Monday, February 2, 2015
FRANCIS CHEKA AFUNGWA MIAKA MITATU JELA
Friday, January 30, 2015
AMCHINJA MPENZIWE NA KUMUUA MANZESE DAR ES SALAAM
Sunday, January 25, 2015
HATIMAYE DALALI WA UMEME PROF SOSPETER MUHONGO AJIUZURU
Kufuatia kuhusishwa na sakata la
uchotwaji wa mabilioni ya fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow, Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo ameamua kumuandikia barua Raisi ya kujiuzulu wadhifa wake.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Profesa Muhongo ameelezea furaha yake ya kupatikana kwa maendeleo ya haraka katika wizara yake kwa kipindi chake akisema kuwa nidhamu na uwajibikaji vilikuwa dira ya maendeleo wizarani hapo.
Profesa Muhongo amekwenda mbali
zaidi na kueleza kuwa anaamini
kujiuzuru kwake kutaisaidia Serikali na
Bunge kutuliza malumbano ya Sakata
hilo ambalo linazidi kurudisha nyuma
maendeleo ya nchi.
Amesema yeye si mwizi na hawezi
kuuza utu wake kwa kupewa rushwa ili
kuwakandamiza watanzania.
“Nimeamua kujiuzuru kwa dhati kabisa
bila kushinikizwa na mtu yeyeote,
inaonekana mimi ndiyo nitamaliza
mjadala huu wa sakata la Escrow, tuna
mambo mengi ya kitaifa yanayotakiwa
kujadiliwa lakini watu wamekazana na
Escrow, nimemuandikia Rais barua
rasmi ya kujiuzuru wadhifa wangu,
amesema Profesa Muhongo.
Amesema pamoja na kujiuzuru
anatarajia mapema kuzungumza na
watanzania ili kuwaeleza ukweli wa
sakata la Escrow na kujiuzuru kwake ili
kuvunja majungu yanayoendelea kuitesa
Tanzania na watu wake.
Amesema yeye amelelewa katika malezi
yenye maadili mema na kwamba tokea
alipomaliza masomo yake aliaswa
kutopokea ama kutotoa rushwa hivyo
hawezi akapokea rushwa kwa ajili ya
kuutukana utu wa mtanzania hicho
ndicho kinachomgharimu.
Friday, January 9, 2015
BABA AJINYONGA BAADA YA KUMTOBOA MTOTO WAKE MACHO
![]() |
| Mtoto Agripina |
Thursday, January 8, 2015
TAJIRI BILL GATES ANYWA MAJI YA KINYESI
Bill Gates anywa maji yaliotengezwa kutokana na kinyesi
Mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates amekunywa maji yaliotengenezwa kutokana na kinyesi cha binaadamu kama maonyesho ya teknolojia mpya itakayoweza kutoa maji safi katika mataifa yanayoendelea.
Mwanzilishi huyo wa Microsoft amesema kuwa ataisambaza mitambo ya teknolojia hiyo mpya kote duniani baada ya kuifanyia majaribio mwishoni mwa mwaka huu.
Teknolojia hiyo imeungwa mkono na shirika la WaterAid ambalo limesema kuwa itasaidia sana katika maeneo ya miji.
Kulingana na shirika hilo la hisani takriban watu millioni 748 hawana maji safi ya kunywa.
katika kanda ya video iliyowekwa katika blogu yake,Bwana Bill Gates alishuhudia kinyesi cha Binaadamu kikiingizwa katika mtambo huo kabla ya kunywa maji yaliokuwa yakitoka kutoka kwa kikombe.
''Maji hayo ni mazuri sana ikilinganishwa na maji yoyote yale niliokunywa,na baada ya kusomea teknolojia hii nitayanywa kila siku.
Maji haya ni salama kabisa'',aliandika katika blogu yake.Kulingana na mtengenezaji wa mtambo huo Peter Janicki,maji taka hayo huchemshwa kabla ya mvuke wa maji hayo kutengwa na taka ngumu.
Taka hizo ngumu baadaye huwekwa katika moto na kutoa mvuke unaoendesha mashine zinazotoa nguvu za umeme kwa mtambo huo na pia kwa wakazi wa eneo hilo.
Maji hayo baadaye hutiwa ndani ya mtambo wa kusafisha maji ili kutoa maji safi ya kunywa.
''lakini kwa nini mtu awe na wazo la kubadilisha uchafu kuwa maji ya kunywa na umeme'',aliuliza Gates.
Jibu aliloandika ni kwamba kwa sababu magonjwa yanayosababishwa na mazingira machafu huwaua watoto 700,000 kila mwaka na huwakinga wengine wengi dhidi ya kuathirika kiakili na kimwili.
Chanzo bbc swahili
Wednesday, January 7, 2015
YANGA WAZIDI KUWAPA WASHABIKI WAO FURAHA
![]() |
| Mbrazil Coutinho akishangilia moja ya magoli yake |




































