Facebook Comments Box

Sunday, March 3, 2013

OMMY DIMPOZ FT VANESSA MDEE - ME AND YOU




MBATIA, ULUOCH WAKATAA KUSHIRIKI KWENYE TUME YA KUCHUNGUZA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

Mh Mbatia

WAKATI Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka hadharani majina ya wajumbe wa Tume ya Taifa ya Kuchunguza Matokeo ya mwaka 2012 ya Kidato cha Nne jana, baadhi ya wajumbe waliopewa heshima hiyo ya kusaidia kutafuta sababu za matatizo ya elimu na jinsi ya kuyatatua, Mbunge wa Kuteuliwa James Mbatia na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekiel Oluoch, wamekataa uteuzi huo. Mbatia katika hoja yake kwa waandishi wa habari jana, alisema kwa kuwa hadi jana hakuwa amepata taarifa ya maandishi kuhusu uteuzi wake, asingeweza kutamka kama amekubali au la, hadi atakapokuwa amepata maandishi hayo akisema atakapoyapata ndipo, “nitafanya uamuzi kwa maslahi ya pamoja ya Watanzania.” Hata hivyo, habari za uhakika kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, zilisema Mbatia alifahamishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lyimo kwa njia ya simu afike Ofisi ya Waziri Mkuu achukue barua yake ya uteuzi kama walivyofanya wajumbe wengine. Oluoch alipotafutwa azungumzie uamuzi wake wa kujitoa kwa mujibu wa barua aliyoiwasilisha Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema yuko mkutanoni akaomba apigiwe baada ya nusu saa na ilivyofanyika hivyo, alikata simu kila alipopigiwa. Ikiwa nia yetu ni thabiti ya na kweli ya kutaka kubadili mwenendo wa mambo yasiyo sahihi katika nchi ya Tanzania, hatuna budi kutii na kufuata sheria tulizojiwekea sisi wenyewe. Kama siyo kasuku, kila leo tunaimbiana misemo maarufu tunayonukuu kutoka kwa watu mahiri, mfano, “insanity: doing the same thing over and over again and expecting different results. ~Albert Einsten” na “walk the walk, talk the talk” (ingawaje hii tumeibadili tunavyojua kwa akili yetu ati, ‘walk the talk’ -- hakuna msemo kama huo! How do you walk the talk? Kupinda tu misemo ya wenyewe). Sasa ikiwa Waziri Mkuu aliripotiwa na Ofisi yake kuwa alikutana na Wajumbe wa Tume aliyoiteua, bila ya kupata hakika ya kila mteuliwa --iwe ni kwa njia ya kumpigia simu kuthibitisha, kutuma ujumbe mfupi wa simu, kutuma barua, nukushi, barua pepe n.k-- kuwa (1) Amepata taarifa rasmi ya uteuzi huo na (2) Ameridhia uteuzi huo; Waziri Mkuu akaitisha kikao ijapokuwa baadhi ya wajumbe hawakuwemo kikaoni bila ya kuwa na hakika kama wanaopelea wametoa taarifa rasmi ya udhuru wa kutokuhudhuria kikao hicho, sioni ni kwa namna gani Mbatia analaumiwa kususia Tume il hali anaifuata sheria. Kuongoza ni mfano na Kiongozi ni mfano. Kwa wasiojali sheria au wanaojiona wapo juu ya sheria ama wenye adabu za woga, hili litakuwa jambo la kipuuzi kwao. Kwao wao amri ya mkubwa inatiiwa bila kuhojiwa hata kama imekiuka sheria, hata kama nchi ni ya utawala wa kiraia na haiendeshwi kijeshi. Kwao kuvunja sheria mama si jambo la ajabu. Ndiyo wale kila leo wanaimba misemo kama kasuku bila kutafsiri wala kujua maana yake. Na hao hawakawii kusema kwa kuwa huyu ni mmoja wa wanachama wa upinzani, basi lolote lile hata liwe jema atapata pa kupinga tu. Na utawasikia majuha hao wakijitapa kwa bezo la kejeli, “sheria Bongo?” Utakuwa na kasoro ukithubutu kusema Mbatia hana nia ya kusaidia nchi kuondokana na tatizo kwa kuhoji utaratibu uliotumika kumfikishia taarifa. Angekuwa hana nia angetumia miaka inayokaribia kumi kutafiti kuhusu elimu na kisha kukusanya vielelezo na kuwasilisha hoja Bungeni kuhusu uozo wa elimu? Kama anaweza kuunda hoja yenye nguvu hivyo kwa maslahi binafsi, je atakapounda hoja inayolihusu Taifa?

SOURCE: WAVUTI

YALIYOJIRI KWENYE KILIMANJARO MARATHON LEO: WAKENYA WAENDELEA KUTAMBA


Washiriki wa Kilimanjaro Marathon wakiwa tayari kabisa kwa ajili ya kukimbia
Vituko hafikukosekana wazungu hawa wao hawakukimbia marathon ila wametembea mpaka wamemaliza

Afisa ujasiliamali watu wa Kilimanjaro Christian Medical University College Victor Selengia katikati akiwa na mwanafunzi wa mwaka wa udakitari Carl Jacob(Kulia) na mwanafunzi wa udakitari mwaka wa nne Nico (kushoto) wakifurahia medali zao baada ya kumaliza kilometa 21
Dr Fransis akifurahia medali na |Carl baada ya kumaliza kilomita 21
Dr Sudai (kulia) akiwa na Dr Joseph (katikati) wakifurahia medali zao

Mwanafunzi wa udakitari David Majule akishuka kumalizia kwa kasi sana. Ameiambia KITONGONI kuwa mwaka huu ameweza kuvunja rekodi yake kwa kupunguza zaidi ya dakika 32 kutoka muda alio utumia mwaka jana. Amekuwa akishangazwa na watanzania kufanya vibaya katika haya mashindano na kuaacha kila mwaka mshindi akitokea Kenya na wakati mashindano yanafanyika Tanzania. Ameomba viongozi wa chama cha riadha wajiangalie upya na ikiwezekana wawajibike kwa hili

Principal Investigator wa MEPI Tanzania kutokea marekani akifurahia medali yake baada ya kumaliza kilomita 21 na Carl Jacob

Motta, Carl na Kimario baada ya kumaliza mbio. \Wanafunzi wengi wa KCMUCo wameshiriki kwenye mashindano haya na kufanya vyema. Japo ushindi umeenda kwa wakenya

Wenye medali zao wakishuka kwa kasi




Wanariadha kutoka Nchini Kenya wameendeleza Umwambawao katika mbio za Nyika za Kilimanjaro ‘Kilimanjaro Marathon 2013’ zilizofanyika leo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Wakenya walidhihirisha umwamba katika Mbio za Kilometa 42 baada ya Mkimbiaji wao Kipsang Kipkemoi kunyakua nafasi ya kwanza katika mbio hizo za mwaka huu upande wa wanaume na Wanawake ilinyakuliwa na Mwana dada Edna Joseph alebeba Medali ya Dhahabu.

Nafasi ya pili hadi ya tano kwa wanaume ni Julius Kilimo, Dominick Kiagor, Onesmo Maithiya Loshile Moikari ambapo upande wa wanawake ni Eunice Muchiri, Frida Too, Rosaline David na Jane Kenyara.
Jumla ya wakimbiaji 65000 walishiriki mbio za Kilimanjaro Marathon 2013.
Kocha wa Taifa Stars Kim Poulsen akiwa na Dr Josephine



Saturday, March 2, 2013

SIMBA WAPOKELEWA VIZURI NA LIBOLO

Kipa wa Simba, Abel Dhaira na mlinzi, Said Nassor Chollo mara baada ya kuwasili Uwanja wa Calulo ambao uko kilomita 300 kutoka Luanda. Ndege inayoonekana pichani ni ya tajiri wa Libolo, Lui Compos ambayo Simba ilitumia kutoka mji mkuu wa Angola, Luanda. Picha na Edo Kumwembe, Angola
SIMBA imetua salama mjini Calulo nje kidogo ya jiji la Luanda, Angola, lakini vifaa vyake muhimu vya kufanyiamazoezi vimepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Hata hivyo, Simba wamefikia katika hoteli ya tajiri wa Libolo huku wakipandishwa katika ndege mbili ambazo pia zinamilikiwa na kipoba huyo.

Wekundu hao wa Msimbazi wanacheza na Recreativo Libolo ya hapa kesho Jumapili katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo Simba ilifungwa bao 1-0 kwenye mchezo wa awali jijini Dar es Salaam.

Simba ilitua Luanda jana Ijumaa saa 5.30 asubuhi za Tanzania na kupakiwa kwenye ndege mbili kwenda mjini Calulo ambako ni umbali wa dakika 30 kutoka Luanda. Ndege ilizopanda Simba zinamilikiwa na tajiri wa Libolo, Rui Campos.

Baada ya kutua Simba walipokewa vizuri na wenyeji wao lakini walilazimika kuhaha kwa dakika kadhaa kutafuta vifaa vyao ambavyo ni bips (vizibao vinavyovaliwa juu ya jezi za mazoezi), koni na mipira ambayo wahumudu wa ndege ya Kenya Airways hawakuwa na jibu zaidi ya kuahidi kuvitafuta zaidi na huenda leo Jumamosi Simba wakavipata.

Mbali na vifaa hivyo hata begi la beki Amir Maftah halikupatikana. Simba iliwasili Calulo saa sita mchana na kufikia hoteli ya Ritz inayomilikiwa na wapinzani wao ambao waliwaazima vifaa kwa ajili ya mazoezi na hali ya hewa na hapa ni joto kali sawa na Dar es es Salaam.

Kiraka Haruna Moshi hayupo na Simba Angola baada ya kupimwa jijini Dar es Salaam na kubainika kwa ana malaria 19 huku kocha wa viungo Moses Basena akibaki kumuuguza mkewe.

Kwenye Uwanja wa ndege wa Calulo, Simba ilipokelewa na wanajeshi na kusindikiwa hadi hotelini ambapo mazingira ya mjini hapa hayajaendelea sana kama ilivyo Luanda na hata uwanja itakapochezwa mechi wa Manispaa ya Calulo Estadio Municipal de Calulo unabeba mashabiki 10,000 tu.

Kocha wa Simba, Patrick Lieweg alisema kikosi chake kipo katika hali nzuri na wako safi kisaikolojia tayari kwa ushindi na kusonga mbele kwenye mashindano hayo.
Nitalazimika kumuanzisha Seseme kwavile Haruna Moshi hayupo lakini kimsingi timu imekuja hapa kushinda na nimewasisitiza wachezaji hilo na wakanielewa, tutapambana mpaka dakika ya mwisho,alisema Mfaransa huyo mwenye miaka 60 ambaye hii itakuwa mechi yake ya 54 kuiongoza klabu kwenye michuano ya kimataifa ya CAF.


SOURCE: MWANASPOTI

FIFA YAWASILISHA MAREKEBISHO 10 YA KATIBA KWA WARAKA

Rais wa FIFA Sepp Blatter akiwa na Rais wa TFF Leodegar Chilla Tenga walipokutana hivi karibuni makao makuu ya FIFA jijini ZurichShirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limetuma mapendekezo 10 ya marekebisho ya Katiba yake kwa wanachama wake kwa njia ya waraka.Mapendekezo hayo yametumwa kwa kila nchi mwanachama kupitia waraka namba 1320, ambapo wanachama kwa kupitia kwa mashirikisho yao ya mabara watapiga kura ya ndiyo au hapa. 
Kwa upande wa Afrika, wanachama wa FIFA wanatakiwa kuwasilisha kura zao kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).Baadhi ya mapendekezo hayo ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa FIFA (FIFA Congress). Makamu wa Rais wa FIFA na wajumbe wa Kamati ya Utendaji wanaochaguliwa katika mabara ambapo itabidi wathibitishwe na FIFA Congress.
Muundo wa Kamati ya Utendaji; nafasi moja ya vyama vya mpira wa miguu vya Uingereza (British FAs) sasa inahamishiwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA). Pia Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi ya FIFA anatakiwa kushiriki vikao vya Kamati ya Utendaji bila kuwa na haki ya kupiga kura.Uchaguzi wa Rais; mgombea anatakiwa kuungwa mkono na idadi ya kutosha ya vyama wanachama kutoka katika mabara mawili tofauti. Ukomo wa uongozi; kuanzisha vipindi vya uongozi. Ukomo wa umri; ukomo wa umri usiozidi miaka 72 wakati wa kugombea utekelezwe.Uwakilishi wa kutosha kwa makundi yenye maslahi katika FIFA; makundi yenye maslahi katika mpira wa miguu kama wachezaji wapate uwakilishi katika Kamati ya Mpira wa Miguu. Uteuzi wa mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia; uteuzi sasa ufanywe na Mkutano Mkuu wa TFF.


Friday, March 1, 2013

ANGALIA MAANDAMANO YA CHADEMA KWA PICHA KATIKA JIJI LA MBEYA
















POLISI MKOA WA KINONDONI YAKAMATA MAJAMBAZI NA SILAHA


Baadhi ya silaha zilizokamatwa klatika msako na Polisi Mkoa wa Kinondoni zikiwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay leo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela akionesha bastola zilizokamatwa na Polisi wakati wa msako wa majambazi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela akionesha nondo zilizokamatwa wakati wa msako huo.


MNYIKA: NCHI IMEINGIA TENA KWENYE MGAO WA UMEME


Mbunge wa jimbo la Ubungo-Chadema Mh John Mnyika-
---
Nchi imeingia tena katika mgawo wa umeme kinyume na ahadi iliyotolewa na Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo bungeni tarehe 28 Julai 2012. 

Hali hiyo ni matokeo ya Serikali kutozingatia tahadhari niliyoitoa bungeni tarehe 27 Julai 2012 kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani na kwa nyakati mbalimbali kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini juu ya hali tete iliyotarajiwa kuwepo na hatua zinazopaswa kuchukuliwa katika utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme. 

Ikiwa ni sehemu ya wajibu wa kibunge wa kuisimamia Serikali nawataka viongozi na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kuacha kuficha hali ya mambo na kuwaeleza ukweli wananchi kuhusu mgawo wa umeme uliojitokeza na hatua za haraka zinazochukuliwa kurekebisha hali hiyo. 

Iwapo Wizara na TANESCO hawatatoa matangazo ya ukweli kwa wananchi, kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini nitaeleza vyanzo vya mgawo wa umeme uliojitokeza ili hatua ziweze kuchukuliwa wakati huu ambapo wajumbe wa kamati ya nishati na madini wenye wajibu wa kuisimamia Serikali kwa niaba ya Bunge katika sekta hizo nyeti hawajateuliwa.


Aidha, pamoja na kutoa maelezo kuhusu mgawo wa umeme, Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO watumie nafasi hiyo pia kueleza hatua zilizochukuliwa kuhusu ukaguzi wa awamu ya pili kuhusu tuhuma za ufisadi katika ununuzi wa vifaa na uzalishaji wa umeme wa dharura ikiwemo kuhusu mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya kufua umeme. 

Ikumbukwe kwamba mwanzoni mwezi Agosti 2012 Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (NAOT) iliunda timu ya wakaguzi kufanya ukaguzi maalum wa hesabu za Shirika la Umeme (TANESCO) kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma zilitajwa bungeni na Waziri Kivuli wa Nishati na Madini katika maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani tarehe 27 Julai 2012 na Waziri wa Nishati na Madini wakati wa majumuisho ya hoja ya Serikali tarehe 28 Julai 2012. 

Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO waeleze pia hatua iliyofikiwa kuhusu uchunguzi mwingine uliofanywa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kuanzia mwezi Agosti 2012 wa mchakato wa ununuzi wa mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya kufua umeme wa dharura kutokana na tuhuma mbalimbali zilizotolewa bungeni kuhusu ununuzi huo suala ambalo Kambi Rasmi ya Upinzani ilitaka pia tarehe 27 Julai 2012 liundiwe kamati teule ya Bunge ili uchunguzi wa kina uweze kufanyika. 


Wenu katika uwakilishi wa wananchi, 

John Mnyika (Mb)
Waziri Kivuli wa Nishati na Madini 

27 Februari 2013
CHANZO CHA HABARI HII: www.dj-sek.blogspot.com


SIRI YA MTUNGI; SEHEMU YA SABA (EPISODE 7)




POLISI WANATUHUMIWA KUMPIGA RISASI MWALIMU HUYU


PictureMwalimu mmoja wa Shule ya Sekondari Kitulo wilayani Makete aliyefahamika kwa jina la Casto Sote Kawamba ameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa Jeshi la Polisi, Makete

Mkuu wa polisi wa wilaya ya Makete, SP Peter Kaiza akizungumza na FrancisGodwin blog kuhusu tukio hilo lililotokea katika eneo la benki ya NMB tawi la Makete juzi majira ya saa moja na robo alisema  kuwa mwalimu huyo alikuwa anakwenda kupata huduma za kibenki kupitia mashine ya  kutolea  pesa ya ATM akiwa na pikipiki, na kuamriwa na askari mmoja aitwaye Jose Msukuma, kuvaa kofia.

Inadaiwa  kuwa kisa cha mauwaji yake ni madai ya kutokuvaa kofia na baada ya kuitwa na askari hao alikaidi amri na kutaka kumgonga askari huyo aliye kuwa lindoni.

Hata  hivyo  mmoja kati ya  askari ambaye   jina lake halikufahamika mara  moja alisikika  akidai kuwa  chanzo cha mtu huyo kupigwa  risasi  ilikuwa akihisiwa  kuwa ni jambazi baada ya  kufika kwa usafiri wa pikipiki (bodaboda) na kuhisiwa kuwa amefika  kwa ajili ya kuora katika benki hiyo na hivyo askari katika hali ya  kujihami alimpiga risasi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Makete, Idd Nganya ambaye ndie mwajiri wa marehemu amesema kuwa mwili wa marehemu bado umehifadhiwa katika Hospitali ya wilaya ya Makete wakati utaratibu wakusafirisha mwili huo kwenda kwao Mbeya kwa ajili ya mazishi ukiendelea.

Mganga mkuu mfawidhi ambaye ni msemaji wa hospitali ya wilaya ya makete Dr Michael Gulaka amesema kuwa wao walipokea mwili wa marehemu na sio majeruhi.
kwa habari zaidi na picha ingia FrancisGodwin blog


RUFAA YA JOHN MNYIKA DHIDI YA UENDESHAJI MBOVU WA BUNGE WA JOB NDUGAI

RUFAA DHIDI YA UENDESHAJI WA BUNGE USIOKUWA WA HAKI NA UKIUKAJI WA KANUNI WA NAIBU SPIKA JOB NDUGAI KATIKA KUONDOA HOJA BINAFSI YA MAJI

Tarehe 28 Februari 2013 nimewasilisha rasmi rufaa kwa mujibu wa Kanuni ya 5 (4) dhidi ya uendeshaji wa Bunge usiokuwa wa haki wa Naibu Spika Job Ndugai kwa kukiuka kanuni ya 58 (5) kwa kulihoji bunge kinyume na kanuni kufanya uamuzi badili wa kuondoa hoja binafsi kuhusu hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa majisafi na ushughulikiaji wa majitaka katika Jiji la Dar es salaam.

Nimefanya hivyo baada ya kupata kumbukumbu rasmi ya Bunge (Hansard) za kikao cha tano cha tarehe 4 Februari 2013 cha mkutano wa kumi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika Mkutano huo Naibu Spika Job Ndugai alisema na kufanya maamuzi kwamba: “Sasa ninahoji wanaoafiki kwamba hoja hii iondolewe waseme ndiyo…..hoja imeondolewa. Walioafiki Wameshinda”; wakati mtoa hoja sikuwa nimeomba idhini yoyote ya hoja yangu kuondolewa.

Maamuzi hayo ni kinyume na Kanuni ya 58 Fasili 5 ambayo inaelekeza kwamba “Endapo hoja imefikishwa Bungeni, mtoa hoja anaweza tu kuiondoa hoja yake kwa kusimama mahali pake na kusema ‘Ninaomba ruhusa kuondoa hoja’ na papo hapo Spika ataliuliza Bunge kama linaafiki hoja hiyo kuondolewa na inapotokea Wabunge walio wengi watakubali, Spika atasema ‘hoja hiyo inaondolewa kwa idhini ya Bunge’ na hoja hiyo itakuwa imeondolewa na Bunge litaendelea na shughuli inayofuata”.

Ushahidi wa Kumbukumbu Rasmi za Bunge (Hansard) za kikao tajwa unathibitisha ukiukwaji huo wa kanuni kama ifuatavyo:

“…WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuwa hoja iliyo mbele ya Bunge lako Tukufu ni kuitaka Serikali kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi na uondoaji wa majitaka Jijini Dar es Salaam, ambalo tayari linatekelezwa na mpango maalumu uliotengewa fedha nyingi na Serikali, hivyo naomba kutoa hoja kwamba hoja hii iondolewe. Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja…

MBUNGE FULANI: Waziri amesema uongo, amedanganya!

NAIBU SPIKA: Sasa ninahoji wanaoafiki kwamba hoja hii iondolewe waseme ndiyo.

WABUNGE FULANI: Sasa utaihoji vipi wakati tuna majadiliano?

WABUNGE FULANI: Ndiyooooooooo!

NAIBU SPIKA: Wanaokataa waseme siyo.

WABUNGE FULANI: Siyooo!

NAIBU SPIKA: Hoja imeondolewa. Walioafiki wameshinda.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)
(Hoja iliamuliwa na Kuafikiwa)
(Hoja Binafsi ya Mheshimiwa John Mnyika iliondolewa na Bunge)

MHE. TUNDU M. LISSU: Aaaaaa! Aaaaaaaaaaah! Aibu!

NAIBU SPIKA: Hoja imeondolewa na Bunge linaahirishwa hadi kesho saa tatu kamili asubuhi…”

Hivyo, pamoja na kuwa Kanuni ya 8 inataka Spika kuendesha shughuli za Bunge na kutoa maamuzi kwa haki, uadilifu na bila chuki wala upendeleo wowote kwa kuongozwa na Katiba ya Nchi na Kanuni za Bunge, Naibu Spika wa Bunge alifanya maamuzi yenye kukiuka kanuni ya 58 Fasili ya 5 kwa kuruhusu hoja yangu kuondolewa kwa hoja iliyowasilishwa na Waziri wa Maji.

Kufuatia rufaa hii Spika atataarifiwa kwa mujibu wa kanuni ya 5 (4) na kuitisha kikao cha kamati ya kanuni kwa mujibu wa kanuni ya 5 (5) ya kanuni za Kudumu za Bunge na kulijulisha bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa.

Wenu katika uwakilishi wa wananchi,
John Mnyika (Mb)



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU