Facebook Comments Box

Monday, February 2, 2015

SOMA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 02 FEBRUARI, 2015 HAPA



















FRANCIS CHEKA AFUNGWA MIAKA MITATU JELA

Bondia maarufu nchini wa ngumi za kulipwa Francis Cheka amehukumiwa kifungo cha miaka 3 jela na kutakiwa kulipa fidia ya shilingi millioni 1 kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi meneja wa baa yake iliyopo huko Morogoro.

Meneja huyo ajulikanaye kwa jina la Bahati inaelezwa alienda kudai fedha zake alizokuwa hajalipwa na bondia huyo wakati akifanya kazi ya umeneja katika baa yake hiyo ndipo Bondia huyo alikataa kumlipa na kumshushia kipigo.
 Francis Cheka akiwa amevaa mkanda wa ubingwa katika moja ya mapambano yake aliyo wahi kucheza na kushinda.
 Francis Cheka hapa akiwa anafanya mazoezi kabla ya mpambano.


Friday, January 30, 2015

AMCHINJA MPENZIWE NA KUMUUA MANZESE DAR ES SALAAM

Kijana mmoja ambaye jina lake halijapatikana alikamatwa na Polisi jana jioni(Alhamisi) katika maeneo ya Manzese baada ya kumchinja mpenzi wake mpaka kufa kwa kile kinacho dhaniwa kuwa ni wivu wa kimapenzi, Kijana huyo nae alijaribu kujiua kwa kutumia kisu hicho bila mafanikio.
Jionee picha za tukio hilo hapo chini:
 Mtuhumiwa wa tukio hilo ambaye Jina lake bado halijapatikana.
Mwili wa Binti anaedaiwa kuchinjwa na mpenzi wake huyo ukitolewa eneo la tukio maeneo ya Friends Corner-Manzese jana(Alhamisi) jioni.


MAGAZETI YA LEO ALHAMIS TAREHE 29 JAN 2015




























Sunday, January 25, 2015

HATIMAYE DALALI WA UMEME PROF SOSPETER MUHONGO AJIUZURU


Kufuatia kuhusishwa na sakata la
uchotwaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow, Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo ameamua kumuandikia barua Raisi ya kujiuzulu wadhifa wake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Profesa Muhongo ameelezea furaha yake ya kupatikana kwa maendeleo ya haraka katika wizara yake kwa kipindi chake akisema kuwa nidhamu na uwajibikaji vilikuwa dira ya maendeleo wizarani hapo.

Profesa Muhongo amekwenda mbali
zaidi na kueleza kuwa anaamini
kujiuzuru kwake kutaisaidia Serikali na
Bunge kutuliza malumbano ya Sakata
hilo ambalo linazidi kurudisha nyuma
maendeleo ya nchi.
Amesema yeye si mwizi na hawezi
kuuza utu wake kwa kupewa rushwa ili
kuwakandamiza watanzania.
“Nimeamua kujiuzuru kwa dhati kabisa
bila kushinikizwa na mtu yeyeote,
inaonekana mimi ndiyo nitamaliza
mjadala huu wa sakata la Escrow, tuna
mambo mengi ya kitaifa yanayotakiwa
kujadiliwa lakini watu wamekazana na
Escrow, nimemuandikia Rais barua
rasmi ya kujiuzuru wadhifa wangu,
amesema Profesa Muhongo.
Amesema pamoja na kujiuzuru
anatarajia mapema kuzungumza na
watanzania ili kuwaeleza ukweli wa
sakata la Escrow na kujiuzuru kwake ili
kuvunja majungu yanayoendelea kuitesa
Tanzania na watu wake.
Amesema yeye amelelewa katika malezi
yenye maadili mema na kwamba tokea
alipomaliza masomo yake aliaswa
kutopokea ama kutotoa rushwa hivyo
hawezi akapokea rushwa kwa ajili ya
kuutukana utu wa mtanzania hicho
ndicho kinachomgharimu.



Friday, January 9, 2015

BABA AJINYONGA BAADA YA KUMTOBOA MTOTO WAKE MACHO

Mtoto Agripina
Mkazi wa Muleba mkoani Kagera Godfrey Joseph Kajuna mwenye miaka 45 amejinyonga mpaka kufa baada ya kumshushia kipigo kikali na kumtoboa macho binti yake Agripina Godfrey mwenye miaka 12.

Bwana Godfrey aliondoka nyumbani kwake akiacha maagizo kuwa wasimfungulie mlango mama yao pindi akirudi nyumbani. Mabinti hao aliporudi mama yao hawakufungua mlango kwa kumuhofia baba yao.

Baba yao aliporudi aliuliza mama yao yupo wapi. Ndipo watoto hao wakamjibu kuwa ameenda kujihifadhi sehemu nyingine kwa kuwa hawaku mfungulia kama maagizo yake aliyo yaache. Baada ya maelezo hayo Bwana Godfrey alianza kumpiga binti huyo ambae ni mkubwa hapo nyumbani na kumtoboa macho.

Baada ya kutenda kitendo hicho bwana Gedfrey alijinyonga akiacha ujumbe kuwa anaogopa kukamatwa kutokana na kitendo hicho na vitendo vingine ambavyo amekuwa akiifanyia familia yake.


Thursday, January 8, 2015

TAJIRI BILL GATES ANYWA MAJI YA KINYESI

Bill Gates anywa maji yaliotengezwa kutokana na kinyesi
Mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates amekunywa maji yaliotengenezwa kutokana na kinyesi cha binaadamu kama maonyesho ya teknolojia mpya itakayoweza kutoa maji safi katika mataifa yanayoendelea.

Mwanzilishi huyo wa Microsoft amesema kuwa ataisambaza mitambo ya teknolojia hiyo mpya kote duniani baada ya kuifanyia majaribio mwishoni mwa mwaka huu.
Teknolojia hiyo imeungwa mkono na shirika la WaterAid ambalo limesema kuwa itasaidia sana katika maeneo ya miji.
Kulingana na shirika hilo la hisani takriban watu millioni 748 hawana maji safi ya kunywa.
katika kanda ya video iliyowekwa katika blogu yake,Bwana Bill Gates alishuhudia kinyesi cha Binaadamu kikiingizwa katika mtambo huo kabla ya kunywa maji yaliokuwa yakitoka kutoka kwa kikombe.
''Maji hayo ni mazuri sana ikilinganishwa na maji yoyote yale niliokunywa,na baada ya kusomea teknolojia hii nitayanywa kila siku.
Maji haya ni salama kabisa'',aliandika katika blogu yake.Kulingana na mtengenezaji wa mtambo huo Peter Janicki,maji taka hayo huchemshwa kabla ya mvuke wa maji hayo kutengwa na taka ngumu.
Taka hizo ngumu baadaye huwekwa katika moto na kutoa mvuke unaoendesha mashine zinazotoa nguvu za umeme kwa mtambo huo na pia kwa wakazi wa eneo hilo.
Maji hayo baadaye hutiwa ndani ya mtambo wa kusafisha maji ili kutoa maji safi ya kunywa.
''lakini kwa nini mtu awe na wazo la kubadilisha uchafu kuwa maji ya kunywa na umeme'',aliuliza Gates.
Jibu aliloandika ni kwamba kwa sababu magonjwa yanayosababishwa na mazingira machafu huwaua watoto 700,000 kila mwaka na huwakinga wengine wengi dhidi ya kuathirika kiakili na kimwili.

Chanzo bbc swahili



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU