Facebook Comments Box

Monday, April 8, 2013

WANAWAKE WAANDAMANA VIFUA WAZI MBELE YA RAIS PUTIN NA ANGELA MERKEL

FEMEN акция  Ганновер Германия
Muandamanaji akidhibitiwa na mlinzi
President Putin was caught by surprise during his trip to Germany today when several topless members of the Femen feminist group burst onto a stage that he was sharing with Chancellor Merkel. Security guards quickly tackled the women, who were protesting Putin's leadership, and whisked them away. 

Read more: http://goo.gl/MbZWV

Watch video: http://goo.gl/9g1aF. (Warning: contains nudity and bad language. 18+)

Picture: A video still of a Femen activist exposing herself to Putin.
Muandamanaji huyu alimkaribia ila alidhibitiwa vilivyo

Raisi wa Urusi bwana Putin alipata bonge la mshangao wakati wa ziara yake ya Ujerumani baada ya waandamanaji kujitokeza. katika waandamanaji hao kulikuwa na wanawake watatu ambao walikuwa vifua wazi ambao walijitokeza nao mbele na kutaka kwenda kumkumbatia rais huyo.

 Bwana Putin alikuwa ameenda katika uzinduzi wa Hanover Messe industrial trade show yeye na mwenyeji wake Chancellor Angela Merkel ndipo walipojitokeza waandamanaji hao wakipinga sera na sheria za nchi yake juu ya mambo mbalimbali ambayo wao wanaona sio sawa

Akiliongelea hilo bwana Putin anasema alilitegemea ila anasema walinzi wa kijerumani walikuwa wakali sana kwa wamama hao kiasi cha kuwala wote chini kwa nguvu na muda mfupi kiasi kwamba hakusikia vizuri maneno waliyo yasema ila anasema alifurahishwa nao.

Pamoja na hayo kulikuwa pia na mabango kwenye mitaa hiyo ya miji ya Ujerumani.



OFISI YA TAALUMA YA SHULE YA IFUNDA SEKONDARI YACHOMWA MOTO

Picture
Tarehe tano mwezi jana gazeti la Majira liliripoti kuhusu vurugu zilizozuka katika shule ya sekondari ya Ifunda, ambapo Mwalimu Mkuu alinusurika kuuawa hali mlinzi wa shule akipigwa.

Juzi, usiku wa kuamkia Jumapili, watu ambao bado hawajafahamika wameitia moto ofisi ya taaluma ya shule hiyo na kusababisha nyaraka zilizokuwa zimehifadhiwa humo kuungua na kuteketea.
Picture


HIVI NDIVYO MZEE ABOUD JUMBE ALIVYO TABIRI VURUGU ZA KIDINI ZA LEO MIAKA 20 ILIYOPITA

Miaka 20 iliyopita, mwaka 1993 Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliandika mfululizo wa makala katika gazeti la kila wiki la Mwananchi wakati huo. Aliziita makala zake, Tuishi bila kubaguana kidini.

Mzee Jumbe akieleza katika makala zake kuwa, aliamua kuchukua uamuzi wa kuandika makala hizo ili wananchi pamoja na viongozi waweze kuchukua hatua juu ya suala la udini ambalo lilikuwa likitishia uhai na umoja wa Taifa letu.

Aliyoyaongelea Mzee Jumbe sasa yameanza kuonekena katika jamii yetu. Tatizo la udini linazidi kukua badala ya kupungua. Wanasiasa wanaongelea udini, viongozi wa dini wanaongelea udini, wanaharakati nao pia wanaongelea uwepo wa udini. Kila mahali utakapopita siku hizi, katika mada zitakazojadiliwa, moja wapo ni mada inayohusu udini.

Kabla sijaendelea na makala yangu haya, ni vema nikanukuu beti za shairi lililotungwa na Kiongozi wetu huyo alilolipa jina la Tanzania ni ya Watanzania wote.

Wito huu nautoa, kwa wote watanzania
Naona hatari yaotea, twendako yangojea
Wajibu wote kuijua, tuchange kuiondoa
Enyi watanzania jueni, Tanzania yetu sote.

Huu si usaliti, pia si uchochezi
Ni onyo tena la dhati, Nilitoalo kwa wakati
Wazeni enyi wananchi, Msije kukosa bahati.
Enyi Watanzania jueni, Tanzania yetu sote.

Umoja na amani, usawa kwa wote nchini.
Akataaye ni nani, mkorofi, adui kisirani.
Aseme wazi hadharani, ya nini chini chini
Enyi Watanzania jueni, Tanzania yetu sote.

Kweli na haki kote, uwe mwendo wa wote
Hadaa au dhuluma yoyote, iwe karaha kwa sote
Hii nchi yetu sote, tufaidike nayo wote.
Enyi Watanzania jueni, Tanzania yetu sote.

Namaliza sikudhulumu, wenyewe mhukumu,
Uhuru na umoja kudumu, bila ya usawa vigumu
Hilo wazi mfahamu, je haki au dhuluma?
Enyi watanzania jueni, Tanzania yetu sote
Watu wengi wamekuwa wakiongelea uwepo wa udini hapa nchini lakini pindi unapowauliza nini hasa maana ya udini wamekuwa wakishindwa kutoa jibu lililo sahihi. Si ajabu ukaambiwa kuwa “jamaa Fulani ni mdini kwa kuwa tu anasali sala tano na muda wote anavaa kanzu na tas’bihi mkononi haimuondoki. Au pia, fulani ni mdini kwa kuwa muda wote amevaa rozali na kuwa hana starehe yoyote zaidi ya kusikiliza kwaya na kusoma Biblia.

Wakati nafikiria kuandika makala haya, niliamua kwanza kutafuta maana ya neno udini. Kitabu cha kwanza kabisa kukikimbilia ilikuwa ni kamusi ya Kiswahili sanifu, toleo la pili ya mwaka 2004. Kwa bahati mbaya, nadhani inaweza kuwa imetokana na kusahaulika au kutokana na makosa ya mchapaji neno udini halipo katika orodha ya maneno katika kamusi hiyo.

Jitihada za pili katika kutafuta maana ya maneno haya niliipeleka katika kazi za wanazuoni mbalimbali ambapo niliamini kuwa lazima watakuwa wamezungumzia neno hilo katika kazi zao. Bahati nzuri maana ya neno udini nililipata kutoka kwa viongozi wawili wa kidini hapa Tanzania. Hawa ni Mwinjilisti Kamara Kasupa na Sheikh Mohamed Issa.

Katika pitia pitia zangu katika maandiko ya Mwinjilisti Kamara Kasupa, yeye aliutafsiri udini kuwa ni Ubaguzi unaoendeshwa katika misingi ya kidini, na aliendelea kufafanua kuwa udini una kawaida nyingine mbaya, nayo ni 
ubinafsi wa kubinafsishwa katika misingi ya kidini, una kawaida nyingine mbaya nayo ni ubinafsi wa kubinafsisha kila kitu.

Tafsiri ya pili ya dhana ya udini niliipata kwa mwanazuoni maarufu wa kiislamu Sheikh Mohamed Issa. Katika mada yake iliyoitoa katika msikiti wa Haq mkoani Morogoro, aliutafsiri udini kuwa ni kupendelea dini yako kiasi cha kuwadhulumu watu wa dini nyingine, na bila kujali taratibu. Akaelezea zaidi kuwa ni kupendelea dini yako na kuwadhibiti watu wa dini nyingine wasije wakapata mafao, mafanikio na maendeleo kama ya dini yako.

Baada ya kupata tafsiri hizo, niliamua kumfuata kiongozi wangu wa dini na kukaa nae huku tukijadili masuala mbalimbali yanayoendelea katika nchi yetu. Katika mazungumzo yetu nilimuuliza, uislamu unatutaka tuishi vipi na wasiokuwa waislamu?

Alinijibu kuwa, katika Quran Tukufu Surat AN-Nisaa aya ya 36
mwenyezi Mungu anasema “Muabuduni Mwenyezi Mungu wala msimshirikishe na
chochote. Na wafanyieni ihsani wazazi wawili, na jamaa na mayatima na masikini na jirani walio karibu na jirani walio mbali, na rafiki wa ubavuni (mwenu) na msafiri aliye haribikiwa, na wale iliyowamiliki mikono yenu ya kulia (kuume). Bila shaka Mwenyezi Mungu hawapendi wenye kiburi wajivunao”.


Funzo kubwa nililolipata katika aya hii ni kuwa muislamu wa kweli hatakiwi kubagua. Anatakiwa kutenda wema kwa wote bila kujali dini, kabila au utajiri wa mtu. Migogoro ya kidini, nini hasa chanzo chake na kwa nini hasa waislamu ndo wanaonekana kama wapenda fujo na vurugu? Hili ndio hasa nataka kulijadili na pia kutoa mbinu za kuiepuka migogoro hii ili isije kuliangamiza taifa hili.

Mwalimu wangu wa chuo Kikuu, Profesa Mwesiga Baregu alipokuwa akitufundisha somo lililohusu Utatuzi wa migogoro na ujenzi wa amani (Peace making and conflicts resolution) alikuwa akisisitiza suala la kusikiliza, kutafakari na hatimaye kuchukua hatua stahiki katika kutatua matatizo. Na baada ya hatua kuchukuliwa ni vema kuwarudishia majibu walalamikaji na walalamikiwa.

Tatizo kubwa tulilonalo sisi ni kwamba tumekuwa wagumu sana kusikiliza malalamiko hasa yanayotolewa na waislamu, na hata ikitokea malalamiko yao yamesikilizwa basi yamekuwa yakitolewa majibu mepesi sana.

Nimekuwa nikijiuliza, kwa nini hasa malalamiko ya waislamu huwa hayapewi uzito sana, huwa nakosa jibu. Labda huwa tunawaangalia watoa malalamiko, kwa kuwa labda wengi wao wanavaa kanzu zilizo chakaa na makubadhi au hata yeboyebo zilizo chakaa, hivyo tunadhani hata akili zao zimechakaa kama kanzu na yeboyebo wanazovaa.

Hili ni tatizo, maana siku hizi mtu mwenye akili anapimwa kwa vitu alivyovaa au anavyomiliki au usafiri anaotumia na hata wapi anaishi. Anayetumia VX huonekana ana akili sana kuliko anayeendesha baiskeli au mtembea kwa miguu. Anayeishi Masaki au Mikocheni na Oysterbay jijini Dar es salaam au Uzunguni, Area C na Area D mkoani Dodoma huonekana kuwa ana akili sana na amestaarabika kuliko mtu anayeishi Mbagala, Manzese hapo hapo Dar au pia anayeishi Chang’ombe mjini Dodoma.

Tumejenga tabia ya kuthamini hata mavazi na lugha. Anayevaa suti na kuongea kiingereza huonekana ana akili sana na amestaarabika kuliko anayevaa kaniki na kuongea Kiswahili.

Kuna suala moja ambalo mimi binafsi limekuwa likinikera sana na ninahisi kwa kila mpenda amani na usawa huwa anakereka. Suala hili ni kuwaita viongozi wa dini kuwa ni wahuni. Hili ni tusi kubwa hasa unapomuita kiongozi wa dini ambaye anaongoza mioyo na imani za watu. Tumeshuhudia watu kama akina Sheikh Ponda, Sheikh Farid na wengine wengi wakiitwa majina ambayo yanaonesha dharau kubwa si kwao pekee bali pia kwa dini yao na taasisi wanazoziongoza.

Lakini sababu ya pili inayowafanya waislamu waonekane kama wapenda fujo na wapenda machafuko kwamba wamekuwa katika harakati za kuitetea dini yao ambayo wanadhani kuwa imekuwa ikdharauliwa na pengine kutothaminiwa kabisa.

Hili nitalielezea. Kwa sasa kumekuwa na wanaharakati wengi na wanasiasa ambao wamekuwa katika harakati za kuhamasisha na kufanya mabadiliko mbalimbali katika mifumo yetu hasa sheria, mabadiliko ambayo kwa njia moja ama nyingine yataathiri imani na ibada za waislamu.

Mathalani, unapoanzisha vuguvugu la kuwepo kwa sheria moja ya mirathi, kitu ambacho kitaleta upinzani mkubwa kutoka katika jamii za waislamu kwa kuwa tayari wana mfumo wao wa mirathi, ambao umeelekeza namna gani mirathi igawanywe na nani apate nini na kwa nini apate hivyo.

Udini umekuwepo siku nyingi sana hapa nchini kwa sura tofauti. Vichwani mwa watu wamekuwa na dhana za ubaguzi wa kidini bila wenyewe kujijiua. Watu wanaoamini katika dini ya kiislamu wamekuwa wakidharauliwa na kukejeliwa sana. Mfano, ukitazama vyombo vya habari hasa magazeti. Mfano, ili kufikisha ujumbe kwa wasomaji, wachora wa picha za magazetini huwatumia sana wazee wenye muonekano wa kiislamu katika kuonesha watu wasiostaarabika.

Utakuta unapotaka kumchora mchawi, mganga wa kienyeji ama mtu anayependa sana kula katika sherehe au misiba, atamchora mzee aliyevaa kanzu, makubadhi, amevaa baraghashia na ameshika bakora vitu ambavyo hutumiwa sana na waislamu ingawa pia katika baadhi ya jamii kama za wahaya mavazi hayo ni mavazi ya heshima kwa wazee bila kujali dini.

Utendaji wa baadhi ya taasisi nao umekuwa ukiibua hisia za kidini. Hii ilidhihirika miaka michache iliyopita wakati hakimu mmoja jijini Dar es salaam ilipoamua kumfunga kifungo cha miezi sita, muislam mmoja aliyehudhuria mahakamani kwa kuwa tu alikataa kuvua kofia aina ya baraghashia. Aliadhibiwa kwa kosa la kudharau mahakama.

Pia upo ubaguzi katika makazi na maeneo. Maeneo mengi ambayo kiasili yamekuwa yakikaliwa na waislamu yamekuwa yakipewa majina yasiyo na nidhamu kama vile uswahilini, uswazi nakadhalika na yamekuwa yakisifika sana kwa sifa ya uchawi, kitu ambacho kimejengwa ndani ya vichwa vya watu na hutokea mpaka wageni kuogopa kuishi ama kuwekeza katika maeneo hayo na hivyo kuyafanya yaendelee kuwa duni siku hadi siku.

Kwa mtu yeyote, ukimueleza maeneo kama Ujiji na Gungu mkoani Kigoma, Isevya mkoani Tabora, Bagamoyo , Rufiji na Tanga, taswira inayojengeka kichwani mwake moja kwa moja ni kuwa, hii ni miji iliyojaaa wachawi na washirikina. Na hii imejengeka kiasi kwamba, iwapo inatokea mtu amekosewa na mwenzake, tishio huwa ni kwamba, nitakuendea Ujiji kama siyo Bagamoyo, Rufiji na Kilwa.

Si rahisi kukuta mfanyakazi wa serikali aliyepangwa kufanya kazi mkoani Kigoma, kukubali kuishi Ujiji au Gungu hata kama ataambiwa bei ya pango kwa nyumba nzima ni Tsh 50,000 kwa mwezi. Mtumishi huyo yupo radhi kuishi Mjimwema ambako atalipa Tsh 200,000 kwa mwezi na ukimuuliza kwa nini hasa hataki kuishi Ujiji ama Gungu, atakueleza kuwa anaogopa kurogwa. Huu pia ni ubaguzi.

Profesa Mahmood Mamdani ametunga kitabu chake alichokipa jina la Good Muslim, Bad Muslim. Katika kitabu hicho anaelezea jinsi waislamu walivyogawanywa katika makundi. Kwa hapa Tanzania Good Muslim ni wale waislamu walio chini ya BAKWATA, ambao wanaiona BAKWATA kama mtetezi na mlinzi wa waislamu na Bad Muslim ni wale wote ambao hawataki msimamo wa BAKWATA na pia hawataki kuitambua BAKWATA, ambao wanaiona BAKWATA kama mnyonyaji na mkandamizaji wa haki za waislamu. Bad Muslims hawasikilizwi na muda wote wamekuwa wakiitwa walalamishi.

Lakini sasa kuna hili suala la kamatakamata ambalo limekuwa likiendeshwa na jeshi la polisi katika kudhibiti viongozi wa dini ambao wanahubiri “uchochezi”. Jambo hili lisipofanywa kwa umakini, linaweza kuingilia uhuru wa watu wa kuabudu. Majuzi nilikuwa natazama kipindi fulani katika TV. Mwanaharakati mmoja kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binaadamu (LHRC) alilalamikia matumizi ya maneno kama vile “kafir” na kuelezea kuwa si vizuri kuyatumia.

Tukumbuke kuwa neno hilo lipo katika kitabu kitukufu cha waislamu, , Quran na kulalamikia kutumika kwa neno hilo ni sawa na kusema liondolewe au lisitumike, kitu ambacho nina uhakika kuwa hakitawezekana kwani kwa mujibu wa mafundisho ya uislamu, dini yao ilikwisha kamilika na hakuna marekebisho yoyote ambayo yanaweza kufanyika.

Lakini pia, niwashukuru viongozi wetu wa dini, kama alivyosema Sheikh Alhad Mussa Salum, Sheikh mkuu wa BAKWATA wa Mkoa wa Dar es Salaam na Muadhama Askofu Kardinali PolycaRp Pengo, kuwa kuna haja ya kukutana kwa viongozi wa dini ili wajadili kwa kina, chanzo hasa cha migogoro na namna ya kuitatua. Na vikao hivyo ni vema vikianzia katika ngazi za vitongoji mpaka ngazi ya taifa.

Nimalizie makala yangu haya, kwa kuwaomba viongozi wetu na watendaji wa serikali kutopuuzia malalamiko ya watu wao. Wayafanyie kazi bila kujali, nani ameyaleta na huyo aliyeyaleta ana miliki nini au ana elimu gani. Na pia nikumbushe maneno ya rais wa zamani wa Iran Mohammed Khatami aliyeelezea majadiliano baina ya tamaduni (Dialogue among Civilizations) kama njia ya kuelewana na kuzuia machafuko yanayojiegemeza katika tamaduni.
 
Alicho kisisitiza Mzee Aboud Jumbe ni TUEPUKE UDINI KWA KUTENDA HAKI



Sunday, April 7, 2013

HATIMAYE MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) APATA JIKO



Akifungisha Ndoa Hiyo Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kusini Njombe Isaya Mengele Amekumbusha Maneno ya Mungu na Kuwataka Wanandoa Kuishi Kwa Misingi ya Dini Kama Ilivyoelekezwa Kwenye Vitabu Vya Dini.
 Kulia ni mkuu wa wilaya ya Njombe Bi.Sarah Dumba akiwa na waziri mkuu Mizengo pinda katikati akifuatiwa na Katibu mkuu wa CCM.
 Kushoto ni msemaji wa familia ya mzee Philip Mangula Dr.Lechion Kimilike ambaye ni Mhadhiri wa chuo kikuu huria cha Tanzania Tawi la Njombe[NJOMBE OPEN UNIVERSITY].
 Waziri mkuu Mizengo pinda akisalimiana na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa wilaya ya Njombe bwana Lupyana Fute[Jacky's]ambaye ni diwani wa kata ya Njombe mjini leo wakati wa Harusi ya Mzee Philip Mangula.
 Hapa ni ndani ya kanisa la KKKT Dayosisi ya kusini Njombe Mjini ambako pingu za maisha kwa mzee wetu Mangula zimefungwa.
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana Katika harusi ya mzee Mangula leo Njombe.
Makamu mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Philip Mangula na Mkewe Yolanda Kaberege leo wakifunga pingu za maisha. Picha na Gabriel Kilamya


Saturday, April 6, 2013

HUU NDIO MSIMAMO WA ZITTO KUHUSU KESI YA RWAKATARE

Kutokana na sakata la Lwakatare na Barua ambayo ilidaiwa kuandikwa na zitto Mwenyewe kuzaga mtandaoni hasa kwa mara ya Kwanza kupitia kwenye mitandao ya kijamii Zitto amejitokeza na kutoa taharifa hifutayo…..

1. Niliandika barua kwa Katibu Mkuu wa chama mnamo tarehe 15 Machi 2013 kutaka chama kifanye uchunguzi wake wa ndani kuhusiana na ukweli wa video iliyowekwa kwenye mitandao inayoonyesha kuwa Kiongozi wetu mwandamizi anapanga mipango ya kumdhuru Mhariri wa moja ya magazeti hapa nchini. Sikuamini kabisa mambo yale na hivyo kutoa ushauri kwa chama kwamba tufanye uchunguzi wetu wa ndani ili kujiridhisha. Uchunguzi wa ndani ungetufanya kuweka mikakati wa namna bora zaidi ya kulinda chama dhidi ya njama zozote, za ndani au za nje ya chama.

2. Mapendekezo yangu ndani ya chama kamwe hayakulenga kumtosa ndugu Lwakatare wakati huu anakabiliwa na changamoto hii bali yalilenga kuhakikisha kuwa wakati tunamlinda na kumtetea ili haki itendeke, lazima tuhakikishe kuwa chama hakitaathirika na sakata hili kwa namna yeyote ile. Ni jukumu letu kuhakikisha sura (image) ya chama inabakia salama maana hatujui mikakati (game plan) ya maadui zetu kisiasa hasa baada ya kauli zao kwamba chama kitakufa kabla ya 2015 ambayo imerudiwa rudiwa sana. Ni lazima kutilia shaka (doubt) kila linalotokea sasa kwa kulipima kwa jicho la mbele zaidi. Ikumbukwe maneno ya Mwenyekiti wetu “Mwenyekiti Freeman Mbowe anataka ikithibitika kuwa Lwakatare alishiriki kurekodi mkanda huo iwe kwa kurubuniwa, ‘kushikishwa’ au kuingizwa mkenge, itamlazimu kuwajibika kwa kosa la kukosa umakini” (Gazeti la Jamhuri).

3. Barua ile ya tarehe 15 Machi 2013 ilikuwa ni ya ndani ya chama, haikuwa ya kiofisi bali ya Zitto Kabwe kwa chama, ilisainiwa na haikukusudiwa kuwa ‘public’. Nimeshangazwa sana kusikia na baadaye kuona barua yenye maudhui kama yale yale ya barua yangu kwa Katibu Mkuu imewekwa mtandaoni. Barua imewekwa masaa machache baada ya kikao cha Kamati Kuu kwisha ambapo tuliweka msimamo wa pamoja wa chama juu ya namna bora ya kushughulikia suala la Lwakatare kama chama. Wakati mweka barua anadai kuwa kulikuwa na mgawanyiko katika kikao, ukweli ni kwamba ajenda hiyo haikuwa na mjadala wenye mgawanyiko kabisa na msimamo wa chama ulipatikana kwa mwafaka bila mgawanyiko. Ni dhahiri kuwa maadui zetu walitaraji mgawanyiko na baada ya kushindwa sasa wanatengeneza mgawanyiko huo kwa kusambaza uwongo wenye uzandiki.


4. Baada ya kufanya uchunguzi mdogo nimegundua kuwa ID iliyoweka video ya Lwakatare mtandaoni na ID iliyoweka barua hii mtandaoni ni IDs za mtu mmoja. ‘Coincidence’ ya namna hii inashangaza na kushtusha, lakini inatuambia jambo moja kubwa ‘kwamba kuna kirusi ndani ya chama kilicho karibu sana na viongozi wa chama chenye kazi moja tu, yani kuonyesha kuwa CHADEMA hapako shwari, kuna migogoro na hatimaye kusambaratisha chama’. Kirusi hiki lazima kina nafasi andamizi au kipo karibu sana na viongozi waandamizi. Inawezekana kabisa kirusi hiki kinahusika na suala zima la Lwakatare katika kupanga, kuendesha na kutekeleza mpango mzima. Maswali kama ‘kwanini Dennis Msacky na Zitto ndani ya Video ya ‘Lwakatare’ lazima sasa yaanze kutafutiwa majawabu.

5. Natoa wito tena kwa viongozi na wanachama wa CHADEMA kwamba, huu ni wakati wa kuwa na umoja na mshikamano kuliko wakati wowote ule katika uhai wa chama chetu. Chama cha Mapinduzi kitatumia njia zote kutugawa, kutugombanisha na kupenyeza chuki miongoni mwetu katika juhudi za wao kubakia madarakani. Umakini wa Kiongozi huonekana wakati wa changamoto kama hizi!

6. Msimamo wa chama umetolewa na Kamati Kuu iliyomaliza vikao vyake jana siku ya ijumaa tarehe 5 Aprili 2013. Huo ndio msimamo wangu pia! Kesi ya Lwakatare ipo mahakamani, chama kimeonyesha dhahiri kumwamini Jaji aliyekabidhiwa kesi hii, sasa tuache mahakama ifanye kazi yake na tusubiri hukumu. Msemaji wa chama kuhusu suala hili ni ndugu Tundu Lissu na amekuwa akitoa ufafanuzi kila inapohitajika.

Asanteni


Kabwe Z. Zitto,MP- Kigoma North, Tanzania. Chairman Public Accounts Committee,
Deputy Secretary General CHADEMA and Deputy Leader of the Opposition,
Shadow Minister of Finance
Mobile: +255756809535
Blog: http://www.zittokabwe.com

AHUKUMIWA MIAKA KUMI JELA KWA KUMNYONYA MTOTO ULIMI

MAHAKAMA Hakimu ya Mkazi ya Wilaya ya Mpanda imemhukumu Kassim Lugendo (41) mkazi wa kijiji cha Kambanga tarafa ya Kabungu kifungo cha miaka 10 jela kwa kosa la kumnyonya ulimi mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 13, anayesoma darasa la tano katika Shule ya Msingi Igalula, bila ridhaa yake.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Chiganga Tengwa alitoa hukumu hiyo jana baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.

Awali katika kesi hiyo, Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Ally Mbwijo aliieleza mahakama hiyo kuwa mshitakiwa Lugendo alitenda kosa hilo Machi 30 mwaka jana, saa sita mchana akiwa nyumbani kwake.

Ilidaiwa kuwa siku hiyo ya tukio mtoto huyo alikuwa akitoka shuleni akielekea nyumbani kwao ndipo mshitakiwa alipoona anapita karibu ya nyumba yake ambapo alimwita msichana huyo na kisha alimwingiza kwa nguvu nyumbani kwake.

Mbwijo aliiambia mahakama kuwa, baada ya mshitakiwa kumwingiza ndani ya nyumba yake msichana huyo, alianza kumnyonya ulimi kwa nguvu huku akimtomasa sehemu za siri kwa vidole.

Ilielezwa mahakamani hapo kuwa wakati akimfanyia uovu huo, mtoto huyo alikuwa akiomba msaada kwa kupiga kelele muda ambapo majirani walifika eneo la tukio na kumkuta mshitakiwa akiwa ameshaanza kumvuta mtoto huyo sketi yake ya shule.

Katika kesi hiyo, upande wa mashitaka ulileta mahakamani hapo mashahidi watatu na mshitakiwa hakuwa na shahidi yeyote.

Akijitetea, Lugendo aliiomba mahakama isimpe adhabu kwa kile alichokieleza kuwa yeye ana familia ya watoto saba na wazazi wake wote wawili ni walemavu, hivyo ana watu wengi wanaomtegemea.

Hata hivyo, Hakimu Chiganga alisema kitendo alichokifanya mshitakiwa ni cha kinyama na hatari kwani kina weza kumsababishia mtoto huyo ugonjwa wa ukimwi. Alimtia hatiani na kumwadhibu kifungo cha miaka kumi jela. SOURSE: HABARI LEO

MALAWI WAAMBIWA WAACHE KUTAPATAPA


 
Waziri wa mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe (wapili kutoka kulia) akizungumza na waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu tamko la Serikali juu ya mgogoro wa mpaka wa ziwa Nyasa. 

SERIKALI ya Tanzania imeomba  Malawi iache kutapatapa kuhusu mgogoro wa mipaka wa ziwa Nyasa kufuatia Rais  wa nchi hiyo, Joyce Banda kutangaza katika  baadhi ya vyombo vya  habari  kuwa atapeleka  suala hilo kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Haki(ICJ), badala yake isubiri uamuzi wa jopo la usuluhishi lifanye kazi na litoe maamuzi.
Aidha serikali  imesema kuwa hata siku moja  haijapelekewa taarifa wala nyaraka za siri kutoka kwa Katibu wa jopo hilo, ambalo linahusisha marais wastaafu wa zamani wa Afrika na wanasheria  kama ilivyodaiwa  na  Rais  Banda katika vyombo hivyo , kuwa kuna Mtanzania anayeitwa Dk. John Tesha ambaye wanaamini ametoa  habari na kuiba nyaraka za siri.
Akilitolea ufafanuzi   jambo hili, Waziri Membe amesema kuwa  Tanzania na jopo hilo   limestushwa juu ya madai hayo na hatua ya Rais Banda kupoteza imani.


Friday, April 5, 2013

POLISI ZANZIBAR WAKANA UPELELEZI WA KESI YA PADRI MUSHI KUFANYWA NA FBI



BAADA ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DDP) kulitaka Jeshi la Polisi kumwachia mtuhumiwa Mussa Omar Makame kutokana na ushahidi kutojitosheleza, jeshi hilo sasa limeingia kwenye mkorogano.

 Katika mahojiano, Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mussa A. Mussa, alikanusha jeshi la polisi kushirikiana na kikosi cha upelelezi cha Marekani (FBI) ili kumkamata Makame.

Kauli yake inakinzana na ile aliyoitoa Machi 23, mwaka huu aliposema uchunguzi huo ulikuwa ukifanywa na makachero wa polisi kwa kushirikiana na wapelelezi kutoka Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) na kufanikisha kumkamata mtuhumiwa huyo.

Katika mkorogano huo wa taarifa kuhusu Makame, tamko rasmi la Jeshi la Polisi nchini lililotumwa kwa vyombo vya habari halikumtaja mtuhumiwa kwa jina likidai uchunguzi unaendelea lakini Kamishna Mussa alimtaja kuwa ni Mussa Omar Makame.

Kamishna Mussa jana alilieleza kuwa licha ya DPP kusema Makame hana hatia, wataendelea kumshikilia kwa uchunguzi zaidi.
“Sisi tutaendelea kumshikilia hata kama DPP hakuridhika na upelelezi tuliofanya, tuna taratibu mbalimbali ambazo si lazima kuzitaja kwa sasa,” alisema.

Alipotakiwa kufafanua kama ni kweli FBI hawakushirikiana nao katika uchunguzi huo, kamishna huyo aliomba apigiwe simu baadaye kwa madai kuwa alikuwa na kazi, lakini alipotafutwa tena hakupokea simu. Naye Kaimu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini, Isaya Mungulu, alipotakiwa kuzungumzia mkorogano huo wa kauli, alidai apigiwe Kamishna wa Zanzibar ndiye anayejua vizuri.


Thursday, April 4, 2013

ANGALIA UWANJA WA YANGA UTAKAVYO KUWA BAADA YA UJENZI KUKAMILIKA


Ramani ya uwanja mpya wa klabu ya Yanga - Kaunda Stadium unavyoekana kwa ndani
















Kampuni ya Beinjing Cosntruction Engineering Group (BCEG) kutoka nchini China, ambayo mwishoni mwa mwaka jana ilisaini makubaliano ya upembuzi akinifu juu ya ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu (Kaunda stadium) leo imewasilisha michoro na makadirio ya bajeti ya ujenzi wa Uwanja mpya eneo la Jangwani.
Kaimu meneja wa kampuni ya BCEG  Zhang Chengwei David amesema upembuzi akinifu umekamilika kuhusiana na suala la ujenzi wa uwanja wa mpya wa klabu ya Yanga eneo la jangwani ambapo taratibu za makadirio na michoro imekamilika tayari na leo kuwasilishwa kwa uongozi wa klabu ya Yanga.
Zhang alisema kwamba kampuni yao BCEG wana uzoefu wa ujenzi wa viwanja sehemu mbali mbali duniani, na mfano mzuri ni ujenzi wa uwanja mpya wa Taifa jijini Dar es salaam ambao ulikua mkubwa kuliko viwanja vyote barani Afrika kabla ya kujengwa kwa uwanja mpya wa nchini Afrika Kusini (Soccer city) uliotumika kwa ajili ya fainali za kombe la dunia 201o.
Aidha Zhang aliendelea kusema pia kwa sasa wanajenga uwanja wa Uhuru Stadium (jirani na uwanja wa Taifa ) ambapo ujenzi wake ulianza mwaka jana mwezi Aprili na wanatarajia kuukamilisha mapema mwaka huu, huku ukiboreshwa kwa kufunikwa uwanja mzima na kuweka viti ambayo vitaweza kubeba watazamaji 20,000.
Katika uwasilishaji huo wa makadirio ya ujenzi wa uwanja wa Kaunda, mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa klabu ya Yanga Francis Kifukwe alisema wanafurahishwa na kampuni ya BCEG kwa kukamilisha zoezi la upembuzi akinfu mapema ambapo leo wamepata fursa ya kujionea na kujua maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo. 
Kufukwe alisema wamepewa nafasi ya kuchangua aina tatu za uwanja, uongozi wa klabu ya Yanga utakaa na kuchagua aina mojawapo ambayo wataiwasilisha kwa kampuni ya BCEG na mwishoni mwa mwezi Mei wanatarajia kusaini mktaba kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mpya wa Kaunda.
Akijibu swali la waandishi wa habari juu ya jinsi gani wataweza kupata fedha za ujenzi wa uwanja, Kufukwe alisema ujenzi wa uwanja wa mpya utajengwa na wanachama, wapenzi na washambiki wa klabu ya Yanga.
Kwa mujibu wa makubaliano ya kampuni ya BCEG na klabu ya Yanga ujenzi wa uwanja mpya wa Kaunda stadium utachukua muda wa miaka miwili, kuanzia utakapoanza ujenzi wake ambapo unatazamiwa kuanza mwezi wa Julai 2013 kulingana na kukamilika kwa taratibu za ujenzi kwa kampuni hiyo.
Kaunda stadium utakuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 40,000, waliokaa kwenye viti, huku ukiwa na sehemu za maegesho ya magari, sehemu ya watu maaalumu (VIP) hostipali, hoteli na hosteli, eneo la waandishi wa habari, eneo la walemavu na huduma zote muhimu zinazopatikana katika viwanja vya michezo.
Ramani ya mchoro wa Uwanja mpya wa Kaunda unavyoonekana kwa nje





AMANI YETU INACHEZEWA SANA

Picture

SAKATA LA MAUAJI YA PADRI MUSHI: DPP HAJAONA USHAHIDI WA KESI YA MAUAJI

DPP wa Serikali Ibrahim Mzee asema hajaona ushahidi ambao ungemuwezesha kumshitaki kijana Omari alituhumiwa kwa mauwaji ya Padri Mushi.

 Na kwa upande wa Mahakama pia umelitaka Jeshi la Polisi kumfikisha mtuhumiwa huyo Mahakamani siku ya Jumatatu na waeleze vielelezo tosha kwanini wamemchelewesha­ kumpeleka mahakamani wakati wanajua kuwa mtuhumiwa hupaswa kukaa kituo cha Polisi kwa muda wa masaa 24 tu na baadae kufikishwa mahakamani.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU