Facebook Comments Box

Tuesday, March 26, 2013

ZITO KABWE, IDD AZAN NAO WAMALIZA MAFUNZO YAO JKT MGAMBO 835KJ - TANGA





Mbunge wa Kigoma CHADEMA, Zitto Kabwe pamoja na Wabunge wenzake kadhaa vijana leo wakemaliza rasmi mafunzo yao ya awali ya JKT katika kambi ya Mgambo 835KJ kilichopo Mkoani Tanga.

Pichani juu ni Zitto Kabwe akijiandaa kwenda katika gwaride la mwisho na picha chini akiwa shambani pamoja na Mbunge mwenzake  Iddi Azan, Abdallah haji, Raya Ibrahim na Antony Mbassa kambi ya Mgambo 835KJ.
Aidha Zitto Kabwe amesema anafuraha isiyo na kifani kumaliza mafunzo hayo na ameweka historia kubwa katika maisha yake leo hii. Anapasha zaidi katika wakati wa Zoezi la kulenga shabaha alifanikiwa kulenga risasi 3 akiwa amelala, 3 akiwa amepiga magoti na 1 akiwa amesimama. 


HATIMAYE WABUNGE WAMALIZA MAFUNZO YA MUDA MFUPI YA JKT RUVU

8E9U3088Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi mbunge wa viti maalum Ester Bulaya leo katika kambi ya RUVU JKT.Rais Kikwete amefunga rasmi mafunzi hayo leo  yaliyofanyika kwa wiki tatu.
8E9U3121


Monday, March 25, 2013

HII NDIO HUKUMU YA MUIGIZAJI KAJALA

Kajala
Muigizaji Kajala amekutwa nahatia katika makosa mawili ambapo ameamriwa kwenda jela miaka mitano au kutoa faini ya Tsh milioni 13 ambapo habari zilizo tufikia punde zinasema mrembo na muigizaji Wema Sepetu ametoa hela hizo zote milioni 13 ili muigizaji huyo awe huru.
Wema Sepetu

Habari zaidi tutazidi kukuletea

ANGALIA VIDEO YA TAIFA STARS VS MOROCCO NA MAGOLI YALIVYOFUNGWA




Saturday, March 23, 2013

ANGALIA VIDEO YA TUNDU LISSU AKIMTUHUMU LUDOVICK NA MWIGULU KUTENGENEZA VIDEO YA RWAKATARE




SERIKALI HAINA MPANGO WA KUBINAFSISHA TANESCO

Serikali imesema haina mpango wa kuuza au kubinafsisha Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kwa sababu za kiusalama, licha ya shirika hilo kushindwa kutimiza baadhi ya majukumu yake.

Mbali na TANESCO, mashirika mengine ambayo pamoja na kufanya vibaya yataendelea kubaki mikononi mwa serikali ni Mamlaka ya Bandari, Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na mengine ambayo kiutendaji yanahusishwa na usalama wa Taifa.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, muda mfupi baada ya kuzungumza na wafanyabiashara kutoka Uingereza.

Wafanyabiashara hao wamekuja nchini baada ya Waziri huyo kutembelea Uingereza na kuwaeleza kuwa Tanzania imefungua milango ya uwekezaji. Wameonyesha nia ya kuwekeza kwenye nishati hasa ya gesi.

Profesa Muhongo alisema kinachoendelea sasa ni kuliboresha shirika kwa kufanya marekebisho makubwa. “Watanzania subirini kidogo, mambo mazuri ya TANESCO yanakuja muda si mrefu,” alisema.

Kwa mujibu wa Profesa Muhongo, madhara ya kuachia mashirika nyeti mikononi mwa wawekezaji ni makubwa kuliko faida, huku akitoa mfano kwa Bandari kuwa inaweza kuingiza meli iliyosheheni silaha za kupindua nchi huku usalama wa Taifa ukiwa hauna taarifa zozote.

“Lazima mashirika nyeti yaendelee kuwepo mikononi mwa serikali ili kujihakikishia usalama,” alisema. Aliongeza kuwa TANESCO itaendelea kununua umeme kutoka kwa wawekezaji kwani haiwezi kuwa wafuaji umeme na wasambazaji.

Alisema TANESCO imekuwa ikinyooshewa vidole kila wakati kwa kuwa inagusa maisha ya watu, huku akisisitiza kuwa mashirika karibu yote yanafanya vibaya lakini hayanyooshewi vidole kama shirika hilo, “mbona watoto wamefeli vibaya...”

Hata hivyo, Profesa Muhongo alisema uchumi wa nchi hauwezi kuimarishwa na serikali pekee, bali kwa kushirikiana na sekta binafsi. Kuhusu wawekezaji wa nje kuja kuwekeza nchini, alisema hawawezi kuachiwa wenyewe ni lazima waingie ubia na kampuni za ndani.

Kuhusu kuwepo wanataaluma waliobobea katika masuala la gesi,  Waziri Muhongo aliwaondoa wasiwasi kwa kuwaeleza kuwa baada ya muda si mrefu wataalamu wa fani hizo watakuwa zaidi ya 200.

Aliwaambia kuwa vipo vyuo vikuu kama cha Dodoma vimeshaanzisha masomo ya masuala ya gesi lakini pia wapo wanafunzi wanaosoma nje ya nchi na kwamba muda si mrefu.

via gazeti la Nipashe



Thursday, March 21, 2013

RIDHIWANI KIKWETE ATEULIWA NA MANJI KUWA MWENYEKITI WA UJENZI WA MAFIA


Ridhiwani Kikwete akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kutambulishwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa eneo la Mafia
Mwenyekiti wa klabu ya Young Africans Sports Club alhaj Yusuf Manji leo amemtambulisha wakili Ridhiwani Kikwete kuwa mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kitega uchumi katika eneo la klabu lililopo makutano ya Mafia/Nyamwezi  eneo la Ilala jijini Dar es salaamAkiongea na waandishi wa habari leo makao makuu ya klabu Manji amesema uteuzi wa Ridhiwani umezingatia uwezo wake kwa taaluma yake, na moyo alionao katika kujitolea katika kazi mbali mbali za klabu ya Yanga"Wote tunamfahamu Ridhiwani amekua ni mwanachama wa Yanga kwa muda mrefu, amekua akijitoa katika kazi mbali mbali za maendeleo ya klabu, hivyo tumeona ni vizuri kumpa fursa hiyo ili aweze kusaidia katika kuleta maendeleo ya klabu" alisema Manji
Katika kamati hiyo ambayo Ridhiwani ameteuliwa , amepewa fursa ya kuteua/kuchagua wajumbe atakaoshirikiana nao katika ujenzi wa kitega uchumi hicho katika mtaa wa mafia, pia atakua na uwezo wa kuongeza wajumbe au kupunguza kulingana na mahitaji kwa kipindi hicho.
Mara baada ya kutambulishwa kwa wanachama na waandishi wa habari, Ridhiwani alisema anashukuru kwa mwenyekiti wa klabu ya Yanga Manji kumteua kushika nafasi hiyo na kuahidi kuwa atajitahidi kadri ya uwezo wake kuhakikisha ujenzi huo unafanikiwa.
 "Nitakaa na kuangalia ni wajumbe gani ambao tutaweza kukaa pamoja na wajenzi (wakandarasi) ili kuweza kufanikiwa katika ujenzi wa kitega uchumi, kwani napenda eneo hilo liwe sehemu ambayo litasaidia katika uchumi wa klabu" alisema Rdihiwani 
Aidha Ridhiwan aliendelea kusema kuwa Kiwanja cha mafia kimekuwepo kwa mda mrrefu bila ya kufanyiwa muendelezeo, ila naamini tutajitahidi ili kuweza kuhakisha historia inajengwa kwa kubadili eneo hilo na kuwa sehemu ya kivutio na ya kuiingiza pesa klabu.
Ridhiwani mwisho alimalizia kwa kusema hawataishia katika ujenzi wa kiwanja cha mafia tu bali wataweka mipango kuhakikisha kuwa hata katika matawi ya Yanga sehemu mbali mbali wanaweza kuwekeza na kujenga majengo ambayo yatasaidia katika kuendeleza uchumui wa klabu. 

AddThis Social Bookmark Button

KIBONZO CHA LEO: KIPANYA NA UTEKAJI TANZANIA




RAILA ODINGA AMCHUKUA WAKILI WA GEORGE W. BUSH


RAILA ODINGA ACHUKUA WAKILI WA GEORGE.W.BUSH NA HOFU KUHUSU HALI YA KISIASA NCHINI KENYA.

Uchaguzi wa Nchi ya kenya imeleta hali ya mtafarakano na kutoelewana baina ya wanasiasa wa Kenya huko Usalama wa Nchi hiyo ikiwa mashakani.

Nchi ya kenya inayoaminika kuwa mmoja kati ya Nchi za Kiafrika inayosifika kwa Rushwa ambayo Mashirika ya Nchi za Magharibi inauona Nchi hiyo Muhimu sana upande wa Mapambano dhidi ya kile wanachokiita Ugaidi/Uislamu.

Waziri mkuu wa Kenya aliyemaliza Muda wake raila Odinga amemchukua Wakili wa George w Bush aliyekuwa Kiongozi wa Kupambana na Uislamu Duniani wakili Wiliam Burck, Siasa ya Nchi ya Kenya unaonekana kuleta tofauti wa kisiasa huko Marekani ambapo wanasiasa hao wamagawanyika kwa Raila na Uhuru Kenyatta, Raila Odinga aliyeingia na Mktaba na Mayahudi ambapo Raila Odinga anapata Usaidizi kutoka kwa Mayahudi ili kuendeleza Mradi wao wa Kupambana na Uislamu ktk Nchi ya Somalia na pia Kupora mali asili ya Nhi hiyo.

Habari kuhusiana na Wakili Wiliam barck imesambazwa na Mashirika ya habari ya Marekani ya Ap na Televisheni ya Fox9,inaonekana Chuki waliyonayo mayahudi Dhidi ya Uislaam wanataka Raila Odinga angeweza Kuchaguliwa,na pia vyombo vya habari vya Nchi za Magharibi inamuunga Mkono Raila Odinga,Nchi ya Somalia ilishindwa kutulia kutokana na Nchi ya Kenya na Ethiopia.

Makabila haya ya Raila Odinga na Uhuru Kenyatta ni mahasimu wa Kisiasa na inahofiwa Nchi hiyo kutumbukia Mchafuko wa Kikabila na wa Kisiasa,Uchaguzi wa Mwaka 2007 Kenya ilitumbukia Mchafuko wa umwagikaji Damu nyingi huko watu wengi wakipoteza Maisha yao na wengine wakihama makwao na kuwa Wakimbizi wa Ndani.

Uchaguzi wa Nchi ya kenya imeleta hali ya mtafarakano na kutoelewana baina ya wanasiasa wa Kenya huko Usalama wa Nchi hiyo ikiwa mashakani.

Nchi ya kenya inayoaminika kuwa mmoja kati ya Nchi za Kiafrika inayosifika kwa Rushwa ambayo Mashirika ya Nchi za Magharibi inaona Nchi hiyo Muhimu sana upande wa Mapambano dhidi ya kile wanachokiita Vita dhidi ya  Ugaidi.


Waziri mkuu wa Kenya aliyemaliza Muda wake Raila Odinga amemchukua Wakili wa George W Bush aliyekuwa Kiongozi aliesababisha vita katika maeneo mbalimbali  Duniani wakili Wiliam Burck.
Siasa ya Nchi ya Kenya unaonekana kuleta tofauti wa kisiasa huko Marekani ambapo wanasiasa hao wamagawanyika kwa Raila na Uhuru Kenyatta.
Habari kuhusiana na Wakili Wiliam barck imesambazwa na Mashirika ya habari ya Marekani ya Ap na Televisheni ya Fox9 inaonekana wamarekani walitaka Raila Odinga  achaguliwe na pia vyombo vya habari vya Nchi za Magharibi inamuunga Mkono Raila Odinga.
Nchi ya Somalia ilishindwa kutulia kutokana na Nchi ya Kenya na Ethiopia. Kenya ndio alikuwa mshiriki mkuu katika vita hivyo na Raila ndio alikuwa mmoja wa wasimamizi wakuu wa vita hivyo kama waziri mkuu

Makabila mawili  ya Raila Odinga na Uhuru Kenyatta ni mahasimu wa Kisiasa na inahofiwa Nchi hiyo kutumbukia Mchafuko wa Kikabila na wa Kisiasa,Uchaguzi wa Mwaka 2007 Kenya ilitumbukia Mchafuko wa umwagikaji Damu nyingi huko watu wengi wakipoteza Maisha yao na wengine wakihama makwao na kuwa Wakimbizi wa Ndani.



KESI YA PONDA YAFUFUA MAZITO

 
KESI inayomkabili Katibu wa Taasisi na Jumuia za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda, imezidi kuibua mambo mazito, ambapo safari hii, waasisi wa Muungano, Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Karume wametajwa katika kesi hiyo.
 Shahidi wa upande wa utetezi, Bilali Wakera (87), mkazi wa Mkoa wa Tabora, ambaye ni kiongozi wa dini alidai mbele ya Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Nyerere na Karume walichangia kudidimiza Uislamu.
Akiongozwa na Wakili Juma Nassoro, Wakera alidai kuwa miaka ya nyuma Waislamu walikuwa dhoofu kwani walikuwa viongozi wawili, Aga khan ambaye alikuwa ni kiongozi wa dunia na Rais wa Misri Nassar walichukua dhamana ya kuwasaidia Waislamu.
Viongozi hao walianzisha East Africa Muslim Welfare Society kama chombo cha kuwasaidia Waislamu wote. Alidai kuwa chombo hicho kilikuwa na mali nyingi, vikiwemo viwanja na kimojawapo kilikuwa ni Kiwanja cha Markaz Chang’ombe. Alidai kuwa dhumuni la kiwanja hicho ilikuwa kujenga Chuo cha Kiislamu. Waikara alidai kiwanja hicho kilitakiwa kijengwe chuo cha ghorofa tatu, lakini anashangaa kilichopo sasa kimejengwa ghorofa moja.
 Hata hivyo, alidai kuwa kwa sababu yeye alikuwa ni kiongozi mkubwa katika chombo hicho, Hayati Mwalimu Nyerere alimwita na kumwambia aachane na mambo hayo kwanza hadi wapate uhuru. Shahidi huyo alidai kuwa Nyerere alimuahidi kuwa watakapopata uhuru atawasaidia Waislamu, lakini hakutekeleza ahadi hiyo.
Alidai kuwa baada ya Nyerere kutotimiza ahadi hiyo aliwaeleza Waislamu kuwa yeye aliwekeana ahadi na Mwalimu, lakini hakuitekeleza ndipo walipoanza kukwanguana na Mwalimu Nyerere.
 Pia alidai kuwa Karume aliwapatia fedha watu wake wazisambaze mikoani ili kuvunja chombo hicho na kwamba walitembelea mikoa 20. Mikoa 12 walikataa chombo hicho kisivunjwe na mikoa iliyobaki walikubali kivunjwe. ”Hata mimi nililetewa sh. 40,000 na Adamu Nasibu, lakini nilizitaa kwa sababu nilikuwa nakitetea chombo cha Waislamu,” alidai Waikera.

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU