi wa Ngurumo kumtumia pesa Ludovick upo wazi, lakini hakuna mtu anayeliangalia hilo kwa sababu tu timu ile iliundwa kumshughulikia Mullinda kwa sababu aliandika vigogo wa TEF ambao wako karibu na viongozi wa TEF.
Nimeamua kujitoa baada ya kubaini kuwa jukwaa linafanya kazi kwa ajili ya maslahi ya watu binafsi.
Kwa taarifa hii naamini utaratibu wa kawaida wa kuagana utazingatiwa.

Charles Mullinda.
 


HUU NDIO WARAKA WA MASHITAKA YA RUGE NA KUSAGA KWA LADY JAY DEE COMMANDO

HUU NDIO WARAKA WA MASHITAKA YANAYO MKABILI MSANII LADY JAYDEE MASHTAKA YALIYOFUNGULIWA NA JOSEHP KUSAGA NA RUGE MTAHABA...
 



INASEMEKANA NANI KAMWAGA POMBE YANGU WA MADEE AME-COPY NA KU-PASTE KUTOKA WIMBO HUU




Wednesday, May 15, 2013

MWANA FA AINGIZA MAMILIONI KWA KUUZA MUZIKI WAKE KAMA RINGTON



IMG_1042
 Hip hop inauza kwa mujibu wa Hamisi Mwinjuma au Mwana FA kama anavyo fahamika kimuziki ambaye leo ameachia wimbo wake mpya, Kama Zamani, hivi karibuni alipokea malipo ya miezi mitatu kutoka kampuni moja ya kuuza miito ya simu yanayofikia shilingi za kitanzania milioni 18.

Akiongea kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, Mwana FA aliyekuwa wa tatu kati ya wasanii waliopata fedha nyingi zaidi kwenye malipo hayo chini ya Rose Mhando na Diamond, amesema ameamua kuweka wazi hilo ili watu waondoe imani kuwa muziki wa hip hop hauuzi.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU