Facebook Comments Box

Sunday, June 16, 2013

WACHEZAJI WAISLAM WA NEWCASTLE WAGOMA KUVAA JEZI ZENYE NEMBO MPYA

imageimage 
Siku chache baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Senegal Pappis Demba Cisse kutoa kauli yakugoma kuvaa nembo ya kampuni ya Wonga ambayo hutoa mikopo yenye riba , mchezaji wa pili ametoka na kuungana na Cisse kwenye msimamo huo wa kutovaa logo ya Wonga kwa kuwa kampuni hiyo inafanya biashara ambayo kwa mujibu wa misingi ya dini ya kiislamu ni Haramu.
Kiungo wa Ivory Coast ambaye atakuwepo uwanjani siku ya jumapili kucheza dhidi ya Taifa Stars Ismael Cheikh Tiote amesema kuwa atazungmza na wanasheria wake kuangalia  wa kutoivaa nembo hiyo . Tiotte kama ilivyo kwa Cisse ni muislamu anayefuata misingi yote ya dini hiyo na kwa mujibu wa sheria za dini yake riba kwenye mkopo unaotolewa kwa mtu mwingine ni haramu.
Newcastle United imesaini mkataba wa miaka minne na kampuni ya Wonga mkataba ambao umeifanya klabu hiyo kuingia kwenye utata na wachezaji wenye imani ya dini ya kiislamu . Newcastle United ina wachezaji wasiopungua watano ambao wamezungmzia kutokuwa tayari kuvaa nembo ya Wonga jambo linaweza kusababisha klabu hiyo kulazimika kuwauza wachezaji kama Pappis Cisse , Tiotte na wenzao kwani hawako tayari kutumiwa kwenye kampeni za matangazo ya kampuni hiyo.


BAADA YA TUKIO LA BOMU UCHAGUZI WA AHIRISHWA ARUSHA


Kufuatia tukio la mlipuko jana jumamosi Arusha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeahirisha chaguzi za madiwani katika kata zote nne (4) jijini arusha hadi jumapili ya tar 30/6/2013.

 Tume ya taifa ya Uchaguzi imesimamisha kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa udiwani ktk kata nne jijini Arusha. Akizungumza kwa njia ya simu na Radio TBC FM,kutoka Zanzibari mwenyekiti huyo wa tume ya uchaguzi alisema kua wameamua kusimamisha uchaguzi huo ili kuwapa nafasi vyombo vya usalama kuchunguza swala hilo.
Alisema kua sheria inawapa mamlaka kufanya hivyo pale wanapogundua kuwa hakutakua na uhuru wa mpiga kura kwenda kupiga kura. Alisema haiwezekani uchaguzi ufanyike ktk hali kama hiyo huku kukiwa na wasiwasi.


ANGALIA HIGHLIGHT YA MECHI YA BRAZIL 3 - 0 JAPAN


Brazil vs Japan 3:0 MATCH HIGHLIGHTS by footballdaily1

Saturday, June 15, 2013

HUYU NDIO RAIS MPYA WA IRAN

Picture
Hassan Rouhani, Rais Mpya wa Iran
Kiongozi mwenye msimamo wa kati kutoka kwenye chama cha Wahafidhina nchini Iran, Hassan Rouhani, ametangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais nchini humo.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iran imesema, Rouhani ameshinda za zaidi ya kura millioni kumi na nane, ambayo ni zaidi ya asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwa.

Wizara hiyo imesema kuwa, idadi kubwa ya raia wa nchi hiyo walijitokeza kupiga kura kiwango ambacho kinakadiriwa kuwa asilimia sabini na tatu ya watu waliosajiliwa.

Mayor wa mji wa Tehran, Mohamad Baqar Qalibaf, alimaliza katika nafasi ya pili


BOMU LALIPUKA KWENYE MKUTANO WA CHADEMA ARUSHA

Watu wawili wanahofiwa kupoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu lililolipuka kwenye mkutano wa CHADEMA katika eneo la Soweto, kata ya Kaloleni jijini Arusha, wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa madiwani katika maeneo ya jiji hilo.

Waliojeruhiwa wamekimbizwa katika hospitali za Seliani na Mount Meru ambapo baadhi ya watu wamejitolea vyombo binafsi vya usafiri na wengine wanashirikiana na Madaktari na Wauguzi wa hospitali hizo kutoa huduma ya kwanza.

Kamanda wa polisi mkoani humo, Liberatus Sabas yupo katika moja ya hospitali hizo.

Bomu hilo linaelezwa kuwa lilipuka kwenye mkusanyiko wa watu meta chache kutoka jukwa kuu, mwendo wa saa kumi na mbili na robo jioni wakati mkutano huo ulipokuwa umekwisha na shughuli ya kukusanya michango ikiendelea.

Viongozi wa juu wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Godbless Lema walikuwepo na wameendelea kuwepo kwenye eneo hilo.

Polisi wapo katika eneo hilo wakijitahidi kutuliza ghasia lakini inasemekana upo upinzani mkubwa kutoka kwa wananchi wanaojaribu kuwafukuza, hali iliyowalazimu kupiga mabomu ya machozi na kukamata watu kadhaa wakiwemo viongozi wa CHADEMA. Mwandishi mmoja wa habari anaripotiwa kunyang’anywa kamera yake baada kwa kupiga picha, hata baada ya kujitambulisha.

Watu wenye hasira wanaripotiwa kuyashambulia na kuyaharibu baadhi ya magari ya kutoa huduma ya kwanza (ambulance) kwa kuwa yalichelewa kufika kuwaokoa majeruhi.

ILANI: Baadhi ya picha zilizopachikwa hapo huenda zikagusa  hisia ya mtizamaji, tafadhali ikiwa huwezi kuvumilia kuona damu usibofye kitufye cha kuelekea mbele



SIKILIZA MAHOJIANO YA MAREHEMU LANGA KILEO NA DR. ISAAC MARO WA CLOUDS FM

www.kitongoni.blogspot.com
Langa Kileo



KIBONZO: JINSI YA KUKUMBUKA NENO LA SIRI




ANGALIA VIDEO ZA SHOW YA LADY JAY DEE NA MWANA FA ILI UJUE NANI KAMFUNIKA MWENZAKE



Komando Jide akifanya vitu vyake jukwaani



Hapa Fa akiongea



Hapa Fa akiimba unanitega



Hapa Fa akiimba yalaiti

Friday, June 14, 2013

TUIUNGE MKONO TIMU YETU YA TAIFA




VIDEO: MCHANGO WA WADAU MBALIMBALI KUHUSU BAJETI YA SERIKALI YA MWAKA WA FEDHA 2013/2014




SERIKALI YAZIRUHUSU YANGA NA SIMBA KWENDA SUDAN


 
Kikosi cha mabingwa wa Tanzania na Afrika mashariki na kati (kagame cup) Yanga Sc
Kikosi cha washindi wa tatu wa Tanzania Simba Sc
 Siku moja baada ya Baraza la Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuziteua timu za URA, Elite Sport ya Chard na Rayon Sports ya Rwanda kuziba nafasi za timu za Tanzania, Serikali jana imetangaza kuziruhusu timu hizo kushiriki michuano hiyo iliyopangwa kuanza Jumanne ijayo Juni 18 Durfur nchini Sudan.

Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo Amosi Makalla alisema jana kuwa Serikali ya Sudan imewahakikishia kwa maandishi kuzipa usalama timu za Tanzania zitakazoenda kushiriki michuano hiyo ambayo Yanga ni bingwa mtetezi.

“Tulikuwa tunakataa kwa vile hatukupata taarifa rasmi ya maandishi kutoka serikali ya Sudan kutuhakikishia usalama wa watu wetu kuanzia uwanja wa ndege zitakapotua, zitakapokuwa Khatoum, ulinzi wa kuzitoa Khatorm hadi Durfur na hoteli watakazofikia, lakini jana imetuhakikishia usalama na siku zote Chama cha Soka cha Sudan ndio kilichokuwa kikituambia kuna usalama tusingeweza kuamini, lakini kwa vile tumepata udhibitisho wa serikali timu ruksa kwenda,” na kusisitiza: “Timu zote zilikuwa zinajiandaa na mashindano ni tarehe 18 kama zinataka kwenda ziende, na hao CECAFA kama wameteua timu nyingine iyo ni juu yao.”

Makala ambaye juzi alitoa msimamo wa serikali akipigilia nyundo kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje, Benard 
Membe alisema serikali ndio inajua hali ya usalama ya Durfur ilivyo hivyo haiwezi kuziruhusu timu za Simba, Yanga na Super Falcon ya Zanzibar zikashiriki michuan hiyo.

Hata hivyo viongozi wa Simba na Yanga jana walipoulizwa kuhusiana na suala hilo walionekana kuduwazwa kwani hawakuwa na taarifa yoyote ya serikali au TFF ikiwajulisha juu ya jambo hilo, huku timu zote zilishatoa msimamo wa kutoshiriki michuano hiyo baada ya kuambiwa Durfur si salama.

Laurance Mwalusako Katibu mkuu wa Yanga, “Hili suala kuna mgongano wa mambo mengi, mpaka sasa hivi klabu hatuna taarifa zozote, na isitoshe sisi jana tumevunja kambi na tumewapa wachezaji wetu mapumziko ya wiki mbili, hata hivyo tukipata tutakaa na kujadili kama tushiriki au la.”

Ismail Aden Rage Mwenyekiti Simba, “Mi sina habari zozote nipo na Waziri huku (Dodoma) mbona hajaniambia chochote, ngoja akishaniambia ndio tunaweza kutoa msimamo wetu lakini kwa sasa hatuna taarifa zozote.”

Hata hivyo licha ya serikali kuziruhusu hadi jana mchana Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kupitia kwa katibu wake Angetile Osiah alisema bado hawajapata taarifa rasmi zaidi ya taarifa ya juzi ambayo serikali waliituma kwa katibu wa CECAFA Nicholaus Musonye ya kutaka wadhibitishiwe kama kweli kuna usalama.

“Rais Tenga juzi aliwatumia barua ya Waziri wa Michezo wa Durfur ya kuwahakikisha usalama wa kutosha kwa timu zetu, zaidi ya hiyo hatujapata taarifa nyingine mpaka sasa hivi,” alisema Osiah.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU