Facebook Comments Box

Monday, November 11, 2013

ALICHOSEMA ZITO KABWE KUHUSU TAARIFA YA SIRI YA CHADEMA

NILIPOKUWA katika ziara ya bara la
Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba
2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia
ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa
ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa
imesambazwa katika mitandao
mbalimbali ya kijamii.
“Taarifa ya Chadema inasema kwamba
chama hicho (chama changu) kilikuwa
kimechunguza mwenendo wangu tangu
mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa
mimi napokea fedha kutoka Chama Cha
Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga
Chadema.
Ripoti hiyo ilinihusisha pia na
mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea
Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti
hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi
kiasi cha dola 250,000 za Marekani
kupitia kwenye akaunti yake binafsi.
Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo
wa kiwango cha kutisha,
imenifadhaisha, kunisikitisha na
kunikasirisha.
Taarifa hii iliibuliwa katika kipindi
ambacho nilikuwa safarini kutetea haki
za Watanzania na Waafrika ambao
utajiri wao wa rasilimali unafaidiwa na
watu wachache waliohifadhi mali katika
nje za nje na pia kupigania makampuni
ya mataifa tajiri yalipe kodi stahiki
katika nchi zetu.
Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni
kutaka kunipoteza kutoka katika nia na
dhamira yangu ya dhati ya kutaka
Watanzania wafaidike na utajiri wao.
Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo
waliamua kutoa taarifa yao unazua
maswali mengi kuliko majibu.
Nafahamu kwamba mimi ni mwanasiasa
ambaye nimekuwa mlengwa (target) wa
mashambulizi kutoka kwa makundi
mbalimbali ya wanasiasa na vikundi
vyao. Kama mwanasiasa, niko tayari
kupokea changamoto zozote zinazokuja
na uanasiasa wangu.
Hata hivyo, ambacho sitakubali ni kwa
watu kutumia jina langu na uanasiasa
wangu kunichafua mimi binafsi na watu
wengine wasiohusika kwa sababu ya
kutaka kutimiza malengo yao ya
kidhalimu.
Raia huyo wa Kijerumani tayari
amekana kuhifadhi fedha zangu. Kwa
maelezo yake kwa baadhi ya viongozi
wa Chadema amekana kuwa na akaunti
inayotajwa na amekana pia kuwepo
nchini Ujerumani katika siku na wakati
uliotajwa kwenye ripoti hiyo.
Ripoti hiyo imemtaja pia mtu kama Dk.
Charles Kimei, Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya CRDB ikidai kwamba nilikutana
naye na alishiriki kwenye igizo hilo la
kunipa fedha.
Niseme mapema kwamba tangu kuzaliwa
kwangu sijawahi hata mara moja
kukutana na Dk. Kimei popote pale ndani
au nje ya nchi. Kumuingiza mtu ambaye
amejenga jina lake kwenye taaluma ya
kibenki kwa sababu tu ya lengo ovu la
kumchafua Zitto Zuberi Kabwe si
uungwana bali ni unyama.
Kutokana na uchafuzi huu wa wazi dhidi
ya taswira yangu binafsi na watu
wengine walioingizwa kwenye mkumbo
huu, nimeandika rasmi kwa Katibu Mkuu
wa Chadema, Dk.Wilbrod Slaa
kumwomba athibitishe kwamba
kinachoitwa Taarifa ya Siri ya Chadema
ni kweli ni taarifa ya chama au
kiikanushe ili niweze kuchukua hatua za
kisheria dhidi ya waandishi wa hekaya
hiyo.
Cha ajabu, nimepokea ujumbe wa
kutishiwa maisha kutoka kwa mtu
anayejiita Theo Mutahaba na kuahidiwa
KUPOTEZWA endapo nitaendelea na
jitihada zangu za kupambana na ufisadi
na kutafuta haki kwa Watanzania wote
pasipo kujali tofauti zao za kiitikadi,
kikanda, kikabila na kidini.
Natarajia kuchukua hatua kali za
kisheria dhidi ya wote ambao
wamehusika na utungaji na uenezi wa
taarifa hii. Nitahakikisha kwamba
wahusika wanatafutwa na kufunguliwa
mashitaka stahiki ya upotoshaji na
kuchafuana.
Ni matarajio yangu kwamba wale wenye
mapenzi mema na Tanzania, mimi
binafsi na utawala wa sheria,
wataelewa nia yangu ya kutafuta haki
katika suala hili.
Nimeamua kujitolea maisha yangu kwa
ajili ya Watanzania na kama alivyopata
kusema Rais Mstaafu wa Afrika Kusini,
Nelson Mandela; “Struggle Is My Life.”
Forward Ever, Backward Never- Kwame
Nkrumah
Zitto Kabwe (Mb)



Friday, November 8, 2013

KOCHA WA AZAM FC AACHIA NGAZI

Kwa mujibu wa tovuti ya Azam Fc kocha wao Stewart Hall amefikia makubaliano na kilabu hiyo ya kusitisha mkataba wao jana

BREAKING NEWS: JUMA KASEJA ASAINI YANGA

Juma Kaseja asaini Yanga.Katika habari ambazo hazijathibitishwa rasmi inasemekana golikipa na nahodha wa zamani wa team ya Simba Sc Juma Kaseja(tanzania 1) amesain mkataba wa mwaka mmoja na team ya Yanga yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani.Katika kuthibitisha hilo kiongozi mmoja wa juu kabisa wa Yanga ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa Kaseja amepewa mkataba wa mwaka mmoja na Yanga na leo mchana ilikuwa wamalizane.Kiongozi alifafanua zaidi akisema baadhi ya viongozi walikuwepo uwanjani kushuhudia mchezo baina  ya Yanga dhidi ya JKT Oljoro na viongozi wengine walikuwa wamebaki kumalizana na Juma Kaseja.Hii itakuwa mara ya pili kwa Kaseja kusajiliwa na Yanga baada ya mara ya kwanza kusajiliwa ambapo aliitumikia kwa mwaka mmoja na baadaye kurejea tena Simba mpaka mwisho wa msimu uliopita ambao Simba waliaamua kumtema kutokana na kile kilichodhaniwa ni kushuka kiwango kwa golikipa huyo n



BREAKING NEWS: KOCHA MKUU WA AZAM AJIUZURU BAADA YA SARE YA 3 -3 CHAMAZI

Kocha muingereza stewart hall ametangaza
kujiuzuru kufundisha klabu ya Azam fc baada
ya kukubalina na wamiliki wa timu hiyo,
stewart aliwaaga benchi la ufundi na
wachezaji mara baada ya mechi na Mbeya
city
Stewart'' ni kweli nimewaaga wachezaji na
benchi la ufundi wenzangu, inabidi niondoke
kwa sababu nimepata kazi sehemu nyingine
na wamiliki wa timu wameridhika, nawatakia
kila la kheri''.



Tuesday, November 5, 2013

BMT YAKUTANA NA SYMBION KUJADILI KUHUSU UJENZI WA KITUO CHA MICHEZO

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Sihaba Nkinga, akisisitiza jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, alipokutana na ujumbe wa kampuni ya Symbion ya Marekani kujadili maandalizi ya ujenzi wa  kituo kikubwa cha maendeleo ya mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), ambayo itashirikiana na Club ya Sunderland ya Uingereza katika kuiendesha Academy hiyo. Katika mpango  huo, Kampuni ya Symbion pia itajenga viwanja vya michezo (sports courts) eneo la Kidongo Chekundu. 
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Symbion, Ndugu. Peter Gathercole akifafanua jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, alipokutana na Uongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuelezea mikakati ya Maandalizi ya ujenzi wa Kituo cha Maendeleo ya mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), pamoja na viwanja vya michezo (sports courts).
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Ndugu. Leonard Thadeo (kushoto) akielezea jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, wakati uongozi wa Wizara ulipokutana na Ujumbe wa Viongozi wa kampuni ya  Symbion ya Marekani Kujadili Maandalizi ya Ujenzi wa Kituo Kikubwa cha Mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), pamoja na viwanja vya michezo (sports courts). Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Tanzania (BMT), Henry Lihaya  na Afisa Michezo Mkuu, Charles Yasse Mattoke. 


Monday, November 4, 2013

KIBONZO: KIPANYA NA VIWANDA VYA TANZANIA




BOBBY WILLIAMSON KOCHA MPYA SIMBA


Bobby Williamson
SIMBA itaanza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, Januari 26 mwakani dhidi ya Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ikiwa na kocha mpya, Mwanaspoti linaweza kuthibitisha.
Maofisa wa ngazi ya juu wa Simba wameanza mazungumzo na kocha Bobby Williamson wa Gor Mahia ya Kenya ili achukue mikoba ya Abdalla Kibadeni.
Williamson (52), ni straika wa zamani wa West Bromwich Albion na katika mechi 53 aliyoichezea timu hiyo alifunga mabao 11.
Williamson, ambaye ni raia wa Scotland alijiunga na Gor Mahia  msimu huu na tayari ameipa ubingwa wa Ligi Kuu Kenya ikiwa ni miaka 18 tangu timu hiyo itwae ubingwa wa Kenya mwaka 1995.
Williamson, ambaye alikuwa kocha wa timu ya taifa ya Uganda na kuipa ubingwa wa Kombe la Chalenji mara nne, ni kocha anayesifika kutokana na kufundisha soka la kisasa kwa timu kushambulia na kukaba kwa pamoja.
Habari kutoka makao makuu ya Simba, barabara ya Msimbazi jijini Dar es Salaam zinasema kuwa maofisa kadhaa wa klabu hiyo wameanza mazungumzo na kocha huyo.
Habari hizo zinasema kuwa Simba ina asilimia kubwa ya kumnasa kocha huyo kwa sababu alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja tu Gor Mahia na kwamba analipwa kidogo.
Simba imeamua kuingiza nguvu zake kwa kocha huyo baada ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu hiyo ambayo inashika nafasi ya nne katika ligi, lakini kubwa zaidi ni kutokana na benchi la ufundi kushindwa kudhibiti nidhamu kwa wachezaji na kucheza mpira wa hovyo uwanjani.
Hakuna kiongozi wa Simba aliyekuwa tayari kulizungumzia hilo, licha ya karibu wote kukiri kuwa hawaridhishwi na jinsi timu hiyo inavyocheza.
Williamson aliteuliwa na Shirikisho la Soka Uganda (Fufa) kuwa  kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo ‘The Cranes’ Agosti 19, 2008  akichukua nafasi ya  Csaba Laszlo, aliyekuwa amejiuzulu Julai 2008 baada ya kuteuliwa kuwa kocha wa klabu ya Hearts inayoshiriki Ligi Kuu Scotland.
Akiwa na kikosi cha Uganda, Williamson ameshinda mataji manne ya Kombe la Chalenji mwaka 2008, 2009, 2011 na 2012.
Uganda nusura itinge katika fainali za Mataifa ya Afrika 2013, lakini ilipoteza mchezo wake wa mwisho wa kufuzu baada ya kupigiana penalti na Zambia.
Hata hivyo, Fufa ilimtimua kazi Williamson Aprili 8, mwaka huu na nafasi yake ikachukuliwa na Kocha wa Serbia Sredojevic Milutin ‘Micho’, ambaye alikuwa ametimuliwa timu ya taifa ya Rwanda.
Julai 5, mwaka huu, Williamson alijiunga na Gor Mahia ya Kenya akichukua nafasi ya Zdravko Logarusic wa Croatia, ambaye alikuwa amefukuzwa siku tisa za nyuma yaani Juni 25 mwaka huu.


 CHANZO: MWANASPOTI



Sunday, November 3, 2013

ANGETILE OSIAH APEWA LIKIZO YA LAZIMA NA RAIS MPYA WA TFF MPAKA MWISHO WA MKATABA WAKE

KIKAO cha kwanza cha Kamati mpya ya Utendaji ya Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF) jana chini ya Rais, Jamal Emil Malinzi kimemuengua
Katibu Mkuu wa kuajiriwa, Angetile Osiah Malabeja.
Rais Malinzi, alifungua kikao kwa ajenda ya kumuengua Angetile na
Wajumbe wakaafiki, lakini wanamng’oa kistaarabu.
Angetile amepewa likizo ya hadi atakapomaliza Mkataba wake mwezi
ujao na kwa sasa, aliyekuwa Ofisa Habari wa shirikisho hilo, Boniface
Wambura Mgoyo atakatimu nafasi yake.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
imemteua Bw. Boniface Wambura kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF.
Uteuzi huo ni kuanzia Novemba 2 mwaka huu.
Aidha aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ameagizwa aende
likizo ya malipo hadi atakapomaliza mkataba wake.
Kamati ya Utendaji inaviomba vilabu, vyama vya wilaya, vyama vya
mikoa, vyama shiriki na wadau wote kumpa ushirikiano Bw. Boniface
Wambura katika utekelezaji wa majukumu yake.
Jamal Malinzi
Rais, Dar es Salaam
Novemba 3, 2013



MSIMAMO WA LIGI KUU YA TANZANIA BARA BAADA YA MECHI ZA JANA




ARSENAL YAIZABA LIVERPOOL KWA MABAO 2 KWA BILA NA KUJIKITA KILELENI

Timu ya Arsenal Imeibamiza Liverpool kwa jumla ya mabao 2 kwa bila katika Uwanja wa Emirates na kujikusanyia point zote tatu na kujikita kileleni na kuendelea kuongoza ligi hiyo ya Uingereza. Mabao yaliyoipa ushindi timu hiyo yaliwekwa kimiani na Santi Cazorla pamoja na Aaron Ramsey.

Arsenal walimiliki mpira mwanzo mpaka mwisho wa mchezo huo ambapo Washambuliaji wa Liverpool Luis Suarez na Dan Sturredge hawakufua dafu kwa mabeki wa watoto wa Jiji la London.

Vikosi vilikuwa kama ifuatavyo:

Arsenal:

Liverpool:  



Par Metasacker akimuangalia Suarez pamoja na Sagna katika moja ya heka heka za mpambano huo.
Hi-res-186633882-kolo-toure-of-liverpool-marshalls-olivier-giroud-of_crop_north Olivier Giroud akichanja mbuga huku Kolo Habib Toure akimfuata kwa karibu.

Ozil akimpongeza Aron Ramse kwa kuifungia Arsenal bao la Pili katika mchezo huo. 

POS
LP CLUB P W D L GF GA GD PTS
1 (1) Arsenal 10 8 1 1 22 9 13 25
2 (2) Chelsea 10 6 2 2 16 8 8 20
3 (3) Liverpool 10 6 2 2 17 10 7 20
4 (7) Manchester City 10 6 1 3 28 11 17 19
5 (5) Southampton 10 5 4 1 11 4 7 19
6 (4) Tottenham Hotspur 9 6 1 2 9 5 4 19
7 (6) Everton 9 5 3 1 14 10 4 18
8 (8) Manchester United 10 5 2 3 17 13 4 17
9 (11) Newcastle United 10 4 2 4 14 16 -2 14
10 (10) Hull City 10 4 2 4 8 10 -2 14
11 (12) West Bromwich Albion 10 3 4 3 10 10 0 13
12 (9) Swansea City 9 3 2 4 12 11 1 11
13 (13) Aston Villa 10 3 2 5 9 12 -3 11
14 (15) West Ham United 10 2 4 4 8 8 0 10
15 (14) Fulham 10 3 1 6 10 15 -5 10
16 (17) Stoke City 10 2 3 5 7 11 -4 9
17 (16) Cardiff City 9 2 3 4 8 13 -5 9
18 (18) Norwich City 10 2 2 6 6 20 -14 8
19 (19) Sunderland 10 1 1 8 7 22 -15 4
20 (20) Crystal Palace 10 1 0 9 6 21 -15 3
POS
LP CLUB P W D L GF GA GD PTS


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU