Facebook Comments Box

Friday, February 13, 2015

TFF YAIPA MATUMAINI MAKUBWA TOTO KURUDI LIGI KUU KWA KUIPA USHINDI DHIDI YA GEITA

Baraka-Kizuguto_3a74e.jpg
Afisa Habari wa TFF Baraka Kizuguto

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imethibitisha ushindi wa pointi 3 na mabao matatu kwa timu za Majimaji na Toto Africans baada ya mechi zao za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kuvurugika kutokana na sababu mbalimbali.

Toto Africans imepewa ushindi huo kwa mujibu wa Kanuni ya 41(3) ya FDL baada ya vurugu za washabiki wa Geita Gold kusababisha mechi hiyo iliyochezwa Februari 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita kuvunjika dakika ya 12.

Pia Kamati hiyo iliyokutana Dar es Salaam jana (Februari 12 mwaka huu) imezuia mechi za FDL kuchezwa kwenye uwanja huo ambao hauna uzio wa kutenganisha wachezaji na washabiki kwa sababu za kiusalama.

Naye mchezaji Venance Joseph wa Geita Gold ambaye alimpiga kichwa refa akipinga adhabu ya penati iliyotolewa dhidi ya timu yake kwenye mechi hiyo amesimamishwa wakati akisubiri kosa lake kusikilizwa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Malalamiko ya Friends Rangers kwenye mechi dhidi ya Majimaji yametupwa na kupigwa faini ya sh. 500,000 kwa kusababisha mchezo huo uliochezwa Januari 29 mwaka huu Uwanja wa Majimaji mjini Songea kuvunjika dakika ya 39. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 28(4) ya FDL.

Friends Rangers imepoteza mechi hiyo kwa mujibu wa Kanuni ya 28(1) ya FDL, Majimaji kama ilivyo Toto Africans imepewa ushindi wa pointi tatu na mabao matatu.

Naye Kocha wa Friends Rangers, Herry Chibakasa (Mzozo) suala lake limepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF ili aweze kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni ya 39(8) ya FDL kwa kuhamamisha vurugu kwenye mechi dhidi ya Majimaji.

Mwamuzi John Mafuru wa Mbeya aliyechezesha mechi ya Majimaji na Friends Rangers amefungiwa miezi 12 (kumi na mbili) kwa kutozingatia sheria kiasi cha kuvuruga mchezo. Adhabu hiyo imezingatia Kanuni ya 37(1) ya FDL.

Pia Kamishna wa mechi hiyo Kim Rajab wa Dodoma amefungiwa miezi 12 (kumi na mbili) kwa mujibu wa Kanuni ya 38(1) ya FDL kwa kutoa taarifa zisizo sahihi.

Lipuli ya Iringa imepewa ushindi wa mabao matatu na pointi tatu baada ya timu ya KMC (Tessema) kumchezesha mchezaji Morris Paulo Katumbo aliyekuwa na kadi tatu za njano kinyume na Kanuni ya 41(12) ya FDL. Katumbo ambaye alipata kadi hizo kwenye mechi namba 85, 100 na 112 alicheza mchezo huo uliomalizika kwa timu ya KMC kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


Tuesday, February 10, 2015

RAIS KIKWETE ALIPOFANYA MAZOEZI YA KUTEMBEA ASUBUHI





RAIS KIKWETE ZIARANI KILIMANJARO LEO

Jengo jipya la kisasa la kitega Uchumi la Mfuko wa Hifadhi ya Jami NSSF mkoani Kilimanjaro

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete leo anatarajia kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Kilimanjaro ambapo miongoni mwa shughuli anazotazamiwa kufanya ni pamoja na
kufungua jengo la kitega uchumi la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mbali na ufunguzi huo Rais Kikwete pia anatarajia kufungua jengo la Upasuaji na kuweka jiwe la msingi katika jengo la wodi ya wazazi na watoto katika hosptali ya rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro ,Mawenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ,mkuu wa mkoa huo Leonidas Gama alisema Rais Kikwete atawasili mkoani humo leo jioni majira ya saa 11:00 jioni ambapo atapokelewa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kuelekea Ikulu ndogo kwa ajili ya kupokea taarifa ya Mkoa.

Alisema Kesho (February 10) Rais Kikiwete atafanya shughuli katika Hospitali ya Rufaa ya Mawenzi ikiwemo ufunguzi wa jengo la Upasuaji (Theater) ambalo limekuwa tatizo la muda mrefu katika hosptali hiyo.

“Kwanza kama mnavyo fahamu tumekuwa na tatizo la muda mrefu ya wodi ya upasuaji katika hospitali yetu ya Mawenzi,lakini kwa juhudi zilizofanywa na serikali na ushirikiano wa wadau mbalimbali lile jengo

la Upasuaji limekamilika na liko katika kiwango kizuri kwa hiyo shughuli ya kwanza atakuja kulifungua rasmi jengo la upasuaji.”alisema Gama.

Gama alisema pia Serikali tayari imefanya juhudi za kujenga jengo jipya la Wodi kwa ajili ya Wazazi na Watoto katika hosptali hiyo na kwamba Rais Kikwete ataweka rasmi jiwe la msingi kwa ajili ya muendelezo wa ujenzi wa jengo hilo.

Alisema kwa mujibu wa ratiba shughuli ya mwisho anayotazamia kufanya Rais Kikwete ni ufunguzi rasmi wa jengo la kitega Uchumi la NSSF, jengo ambalo litatumika kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi .

“Ufunguzi rasmi wa jengo hili utabadilisha taswira ya mji wetu,ni jengo la kisasa lenye Hotel,Maofisi mbalimbali,Kumbi za mikutano na maduka mbalimbali makubwa kwa madogo ambayo yatahudumia wananchi wote”alisema Gama.

Gama alitoa wito kwa viongozi na wananchi wote wa mkoa wa Kilimanjaro kujitokeza kwa wingi katika ufunguzi wa jengo hilo la NSSF majira ya saa 2:00 asubuhi ambapo rais Kikwete pia atapata nafasi ya kuzungumza na wananchi.

“Lengo la Rais Kikwete kuja ni kutuunga mkono sisi wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro katika miradi yetu ya maendeleo hivyo basi tufike mapema katika maeneo hayo ili tumsubiri na tumuone rais na kumshangilia”alisema Gama.
  • Dixon Busagaga, Moshi via Michuzi Blog


TEKNOLOJIA YATUMIKA KATIKA KESI YA SHEIKH PONDA

UPANDE wa Mashikata kesi inayomkabili Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shehe Ponda Issa Ponda umewasilisha ushahidi muhimu wa mkanda wa video unaodaiwa kuonesha uhalisia wa tukio zima la kesi yake inayomkabili ya kutoa maneno ya uchochezi.

Mkanda huo wa video uliletwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro, Mary Moyo na kuoneshwa na shahidi wa tano wa kesi hiyo ambaye ni askari kutoka makao makuu ya Jeshi la Polisi kitengo maalumu cha uchunguzi wa picha,

Aristides alieleza vigezo alivyovitumia kuitambua uhalisia wa video hiyo iliyochukuliwa Agosti 10 mwaka 2013.
Shahidi huyo akiongozwa na Wakili wa Serikali, Benard Kongola alieleza mahakamani hapo kuwa video aliichunguza na kugundua kuwa ilichukuliwa katika eneo la tukio kupitia kamera ndogo aina ya JVC na kwamba baada ya kuichunguza aliandika hati na taarifa iliyoeleza vigezo alivyovitumia
katika uchunguzi huo na yale aliyoyaona na kuyasikia katika video hiyo ambayo aliitoa mahakamani kama kielelezo.
Pamoja na ushahidi wake, lakini pia aliionesha video hiyo mahakamani hapo ambapo ilionesha tukio zima pamoja na maneno aliyoyatoa Shehe Ponda ambayo yanadaiwa kuwa yalikuwa ya uchochezi na yaliyoumiza imani ya dini nyingine.
Shahidi huyo pia alitoa kamera, DVD, hati na taarifa ya uchunguzi wa video hiyo kama kielelezo na kupokewa na mahakama hiyo.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna msaidizi wa Polisi, Faustine Shilogile alikuwa shahidi wa nne katika kesi hiyo ambaye alieleza kuwa baada ya kupata taarifa za kutafutwa kwa Shehe Ponda kufuatia tuhuma mbalimbali zilizomkabili yeye kama kiongozi wa jeshi la polisi
mkoa aliandaa askari kwa ajili ya kumkamata baada ya kufika mkoani Morogoro.

Shahidi huyo alidai kuwa taarifa hizo za kiintelijensia zilimhusisha Ponda na tuhuma za kumwagia tindikali wasichana wawili raia wa Uingereza huko Zanzibar na tuhuma za kutoa maneno ya uchochezi jijini Dar es Salaam na kwamba tuhuma hizo alizipata wakati akiwa kwenye adhabu ya kifungo cha nje cha mwaka mmoja ambapo pia alitakiwa kutofanya kosa lolote katika kipindi hicho cha mwaka mmoja.

Upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Juma Nasoro ulimuuliza maswali shahidi huyo, hata hivyo baadhi ya watu waliokuwepo mahakamani hapo walishindwa kuzuia vicheko vyao kutokana na aina ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa pamoja na majibu yaliyokuwa yakitolewa.

Wakili wa utetezi: “Je wewe ulijuaje kama Shehe Ponda alitoa maneno ya uchochezi?”

Shahidi: “Niliambiwa na OCD wangu kupitia radio call (simu ya upepo) kwani alikuwepo eneo la tukio.”

Wakili: “Je, unayajua mashitaka yanayomkabili Shehe Ponda?”

Shahidi: ”Siyafahamu kwa kuwa mimi sio muandaaji wa hati ya mashitaka.”

Wakili: “Ni askari wangapi uliwaandaa kumkamata Shehe Ponda?”

Shahidi: “Sikumbuki”

Wakili: “Je, hukuandaa askari 25 hadi 30 kwa ajili ya kumkamata Shehe Ponda? “

Shahidi: “Wewe ndio utakuwa umeeleza hiyo idadi”

Wakili: ”Je, askari wako walikuwa na silaha na kama walikuwa nazo tunaweza kuamini kuwa wao ndio waliomjeruhi Shehe Ponda?”

 Shahidi: “Ndiyo baadhi ya askari wangu walikuwa na silaha lakini siwezi kufahamu Shehe Ponda
alijeruhiwa na nini.”

Wakili: “Je, unajua kama Msemaji wa Polisi, Advera Senso alitoa taarifa kuwa kuna askari alisimamishwa kazi kupisha uchunguzi?”

Shahidi: “Sina taarifa na kama alitoa taarifa hizo basi ni yeye na sio mimi.”

Wakili: “Je, kibali cha kufanya kongamano kilitolewa na nani na je uliambiwa kama Shehe Ponda ni mzungumzaji katika kongamano hilo?”

Shahidi: “Kibali kilitolewa kwa OCD na sikuwa na taarifa kama Shehe Ponda atakuwa mzungumzaji.”

Awali, upande wa mashtaka ulipanga kusikiliza mashahidi watano hata hivyo mahakama ilishindwa kuendelea kusikiliza mashahidi wengine watatu kutokana na muda kuwa umekwisha hivyo mashahidi hao watatu wataendelea kusikilizwa leo Februari 10 katika mahakama hiyo.

Hata hivyo, kesi imeendelea kuvuta hisia za wakazi wengi wa mkoa wa Morogoro na maeneo mengine huku hali ya ulinzi katika viwanja vya mahakama hiyo ikiwa imaimarishwa na kufikia hatua ya kuweka vifaa maalumu vya kuwakagua watu wanaoingia katika mahakama hiyo.

Monday, February 2, 2015

SOMA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 02 FEBRUARI, 2015 HAPA



















FRANCIS CHEKA AFUNGWA MIAKA MITATU JELA

Bondia maarufu nchini wa ngumi za kulipwa Francis Cheka amehukumiwa kifungo cha miaka 3 jela na kutakiwa kulipa fidia ya shilingi millioni 1 kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi meneja wa baa yake iliyopo huko Morogoro.

Meneja huyo ajulikanaye kwa jina la Bahati inaelezwa alienda kudai fedha zake alizokuwa hajalipwa na bondia huyo wakati akifanya kazi ya umeneja katika baa yake hiyo ndipo Bondia huyo alikataa kumlipa na kumshushia kipigo.
 Francis Cheka akiwa amevaa mkanda wa ubingwa katika moja ya mapambano yake aliyo wahi kucheza na kushinda.
 Francis Cheka hapa akiwa anafanya mazoezi kabla ya mpambano.


Friday, January 30, 2015

AMCHINJA MPENZIWE NA KUMUUA MANZESE DAR ES SALAAM

Kijana mmoja ambaye jina lake halijapatikana alikamatwa na Polisi jana jioni(Alhamisi) katika maeneo ya Manzese baada ya kumchinja mpenzi wake mpaka kufa kwa kile kinacho dhaniwa kuwa ni wivu wa kimapenzi, Kijana huyo nae alijaribu kujiua kwa kutumia kisu hicho bila mafanikio.
Jionee picha za tukio hilo hapo chini:
 Mtuhumiwa wa tukio hilo ambaye Jina lake bado halijapatikana.
Mwili wa Binti anaedaiwa kuchinjwa na mpenzi wake huyo ukitolewa eneo la tukio maeneo ya Friends Corner-Manzese jana(Alhamisi) jioni.


MAGAZETI YA LEO ALHAMIS TAREHE 29 JAN 2015




























Sunday, January 25, 2015

HATIMAYE DALALI WA UMEME PROF SOSPETER MUHONGO AJIUZURU


Kufuatia kuhusishwa na sakata la
uchotwaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow, Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo ameamua kumuandikia barua Raisi ya kujiuzulu wadhifa wake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Profesa Muhongo ameelezea furaha yake ya kupatikana kwa maendeleo ya haraka katika wizara yake kwa kipindi chake akisema kuwa nidhamu na uwajibikaji vilikuwa dira ya maendeleo wizarani hapo.

Profesa Muhongo amekwenda mbali
zaidi na kueleza kuwa anaamini
kujiuzuru kwake kutaisaidia Serikali na
Bunge kutuliza malumbano ya Sakata
hilo ambalo linazidi kurudisha nyuma
maendeleo ya nchi.
Amesema yeye si mwizi na hawezi
kuuza utu wake kwa kupewa rushwa ili
kuwakandamiza watanzania.
“Nimeamua kujiuzuru kwa dhati kabisa
bila kushinikizwa na mtu yeyeote,
inaonekana mimi ndiyo nitamaliza
mjadala huu wa sakata la Escrow, tuna
mambo mengi ya kitaifa yanayotakiwa
kujadiliwa lakini watu wamekazana na
Escrow, nimemuandikia Rais barua
rasmi ya kujiuzuru wadhifa wangu,
amesema Profesa Muhongo.
Amesema pamoja na kujiuzuru
anatarajia mapema kuzungumza na
watanzania ili kuwaeleza ukweli wa
sakata la Escrow na kujiuzuru kwake ili
kuvunja majungu yanayoendelea kuitesa
Tanzania na watu wake.
Amesema yeye amelelewa katika malezi
yenye maadili mema na kwamba tokea
alipomaliza masomo yake aliaswa
kutopokea ama kutotoa rushwa hivyo
hawezi akapokea rushwa kwa ajili ya
kuutukana utu wa mtanzania hicho
ndicho kinachomgharimu.



Friday, January 9, 2015

BABA AJINYONGA BAADA YA KUMTOBOA MTOTO WAKE MACHO

Mtoto Agripina
Mkazi wa Muleba mkoani Kagera Godfrey Joseph Kajuna mwenye miaka 45 amejinyonga mpaka kufa baada ya kumshushia kipigo kikali na kumtoboa macho binti yake Agripina Godfrey mwenye miaka 12.

Bwana Godfrey aliondoka nyumbani kwake akiacha maagizo kuwa wasimfungulie mlango mama yao pindi akirudi nyumbani. Mabinti hao aliporudi mama yao hawakufungua mlango kwa kumuhofia baba yao.

Baba yao aliporudi aliuliza mama yao yupo wapi. Ndipo watoto hao wakamjibu kuwa ameenda kujihifadhi sehemu nyingine kwa kuwa hawaku mfungulia kama maagizo yake aliyo yaache. Baada ya maelezo hayo Bwana Godfrey alianza kumpiga binti huyo ambae ni mkubwa hapo nyumbani na kumtoboa macho.

Baada ya kutenda kitendo hicho bwana Gedfrey alijinyonga akiacha ujumbe kuwa anaogopa kukamatwa kutokana na kitendo hicho na vitendo vingine ambavyo amekuwa akiifanyia familia yake.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU