Friday, November 1, 2013
YANGA KWELI BABA LA BABA: SASA WANAONGOZA LIGI
YANGA SC imepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya JKT Ruvu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Yanga SC itimize pointi 25 baada ya kucheza mechi 12, ikizishusha Azam FC na Mbeya City ambazo zina pointi 23 kila moja. Lakini timu hizo zinaweza kurejea kileleni baada ya mechi za kesho zikishinda.
Usindi wa Yanga leo umetokana na mabao ya mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa dakika za tatu na 12.
Shujaa; Ngassa amefunga mabao mawili peke yake leo
Ushindi huo, unaifanya Yanga SC itimize pointi 25 baada ya kucheza mechi 12, ikizishusha Azam FC na Mbeya City ambazo zina pointi 23 kila moja. Lakini timu hizo zinaweza kurejea kileleni baada ya mechi za kesho zikishinda.
Usindi wa Yanga leo umetokana na mabao ya mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa dakika za tatu na 12.
Shujaa; Ngassa amefunga mabao mawili peke yake leo
![]() |
| Mrisho Khalfan Ngassa akishangilia goli leo |
Ngassa alifunga bao la kwanza kwa shuti kali la umbali wa mita 20, baada ya kufanikiwa kuwatoka mabeki wawili wa JKT Ruvu, wakati bao la pili alifunga kwa kichwa akiunganisha mpira wa kurushwa na beki Mbuyu Twite.
Pamoja na kumaliza dakika 45 za kwanza wakiwa nyuma kwa 2-0, lakini JKT Ruvu ndiyo waliocheza soka ya kuvutia ya pasi za hapa na pale, huku Yanga wakitumia mashambulizi ya haraka kwa mabeki kupeleka mipira pembeni, ambako mawinga wanatia krosi washambuliaji wagombanie goli.
Kipindi cha pili, Yanga SC waliendelea na staili yao kushambulia kutokea pembeni, huku JKT Ruvu wakionekana kuanza kupoteza mwelekeo na kutoa mwanya zaidi wa kushambuliwa.
Beki Oscar Joshua aliipatia Yanga bao la tatu dakika ya pili ya kipindi cha pili, akiunganisha kona maridadi iliyochongwa na kiungo Simon Msuva.
Kona hiyo ilitokana na kazi nzuri ya kipa wa JKT Ruvu, Sadick Mecks aliyepangua shuti kali la kiungo wa Yanga, Frank Domayo.
Jerry Tegete alikamilisha karamu ya mabao ya Yanga SC dakika ya 88 kwa pasi ya Simon Msuva na kuwafanya mashabiki wa timu hiyo waimbe nyimbo za furaha kuwabeza wapinzani, Simba SC ambao jana walilazimishwa sare ya 1-1 na Kagera Sugar kwenye Uwanja huo.
Yanga SC; Deo Munishi ‘Dida’, Mbuyu Twite/Ibrahim Job dk45, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan/Relianst Lusajo dk78, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbangu/Jerry Tegete dk64, Mrisho Ngassa na Hamisi Kiiza.
JKT Ruvu; Sadick Mecks, Mussa Zuberi, Kessy Mapande, Omar Mtaki, Damas Makwaya/Richard Msenyi dk64, Nashon Naftali, Amos Mgisa, Haruna Adolph, Paul Ndauka, Samuel Kamutu/Abdallah Bunu dk 64 na Sosthenes Manyasi/Emmanuel Pius dk59.
Raundi ya 12 ya ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi nne zitakazochezwa katika miji minne tofauti.
Mgambo Shooting na Coastal Union zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Mbeya City na Ashanti United zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).
Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Tanzania Prisons itakuwa mwenyeji wa Oljoro kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashanti United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.
Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City, Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Rhino itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons.
CHANZO: BIN ZUBEIRY
MRAGE KABANGE AWASHANGAA SIMBA
KOCHA Msaidizi wa Kagera Sugar, Mrage Kabange amewashangaa mashabiki wa Simba kufanya fujo jana baada ya refa kuongeza dakika nne kipindi cha pili katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baina ya timu hizo, ambazo timu yake ilizitumia kupata bao la kusawazisha na kutoa sare ya 1-1 ugenini.
Akizungumza n BIN ZUBEIRY leo, Kabange aliyewahi kuchezea Simba SC miaka ya 1980, alisema kwamba katika kipindi cha kwanza refa Mohamed Theofile wa Morogoro aliyesaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara, aliongeza dakika tano ambazo Simba SC walizitumia kupata bao la kuongoza.
Mrage Kabange amewaona Simba SC wa ajabu sana
Mrage Kabange amewaona Simba SC wa ajabu sana
![]() |
| Mrage Kabange kocha msaidizi wa kagera sugar |
“Simba walipata bao lao baada ya dakika 45 za kipindi cha kwana, lakini hawakuona, ila sisi kipindi cha pili tulipopata bao la kusawazisha ndani ya dakika nne za nyongeza, wameleta fujo, huo siyo uungwana,”alisema.
Kabange alisema anawaheshimu Simba SC ni timu kubwa, lakini anaomba wawe tayari kukabiliana na changamoto za Ligi Kuu na wajue pia mpira ni dakika 90.
“Wao walitakiwa kulinda bao lao hadi filimbi ya mwisho, ni kweli tulipata nafasi nyingi tukashindwa kuzitumia kwa muda mrefu wa mchezo, lakini hatimaye dakika za mwishoni tukafanikiwa kupata sare ya ugenini ambayo sio mbaya,”alisema.
Baada ya Kagera kusawazisha dakika ya pili ya muda wa nyongeza baada ya kutimia kwa dakika 90, Uwanja wa Taifa, uligeuka eneo la vita baina ya Polisi mashabiki wa Simba SC.
Baada ya Salum Kanoni kukwamisha nyavuni mkwaju wake wa penalti, mashabiki wa Simba waliokuwa viti vya Rangi ya Bluu na Chungwa, walianza kung’oa viti na kuvitupia uwanjani.
Mara moja, Polisi walianza kupambana na mashabiki hao kwa kuwatupia mabomu ya machozi, ndipo wakaanza kukimbia. Makocha na wachezaji wa Simba kwa pamoja waliwafuata waamuzi kuwalalamikia- hali ambayo ilifanya watolewe kwa kusindikizwa na Polisi.
Bao la Simba lilifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Amisi Tambwe dakika ya 45 baada ya kupokea pasi nzuri ya Betram Mombeki na kumpiga chenga beki Salum Kanoni, kabla ya kumchambua kipa Hannington Kalyesebula.
Kagera ilipata pigo mapema dakika ya 22 kipa wake Agathon Anthony kuumia katika harakati za kuzuia shambulizi la Tambwe na nafasi yake ikachukuliwa na Mganda, Kalyesebula.
Kwa ujumla timu zote zilishambuliana kwa zamu kipindi cha kwanza, ingawa Simba SC ndiyo waliotengeneza nafasi nyingi zaidi za kufunga.
Kipindi cha pili, Simba SC iliendelea kusukuma mashambulizi mengi langoni mwa Kagera, lakini washambuliaji wake walikosa umakini wa kutumia nafasi.
Kagera nayo iliendelea kushambulia na kwa ujumla mchezo ulizidi kunoga kadiri muda ulivyokuwa ukisonga mbele kutokana na ushindani mkali.
Wakati refa wa akiba, Hussein Kalindo wa Kinondoni, amekwishaonyesha dakika nne za nyongeza, Kagera ikafanya shambulizi langoni mwa Simba na Daudi Jummane akaangushwa kwenye eneo la hatari na beki wa Simba SC, Joseph Owino na refa akaamuru penalti.
Beki wa zamani nwa Simba SC, Salum Kanoni akaenda kumchambua vizuri kipa Abuu Hashimu kuisawazishia Kagera dakika ya 90+2.
CHANZO: BIN ZUBEIRY
MAZISHI YA LUTENI RAJAB MLIMA ALIYEUAWA CONGO YAFANYIKA KATIKA MAKABURI YA KISUTU
Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wakiwa wameinamia kwa
huzuni jeneza lenye mwili wa askari mwenzao, marehemu Luteni Rajab
Mlima wakati wa maziko yaliyofanyika jana katika makaburi ya Kisutu, Dar
es Salaam jioni hii. Mlima ambaye alikuwa katika Jeshi la Umoja wa
Mataifa la Kulinda Amani DRC Congo aliuawa akiwa kazini katika Mlima
Gavana eneo la Goma.
Waombolezaji wakijiandaa kufanya maziko
Waombolezaji wakifanya maziko
Askari wa JWTZ wakitoa heshima wakati wa maziko
Meja Leonidas Luangisa akisoma wasifu wa marehemu Luteni Mlima.
Mseamaji Mkuu wa Familia ya Mlima, Balozi Alhaji Saleh Tambwe akisoma
salamu za familia na kuwashukuru watu wote walioshiriki kwenye mazishi
hayo.
Thursday, October 31, 2013
SIMBA WAFANYA VURUGU BAADA YA KUTOKA SULUHU NA KAGERA SUGAR
UWANJA wa Taifa, Dar es Salaam
leo uligeuka eneo la vita baina ya Polisi mashabiki wa Simba SC, kufuatia
Kagera Sugar kupata bao la kusawazisha dakika ya pili ya muda wa nyongeza baada
ya kutimia kwa dakika 90 za mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, timu hizo
zikitoka 1-1.
Baada ya Salum Kanoni kukwamisha nyavuni mkwaju wake wa penalti, mashabiki wa Simba waliokuwa viti vya Rangi ya Bluu na Chungwa, walianza kung’oa viti na kuvitupia uwanjani.
Baada ya Salum Kanoni kukwamisha nyavuni mkwaju wake wa penalti, mashabiki wa Simba waliokuwa viti vya Rangi ya Bluu na Chungwa, walianza kung’oa viti na kuvitupia uwanjani.
![]() |
| Salum Kanoni akishangilia na Themi Felix kulia baada ya kuisawazishia Kagera |
![]() |
| Ramadhani Singano kulia na William Lucian kushoto wakimpongeza Tambwe baada ya kufunga bao la Simba |
Bao
hilo lilifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Amisi Tambwe
dakika ya 45 baada ya kupokea pasi nzuri ya Betram Mombeki na kumpiga
chenga beki Salum Kanoni, kabla ya kumchambua kipa Hannington
Kalyesebula.
Kagera ilipata pigo mapema dakika ya 22 kipa wake Agathon Anthony kuumia katika harakati za kuzuia shambulizi la Tambwe na nafasi yake ikachukuliwa na Mganda, Kalyesebula.
Kwa ujumla timu zote zilishambuliana kwa zamu kipindi cha kwanza, ingawa Simba SC ndiyo waliotengeneza nafasi nyingi zaidi za kufunga.
Kipindi cha pili, Simba SC iliendelea kusukuma mashambulizi mengi langoni mwa Kagera, lakini washambuliaji wake walikosa umakini wa kutumia nafasi.
Kagera nayo iliendelea kushambulia na kwa ujumla mchezo ulizidi kunoga kadiri muda ulivyokuwa ukisonga mbele kutokana na ushindani mkali.
Wakati refa wa akiba, Hussein Kalindo wa Kinondoni, amekwishaonyesha dakika nne za nyongeza, Kagera ikafanya shambulizi langoni mwa Simba na Daudi Jummane akaangushwa kwenye eneo la hatari na beki wa Simba SC, Joseph Owino na refa akaamuru penalti.
Beki wa zamani wa Simba SC, Salum Kanoni akaenda kumchambua vizuri kipa Abuu Hashimu kuisawazishia Kagera dakika ya 90+2.
Simba SC; Abuu Hashim, Nassor Masoud ‘Chollo’, Issa Rashid, Joseph Owino, Hassan Khatib, Jonas Mkude, Ramadhani Singano, Said Ndemla, Betram Mwombeki, Amisi Tambwe na William Lucian.
Kagera Sugar; Agathon Anthony/Hannington Kalyesebula dk22, Salum Kanoni, Martin Muganyizi, Ernest Mwalupani, Malegesi Mwangwa, Zuberi Dabi/Juma Mpola dk46, Benjamin Asukile/Adam Kingwande dk46, George Kavilla, Themi Felix, Daudi Jumanne na Paul Ngwai.
Kagera ilipata pigo mapema dakika ya 22 kipa wake Agathon Anthony kuumia katika harakati za kuzuia shambulizi la Tambwe na nafasi yake ikachukuliwa na Mganda, Kalyesebula.
Kwa ujumla timu zote zilishambuliana kwa zamu kipindi cha kwanza, ingawa Simba SC ndiyo waliotengeneza nafasi nyingi zaidi za kufunga.
Kipindi cha pili, Simba SC iliendelea kusukuma mashambulizi mengi langoni mwa Kagera, lakini washambuliaji wake walikosa umakini wa kutumia nafasi.
Kagera nayo iliendelea kushambulia na kwa ujumla mchezo ulizidi kunoga kadiri muda ulivyokuwa ukisonga mbele kutokana na ushindani mkali.
Wakati refa wa akiba, Hussein Kalindo wa Kinondoni, amekwishaonyesha dakika nne za nyongeza, Kagera ikafanya shambulizi langoni mwa Simba na Daudi Jummane akaangushwa kwenye eneo la hatari na beki wa Simba SC, Joseph Owino na refa akaamuru penalti.
Beki wa zamani wa Simba SC, Salum Kanoni akaenda kumchambua vizuri kipa Abuu Hashimu kuisawazishia Kagera dakika ya 90+2.
Simba SC; Abuu Hashim, Nassor Masoud ‘Chollo’, Issa Rashid, Joseph Owino, Hassan Khatib, Jonas Mkude, Ramadhani Singano, Said Ndemla, Betram Mwombeki, Amisi Tambwe na William Lucian.
Kagera Sugar; Agathon Anthony/Hannington Kalyesebula dk22, Salum Kanoni, Martin Muganyizi, Ernest Mwalupani, Malegesi Mwangwa, Zuberi Dabi/Juma Mpola dk46, Benjamin Asukile/Adam Kingwande dk46, George Kavilla, Themi Felix, Daudi Jumanne na Paul Ngwai.
BARAZA LA MITIHANI LATOA VIWANGO VIPYA VYA UFAULU; SASA KUNA DARAJA LA TANO (DIVISION FIVE)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome akifafanua kwa waandishi wa habari (hawapo
pichani) juu ya upangaji wa viwango vya alama, matumizi ya alama endelevu ya mwanafunzi
na ufaulu leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Kamishna wa Elimu Profesa
Eustella Bhalasesa.
|
| Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Sifuni Mchome (hayupo pichani). |
Waandishi wa habari na maafisa wa Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Sifuni Mchome(hayupo pichani). Picha zote na Eliphace Marwa (MAELEZO).
|
======== ======= ========
UPANGAJI
WA VIWANGO VYA ALAMA, MATUMIZI YA ALAMA ENDELEVU YA MWANAFUNZI NA UFAULU
UTANGULIZI
Wizara imekusanya maoni ya Wadau
wa Elimu kuhusu Upangaji wa Viwango vya Alama (Grade Ranges) katika Mitihani ya
Kuhitimu Kidato cha Nne na cha Sita pamoja na Matumizi ya Alama za Tathmini
Endelevu ya Mwanafunzi (Continuous Assessment ama CA) kwa ajili ya kuamua kiwango cha ufaulu wa mwanafunzi. Maoni ya
wadau yamekusanywa kwa sababu kwa muda mrefu sasa upangaji wa viwango vya alama
vinavyotumika na utaratibu wake katika mitihani ya kuhitimu Kidato cha Nne na
Kidato cha Sita umekuwa haufanani pamoja na kwamba mitihani hiyo yote ni ya
elimu ya sekondari. Pia mfumo masuala mbalimbali ya mitihani katika elimu ya
sekondari umekuwa na miundo tofauti ikiwemo ule unaotumika shuleni na ule wa
Baraza la Mitihani la Taifa. Kwa sasa kuna miundo mikuu miwili katika mfumo
huo.
Muundo wa Kwanza ni upangaji wa
viwango katika ngazi ya Shule ambapo Alama Mgando (Fixed Grade Ranges)
zifuatazo hutumika kupanga madaraja: A = 81 – 100; B = 61 – 80; C = 41 – 60; D
= 21 – 40 na F = 0 – 20. Muundo huu umetumika kwa muda mrefu na umezoeleka kwa
walimu na wanafunzi wa elimu ya sekondari kwa ujumla.
Muundo wa Pili ni wa viwango
vinavyotumiwa na Baraza la Mitihani la Taifa ambapo ambapo kabla ya mwaka 2012
muundo wa viwango nyumbufu (flexible
grade ranges) ulitumika. Katika muundo huu uwigo wa alama ulibadilika
badilika kulingana na hali ya matokeo ilivyokuwa kwa mwaka husika. Lakini
kuanzia mwaka 2012, Serikali iliamua kutumia mfumo wa Upangaji wa Alama Mgando
(Fixed Grade Range) kwa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita. Katika mtihani wa
Kidato cha Nne mwaka 2012 Baraza lilitumia mfumo huu wa alama mgando ambapo: A
= 80 – 100, B = 65 – 79, C = 50 – 64, D = 35 – 49, F = 0 – 34. Kwa upande wa
Kidato cha Sita Baraza lilitumia mfumo wa A = 80 – 100; B = 75 - 79; C = 65 –
74; D = 55 – 64; E = 45 – 54; S = 40 – 44 na F = 0 – 39. Mifumo hii ya Baraza
haikuwa inafahamika kwa wadau na hivyo kuwa sehemu ya malalamiko katika sekta
ya elimu na mafunzo.
Vilevile, Sera ya Elimu na
Mafunzo ya mwaka 1995 imeelekeza kwamba katika kuamua kiwango cha ufaulu wa
mwanafunzi wa elimu ya sekondari, Alama za CA
zitachangia asilimia hamsini (50%) na Mtihani wa mwisho utachangia asilimia
hamsini (50%). Kwa upande wa Zanzibar, CA
zimekuwa zikiandaliwa kwa mfumo wa asilimia arobaini (40%) na mtihani wa mwisho
asilimia sitini (60%). Pamoja na kwamba Baraza halijawahi kuutumia mifumo hii
tangu ilipowekwa, kumekuwa na mitazamo, maoni na mapendekezo tofauti katika
muundo na matumizi ya alama za CA.
Kuna mawazo pia kwamba mfumo wa CA
kuchangia matokeo ya mwisho ya mwanafunzi pia utumike kwa watahiniwa wa
kujitegemea (private candidates). Kwa
sasa matokeo ya mitihani ya watahiniwa hawa yamekuwa yakitumia alama za mtihani
wa mwisho tu na hivyo kutafsiriwa kama utaratibu ambao unamwonea mwanafunzi
ambaye anahamu ya kujiendeleza kielimu lakini anakwama kwa sababu mfumo
unaotumika siyo rafiki kwa mtahiniwa.
Kwa mantiki hii, Wizara
imedhamiria kufanya harmonization ya
masuala ya alama katika mitihani ya Kidato cha Nne na Kidato cha Sita ili
kupata muundo mmoja na ulio wazi kwa wadau wote wa elimu ya sekondari. Lakini
pia serikali imedhamiria kuhakikisha tathmini za wanafunzi katika ngazi
mbalimbali zinakwenda sambamba na matarajio ya mitaala inayotumika na ambayo
inahuishwa mara kwa mara ili iendane na wakati na mahitaji ya elimu katika
ngazi mbalimbali.
VIWANGO
NA UTARATIBU KUANZIA MWAKA 2013 KWA KIDATO CHA NNE NA
MWAKA
2014 KIDATO CHA SITA
Baada ya kufanya tathmini ya maoni mbalimbali ya
wadau, misingi ifuatayo ilizingatiwa katika maamuzi kuhusu makundi ya alama na
muachano wake:
a) Alama
zitakazotumika zitakuwa A, B, C, D, E na F. Muachano
wa alama kati ya kundi moja hadi jingine utafanana, isipokuwa tu pale ambapo
itaonekana kuna sababu na hakuna athari za kuwa na muachano tofauti na ule
ambao umetumika katika makundi mengine.
b) Makundi ya
alama hayatakuwa na clusters
isipokuwa pale ambapo itaonekana kufanya hivyo kunaleta tija katika kupata
picha ya wahitimu kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Kwa mantiki hii
(i) makundi ya alama A, C, D, E na F yabaki na cluster moja moja bali kundi la alama B litakuwa na clusters mbili.
Kundi la kwanza litakuwa la wale ambao wamepata alama kati ya 50 mpaka 59 na
litaitwa B na lingine litakuwa la wale ambao wamevuka uwigo wa 50 hadi 59 na
kuelekea uwigo wa 60 hadi 74 na hili litaitwa B+ (angalia jedwali hapo chini).
(ii) Pamoja na kuwa na muachano wa alama 26
kama jedwali linavyoonesha hapo chini, alama A kwa miaka
mingi imekuwa ikianzia alama 75 hadi 100 na kwamba pamoja na uwigo huo bado
wanaofaulu kwa kiwango hicho ni wachache sana. Kwa mantiki hii, hakuna haja ya
kubadilisha uwigo ila juhudi ziendelee katika ufundishaji na ujifunzaji ili
kiwango cha ufaulu kiongezeke na kupata wanafunzi wengi zaidi wanaofaulu katika
kundi hili.
(iii)
Pia, pamoja na kuwa na muachano wa alama
20 kama jedwali linavyoonesha hapo chini kwa miaka mingi, huko shuleni
mwanafunzi aliyepata alama 21 na hadi 30 alihesabiwa kuwa na ufaulu wa
chini
kabisa au hafifu kwa kiwango cha alama D na ingawa
ilikubalika ufaulu wa aina hiyo kwa mazingira ya nchi yetu unaridhisha.
Alama F ilikuwa ni kwa wale waliopata chini ya hapo. Hivyo, alama F
itaendelea kuwepo na itaanzia alama 0 hadi 19 na E itaanzia
alama 20 hadi 29 na D – 30 -39. Lengo la muundo huu
ni kuwa alama mbalimbali, isipokuwa kwa makundi machache, zianzie kwenye
0 yaani
0, 10, 20, 30, 40 na kuendelea badala ya kuanzia kwenye moja yaani 1,
11, 21,
31, 41 na kuendelea. Hii ni kwa ajili ya kuleta mtizamo unaofanana
katika ngazi
mbalimbali za elimu ambapo kwa sasa ngazi ambazo siyo za elimu msingi na
sekondari zinatumia muundo wa kuanzia kwenye 0 badala ya 1.
c) Uwigo wa
jumla wa alama kwa Kidato cha Nne na Kidato cha Sita utaendelea kuwa wa alama 0
hadi 100 na kila kundi katika uwigo huu limepewa tafsiri kwa ajili ya kuamua
mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo ya mwanafunzi kulingana na malengo ya
mtihani husika. Kimsingi, tafsiri zifuatazo zitakatumika
(i) Alama A itakuwa na
maana ya ufaulu uliojipambanua (distincion
or outstanding performance),
(ii) Alama B+ itakuwa na
maana ya ufaulu bora sana (excellent
performance),
(iii) Alama B itakuwa na
maana ya ufaulu mzuri sana ( very good
perfomance),
(iv) Alama C itakuwa na
maana ya ufaulu mzuri (good performance);
(v) Alama D itakuwa na
maana ya ufaulu wa wastani (low
performance),
(vi) Alama E itakuwa na maana ya ufaulu hafifu (very low performance), na
(vii) Alama F itakuwa na
maana ya ufaulu usioridhisha (unsatisfactory
performance).
Wataalamu katika maeneo
mbalimbali ya elimu na ulimwengu wa kazi, kwa kushirikiana na Wizara, watatoa
maana ya tafsiri hizi kiutendaji katika maeneo yao kulingana pia na mahitaji
yao.
d) Alama C iwe ndiyo alama ya ufaulu mzuri ambao hauhitaji urekebu wa lazima,
wakati alama D na E ni alama za ufaulu unaohitaji urekebu kadri mwanafunzi atakavyokuwa
anaendelea na masomo ili kuthibitisha kama mlengwa anaweza na kulingana na
mahitaji ya eneo husika (targeted
remediation). Alama F iwe alama
ya eneo linalohitaji urekebu wa hali ya juu (intesive remediation) ili mwanafunzi huyo aweze kumudu masomo kadri
anavyoendelea kukua kielimu ama atakapoingia katika ulimwengu wa kazi.
e) Makundi ya
alama yatajumuisha CA kwa kiwango cha asilimia
isiyozidi 40 na mtihani wa mwisho kwa asilimia isiyozidi 60 kwa makundi yote ya
watahiniwa ikiwemo wale wa kujitegemea (private
candidates). Hii ni kwa kuzingatia kwamba CA siyo vizuri
izidi uwigo wa alama ya ufaulu mzuri unapoanzia ambayo ni C au 40.
f) CA kwa upande wa Kidato cha Nne zitokane na mtihani wa
Kidato cha Pili (alama 15), matokeo ya Kidato
cha Tatu (alama 5 kwa kila muhula, na hivyo jumla ya alama 10), mtihani
wa Mock (alama 10) na kazi mradi au Projects (alama 5). Kwa upande wa Kidato
cha Sita, CA iendelee kutokana na muundo unaotumika sasa.
g) CA zitumike pia kwa watahiniwa wa kujitegemea. Kwa
upande wa watahiniwa wa kujitegemea ambao wanarudia Mitihani, CA zao zitumike
zile zilizotumika kutoa matokeo yake ya mitihani ya awali. Kwa watahiniwa wa kujitegemea waliopitia
mfumo wa Qualifying Test (QT), matokeo
ya QT yatumike kama CA na mtihani
wa mwisho uchangie alama 60.
h) Kwa vile
alama endelevu kwa mwaka 2013 kwa wanafunzi wa Kidato cha Nne tayari
zimeshawasilishwa Baraza la Mitihani
Tanzania, alama hizo zichangie asilimia 40 katika mtihani wa Kidato cha
Nne mwaka 2013.
i)
Muundo wa wastani wa alama katika ufaulu (Grade Points Average ama GPA)
utaandaliwa na kuanza kutumika pale utakapokuwa tayari na wadau wataelimishwa
kuhusu muundo huo ili wapate kuufahamu na manufaa yake katika elimu ya
sekondari.
j)
Muundo huu mpya wa alama utatumika kwa mzunguko wa
miaka minne kabla haujahuishwa tena ili kuupa muda wa kutosha kuona aina ya
changamoto zinazojitokeza na jinsi ya kuzishughulikia. Aina hii ya muda
itaruhusu vidato vinne vya elimu ya sekondari ya kawaida na nane ya elimu ya
sekondari ya juu kupimwa. Hata hivyo, uhusihaji wa masuala ya mitihani unaweza
ukafanyika iwapo matokeo ya uhuishaji wa mitaala kwa ujumla utahitaji pia eneo
la mitihani liguswe na kuhuishwa pia.
Kwa mantiki hii, viwango vya alama na ufaulu ni kama
inavyooneshwa kwenye jedwali la 1 hapa chini:
Jedwali Na 1
MUUNDO WA ALAMA NA UFAULU
ALAMA
|
UWIGO WA ALAMA
|
IDADI YA ALAMA
|
TAFSIRI
|
A
|
75 - 100
|
26
|
Ufauli
Uliojipambanua
|
B+
|
60 - 74
|
15
|
Ufaulu
bora sana
|
B
|
50- 59
|
10
|
Ufaulu
mzuri sana
|
C
|
40 - 49
|
10
|
Ufaulu
mzuri
|
D
|
30 - 39
|
10
|
Ufaulu
Hafifu
|
E
|
20 - 29
|
10
|
Ufaulu
hafifu sana
|
F
|
0 - 19
|
20
|
Ufaulu
usioridhisha
|
Kwa aina hii ya muundo wa alama, na kwa kuwa muundo
wa GPA utaanza kuandaliwa na wadau kuelimishwa kabla haujaanza kutumika, katika
kipindi hiki mpaka wakati huo, muundo wa madaraja utakuwa kama inavyooneshwa
kwenye jedwali la 2 hapa chini.
Jedwali Na 2
MUUNDO WA MADARAJA
MUUNDO
WA ZAMANI
|
MUUNDO
MPYA
|
MAELEZO
|
||
POINTI
|
DARAJA
|
POINTI
|
DARAJA
|
|
7-17
|
1
|
7-17
|
I
|
Kundi la
ufaulu uliojipambanua na bora sana
|
18-21
|
II
|
18-24
|
II
|
Kundi la
ufaulu mzuri sana
|
22-25
|
III
|
25-31
|
III
|
Kundi la
ufaulu mzuri na wa wastani
|
26-33
|
IV
|
32-47
|
IV
|
Kundi ufaulu hafifu
|
34-35
|
0
|
48-49
|
V
|
Kundi la ufaulu
usioridhisha
|
Wataalamu wa mifumo ya
mitihani watalifanyia kazi zaidi jedwali hili la madaraja ili liweze kutumika
kwa ufanisi katika kipindi hiki cha mpito.
Kwa mantiki hii, Daraja Sifuri linafutwa na kuwekwa daraja
litakalojulikana kama Daraja la Tano na ambalo litakuwa ndilo la mwisho kabisa
katika ufaulu.
HITIMISHO
Mabadiliko haya yamefanyika ili kuendelea kuimarisha
mfumo wetu wa elimu na kuweka wazi taratibu mbalimbali kwa ajili ya mitihani na
masuala mengine. Yako mambo mengi mengine ambayo hayana budi kuendelea
kuimarishwa ikiwemo mfumo wa mitaala, walimu, mazingira ya kujifunzia na
kufundishia pamoja na vitabu na vifaa vingine muhimu katika elimu. Masuala haya
yanaendelea kuangaliwa kupitia mikakati mbalimbali ikiwemo mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa ama Big Results Now
(BRN). Ushirikiano wa wadau wote ili kuleta tija kwenye elimu ni muhimu sana na
hivyo wizara itaendelea kuwashirikisha wadau wote kwa kadri itakavyohitajika na
wadau pia wanaombwa wasiache kuishirikisha wizara pale watakapokuwa na jambo
lolote ambalo linahitaji ushirikiano ili kwa pamoja tuweze kupata mafanikio
katika sekta ya elimu.
Imetolewa,
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
Subscribe to:
Posts (Atom)




