Facebook Comments Box

Friday, November 27, 2015

RAIS AMSIMAMISHA KAZI KAMISHNA WA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (T.R.A)


Rais Dk John Pombe Magufuli amemsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa mamlaka ya mapato Tanzania ( TRA) Rished Bade na kumteua Philiph Mpango kukaimu nafasi hiyo.


Taarifa kutoka ikulu zimesema kuwa uamuzi huo wa Rais Magufuli umefuatia ziara ya waziri mkuu bandarini iliyobaini upotevu wa makontena 349.



Aidha Rais Magufuli amemtaka Rished Bade kutoa ushirikiano kwa Philiph Mpango wakati uchunguzi ukiendelea.



RISHED BADE aliyesimamishwa kupisha uchunguzi.
www.facebook.com/eatv.tv


MSHAURI WA RAISI WA BURUNDI ANUSURIKA KIFO

Mshauri wa Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amenusurika shambulio alipokuwa akitoka nyumbani kwake katika eneo la Kajaga, magharibi mwa mji mkuu Bujumbura.
Zenon Ndaruvukanye alinusurika bila majeraha yoyote, lakini mlinzi wake, ambaye alikuwa afisa wa polisi, alifariki kutokana na majeraha ya risasi.
Washambulijai walitoroka wakitumia gari aina ya Toyota  Hilux lakini polisi walipashana habari na gari lao likazuiwa maili kadha kutoka Kajaga. Waliacha gari hilo na kutorokea soko lililo karibu, lakini mwishowe wawili walikamatwa. Mmoja wao alifanikiwa kutoroka.

Gari hilo aina ya Toyota Hilux lilipatikana na silaha mbalimbali zikiwemo bunduki aina ya AK47 na guruneti. 
Polisi baadaye walipelekwa kwenye nyumba moja viungani mwa mji wa Bujumbura ambapo walipata silaha zaidi.
Mji wa Bujumbura umekumbwa na machafuko ambayo yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 200 tangu Aprili.


SOMA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 27-11-2015 HAPA




MBUNGE WA JIMBO LA UBUNGO KUPITIA CHADEMA ANAEWAKILISHA UKAWA SAID KUBENEA AWATEMBELEA WANANCHI WAKE

Kubenea akizungumza na waandishi wa habari na wananchi katika Soko la Ndizi la Mabibo.

Said Kubenea Mbunge wa jimbo la Ubungo, akiongea na wananchi katika Stendi ya Mabasi ya Ubungo Dar es Salaam kuwashukuru kwa kumchagua na kujua changamoto zao mbalimbali. Mbunge huyo alitembelea Soko la Mabibo, Kituo cha Mabasi cha Mawasiliano.
Hapa akiwaunga mkono wananchi kununua mananasi katika soko la ndizi la mabibo.
Vijana wakiserebuka baada ya kuzungumza na mbunge wao Said Kubenea katika Soko la Mabibo.
Said Kubenea akiwahutubia wananchi katika soko la Mabibo.


Wednesday, July 15, 2015

HATIMAYE CUF WATOA MSIMAMO WAO KUHUSU KUJITOA / KUBAKIA UKAWA

Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kama wanavyo onekana wakiteta jambo Toka kushoto ni Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, wa katikati yao ni Profesa Lipumba wa CUF na mwisho ni Joseph Mbatia wa NCCR.

Viongozi hao wakiwa wameshikana mikono kuonesha kuwa wao ni wamoja.

Baada ya Chama cha mapinduzi CCM kumpata Mgombea wake wa kiti cha urais wiki iliyopita mkoani Dodoma ambae ni John Pombe Joseph Magufuli.
 
Wanachama wa Umoja wa Katiba ya wananchi (UKAWA) wamekuwa na duku duku la kufahamu mgombea wao atakuwa nani.

Hali hiyo imeleta hamasa sana kwa wanachama hao kiasi cha kuona kama viongozi wao wanachelewa kuwajulisha mgombea wao ni nani na pia kuleta hofu kuwa CUF wamejitoa katika umoja huo.

Lakini CUF kupitia Naibu Katibu Mkuu wao wa Bara Magdalena Sakaya ametoa ufafanuzi kuhusu taarifa zinazoendelea kuenea, amethibitisha kuwa wao hawaja jitoa Ukawa na kuhusu kutokuwepo kwenye kikao akasema walichelewa kupata taarifa za kikao hicho maana hata wao wana vikao vingi ambapo wanajadili jinsi ambavyo madaraka yatakavyo kuwa endapo wakishinda uchaguzi mkuu huo ambao utafanyika Oktoba.
Naibu Katibu Mkuu wa Cuf Bi Magdalena Sakaya akijibu baadhi ya Tuhuma hizo


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU