Facebook Comments Box

Wednesday, December 31, 2014

TAHADHARI KWA PICHA: MTU MMOJA AMEKUFA NA KUNING'INIA GETINI HEBU JIONEE MWENYEWE

 Mtu huyo anaitwa Abdul Koroma ni raia wa Siera Leone akiwa amening'inia getini akiwa amekufa, kwa kile inachosemekana kuwa ni mtuhumiwa wa dawa za kulevya na alikuwa anatoroka mahakamani kabla ya kupigwa risasi na kufa juu ya geti ambapo alitaka aruke na kukimbia.
 Hapa askari Magereza wakijaribu kumuondoa mahali alipokuwa amenasa juu ya geti la mahakama ya kisutu
 Mtu huyo hapa baada ya kushushwa chini toka juu ya geti.



Picha na Camera yetu mtaani:

FUNGA MWAKA NA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 31-12-2014 HAPA


















PICHA: BASI LA ABOUD LAPATA AJALI MLANDIZI ASUBUHI HII

Picha chini basi la Aboud likiwa limeanguka baada ya kupata ajali mlandizi asubuhi hii.  Haijajulikana idadi ya majeruhi na waliopoteza maisha.



HAKIMU AJITOA KESI YA UAMSHO




 Sheikh Farid Katikati ya Askari Magereza.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Hellen Liwa amejitoa kusikiliza kesi ya ugaidi inayowakabili viongozi 23 wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI).
 
Hakimu huyo amefikia uwamuzi huo baada ya wakili wa washtakiwa hao wa ugaidi, Abubakar Salim kumtaka ajitoe kuisikiliza kesi hiyo ili iweze kupangiwa hakimu mwingine ambaye atatoa uamuzi juu ya hoja zao walizozitoa mahakamani hapo Septemba 19,2014.

Salim aliiambia mahakama kuwa baada ya kushauriana na wateja wao na uamuzi uliotolewa na Jaji wa Mahakama Kuu, Dk Fauzi Twaib wakaona kuwa ni ukweli kuwa Hakimu Liwa alikwisha toa uamuzi wake juu ya hoja zao Oktoba Mosi, 2014 kuwa mahakama hiyo ya kisutu haina mamlaka ya kusikiliza hoja hizo. 

Alidai Mahakama Kuu katika uamuzi wake uliotolewa na Jaji Twaib umeelekeza kuwa Mahakama ya Kisutu inayo mamlaka ya kuzisikiliza hoja za washtakiwa hao wa ugaidi na hata kuzitolea uamuzi.

"Mahakama Kuu imeelekeza mawakili wa upande wa utetezi kama tutakuwa na hoja mpya ama  zile za awali tuzitoe kwenye mahakama hii ya Kisutu ili ziweze kutolewa maamuzi hivyo naona ni bora ujitoe tupate neno kutoka kwa hakimu mwingine."Alisisitiza kusema wakili huyo mahakamani hapo.

Wakili wa Serikali Mkuu, Benard Kongola alimuomba Hakimu Liwa asijitoe katika kuisikiliza kesi kwa madai sababu zilizotolewa na upande wa utetezi za kumtaka ajitoe hazina msingi.

Kongola alieleza kuwa uamuzi uliotolewa na Jaji Twaib aliamuru utekelezaji wa hoja za upande wa utetezi katika kesi hii ya ugaidi zisikilizwe na kutolewa uamuzi katika Mahakama ya Kisutu.

"Tukiendekeza hii tabia tutamaliza mahakimu wote wa mahakama hii tunasisitiza upande wa utetezi utoe sababu za msingi za wewe kujitoa."Alisema Kongola.
Akijibu hoja hizo, Wakili Salim alieleza kuwa ili haki ionekane inatendeka wewe Hakimu Liwa ujitoe ili hakimu mwingine atoe maamuzi wa hoja zetu.

Hakimu Liwa alisema ni kweli nilikwisha toa uamuzi wangu juu ya maombi ya washtakiwa lakini Mahakama Kuu imeona kivingine kuwa sijatumia mamlaka yangu vizuri nakubaliana na uamuzi huo.
Lakini uamuzi huo wa Jaji Twaib haukufafanua nini kifanyike, umetuacha hoi, ila alitoa angalizo kuwa ushahidi wa kesi hauwezi kutoka hewani na kwamba maelezo yaliyomo katika hati ya mashtaka ya kesi hiyo yapo sahihi.

"Kitu ambacho hata mimi nilikuwa nakishangaa ni hii hati ya mashtaka kuletwa Tanzania Bara badala ya Visiwani, lakini nilipoisoma sheria ya ugaidi nikabaini mtu anaweza kushtakiwa mahali popote." Alisema Hakimu Liwa.Alisisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria Mahakama Kuu ndiyo yenye uwezo wa kuisikiliza kesi hii na siyo mahakama ya Kisutu hivyo yeye hawezi kusema kitu labda kesi ingekuwa imefikia kwenye mwenendo wa uhamishaji shauri (Committal Preceding).

Hatua hiyo inafikiwa baada ya upelelezi wa kesi kukamilika inahamishwa kutoka mahakama ya Kisutu kwenda Mahakama Kuu ambayo inamlaka ya kusikiliza kesi hizo.

"Mimi nimejifunza kitu hapa, kuwa mimi najua nini na wenzangu wanajua nini hivyo siwezi kuendelea na kesii haitakuwa haki najitoa."Aliongeza kusema Hakimu Liwa na akajitoa na kuiahirisha hadi Januari 13,2015 ili ipangwe kwa hakimu mwingine.


Tuesday, December 23, 2014

KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI ASIMAMISHWA KAZI

Kutokana na hotuba ya Mh Rais Prof Jakaya Mrisho Kikwete kutaka uchunguzi ufanyike ili ajiridhishe kuhusu sakata la Escrow katibu mkuu kiongozi amemsimamisha katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini ili uchunguzi ufanyike.

Chini ni tangazo lililoelezea kuzimamishwa kazi kwa katibu mkuu huyo.





HII NDIO CV YA KATIBU MKUU MPYA WA YANGA

Dr. Jonas B. Tiboroha (Ph. D)
Personal Particulars
• Date of Birth: 25th September 1969.
• Place of Birth:  Kasulu.
• Marital status: Married
• Nationality: Tanzanian.
• Employer: University of Dar es salaam (UDSM)
Education Background
• PhD (Education), Malmo University, Sweden Sept
2010 – August 2013, Awarded at the University of
Dar es Salaam, November, 2013.
• MSc. Exercise and Sports Sciences (Training
Methods); Norwegian University of Sport and
Physical Education – Oslo, Norway, August 2002 –
Feb 2004
• BSc Exercise and Sport Sciences: Norwegian
University of Sport and Physical Education- Oslo,
Norway, August 1999 - June, 2002
• Norwegian Language Certificate for Foreigners:
University of Oslo, Norway; September 1998 – May
1999.
• BEd. Physical Education Sport and Culture;
University of Dar es Salaam- Tanzania – Sept 1994
– May 1998.
Professional Experiences and Community Services
• Technical Development Officer at the Tanzania
Football Federation, October 2014 – Now.
• Part time Lecturer Saint Augustine University
College, Tabora campus, 2013 – Now.
• Part time Lecturer University of Gaborone –
Botswana, 2013 –Now.
• U-15 Manager, Malmo Football Club, Malmo
Sweden; October 2010 - 2013
• Lecture: School of Education, Department of
Physical Education and Sport Science, University
of Dar es salaam – since Jan, 2008 – Now.
• Assistant Lecturer; The School of Education,
Department of Physical Education and Sport
Science, University of Dar es salaam – since Jan,
2005 – 2008
• Lecturer in Sports Biomechanics, Exercise
physiology, Theories and Methods of Sports
Training, Measurement and evaluation of Higher
Performance Athletes and Research Methodology
in Physical Education and Sports Science, 2005 -
Now.
• Reporteur TAFCA Conference on Key Aspects of
Football Development in Tanzania. Held at the
Waterfront Conference Center from 18th – 22th
September 2008. Report Submitted.
• Founder and Director of Talent Identification,
Mobilization and Development Organization
(TIMaD); A Community Based Organization for
Promoting Football Talents in Youth – since
December 2004 - Now.
• Chief Coach Wakati Ujao Football Academy; An
academy led by TIMaD for Promotion of Youth
football Talents, 2004 – Now.
Professional Courses, Seminar and Conferences
Attended.
• Conference of Sports Management held at UDSM
November, 2013
• European Conference of Sports Science held at
Malmo, Feb 2012.
• CAF License C  in September 2011
• Conference on Coach Education on Analysis of
Global Issues and Challenges held in Amsterdam,
Netherland, 10th – 15th January 2011.
• FIFA Comm-Unity Seminar on Women Football
Development Held at PPF Tower Dar es Salaam,
Tanzania from 25th – 28th October 2011.
• Symposium on Women and Sport for
Empowerment held in Stockholm, Sweden, from
8th – 12th Feb 2011.
• MRC/UCT Conference on Sports Medicine Held at
the University of Cape Town, South Africa from
16th – 19th September, 2009.
• TAFCA Conference on Key Aspects of Football
Development in Tanzania. Held at the Waterfront
Conference Center in Dar es salaam, Tanzania,
from 18th – 22th September 2008, Report
Submitted.
• DFB Advanced Football Coaching Course for
Youth Football Development, held at the
Department of Physical Education and Sports
Science University of Dar es salaam, Tanzania
from 14th – 18th September, 2007.
• KNVB Course for Coaching Youth Football held at
the International School of Tanganyika Dar es
salaam, Tanzania in 2002.
• The FIFA Course on Coaching Youth Football,
Held at the National Stadium in 2007.
• The TFF/TAFCA Course on Youth Football and
Grassroots Development held at the TFF
Conference Hall, Dar es salaam, Tanzania, 2006.
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway November 2004
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway, November 2003
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway, November 2002
• Annual Symposium on Key Issues in the
Norwegian Football League held at the Norwegian
University of Physical Education and Sport
Sciences, Oslo, Norway, November 2001
• Intermediate Course in Coaching Football in Dar
es salaam, Tanzania in 2001.
• Preliminary Course in Coaching Football in Dar es
salaam, Tanzania in 1996.
Sports Activities and Youth Development
Programs Participated as a Coach
• The EDUSPORT Regional Football Tournaments
for Youth in Lusaka, Zambia 2010 and 2011 with
Wakati Ujao.
• The Rollingstone Youth Tournaments in Arusha,
2009, 2010 and 2011 with Wakati Ujao.
• Taysa Tournaments in Dar es salaam 2005, 2006,
2007 and 2008 With Wakati Ujao.
• Gorthia Cup in Gotenberg, 2000, 2001, 2002 and
2004 with Staeback youth team of Oslo.
• Norway Cup; 1999, 2000, 2001, 2002, 2003 and
2004 with Staeback youth team of Oslo.
• Tivoli Cup; 2000, 2001, 2002 and 2004 with
Staeback youth team of Oslo.
• Gorthia Cup 2006 with Wakati Ujao of Dar es
salaam, Tanzania
• Tivoli Cup 2006 with Wakati Ujao of Dar es
salaam, Tanzania.
• Norway Cup 2006 with Wakati Ujao Dar es
salaam, Tanzania.
Sports Related Publications, Reports and Papers
Presented
• Tiboroha, J (2014). The development dilemma
facing youth football coaches: A case of Managing
and engaging volunteer academy coaches.
Submitted at the International Journal of Sports
and Coaching.
• Tiboroha, J. (2014) Adoption of FIFA Youth
Football Coach Education: A rhetoric or reality. In
for publication, Scandinavian Journal of Sports
Studies
• Tiboroha, J. (2013). Transnational Coaching
Education Courses in Tanzania: An investigation
on the Adoption Process and Barriers for Coaches
to Participate. A Thesis Submitted in Fulfilment of
the Doctoral Degree in Sports Science at the
University of Dar es Salaam.
• Tiboroha, J. (2005). The Influence of Strength
and Endurance on Elite football players’ Jumping
and Sprinting Abilities: A comparative Study on
Tanzanian and Norwegian Elite football Players,
ActaScandinavia Journal, 5(2) 14-16.
• Tiboroha, J. Physiological Demands of Young
Amateur football Players: A study on Dar es
salaam UMISETA, Team-Manuscript, Idrotts forum
journal, October 2009.
• Tiboroha, J. The Implementation of Health School
Programs in Tanzania: A Critique to the
Implementation of the MDGs in Tanzanian
Education System. A paper presented at the
EdQUAL Doctoral Conference held at the University
Bouya, Cameroon, 8th – 15th December, 2010.
• The Physical Status of Tanzanian Olympic
Swimmers one Year after Beijing: What do we learn
on the demands and levels of competitiveness? A
paper presented at the Tanzanian Swimmers
Association Seminar, Held at the Millennium
Towers Hotel 12 – 14 December, 2009.
• Tiboroha, J. The Making of Professionals in the
Development of Quality Physical Education. Paper
presented in the Annual analysis of Physical
Education status in Sub Saharan African
Countries, Bulawayo, Zimbabwe, March, 2007
• Tiboroha, J. Challenges and Prospect of Fitness
and Health promotion in Tanzanian Primary
Schools, Papers in Education and Development
Journal, May 2006.
• Tiboroha, J. Mainstreaming Physical Education in
Primary and Secondary schools for Promotion of
Sports, Tanzania Institute of Education Quarterly,
May 2009.
• Tiboroha, J. Challenges in Organizing Physical
Activities to promote Health in People with special
needs – Paper presented to the Eastern African
conference for Fitness and Health to People with
Special Needs – October 2005
Academic Visits and Scholarships Received
• The World Bank’s “Quick Wins Project”,
Scholarship for PhD Study on The Transnational
Youth Football coaching courses in Tanzania: An
investigation on the adoption process and barriers
for coaches to participate, August 2010 – May
2013
• The SIDA-SAREC research fund on the desk-
review of the eliciting factors for poor youth socio-
economic development in Tandale: What can youth
football do to avail the situation? August, 2009 –
February, 2010
• The SIDA-Linnaeus Palme Scholarship, Academic
Visit to Malmo Sweden, Jan 2009 – June 2009.
• EdQUAL Prospective Doctoral Students’
Workshop on Qualitative Research Method held at
The University of Bouya, Limbe, Cameroon, 2nd –
12th December, 2008
• Norwegian State Educational Fund (NSEF), MSc
Studies, September 2002 - February 2004.
• Norwegian State Educational Fund (NSEF), BSc
Studies in Exercise and Health Sciences,
September 1999 – June 2002
• Norwegian State Education Fund (NSEF),
Norwegian Language Course for Foreign Students
at the University of Oslo Norway, August 1998 –
June 1999.
Referees
1. Dr Hamad Said Ndee
Head of Department
Department of Physical Education and Sports
Sciences
hndee@yahoo.com
2. Rune Hansen
Director of Youth Football Development
Staebeck Football Club
Oslo, Norway
E-Mail: rune.hansen@staebeckfk.no
3. Peter Tape Kristiansen,
Development Executive Director
Malmo Football Club
Malmo, Sweden
E-mail: peter.taper@mff.se
4 Prof. Susanna Hadenberg
Malmo University,
20506 Malmo, Sweden.
E-mail; sussana@mah.se
I Jonas B. Tiboroha, hereby certify that the above
given are my true personal information. Signed on
17th November, 2011.


Friday, December 19, 2014

HII NDIO HABARI MPYA KUTOKA YANGA

Mwenyekiti wa Yanga amefanya mabadiliko katika Safu za uongozi wa klabu hiyo huku akiweka vijana ili waweze kuitumikia klabu kwa muda mrefu. Mmoja wa vijana aliepata bahati hiyo ni Jerry Muro ambae amekuwa msemaji wa timu. Katibu Mkuu atakuwa Dr Jonas B Tiboroha.

Pamoja na hayo mwenyekiti Manji amelibadilisha benchi la ufundi kwa kumuondoa kocha Maximo na kumleta Kocha mpya mdachi Bw Hans van Pluijm akiwa anasaidiwa na mzawa Bw CharlesMkwasa.  




SSERUNKUMA MAJANGA SIMBA: HUENDA ASICHEZE MECHI YOYOTE YA LIGI

Wakati Simba SC ikidai kumalizana na mshambuliaji Mganda Simon Sserunkuma na kupata Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC), klabu yake ya Express imesema imechezewa rafu na itavunja uhamisho huo sanjari na kuipeleka
Simba mahakamani kwa kughushi nyaraka.

Baada ya kufanya vizuri katika mechi yao ya kwanza ya majaribio Tanzania wakiisaidia Simba kuifunga Yanga mabao 2-0 Jumamosi, Sserunkuma na beki wa kati Juuko Murshid (Mganda pia),walisaini mikataba ya kuitumikia
klabu hiyo ya Msimbazi. Sserunkuma alisaini mkataba wa miaka miwili wakati Murshid alisaini miaka mitatu.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Express SC Francis Ntalazzi amekaririwa na mtandao wa Kawowo Sports leo akilia kufanyiwa rafu na Simba katika kukamilisha usajili wa Sserunkuma uliofanyika Jumapili, siku moja baada ya mechi ya ‘ndondo’
ya ‘Nani Mtani Jembe 2′.

Akielezea faulo iliyofanywa na Simba kufanikiwa usajili wa Sserunkuma, Ntalazzi anahoji juu namna saini yake ilivyoghushiwa kwenye mkataba wa mchezaji huyo.

“Binafsi, sikusaini nyaraka yoyote kuthibitisha uhamisho wa mchezaji husika (Sserunkuma) hivyo saini ilighushiwa,” kiongozi huyo wa juu
amesema huku akiweka wazi kusudio la kuipeleka Simba mahakamani kwa udanganyifu na amejipanga kuhakikisha anavunja uhamisho wa mchezaji huyo.

Ingawa uongozi wa Simba haukuwa tayari kuweka wazi fungu ambao nyota huyo amepewa kabla ya kukubali kumwaga wimo, ilielezwa jana kuwa ilimpatia dola la Marekani 40,000 (Sh. milioni 67).

Baada ya kusaini dili hiyo, (Sserunkuma) alirejea kwao Uganda na katika hali ya kushtusha Jumanne alikuwa miongoni mwa nyota wa Express, timu hiyo ilipochapwa mabao 2-1 dhidi ya Kikosi cha Bul F.C katika mechi ya Ligi Kuu ya
Uganda msimu huu.

Kabla na baada ya mechi hiyo, Sserunkuma alionekana akigawa pesa kwa wachezaji wenzake na viongozi wa Express kama ishara ya kuagana.
Sserunkuma, ambaye aliwahi kukipiga na klabu za Kyegenra Happy Boys F.C, Victors, SC Villa, Vipers na Express alisema; “Nimefurahi kuhamia Simba na ninawashauri wachezaji wenzangu kujifua kwa bidii, kuwa na nidhamu, kila mmoja na muda wake maalum katika maisha.”

SIMBA WANASEMAJE
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope, baada ya kutafutwa na mtandao huu kuzungumzia suala hilo, amesema Sserunkuma hana mkataba na klabu, bali wakala wake ndiye amekuwa akiingia mikataba na klabu zinazomsajili.

“Mkataba wa Sserunkuma na Express ulionesha kwamba hamzuii kujiunga na timu yoyote muda wowote. Sisi tumeingia mkataba na wakala wake kama ilivyokuwa kwa Express,” amesema
Hanspope. Ameongeza kuwa walipata ITC ya mchezaji huyo kutoka Shirikisho la Soka la Uganda (FUFA) siku mbili baada ya kumsainisha mkataba (Jumanne).

Kuhusu kucheza mechi ya Ligi Kuu ya Uganda akiwa na Kikosi cha Express ilhali amejiunga na Simba, Hanspope amedai hawana taarifa hizo huku akiahidi kufuatilia suala hilo.


Tuesday, December 16, 2014

KOCHA WA YANGA PRUIJM ATUA DAR

Van Der Pruijm alipotua usiku wa saa nane na nusu
Kocha wa zamani wa Yanga mdachi Hans Van Der Pruijm amesema amerudi tena kwenye timu yake ya zamani kuendeleza pale alipoishia,

‘Falsafa yangu ipo pale pale ya kucheza soka la kushambulia, kwasababu naamini ili ushinde mchezo ni lazima ufunge mabao ya kutosha’.

akiwasili jijini Dar
Kocha huyo amesema bado hajasaini mkataba ila ana matumaini makubwa atamalizana na wakurugenzi wa klabu pale watakapokutana, Van Pruijm anakuja kuziba pengo la kocha aliye timuliwa Mbrazil Marcio Maximo .

 Ahsante: Shaffih Dauda


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU