Facebook Comments Box

Monday, December 31, 2012

MATOKEO YA SENSA YA MWAKA 2012

Picture
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi waliohudhuria uzinduzi wa matokea ya awali ya sense ya watu na mazi Mjini Dar es Salaam

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ina idadi ya watu Milioni 44,929,002 kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya watu na Makazi iliyofanyika mwezi Agosti mwaka huu wa 2012.

Matokeo hayo yanaonyesha ongezeko la idadi ya watu Nchini Tanzania lililofikia watu Milioni 33,000,000 ikilinganishwa na lile la sensa ya watu la Milioni 12,313,054 baada ya Uhuru .

Akitangaza matokeo ya awali ya sensa ya idadi ya watu katika viwanja vya Mnazi Mmoja Mjini Dar es salaam Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alisema matokeo hayo yanaifanya Tanzania bara kuwa na Idadi ya Watu Milioni 43,625,434 wakati Zanzibar ina watu Milioni 1,303,568.

Rais Kikwete alifahamisha kwamba takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania inakadiriwa kufikia watu zaidi ya Milioni 51,000,000 ifikapo mwaka 2016 kiwango kisichokidhi mahitaji halisi ya uchumi na mipango mengine.

Dkt. Kikwete alitahadharisha kwamba idadi ya watu imekuwa kwa kiwango kikubwa na ongezeko lijalo linaweza kuwa mzigo mkubwa kwa Taifa ambapo alishauri kuwepo kwa mikakati katika kipindi cha miaka minne ijayo ili kukabiliana na ongezeko hilo.

Alizishauri familia kuzingatia zaidi umuhimu wa suala la kuwa na uzazi wa mpango kwa lengo la kuwawezesha wazazi kuwa na uwezo na mbinu za kuzihudumia familia zao.

Rais Kikwete aliupongeza Umma, Washirika wa Maendeleo pamoja na Viongozi wa nyadhifa tofauti kwa juhudi zao zilizopelekea kufanikisha zoezi ya sense ya watu na makazi na kuviomba vyombo vya habari vilivyotoa mchango mkubwa katika zoezi hilo kuendelea kuelimisha ummamatumizi bora ya Takwimu za sense kwa kudumisha ustawi wa Jamii.

Akimkaribisha Mgeni rasmi katika uzinduzi huo wa awali wa matokeo ya sense ya watu na makazi Mwenyekiti wa Kamati kuu ya Taifa ya Sensa ambae pia ni Waziri Mkuu Mh. Mizengo Peter Pinda alisema asilimia 90% ya gharama za zoezi zima la sense limesimamiwa na Serikali yenyewe.

Mh. Pinda alisema Kiwango hicho kimepindukia asilimia 20% ya gharama za sensa ikilinganishwa na Sensa ya mwaka 2002 ambapo zaidi ya asilimia 70% zilitumika katika zoezi hilo.

Akitoa salamu wakati wa uzinduzi wa matokeo ya awali ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 mwenyekiti Mwenza wa kamati kuu ya Taifa ya Sensa ya Watu Tanzania Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema matokea ya sense yatakuwa na maana katika Taifa pale Taarifa zake zitakapotumika kikamilifu katika kupanga maendeleo ya Nchi.

Balozi Seif aliwaomba washirika mbali mbali zikiwemo Taasisi za Serikali, Sekta binafsi, washirika wa maendeleo na Wananchi kuzifuatilia takwimu za sense kwa kuzitumia katika kupanga mipango ya maendeleo katika maeneo yao ya kazi.
Alisema hatua hiyo itasaidia kufanikisha malengo ya mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini Tanzania (MKUKUTA) na mpango wa kukukuza uchumi na kupunguza umaskini Zanzibar (MKUZA).

Mwenyekiti huyo mwenza wa Kamati Kuu ya Sensa Tanzania Balozi Seif amewashukuru Viongozi wote wa juu, kati, Wananchi pamoja na washirika wa maendeleo kwa kuitikia wito wa serikali zote mbili wa kuwataka washiriki katikamzoezi la sensa ya mwaka 2012.

Naye kwa upande wake mwakilishi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa Nchini Bibi Maryam Khan alisema Taasisi za Umoja huo zitaendelea kusaidia kitaaluma na uwezeshaji katika kuona Mataifa wanachama yanafanikiwa katika utekelezaji wa Mipango yao ya Maendeleo.

Bibi Maryam Khan alisema sensa ndio msingi muhimu inayotoa mwanga wa mipango ya maendeleo kwa kuimarisha miundo mbinu na kuipongeza Tanzania kwa juhudi zake za kujiletea maendeleo kwa kutambua umuhimu wa kujua idadi ya watu wake.

Mapema Kamishna wa Sensa Tanzania Hajat Amina Mrisho alisema watendaji wa kamati ya sensa watahakikisha machapisho yote ya sensa yatatolewa na kuchapishwa kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.

Hajat Amina ameelezea faraja yake kutokana na watendaji wake kutimiza ahadi ya kutangaza matokeo ya sensa kama ilivyojipanga na inajivunia ufanisi mkubwa iliyoupata katika zoezi zima la sense ya watu na makazi ya mwaka 2012.

“ Katika kipindi kifupi tumeweza kutoa matokeo ya awali ya sense ambapo inaonyesha umahiri mzuri walionao watendaji wa sense. Uzoefu wa Kitaifa na Kimataifa mara nyingi unaonyesha kuchelewa kwa matokeo ya takwimu za Sensa”. Alifafanua Hajat Amina Mrisho.
Picture
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba leo Desemba 31, 2012 wakati wa kupiga picha baada ya kuzindua matokeo ya sensa ya watun na makazi katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. (PICHA: IKULU)




Sunday, December 30, 2012

HIVI NDIVYO MOTO ULIVYOTEKETEZA MAGHALA YA KUHIFADHIA BIDHAA ZA WAFANYA BIASHARA WA MWANJELWA TAZAMA PICHA ZOTE HAPA,

Maghala ya kuhifadhia bidhaa mbali mbali za wafanya biashara wa mwanjelwa Mbeya yameteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo maghala hayo yapo maeneo ya uwanja wa ndege wa mwanjelwa
Wanausalama wakiwa makini na vibaka ambao walitaka kuvamia eneo hilo la moto kutaka kupora mali kujifanya wanaokoa mali hizo
Hakika kikosi cha zimamoto cha jiji la mbeya wakishirikiana na kikosi cha zimamoto uwanja wa ndege wa songwe walijitahidi kuuzima moto huo ingawa mara kwa mara waliishiwa maji kutokana na uwezo mdogo wa magari hayo kubeba maji ya kuzimia moto
Moja ya gari ya kampuni ya jambo ikiungua moto katika maghala hayo
Moja ya wafanyabiashara hao ambaye anamizigo yake katika maghala hayo akikatazwa na mwanausalama kwamba asiende kmuokoa mali zake kwani moto ni mkubwa awaachie kikosi cha zimamoto kifanye kazi yake
Mfayabiashara huyo haamini mcho yake huku akilia akiona bidhaa zake zikiteketea kwamoto
Kama kawaida kmufa kmufaana hapa vibaka wakigombea sahani na masufuria kwenye box
Hakika jeshi la polisi linastahili pongezi kwa kazi kubwa ya kuokoa mali za wafanyabiashara ambao bidhaa zao zilikuwa katika maghala hayo hapa polisi wakiwa wamemshika kibaka aliyetaka kuiba mafuta ya kupikia
Kwakweli ilikuwa hatari kwani vibaka walikuwa wanarusha mawe kwa polisi na kwa baadhi ya magari hapa hili gari ikitoka katika ghala hilo likiwa limevunjwa kioo cha mbele
Baadhi ya wananchi wengi wakiwa katika tukio hilo
Haya si maji bali ni mafuta ya kula ambayo yamemwagika baada ya blastiki kuyeyuka kwa moto
Asubuhi hii moto ndiyo unaishia
Hali halisi baada ya kuungua kwa maghala hayo hili si tope mali ni mafuta ya kula yaani mafuta ya kupikia
Baadhi ya wafanyabiashara wakijaribu kuokota baadhi ya mabaki ya bidhaa zao zilizopona katika moto huo
Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Athuman Diwani akiongea na waandishi wa habari leo amesema anawapongeza sana wakazi wa Mbeya hasa wale wa maendeo yanayozunguka maghala yalioteketea kwa mtoto kwa ushirikiano wao kuwezesha kuokoa baadhi ya bidha za wafayabiashara licha ya vijana wachache kutaka kuiba na kutupa mawe askari wake ili wafanye uhalifu wa kupora bidhaa zilizokuwa zinaokolewa hapo mpaka sasa vijana wawili wamekamatwa kwa kutupiaaskari mawe na kuiba bidhaa zilizokuwa zinaokolewa
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kamanda diwani 


PROF LIPUMBA: MADAI YA WANANCHI WA MTWARA YASIPUUZWE


Tarehe 27 Desemba maelfu ya wananchi wa Mtwara waliandamana kudai gesi ya Mnazi Bay itumiwe kuendeleza viwanda katika mkoa wa Mtwara kabla ha

ijasafirishwa kwenda kutumiwa maeneo mengine ya nchi. Kwa muda mrefu CUF Chama cha wananchi kimekuwa kikisisitiza kuwa na sera zitakazohakikisha kuwa maliasili na rasilimali za nchi zinawanufaisha Watanzania wote kwa ujumla na hususani wananchi wanaoishi katika maeneo ambayo maliasili hiyo imegunduliwa.

Katika nchi nyingi utajiri mkubwa wa gesi na mafuta umeleta balaa badala ya kuleta neema. Nchini Nigeria katika delta ya mto Niger ambako ndipo mafuta yanachimbwa kuna ghasia kubwa za kisiasa kwa madai kuwa wananchi wa eneo hilo hawanufaiki na rasilimali yao.

Wananchi wa mikoa ya kusini wana sababu za msingi za kulalamika kuwa  kwa muda wa miaka 51 ya uhuru wa
Tanzania Bara bado hawajatendewa haki. Serikali ya mkoloni wa Kiingereza ilijenga reli kuunganisha Nachingwea na Mtwara ilipoanzisha mradi wa kilimo cha karanga. Mradi huu haukufanukiwa. Badala ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo na kuendeleza uzalishaji wa mazao mengine kama vile korosho, ufuta, alizeti, kunde na mbaazi, Serikali ya TANU baada ya kupata uhuru ikaamua kun’goa reli ya Nachingwea – Mtwara na kuihamishia Kilosa Mikumi.

Zambia ilipokuwa inakabiliwa na tatizo la kusafirisha mizigo yake isipitie Rhodesia iliyokuwa inatawaliwa na wazungu wachache, walipendekeza kwa serikali ya Tanzania kujenga reli kwenda Mtwara kwani bandari ya Mtwara ni nzuri, ina kina kirefu na haina msongamano. Shaba ya Zambia ingepakuliwa kwa haraka na kusafirishwa kwenda nchi za nje. Vile vile mizigo inayoagizwa kutoka nje ingepakuliwa haraka na kusafirishwa kwenda Zambia. Serikali ya Tanzania haikuafiki pendekezo la Zambia na ikasisitiza reli ya TAZARA iende Dar es Salaam.

Gesi ya Songosongo ilikuwa itumiwe kama malighafi katika kiwanda cha mbolea cha Kilwa Ammonium Company. Prof Cleophace Migiro alienda kusomea PhD ya Chemical engineering kwa maandalizi ya kuja kufanya kazi KILAMCO. Ardhi ya kujenga kiwanda ilinunuliwa Kilwa Masoko, kiwanja cha ndege kikatengenezwa, mpango wa kuimarisha bandari ya masoko ukaandaliwa. Mgogoro wa uchumi wa miaka ya 1980 ikatibua mambo.

Dr. Shija waziri wa Nishati na Madini katika kipindi cha kwanza cha Rais Mkapa alizungumzia umuhimu wa kufufua mradi wa KILAMCO lakini hakuna kilichotendeka. Gesi ilipoanzwa kuchimbwa Songosongo likajengwa bomba dogo la nchi 12 kusafirisha gesi chini ya bahari toka Songosongo hadi Somanga. Bomba la nchi 14  lilijengwa toka Somanga hadi Dar es Salaam.

Uwezo wa mabomba haya ni mdogo ukilinganisha na gesi inayopatikana Songosongo na mahitaji yake kwa shughuli ya kufua umeme na kutumia viwandani. Mkopo wa kujengea bomba la Songosongo hadi Dar es Salaam ulighubikwa na tuhuma za ufisadi za ujenzi wa kituo cha kufua umeme cha IPTL kinachotumia mafuta mazito ambacho gharama zake za kufua umeme ni za juu sana. Mkataba wa TANESCO na IPTL uliiwajibisha TANESCO kuilipa IPTL dola milioni moja kila mwezi hata kama haijazalisha umeme wowote. Mkataba huu ulidhoofisha sana hali ya fedha ya TANESCO.

Kampuni ya Artumas iligundua kuwepo kwa gas Mnazi Bay, Mtwara na kuanza utaratibu wa kuichimba mwaka 2006 na kuitumia kufua umeme wa Megawati 18. Kabla ya mtikisiko wa sekta ya fedha na uchumi wa dunia wa mwaka 2008, Artumas ilikuwa na mpango wa kuwekeza kwenye mtambo wa kufua umeme Mtwara wa Megawati 300 na kuunganisha Mtwara kwenye gridi ya taifa. Mpango huu ulikubaliwa na serikali na ukaingizwa katika Mpango Kabambe wa Taifa wa kufua na kusambaza umeme (National Power Development Master Plan). Mradi huu wa kufua umeme MW 300 Mtwara ulipangwa uwe umekamilika mwaka huu wa 2012.

Mtikisiko wa uchumi na fedha duniani wa 2008 uliikumba kampuni ya Artumas. Thamani ya hisa za Artumas iliporomoka katika soko la mitaji Canada na Norway. Artumas iliiomba serikali dola milioni 7 kunusuru Mradi wa Nishati wa Mtwara (Mtwara Energy Project). Uwezo wake wa kutekeleza mpango wa kufua umeme Mtwara ukatetereka pamoja na kuwa mradi huo una faida ya muda mrefu. Kampuni ya Artumas Group Inc. iliamua kubadilisha jina lake na kuwa Wentworth Resources Limited.

Wananchi wa Mtwara wanahitaji kujua kwa nini serikali haikutafuta njia mbadala ya kugharamia mpango wa kufua umeme na kuiunganisha Mtwara na gridi ya taifa?

Wentworth Resources wamefanya upembuzi yakinifu (feasibility study) na kubaini kwamba njia nzuri ya kibiashara na kiuchumi ya kutumia gas wanayoweza kuzalisha Mnazi bay hivi sasa ni kuanzisha kiwanda cha kutengeneza mbolea na kemikali nyingine Mtwara. Hata hivyo serikali imewamrisha kupeleka gesi watakayozalisha kwenye bomba la gesi la kwenda Dar es Salaam. Gazeti la Financial Time la London la tarehe 6 Desemba 2012 linaeleza

“Bob McBean, executive chairman of Wentworth Resources, which explores in Mnazi Bay, had been planning to use any gas finds together with an existing discovery to power a petrochemical plant to make Africa’s first home-produced fertiliser. “We can supply 80[bcf] right away but we’d have made more money with the plant,” anasema Bw.Mc Bean ambaye kampuni yake imetakiwa kusafirisha  gesi kwenda Dar es Salaam.

Kampuni inayochimba gesi inaamini kuwa kujenga kiwanda cha kutengeneza mbolea Mtwara kitakuwa na faida kubwa kwa kampuni yake. Isitoshe kiwanda hicho kitaongeza ajira kwa vijana wa Mtwara. Kitaanza kuijenga Mtwara kama kituo cha sekta ya gesi na viwanda vyake. Upatikanaji wa mbolea ya bei inayotengenezwa hapa nchini utasaidia kuendeleza kilimo na kuifanya kaulimbiu ya Kilimo Kwanza kutekelezwa kwa vitendo. Hatua ya serikali kuilazimisha Wentworth Resources kuipeleka gas ya Mnazi Bay kwenye bomba la gesi ili isafirishwe Dar es Salaam kunaathiri maendeleo ya Mtwara na Tanzania kwa ujumla.

Ujenzi wa bomba la Mtwara umeanza bila kuwa na mipango ya kuhakikisha kuwa kutakuwepo na gesi ya kutosha kuisafirisha hadi Dar es Salaam. Bomba hili litakuwa na uwezo wa kusafirisha futi za ujazo bilioni 200. Uwezo wa gesi ya Mnazi Bay kwa hivi sasa ni futi za ujazo bilioni 80. Hakuna mpango unaoeleweka wa kupata futi za ujazo bilioni 120 ili bomba la gesi liweze kutumiwa kikamilifu. Mpaka hivi sasa gesi kiasi cha futi za ujazo trilioni 33 imegunduliwa hasa katika bahari yenye kina kirefu. Kuna uwezekano wa kugundua mafuta. Uchimbaji wa gesi hii bado haujaanza. Inaweza kuchukukua miaka 7 – 10 kabla ya shughuli ya uchimbaji wa gesi kukamilika na kuanza kuitumia ndani ya nchi au kuiuza nje ya nchi.

Upatikanaji wa mkopo wa masharti nafuu kutoka China wakujenga bomba la gesi ndiyo umeishawishi serikali kutekeleza mradi  huu haraka bila maandalizi ya uzalishaji wa gesi ya kutosha.Ni vyema serikali ingetekeleza mradi wa kufua umeme Mtwara na kuunganisha Mtwara na gridi ya taifa na kuruhusu kiwanda cha mbolea kuanzishwa Mtwara.

CUF Chama cha wananchi tunaitaka serikali kuzingatia kuwa, kwa kuwa mradi wa kujenga bomba la gesi uko katika hatua za mwanzo ni vyema serikali ikatathmini upya mantiki na faida za mradi huo. Mradi unaweza kutekelezwa kwa awamu. Awamu ya kwanza iwe kujenga bomba la gesi had Somanga Kilwa ili kuongeza uwezo wa kusafirisha gesi ya Songosongo kuja Dar es Salaam.

Kama nchi bado tuna udhaifu mkubwa wa kuandaa mipango na kusimamia utekelezaji wake. Serikali itufahamishe utekelezaji wa National Power Development Master Plan umefikia wapi? Vipi Mtwara development Corridor bado ipo?

Katika kusimamia sekta ya gesi tujifunze toka nchi ya Norway, Ili kuendesha shughuli za mafuta kwa ufanisi, Norway iliamua mapema kuwa makao makuu ya shughuli za mafuta utakuwa Stavange na siyo mji mkuu wa Oslo. Uamuzi huu umeufanya mji wa Stavange kukua na kuwa kituo cha biashara ya mafuta. Mtwara uwe mji mkuu wa shughuli zote za mafuta na gesi kwa sababu ina bandari asilia yenye kina kirefu na gesi imeanza kugunduliwa kanda ya kusini ya bahari ya Tanzania.

CUF tunasisitiza kwamba, malalamiko ya wananchi wa Mtwara ni ya msingi na wala hayaathiri umoja wa kitaifa. Maoni yao ya kuwa na viwanda vinavyotumia gesi Mtwara na maeneo mengine ya kusini yana mantiki ya kiuchumi. Serikali iwasikilize isiwabeze. Msimamamo wa CUF wa Dira ya Mabadiliko ni kuhakikisha kuwa maliasili na raslimali za nchi zinatumiwa vizuri kuleta neema kwa wananchi wote. Wananchi wa Mtwara wana haki ya kunufaika na neema ya gesi ya Mnazi Bay.

Mwisho Watanzania wote heri ya mwaka mpya – Happy New Year.

Imetolewa na

Mwenyekiti wa CUF-Chama cha wanachi, Taifa
Mhe. Prof. Ibrahim Lipumba


ALIYETANGAZA KUGOMBEA URAIS 2015 AJIONDOA CHADEMA

   

  Uamuzi huo wa Kisandu umekuja siku chache baada ya kutangaza maandamano kwa nchi nzima kupinga hatua ya Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Wilbrod Slaa, kumiliki kadi mbili ikiwemo ya CCM.


Akizungumza jana na blog hii ya www.kitongoni.blogspot.com Jumapili kwa njia ya simu, Kisandu alisema hatua ya kujiondoa ndani ya CHADEMA imekuja baada ya viongozi wa Taifa wa chama hicho kumuandama kutokana na msimamo wake.
Kwa muda mrefu hasa baada ya kutangaza nami nitagombea nafasi ya urais nimeonekana kuwa ninatumiwa na CCM. Na hata nilipotoa tamko la kuitishwa maandamano kwa nchi nzima ya kutaka Dkt. Slaa, ajiuzulu kutokana na kumiliki kadi ya CCM, imekuwa ni chuki na uhasama baina yangu na viongozi.

Kwa hali hiyo nimetafakari kwa kina na leo hii (jana), ninatangaza rasmi kujivua nafasi zote za uongozi pamoja na unachama wa CHADEMA, huku bado nikibaki na dhamira yangu ya kuendelea kuwa mpigania haki. Nitabaki na msimamo wangu wa kugombea urais mwaka 2015 hata kwa kuwa mgombea binafsi bila kupitia chama chochote. Kwa sasa siwezi kusema nitaelekea chama gani ila baada ya muda ninaweza kusema ninaelekea chama gani ingawa si CCM.

Ninajua wazi sisi watu wa kanda ya ziwa ndani ya CHADEMA tumekuwa tukionekana kama virusi kwani alianza Shibuda, kutangaza nia ya kugombea urais, kila kona alipigwa vita na baadaye Zitto nchi nzima inajua hadi leo hii namna ambavyo anavyosakamwa ndani ya chama. Hata nami nilipotangaza hilo, viongozi wa kitaifa waliweza kuwatumia viongozi wa ngazi za chini katika mkoa huu na kwa muda mrefu sasa kumekuwa na hisia hasi juu yangu na Mkoa wa Tanga kwa ujumla, juu ya ushiriki wangu kwenye shughuli za chama.

Natambua kwamba wapo ambao tayari wameniona mnafiki, mamluki na msaliti kwasababu tu ya kutopenda kutambua ukweli juu ya mwenendo wa chama changu cha CHADEMA

alisema Kisandu.
Akizungumzia ziara za Vugu vugu la Mabadiliko (M4C) zimekuwa za kiupendeleo zaidi, bila kuzingatia maeneo ambayo hayakufikiwa na kampeni za Urais mwaka 2010.

Alisema Mkoa wa Tanga umekuwa ukitengwa sana na kutokuthaminiwa katika ujenzi wa chama, huku chama hicho kikijengwa kwa misingi ya kujitolea lakini kutokana na ubinafsi wa viongozi imekuwa ni kikwazo.

“Ninashindwa kuelewa vigezo vya M4C katika kuchagua viongozi wanaotakiwa kushiriki ziara za vuguvugu la mabadiliko (M4C). Inanishangaza kuona mwanachama aliyejiunga jana CHADEMA akitokea CCM, leo anapewa kipaumbele kuliko viongozi waliojenga chama kwa muda mrefu. Tumejenga chama kwa nguvu ya kujitolea hasa huku mikoani, wilayani na majimboni bila kulipwa chochote, leo hii tunaonekana hatufai hatuna maana,” alisema.



Friday, December 28, 2012

BASI LA ABIRIA USO KWA USO NA LORI LEO

Basi la Abiria limegongana uso kwa uso katika eneo lijulikanalo kwa jina la PIPE LINE INYALA Mbeya baada ya Dereva wa Lori kulipita gari lingine mlimani na ndipo alipokutana na Basi hilo uso kwa uso. Zaidi ya abiria 40 wamenusurika kufa katika ajali hiyo, Dereva wa Lori ambaye ndiye aliyetajwa kuwa na makosa alikimbia kusikojulikana baada ya ajali hiyo na bado anasakwa kwa udi na uvumba.

SAKATA LA ELIMU FEKI: MULUGO YUPO TAYARI KUTHIBITISHA

NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bw. Philipo Mulugo, amesema yupo tayari kumthibitishia Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Bw. Joseph Mbilinyi, maarufu 'Sugu', juu ya elimu aliyonayo kama alivyodai mbunge huyo. Bw. Mulugo aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu madai ya Bw. Mbilinyi ambayo ameyatoa katika vyombo vya habari kuwa, Waziri huyo ana elimu ya kuunga unga na jina lake kamili ni Amim. Alisema kauli ya Bw. Mbilinyi haina ukweli wowote bali yeye ni msomi na yupo tayari kuthibitisha ukweli huo kwa umma. “Mimi na Bw. Mbilinyi tuna vilema vingi, akitaka tuumbuane yatabainika mengi hasa katika upande wake, namfahamu muda mrefu kwa sababu nimesoma naye shule moja, nafahamu mambo yake mengi lakini kutokana na hekima zangu sihitaji malumbano na yeye,” alisema Bw. Mulugo. Alidai kumshangaa Bw. Mbilinyi, kuzungumzia jambo ambalo halifahamu lakini kwa kumsaidia ili asielendelee kuonekana mwanasiasa muongo, aitishe mkutano na waandishi wa habari na yeye atakuwa tayari kuthibitisha elimu yake kwa umma. Bw. Mulugo aliongeza kuwa, ni kweli wakati anasoma alikuwa akitumia jina la Amim na baada ya kufika elimu ya juu alianza kutumia jina la Philipo ambalo ni la ukoo ambapo Bw. Mbilinyi kama angekuwa makini, angefuatilia kwenye ukoo wake ili kujua jina hilo linamuhusu au la. Aliongeza kuwa, dhamira yake ni kuhakikisha kuwa Jimbo la Mbeya Mjini ambalo hivi sasa linashikiliwa na Bw. Mbilinyi, mwaka 2015 linarudi CCM na ukweli huo utathibitika katika uchaguzi. “Mimi ni Waziri kutoka CCM na Mjumbe wa Halmashauri Kuu NEC, hivyo Bw. Mbilinyi, asifikiri kuzua maneno hayo yatanitisha hadi nishindwe kutekeleza sera za chama changu,” alisema. Alisema ibara ya 5 ya Katiba ya CCM, inamwongoza kuhakikisha chama chake kinashinda uchaguzi wa dola wa ngazi zote pamoja na kulirudisha jimbo la Mbeya Mjini kutoka upinzani. “Katika Uchaguzi Mkuu ujao, nitatumia nguvu zote kuhakikisha jimbo la Mbeya Mjini linarudi CCM, ninachoweza kumshauri Bw. Mbilinyi, ajifunze kutokana na makosa kwani ameanza kunitafuta siku nyingi lakini mimi sikuwa na muda wa kumjibu bali niliendelea kutekeleza majukumu niliyonayo,” alisema. Alisema Mbunge huyo na chama chake walijibiwa na wananchi wa Saza katika mkutano wa CHADEMA uliofanyika katika Wilaya ya Chunya na kusahau kilichowapeleka ni kampeni hatimaye wakaanza kunadi elimu ya Mulugo badala yake waliambulia kufukuzwa. Aliongeza kuwa, Bw. Mbilinyi alipaswa kulisema na hilo kama walifukuzwa na wananchi wa Saza ambao walimwambia wao, wanamfahamu vizuri Bw. Mulugo na wamemsomesha wenyewe kwa pesa zao baada ya kuthibitika ni yatima. Alisema wananchi hao walidai kuchoshwa na matusi ya Bw. Mbilinyi dhidi yake na kumtungia uongo lakini yeye hana muda wa kulumbana naye bali atamjibu kwa ushahidi. Kauli ya Bw. Mulugo imekuja siku chache baada ya Bw. Mbilinyi kudai kuwa, elimu ya Waziri huyo ni ya kuunga unga kwani alisoma naye Sekondari ya Mbeya Day, wakati huo akiitwa Amim si Philipo Mulugo hivyo kuanzia sasa ataendelea kumuita jina lake halisi na kusisitiza hana uwezo wa kumng'oa jimboni kwake.

Tuesday, December 25, 2012

MARA HII URAIS WA MUUNGANO NI ZAMU YA ZANZIBAR

Imeandikwa na Stonetown (Kiongozi) Miaka mitatu kutoka sasa, Tanzania itafanya uchaguzi wake mkuu utaohitimisha miaka kumi ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete. Tanzania kama nchi nyengine duniani, inafata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katika mfumo wa vyama vingi, na iwapo kuna demokrasia ya kweli, basi ni matarajio yetu kuwa chama chchote kitakachoshinda kitapewa haki yake na ridhaa ya kuongoza nchi. Lakini pamoja na hayo, suali la uwiano wa Ugombea wa kiti cha Urais kwa pande mbili za Muungano, limekuwa likipuuzwa sana kuanikwa katika mijadala mbalimbali nchini. Suali la makubaliano ya mapokelezano ya wadhifa huu mkuu wa nchi baina ya sehemu mbili za Muungano, haujawekwa sawa na ni moja kati ya changamoto kongwe zinazoungana na mkururo wa kero za Muungano hapa nchini. Tangu tuungane, ni miaka takribani 49 sasa. Wakati Zanzibar ikiwa na marais saba tangu 1964, Jamhuri ya Muungano ndio inatimiza nusu tu ya wale waliokwisha tawala Zanzibar, ikiwa na marais wane tu hadi sasa. Mara baada ya Muungano, Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalim Julius Nyerere, alishika hatamu ya kuiongoza Jamhuri hadi pale ‘alipong’atuka’ madarakani kwa hiari yake mwaka 1984/85. Katika kipindi hichi cha miaka 20, Mwalimu hakuwahi kueleza wala kufafanua lolote kuhusu mpokezano wa madaraka kwa zamu baina ya nchi zetu hizi mbili. Naamini alifanya hivi sio kwa kutojua umuhimu wa kitendo hicho muhimu. Kitendo ambacho kingeashiria usawa mkubwa na haki inayosimamiwa na Muungano wetu. Mwalimu hakulijadili hili kwa sababu alijua wazi kufanya hivyo kungeviza ajenda yake binafsi ya kuimeza Zanzibar ndani ya matumbo ya Tanganyika na kuiondoa kabisa katika ramani ya dunia. Hili ndio lililokuwa lengo lake, bila shaka. Mungu akikupangia nakama, huna ujuzi wala ujanja. Kwani hayati Sheikh Abeid Karume, ambae ndie aliyekuwa Rais pekee wa Zanzibar aliekuwa akithubutu kumhoji na kumjibu Mwalimu lolote, lakini lakuvunda halina ubani, Sheikh Karume alikufa mapema mno. Tena wakati huo anakufa, bahati mbaya zaidi, ilikuwa Muungano huu haujawa na sura mbaya iliyo wazi wazi kama sasa, japo kiwingu cha dalili hizo mbaya kilianza kuonekana kwa mbali. Sheikh Karume akauwawa, na sababu ya kifo chake, ikafikichwa fikichwa, kisijulikane cha ukweli hadi leo.Ni begeje tu. Na kwanini, watu washuhulike na hili wakati, kufa kwa panzi ni neema ya kunguru? Aliekufa ndio kafa! Rais Jumbe, alijaribu kwa sana kuhoji hali kama hii. Lakini alichelewa mno.Na kwa jinsi Mwalimu alivyokuwa amejipanga kikazi kiulinzi na kiusalama, juhudi za Sheikh Jumbe zikawaka na moto. Zikaunguwa na kusakatuka kama kijungu cha dagaa tonge, kilichosahauliwa na mpishi aliekwenda kujisuka akisahau kuwa moto hauna sumile. Sheikh Jumbe akang’oka kama Mbuyu uliopigwa halbadiri ya mbayana. Akakunguzuka na mashina yake yote! Njia nyeupe! Baada ya majaribio haya mawili ya kujitokeza kwa Wazanzibari waliowakijifanya hawaogopi kumuhoji Nyerere, kilichofata ni mpango wa kudhibiti nani awe Rais wa Zanzibar. Ikawa Rais anaewekwa huku kwetu si katika yoyote anaeweza kuuhoji wala kuujadili Muungano, ‘imma faimma’ Nyerere awe hai, au awe ameshakufa. Na hili likafanikiwa. Bahati nzuri tu ‘Mtu si mbwa’. Hawa unaowaona walihoji kidogo wakaitwa ‘samaki’ na wavyele wao, ni matokezeo tu. Kwani haki haizami na dhulma haidumu. Viongozi wetu wa Zanzibar, ni watu waliopangwa maalum kufuata utaratibu waliopangiwa na wakubwa zao kule bara. Na kwa maana hii hakuna aliyewahi tena kuhoji kuhusu mgawano wa nafasi ya Urais wa Muungano. Ambapo, penye Uungwana na haki ndani ya Muungano huo, bila shaka tulikuwa tupokelezane zamu. Hata kama tuko katika mfumo wa vyama vingi kiasi gani. Kwa upande wa CCM bara, hili walikuwa walione pia. Hasa wao wakiwa kama chama chenya nguvu na chenye kushika hatamu. Ipo haja, tena bila kuzozana, kuipa nafasi Zanzibar kuongoza katika Jamhuri ya Muungano, tena katika wadhifa wa Urais, jambo ambalo linaonekana kuwa zaidi ya ndoto ya ‘Alinacha’ kwa sasa. Suali la kumpa Mzanzibari Urais wa Muungano ni ndoto ya Alinacha kwa sababu nyingi. Kwanza tuchukulie chama cha CCM kiwe na matumaini makubwa ya kushinda. Ukweli ni kwamba CCM na Muungano ni mtu na mama yake mzazi. Nasema ni mama kwa sababu hutokea watoto wasio baba kabisa, wala watu wengine, lakini hakuna mtoto asie na mama. Na mapenzi ya mama kwa motto hayana kifano chake. Na tunategemea vivyo hivyo kwa mtoto na mama yake. Kama haya ni kweli, na dhamira ya Muungano ni ile ile ya kuelekea nchi moja. Tena wakati ambao Wazanzibari wanahitaji ‘kupumuwa’ kwa nguvu zote. Hili ni gumu. Isitoshe, ukiwauliza zamu ya Zanzibar lini, wanakujibu kuwa Mwinyi alikuwepo hapa. Hivi Mwinyi ni Mzanzibari? Kwa kigenzo kipi? Na haya naawe huyo Mzanzibari kama ataamuwa kujinadi hivyo, lakini sula linabaki kuwa Marais wawili sasa, yaani miaka 20, Urais uko bara. Kuna ubaya tena gani wakitupa tena kumi, kama kweli tuna nia njema?Hapa panahitajika tuwe wakweli wadadisi kidogo juu ya hili. Ama kwa upande wa CHADEMA, naona wazo hili si mahala pake hata kidogo. Ingawa CCM na chadema lao moja, na ndio ukaona CHADEMA iliibuka tu kutoka katika ombwe, na kuja kuwa chama chenye nguvu hata kuliko CUF kule bara ambayo ilikuwa inaimarika vizuri siku hadi siku. Lengo, ni kuiondoa na kuizima nyota ya CUF kule wakiamini kuwa, kuanguka kwa CUF bara ni mafanikio makubwa ya kuzima nguvu ya wazanzibari kutaka kujitawala na ‘kupumuwa’. Na hili wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa. Kuna kila dalili kuwa CHADEMA, hawana mpango na Zanzibar zaidi ya kuimaliza zaidi. Na kama hili linasomeka hivyo katika ajenda zao za siri, hawana mpango wa kumpa Mzanzibari nafasi yoyote ile hata ya Ubunge sembuse Urais. Na hii ni kwa sababu moja kuu: CHADEMA ni wabaya zaidi kuliko CCM, kwani ubaya wao haujifichi. Isitoshe, mfungamano wao mkubwa na kanisa ambalo kwa kiasi kikubwa ndio linaloipa kiburi CHADEMA, unaifanya hali ya uwezekano wa Zanzibar wa kuwa na nafasi kubwa kama hio katika Muungano kuwa ya tembo kupenya tundu ya sindano. Pamoja na hayo, tusikate tamaa. Ipo haja kwa kila mmoja wetu wakiwemo viongozi kuhoji nafasi ya Zanzibar katika uongozi wa juu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Ijapokuwa tunaonekana kukubaliana na kuridhika kabisa na kitazonge, na changa la macho la kupewa kwetu Umakamo wa Rais. Nafasi ambayo haina athari yoyote kwa taifa zaidi ya kufunguwa vikao, kujulia wagonjwa na kuhutubia mikutano ya mazingira na Ukimwi. Pia tumeridhika na suala la Rais wetu kuwa Waziri katika Jamhuri ya Muungano, jambo ambalo haliingia akilini kabisa. Maana naamini wazi Makamo wa Rais bara, kiitifaki ni mkubwa zaidi kuliko Waziri, ambae pia ni Rais akiwa Zanzibar. Huu ni mchezo wa kitoto au wa kuku lala, tustiane majivu ya macho. Ukweli tunatakiwa tusitosheke na hapo. Tuhoji, tudai, na tutoe kauli moja, ‘Mara hii Urais wa Muungano, ni Zamu ya Zanzibar’. Tuwatazame na pumzi zao! Natoa hoja.

NBC’s Managing Director, Lawrence Mafuru resigns

The managing director of National Bank of Commerce (NBC), Mr Lawrence Mafuru, has resigned from the financial institution to which he had been reinstated about two months after a three-month suspension spell. Mr Mafuru was suspended by the board of directors in July to pave the way for investigations into alleged irregularities within the National Bank of Commerce (NBC).

The allegations which originated from a whistleblower report raised issues around irregular governance practices, fraud and corruption against the NBC executive management team. The statement issued upon his reinstatement in October, and which was signed by board chairman Dr Musa Assad, pointed out, in part, that, the board “had resolved appropriately all the matters arising out of the investigation.”

Mr Mafuru told The Citizen yesterday that his resignation starts effective December 24 as he looks for other opportunities, “I am a professional banker and think it is high time I pursued other opportunities outside the bank,” he said, adding: “After four years of a very progressive career at NBC, first as country treasurer since August 2007 and later as chief executive officer since June 2010 to date, I think that it is appropriate to seek other challenges elsewhere and allow others to steer the ship at NBC.”

The head of Marketing, Communications and Corporate Affairs at NBC, Ms Mwinda Kiula-Mfugale , confirmed to The Citizen that it was true that Mr Mafuru has resigned, but said she would issue a statement only after getting instructions from the board of directors.

Mr Mafuru was appointed managing director of one of the largest financial service providers in Tanzania in June 2010, succeeding Mr Christo de Vries from South Africa.

NBC is one of the oldest banks in Tanzania, tracing its origins to 1967 when the government nationalised financial institutions, including banks, before the banking industry was deregulated in 1991.
In 1997, NBC was split into three separate entities – NBC Holding Corporation, National Microfinance Bank (NMB) and NBC (1997) Limited.

In 2000, South Africa’s Absa Group Limited acquired a majority stake in NBC (1997) Limited. The government retained 30 per cent shareholding and the International Finance Corporation (IFC), a member of the World Bank Group, took a 15 per cent stake.

Speaking of the success he has had with the bank in the four years that he worked with it, Mr Mafuru remarked: “ I am very satisfied with the success I have had especially on the transformation agenda of NBC operations. We now have a much cleaner balance sheet, a stronger pool of talented young men and women; our customer experience has improved relative to where we are coming from and even more important we are well positioned for strong and sustainable growth in the next three years.”

He added: “On a personal note, I have had the opportunity to grow and develop professionally – I have grown both as business manager and a leader not only in the bank but also at industry level where I was privileged to serve as Chairman of Tanzania Bankers Association; I take pride that I also have been actively involved in shaping the future of banking in Tanzania.”



Tuesday, December 18, 2012

NDEGE KUBWA KUANZA KUTUA KIGOMA




NDEGE kubwa za abiria za kimataifa zinatarajiwa kuanza kutua Uwanja wa Ndege wa Kigoma kuanzia Desemba 15 mwaka huu baada ya uboreshaji wake kufikia hatua nzuri.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na blog hii mjini Kigoma, Meneja wa Mamlaka ya Usafiri na Usalama wa Anga (TCAA), Godlove Hongore amesema hadi kufikia katikati ya mwezi ujao meta 1,450 za kuruka na kutua ndege zitakuwa zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami kati ya meta 1,800 zinazotarajia kujengwa.
Alisema mkataba wa ujenzi wa mkandarasi wa uwanja huo unaisha Juni mwakani lakini ujenzi umeelezwa na msimamizi wa Kampuni ya Synohydro ya China kwamba unaweza kukamilika mapema zaidi ya muda uliopangwa.
Meneja wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege mkoani Kigoma, Elipid Tesha alisema mazungumzo yanaendelea vizuri ili kampuni hiyo ya Synohydro ya China iendelee na sehemu ya pili ya mradi huo katika mwaka ujao wa fedha utakaohusisha ujenzi wa njia ya kurukia ndege kufikia meta 3,000 na jengo la utawala na abiria uwanjani hapo.
Alisema tayari fedha za fidia kwa ajili ya eneo la makaburi ambalo litatumika kwa upanuzi huo, ipo na mazungumzo yanaendelea ni kuwezesha mkandarasi huyo kuendelea na sehemu hiyo ya pili ya mradi huo.
Meneja huyo wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Mkoa, alisema kukamilika kwa Awamu ya Pili ya ujenzi wa awanja huo kutaufanya Uwanja wa Ndege wa Kigoma kuwa na hadhi ya kimataifa na kuruhusu ndege kubwa zaidi ya tani 70 kutua.
Alibainisha kuwa uwanja huo ukikamilika, utakuwa kitovu cha ndege nyingi kutoka nchi za ukanda wa Maziwa Makuu na Afrika ya Kati kwenda Kusini na Kaskazini mwa Bara la Afrika na nje ya bara hilo.


KIGOMA UJIJI YATOA MWANAFUNZI BORA WA SAYANSI

SHULE ya Sekondari ya Kichangachui katika Manispaa ya Kigoma Ujiji imetoa mwanafunzi bora wa masomo ya sayansi kwa Kanda ya Magharibi katika mtihani wa majaribio (Mock Test) wa kidato cha nne uliofanyika hivi karibuni.
Akitoa taarifa kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Chung IL aliyefika shuleni hapo kukabidhi rasmi maabara kwa uongozi wa shule hiyo Mkuu wa Shule hiyo, Harles Lugenda alisema kuwa mafanikio hayo yametokana na kuanzishwa kwa maabara ya masomo ya sayansi katika shule hiyo.
Lugenda alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Justus Ferdinand ambaye aliongoza katika masomo ya Fizikia na Kemia ambapo alisema kwamba kuwepo kwa maabara hiyo iliyoanza kufanya kazi Januari mwaka huu kumeinuka ari ya wanafunzi wa shule hiyo kusoma masomo ya sayansi na kuahidi kufanya vizuri.
Maabara hiyo imetolewa na serikali ya Jamhuri ya Watu wa Korea kupitia Shirika lake la Maendeleo (KOICA) ambapo kiasi cha Sh milioni 25 zimetumika kwa ajili ya ukarabati wa vyumba viwili vya madasara vinavyotumika kama vyumba vya maabara na vifaa vyake.
Sambamba na ujenzi wa vyumba hivyo vya maabara pia Serikali ya Korea kupitia shirika hilo inagharamia masomo ya wanafunzi wanane wanaosoma masomo ya sayansi shule hapo ambapo tayari wameshalipiwa ada kwa miaka minne ahadi watakapomaliza masomo yao ya sekondari.
Akizungumza katika makabidhiano hayo Balozi Chung IL alisema kuwa msaada huo umelenga kunaimarisha ushirikiano wa kindugu uliopo baina ya serikali hizo mbili na watu wake.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispa ya Kigoma Ujiji , Alfred Luanda alisema kuwa pamoja na msaada huo bado Manispaa hiyo inakabiliwa na upungufu wa maabara za sayansi na vifaa vyake katika shule zake mbalimbali na kwamba kama ipo fursa ya kupata tena msaada zaidi aliomba serikali ya Korea kuangalia uwezekano huo.


BREAKING NEWS: MTU MMOJA AUWAWA KATIKA MAJIBIZANO YA RISASI KATI YA POLISI NA MAJAMBAZI KARIAKOO LEO HII

Mtu mmoja ameuwawa mida hii katika majibizano ya risasi yaliyotokea maeneo ya Msimbazi kariakoo, mtaa wa Livingstone kati ya Polisi na majambazi waliotaka kupora fedha zilizokuwa zinapelekwa benki ya NBC.

Majambazi hao waliokuwa wamevalia nguo za kiraia inasemekana walijua fedha hizo zinapelekwa leo hivyo walijiandaa kupora na Mapolisi nao waligundua hilo mapema hali iliyofanya majambazi hao kurusha risasi hovyo na kukimbia ili kukwepa kukamatwa.

Hadi sasa ni mtu mmoja anayeripotiwa kuuwawa ila bado haijajulikana kama ni raia au jambazi wale maana pia majambazi walivaa kiraia.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU