Mwenyekiti wa Yanga amefanya mabadiliko katika Safu za uongozi wa klabu hiyo huku akiweka vijana ili waweze kuitumikia klabu kwa muda mrefu. Mmoja wa vijana aliepata bahati hiyo ni Jerry Muro ambae amekuwa msemaji wa timu. Katibu Mkuu atakuwa Dr Jonas B Tiboroha.
Pamoja na hayo mwenyekiti Manji amelibadilisha benchi la ufundi kwa kumuondoa kocha Maximo na kumleta Kocha mpya mdachi Bw Hans van Pluijm akiwa anasaidiwa na mzawa Bw CharlesMkwasa.
Friday, December 19, 2014
SSERUNKUMA MAJANGA SIMBA: HUENDA ASICHEZE MECHI YOYOTE YA LIGI
Wakati Simba SC ikidai kumalizana na mshambuliaji Mganda Simon Sserunkuma na kupata Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC), klabu yake ya Express imesema imechezewa rafu na itavunja uhamisho huo sanjari na kuipeleka
Simba mahakamani kwa kughushi nyaraka.
Simba mahakamani kwa kughushi nyaraka.
Baada ya kufanya vizuri katika mechi yao ya kwanza ya majaribio Tanzania wakiisaidia Simba kuifunga Yanga mabao 2-0 Jumamosi, Sserunkuma na beki wa kati Juuko Murshid (Mganda pia),walisaini mikataba ya kuitumikia
klabu hiyo ya Msimbazi. Sserunkuma alisaini mkataba wa miaka miwili wakati Murshid alisaini miaka mitatu.
klabu hiyo ya Msimbazi. Sserunkuma alisaini mkataba wa miaka miwili wakati Murshid alisaini miaka mitatu.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Express SC Francis Ntalazzi amekaririwa na mtandao wa Kawowo Sports leo akilia kufanyiwa rafu na Simba katika kukamilisha usajili wa Sserunkuma uliofanyika Jumapili, siku moja baada ya mechi ya ‘ndondo’
ya ‘Nani Mtani Jembe 2′.
ya ‘Nani Mtani Jembe 2′.
Akielezea faulo iliyofanywa na Simba kufanikiwa usajili wa Sserunkuma, Ntalazzi anahoji juu namna saini yake ilivyoghushiwa kwenye mkataba wa mchezaji huyo.
“Binafsi, sikusaini nyaraka yoyote kuthibitisha uhamisho wa mchezaji husika (Sserunkuma) hivyo saini ilighushiwa,” kiongozi huyo wa juu
amesema huku akiweka wazi kusudio la kuipeleka Simba mahakamani kwa udanganyifu na amejipanga kuhakikisha anavunja uhamisho wa mchezaji huyo.
amesema huku akiweka wazi kusudio la kuipeleka Simba mahakamani kwa udanganyifu na amejipanga kuhakikisha anavunja uhamisho wa mchezaji huyo.
Ingawa uongozi wa Simba haukuwa tayari kuweka wazi fungu ambao nyota huyo amepewa kabla ya kukubali kumwaga wimo, ilielezwa jana kuwa ilimpatia dola la Marekani 40,000 (Sh. milioni 67).
Baada ya kusaini dili hiyo, (Sserunkuma) alirejea kwao Uganda na katika hali ya kushtusha Jumanne alikuwa miongoni mwa nyota wa Express, timu hiyo ilipochapwa mabao 2-1 dhidi ya Kikosi cha Bul F.C katika mechi ya Ligi Kuu ya
Uganda msimu huu.
Uganda msimu huu.
Kabla na baada ya mechi hiyo, Sserunkuma alionekana akigawa pesa kwa wachezaji wenzake na viongozi wa Express kama ishara ya kuagana.
Sserunkuma, ambaye aliwahi kukipiga na klabu za Kyegenra Happy Boys F.C, Victors, SC Villa, Vipers na Express alisema; “Nimefurahi kuhamia Simba na ninawashauri wachezaji wenzangu kujifua kwa bidii, kuwa na nidhamu, kila mmoja na muda wake maalum katika maisha.”
Sserunkuma, ambaye aliwahi kukipiga na klabu za Kyegenra Happy Boys F.C, Victors, SC Villa, Vipers na Express alisema; “Nimefurahi kuhamia Simba na ninawashauri wachezaji wenzangu kujifua kwa bidii, kuwa na nidhamu, kila mmoja na muda wake maalum katika maisha.”
SIMBA WANASEMAJE
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope, baada ya kutafutwa na mtandao huu kuzungumzia suala hilo, amesema Sserunkuma hana mkataba na klabu, bali wakala wake ndiye amekuwa akiingia mikataba na klabu zinazomsajili.
“Mkataba wa Sserunkuma na Express ulionesha kwamba hamzuii kujiunga na timu yoyote muda wowote. Sisi tumeingia mkataba na wakala wake kama ilivyokuwa kwa Express,” amesema
Hanspope. Ameongeza kuwa walipata ITC ya mchezaji huyo kutoka Shirikisho la Soka la Uganda (FUFA) siku mbili baada ya kumsainisha mkataba (Jumanne).
Hanspope. Ameongeza kuwa walipata ITC ya mchezaji huyo kutoka Shirikisho la Soka la Uganda (FUFA) siku mbili baada ya kumsainisha mkataba (Jumanne).
Kuhusu kucheza mechi ya Ligi Kuu ya Uganda akiwa na Kikosi cha Express ilhali amejiunga na Simba, Hanspope amedai hawana taarifa hizo huku akiahidi kufuatilia suala hilo.
Tuesday, December 16, 2014
KOCHA WA YANGA PRUIJM ATUA DAR
![]() |
| Van Der Pruijm alipotua usiku wa saa nane na nusu |
Kocha wa zamani wa Yanga mdachi Hans Van Der Pruijm amesema amerudi tena kwenye timu yake ya zamani kuendeleza pale alipoishia,
‘Falsafa yangu ipo pale pale ya kucheza soka la kushambulia, kwasababu naamini ili ushinde mchezo ni lazima ufunge mabao ya kutosha’.
‘Falsafa yangu ipo pale pale ya kucheza soka la kushambulia, kwasababu naamini ili ushinde mchezo ni lazima ufunge mabao ya kutosha’.
![]() |
| akiwasili jijini Dar |
Kocha huyo amesema bado hajasaini mkataba ila ana matumaini makubwa atamalizana na wakurugenzi wa klabu pale watakapokutana, Van Pruijm anakuja kuziba pengo la kocha aliye timuliwa Mbrazil Marcio Maximo .
Ahsante: Shaffih Dauda
Ahsante: Shaffih Dauda
RASMI: YANGA WAMTIMUA MAXIMO
Baada ya kuchapwa mabao 2-0 na mahasimu wao wa soka Simba SC katika mchezo wa ‘ Hisani Nani Mtani Jembe’ siku ya Jumamosi iliyopita, klabu ya Yanga SC imeamua kufikia maamuzi magumu ya kumfuta kazi kocha Marcio Maximo na ni wazi Mholanzi, Hans Van De Pluijm atachukua nafasi hiyo.
Hii ni mara ya pili kwa Yanga kumfukuza kazi kocha wao mara baada ya kufungwa na Simba. Ikumbukwe mwaka uliopita, Mholanzi, Ernie Brandts aliondoshwa baada ya kufungwa mabao 3-1 katika Mtani Jembe.
Tofauti na ilivyokuwa kwa Brandts ambaye aliifundisha Yanga kwa mwaka mmoja na kuisaidia kutwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania Bara msimu wa 2012/13, Maximo yeye amefukuzwa baada ya kuiongoza timu hiyo katika michezo tisa ndani ya miezi mitatu.
Yanga imepoteza michezo miwili kati ya saba ya ligi kuu msimu huu, Maximo ambaye alianza vizuri klabuni hapo kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ngao ya Jamii, alipoteza mchezo wa kwanza tu wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Yanga imeshinda michezo minne msimu huu, lakini hadi l,igi inasimama katika raundi ya saba hakuna mtu alikuwa na shaka kuhusu uwezo wa Maximo. Kocha huyo wa zamani wa timu ya Taifa
ya Tanzania, Taifa Stars amechokwa haraka sana na mashabiki, wapenzi, wanachama na viongozi wa klabu yake kutokana na kiwango kidogo cha uchezaji. Mifumo yake ya ufundishaji imekosa mvuto, lakini kitendo cha kufungwa kidhaifu na Simba kimeshindwa kuvumilika.
ya Tanzania, Taifa Stars amechokwa haraka sana na mashabiki, wapenzi, wanachama na viongozi wa klabu yake kutokana na kiwango kidogo cha uchezaji. Mifumo yake ya ufundishaji imekosa mvuto, lakini kitendo cha kufungwa kidhaifu na Simba kimeshindwa kuvumilika.
COUTINHO, JAJA, EMERSON WAMPONZA?
Ndiyo sababu kubwa, ukitoa mbinu zake, Maximo alikuwa akiwakumbatia zaidi wachezaji raia wa Brazil, Andrey Coutinho, Geilson Santos ( ambaye aliomba mwenyewe kuachwa baada ya michezo saba), kwa Emerson Oliveira siwezi kuzungumzia kwa sababu mchezaji huyo wa nafasi ya kiungo alicheza katika kiwango cha kawaida wakati alipoichezea Yanga kwa mara ya kwanza.
Jaja alifunga mara mbili dhidi ya Azam, ila alikosa makali katika ligi kuu kiasi cha kufunga bao moja tu katika michezo saba ya ligi kuu. Alishindwa kumudu presha ya mashabiki wa Yanga ambao hawakuwa wakipendezwa na kiwango chake huku uchezaji wake wa taratibu ukiwaboa wengi.
Maximo aliwanyima nafasi washambuaji kama Said Bahanunzi, Jerry Tegete, Saimon Msuva, Hussein Javu na Hamis Kizza hata pale wachezaji hao wa Kibrazil waliposhindwa kufanya vizuri.
Kuwang’ang’ania wachezaji hao na kuwanyima nafasi wale wenye uwezo kumewakera . Brandts aliondolewa baada ya kufungwa 3-1 licha ya kusaini mkataba mpya wa miaka miwili zaidi, yeye aliondolewa kwa kuwa alipingana na uamuzi wa viongozi kuwasajili baadhi ya wachezaji ambao hakuwataka wakati ule.
Brandts ndiye mwalimu aliyeifanya Yanga kucheza mchezo mzuri wa kupasiana na ndiye aliyeimarisha kiwango cha wachezaji kama, Saimon Msuva, Frank Domayo ( yuko Azam FC kwa sasa), Juma Abdul, Oscar Joshua na wengineo lakini kwa Maximo imekuwa ni tofauti,
wachezaji wengi wameshuka viwango na
ameshindwa kuwaimarisha wachezaji ambao ‘ wanasua-sua’.
wachezaji wengi wameshuka viwango na
ameshindwa kuwaimarisha wachezaji ambao ‘ wanasua-sua’.
Yanga wamefanya uamuzi sahihi kwa kumuondoa Maximo na Coutinho.
Ahsante: Shaffih Dauda
Monday, December 15, 2014
BREAKING NEWS: HAMIS TAMBWE ASAJILIWA NA YANGA
MWANAMUZIKI MKONGWE WA BENDI YA TABORA JAZZ AFARIKI DUNIA

Shem Karenga wapili kutoka kushoto waliosimama.
Shem Ibrahim Karenga, mkongwe wa muziki wa dansi Alizaliwa mwaka
1950, Bangwe, Kigoma na kupata elimu ya msingi katika shule ya
kimishionari ya Kihezya kuanzia mwaka 1957 hadi mwaka 1964.
“Kiukweli, nilianza kujifunza muziki tangu nikiwa shuleni kwa sababu mimi nimesoma shule ya Wamishionari, sasa kule tulikuwa tukifundishwa fani hiyo,” ndivyo anavyoanza kusema Karenga.
Karenga anasema kuwa, baada ya kumaliza shule huku shetani muziki akiwa kampanda kichwani, mwaka 1964 alijiunga na bendi ya Lake Tanganyika Jazz ambayo maskani yake yalikuwa mjini Kigoma.
“Kiukweli, nilianza kujifunza muziki tangu nikiwa shuleni kwa sababu mimi nimesoma shule ya Wamishionari, sasa kule tulikuwa tukifundishwa fani hiyo,” ndivyo anavyoanza kusema Karenga.
Karenga anasema kuwa, baada ya kumaliza shule huku shetani muziki akiwa kampanda kichwani, mwaka 1964 alijiunga na bendi ya Lake Tanganyika Jazz ambayo maskani yake yalikuwa mjini Kigoma.
Anakumbuka
kuwa, aliingia Lake Tanganyika akiwa mwimbaji na mcharazaji wa gitaa la
besi, ambako pia alikuwa na ujuzi wa kutengeneza gitaa kwa kutumia
vifaa vya kuokoteza. Akiwa na Lake Tanganyika Jazz, aliyodumu nayo kwa
miaka minane, alianza pia kujifunza vyombo vingine vya muziki kama vile;
Drums, Kinanda, gitaa la Rithym na la Solo’.
“Mwaka
1972, aliitwa kwenye bendi ya Tabora Jazz kama mwanamuziki mwenye
kipaji cha utunzi, mwimbaji na mpigaji wa gitaa la Solo, alijiunga na
Tabora Jazz akiwa na vibao vyake Dada Asha na Lemmy alivyovitungia
Lake Tanganyika, ambavyo vilimpa umaarufu mkubwa alipo vipakua hapo
Tabora Jazz'.
Anasema, Tabora jazz walimchukua akiwa
Mtaalam wa muziki, ambako hata hivyo alipokuwa na bendi hiyo alikuwa
akijiendeleza zaidi kwa masomo ya jioni kwenye shule ya Sekondari ya
Milambo, Tabora pamoja na kusoma vitabu mbalimbali vya muziki.
Katika bendi ya Tabora Jazz ambako alikuwa pia kama Kiongozi wa bendi, Karenga alikutana
na wakali wengine wa muziki kama vile Kassim Kaluona na Athuman Tembo
ambao kwa sasa ni marehemu pamoja na Salum Muzila.
Kutokana na sababu binafsi ambazo hakutaka kuziweka wazi, mwaka 1983 alijiengua kutoka Tabora Jazz na kusimama kabisa kujihusisha na muziki, ambako kilichofuatia ilikuwa ni kifo cha bendi hiyo.
“Mwaka 1990 aliondoka Tabora na kutua jijini Dar es Salaam alipokutana na Baraka Msilwa katika mwaka huohuo na kuniomba nijiunge na MK Beats ili kuiongezea nguvu,” anasema Kalenga.
Ndani ya MK Beats iliyokuwa ndugu na bendi nyingine iliyotamba vilivyo enzi hizo, MK Group, Karenga alikutana na wakali kama Malik Star, Sisko Lulanga, Fungo Shomari na Bwami Fanfan.
Baada ya kujiunga na MK Beats iliyokuwa ikitumia mtindo wa ‘Tukunyema’, Karenga aliisuka vema na kuinyanyua vilivyo hasa kwa vibao moto wa kuotea mbali vilivyozitetemesha vikali bendi nyingine
zote za wakati huo.
Mwaka 1995, MK Beats ilisambaratika, ambako mwaka uliofuata, yaani 1996 alianzisha bendi ya Tabora Jazz Star kwa kushirikiana na mtu aliyemtaja kwa jina la Ibrahim Didi.
“Bendi ya Tabora Jazz Star ndio niliyo nayo hadi sasa nikiwa Mkurugenzi Msaidizi, ambako nafasi ya Mkurugenzi Mkuu imeshikiliwa na Didi mwenyewe,” alisema Karenga.
Akizungumzia anavyouona ushindani wa kimuziki akiwa na bendi yake hiyo ya Tabora Jazz Star, Karenga alisema kwa upande wake mambo si mazito sana kwa kuwa ana mashabiki wake wa tangu huko nyuma.
Kwa upande wa mafanikio, Karenga anasema ukiondoa nyumba nzuri aliyoiporomosha nyumbani kwao Kigoma, anashukuru kuona ana marafiki wengi na anaishi atakavyo akiwa anamudu vema kuitunza familia yake.
Ushauri alioutoa kwa wanamuziki na mashabiki wa dansi ni kuwa, wasibabaike kwani muziki huo ni wa kudumu, ambako hata hivyo alisikitika kuona kuna uhaba mkubwa wa vijana warithi wa miondoko hiyo
kwa sasa.
“Unajua, sisi tulirithi dansi kutoka kwa baba, kaka na wakubwa zetu wengine, lakini ni masikitiko makubwa kuona vijana wetu wa sasa wanarithi muziki hewa wa Bongo Fleva,” alisema.
Alisema, sababu ya kuuita muziki wa Bongo Fleva kuwa hewa ni namna wasanii wake wanavyopora midundo na ala kutoka nje huku wakijidai kuwa ni mtindo mpya wa muziki hapa nchini.
Mkongwe huyo aliyebainisha siri yake ya kukubalika katika muziki kuwa ni bidii na juhudi za dhati kwenye fani hiyo, alisema anavutiwa na wasanii wote wanaofanya vema katika sanaa.
Kama ilivyo kwa wakongwe wengine wengi wa muziki, Karenga alifaulu kuwarithisha muziki watoto wake wawili wa kiume ambao ni Ramadhan na Mussa waliowahi kuwika vilivyo katika bendi ya TOT Plus.
“Mussa ni mwimbaji na rapa mahiri, ambako kaka yake, Ramadhan ni mcharazaji wa gitaa kiongozi, Solo,” anasema Karenga, baba wa watoto sita.
Watoto wengine wa Karenga ambao hawakubahatika kurithi kazi yake ya muziki ni Tausi, Biata pamoja na Rehana.
Kutokana na sababu binafsi ambazo hakutaka kuziweka wazi, mwaka 1983 alijiengua kutoka Tabora Jazz na kusimama kabisa kujihusisha na muziki, ambako kilichofuatia ilikuwa ni kifo cha bendi hiyo.
“Mwaka 1990 aliondoka Tabora na kutua jijini Dar es Salaam alipokutana na Baraka Msilwa katika mwaka huohuo na kuniomba nijiunge na MK Beats ili kuiongezea nguvu,” anasema Kalenga.
Ndani ya MK Beats iliyokuwa ndugu na bendi nyingine iliyotamba vilivyo enzi hizo, MK Group, Karenga alikutana na wakali kama Malik Star, Sisko Lulanga, Fungo Shomari na Bwami Fanfan.
Baada ya kujiunga na MK Beats iliyokuwa ikitumia mtindo wa ‘Tukunyema’, Karenga aliisuka vema na kuinyanyua vilivyo hasa kwa vibao moto wa kuotea mbali vilivyozitetemesha vikali bendi nyingine
zote za wakati huo.
Mwaka 1995, MK Beats ilisambaratika, ambako mwaka uliofuata, yaani 1996 alianzisha bendi ya Tabora Jazz Star kwa kushirikiana na mtu aliyemtaja kwa jina la Ibrahim Didi.
“Bendi ya Tabora Jazz Star ndio niliyo nayo hadi sasa nikiwa Mkurugenzi Msaidizi, ambako nafasi ya Mkurugenzi Mkuu imeshikiliwa na Didi mwenyewe,” alisema Karenga.
Akizungumzia anavyouona ushindani wa kimuziki akiwa na bendi yake hiyo ya Tabora Jazz Star, Karenga alisema kwa upande wake mambo si mazito sana kwa kuwa ana mashabiki wake wa tangu huko nyuma.
Kwa upande wa mafanikio, Karenga anasema ukiondoa nyumba nzuri aliyoiporomosha nyumbani kwao Kigoma, anashukuru kuona ana marafiki wengi na anaishi atakavyo akiwa anamudu vema kuitunza familia yake.
Ushauri alioutoa kwa wanamuziki na mashabiki wa dansi ni kuwa, wasibabaike kwani muziki huo ni wa kudumu, ambako hata hivyo alisikitika kuona kuna uhaba mkubwa wa vijana warithi wa miondoko hiyo
kwa sasa.
“Unajua, sisi tulirithi dansi kutoka kwa baba, kaka na wakubwa zetu wengine, lakini ni masikitiko makubwa kuona vijana wetu wa sasa wanarithi muziki hewa wa Bongo Fleva,” alisema.
Alisema, sababu ya kuuita muziki wa Bongo Fleva kuwa hewa ni namna wasanii wake wanavyopora midundo na ala kutoka nje huku wakijidai kuwa ni mtindo mpya wa muziki hapa nchini.
Mkongwe huyo aliyebainisha siri yake ya kukubalika katika muziki kuwa ni bidii na juhudi za dhati kwenye fani hiyo, alisema anavutiwa na wasanii wote wanaofanya vema katika sanaa.
Kama ilivyo kwa wakongwe wengine wengi wa muziki, Karenga alifaulu kuwarithisha muziki watoto wake wawili wa kiume ambao ni Ramadhan na Mussa waliowahi kuwika vilivyo katika bendi ya TOT Plus.
“Mussa ni mwimbaji na rapa mahiri, ambako kaka yake, Ramadhan ni mcharazaji wa gitaa kiongozi, Solo,” anasema Karenga, baba wa watoto sita.
Watoto wengine wa Karenga ambao hawakubahatika kurithi kazi yake ya muziki ni Tausi, Biata pamoja na Rehana.
BREAKING NEWS: PRUIJM KUREJEA KUINOA YANGA
kocha Mdachi Hans Van Der Pruijm huenda akarejea nchini kuifundisha tena YANGA,kutoka chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya klabu hiyo kinasema kocha huyo wa zamani wa klabu hiyo huenda akawasili usiku wa leo kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya awali.
Mwishoni mwa juma hili kwenye mchezo wa NANI MTANI JEMBE Yanga ilifungwa na mtani wake wa jadi Simba mabao 2-0 huku timu hiyo inayonolewa na Mbrazil Marcio Maximo ikionyesha kiwango cha kawaida kwenye mchezo huo ikilinganishwa na kipindi cha mdachi huyo.
AHSANTE: SHAFFIH DAUDA
Friday, December 12, 2014
KIIZA ATUPWA NJE YANGA
![]() |
| Hamisi Kiiza "Diego " |
Taarifa za kuaminika ambazo tumezipa hivi punde, klabu ya Yanga ipo mbioni kukatisha mkataba na mshambuliaji Hamis Kiiza raia wa Uganda.
Mmoja wa watu ambao wanashughulika na usajili wakati akiongea na mtandao huu amesema
‘’Tutakaa chini kuzungumza na Kiiza ili kuangalia namna ya kuachana kwa amani,baada ya Mliberia kufuzu vipimo vya afya hatuna jinsi lazima tuliondoe jina la Kiiza kwenye usajili wetu,kilisema chanzo hicho ‘’
Yanga inalazimika kupunguza mchezaji mmoja wa kigeni hasa baada ya mshambuliaji Kpah Sean Sherman kufuzu vipimo vya afya na kuwa mbioni kusaini mkataba na klabu hiyo.
Hivi karibuni Yanga ilimsainisha kiungo Emerson toka nchini Brazil mkataba wa mwaka mmoja, ukiachana na Kiiza wachezaji wengine wa kigeni ndani ya klabu ya Yanga ni Mbuyu Twite,Haruna Niyonzima, Kpah Sean Sherman na wabrazil Courtinho na Emerson.
Ikumbukwe Idadi ya wachezaji wa kigeni wanaotakiwa kusajiliwa na timu ni watano.
Thursday, December 11, 2014
DAVIDO AMWAMBIA DIAMOND AWE NA SHUKRANI
![]() |
| DAVIDO AND DIAMOND |
Yote yalianza baada ya Davido kutweet ‘N they cheat again, Lol’ baada ya Idris kutangazwa mshindi wa Big Brother Hotshots. Tweet hiyo ikimfanya Davido atukanwe matusi ya kila aina kutoka kwa Watanzania.
Usiku huo huo, Diamond alishinda tuzo za TFA (The Future Awards) za Nigeria na kuandika:
Thanks God, we have cheated another one on The.Future Awards Africa in Lagos Nigeria… #SameDay.#SameNight Thank you Allah.”
Ujumbe huo moja kwa moja ukaashiria kuwa jibu kwa.Davido ambaye matusi kutoka Tanzania yaliendelea kumsakama.
Baadaye, Davido anayeaminika (na huo ndio ukweli) kuwa msanii aliyesaidia kumtambulisha Diamond kimataifa, aliandika ujumbe kwenye Twitter. unaoshiria kumlenga Diamond.
An ungrateful stone will eventually fall… I will always be grateful to pple that have helped me climb this tall ladder of success,” alitweet Davido.
Tweet hiyo ilimaanisha: Jiwe lisilo na shukrani hatimaye huanguka… Nitakuwa mwenye shukrani siku zote kwa watu walionisaidia kuipanda ngazi ya mafanikio.”
Hata hivyo naye Diamond alitumia siku ya Uhuru wa Tanganyika jana kutoa nasaha zake kuhusiana na mikwaruzano baina ya wasanii wa Afrika kwa kuandika:
Badala ya wasanii kuwa ndio mfano bora wa kuweka karibu nchi zao na kujenga Afrika yenye upendo na amani…eti wao ndio wanakua chanzo cha kutenganisha nchi zao. Namna hii kweli tutajenga Afrika? Anyway, Happy Independence day Tanzania.”
Thanks: BongoClan
Thanks: BongoClan
Tuesday, December 9, 2014
BREAKING NEWS: KUNA MAPIGANO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI DUMILA
![]() |
| Abiria wakishirikiana na polisi kuzima moto uliowashwa barabarani |
![]() |
| Polisi wa kutuliza ghasia wakielekea kwenye tukio |
Polisi wa kutuliza ghasia (FFU) wameelekea huko kutuliza ghasia hizo.
![]() |
| kwenye moshi ndio eneo la mapigano |
![]() |
| Foleni ya magari iliyosababishwa na mapigano hayo |
DANNY MRWANDA ASAINI YANGA KWA MKATABA WA MWAKA MMOJA
Subscribe to:
Posts (Atom)











