Facebook Comments Box

Saturday, November 29, 2014

HELKOPTA YA MALI ASILI YAANGUKA UKONGA MOMBASA

Wananchi wakiangalia helkopta hiyo
Helicopter mali ya serikali wizara ya mali asili yaanguka maeneo ya moshi bar mombasa Dar na kuua wote walio kuwemo na kuangukia nyumba za wananchi.

Polisi wameshafika eneo la tukio
Wananchi wenye nyumba hizo bado haijajulikana kama wamekufa ama hawakuwemo. Rubani na capt wa ndege hiyo inasemekana walikuwa na uzoefu mdogo sana(masaa machache sana) kutoka chuo cha 44 cha huko south African.





Thursday, November 27, 2014

SHEIKH PONDA AACHIWA HURU


APPEAL YA SHEIKH PONDA IMESOMWA AMESHINDA HUKUMU YA KUMTIA HATIANI ILIYOTOLEWA NA MAHAKAMA YA KISUTU IMEFUTWA SHEIKH YUKO HURU SASA NA WANAKWENDA MOROGORO.
Maandamano kuelekea Mtambani kuwasikiliza viongozi wa kiislamu

JAJI AMEMTANGAZA SHEIKH KUWA NI ULAMAA MKUBWA WA DINI YA KIISLAMU.

BAADA YA KUFUTIWA KESI HIYO NA KUACHIWA HURU POLISI WALIMKAMATA TENA KWA KUWA KESI YA MOROGORO BADO HAIJAISHA.


 HAWAJAWEKA WAZI KAMA KESI HIYO INA DHAMANA AU HAINA.





Sunday, November 23, 2014

TAMKO LA HIZB UT-TAHRIR JUU YA YANAYOTOKEA KENYA

Kwa mara nyengine tena Waislamu nchini Kenya   wameshuhudia uvamizi wa polisi wa misikiti miinne Sakina Musa, Swafaa na Minaa Mjini Mombasa.

Kitendo hiki cha kinyama kilichopelekea
mauaji ya mwanafunzi mmoja huku vijana wapato mia mbili na hamsini kutiwa mbaroni, kilifanywa chini ya kisingizio cha kuwafurusha vijana wenye misimamo mikali. Harakati ya Hizb
ut-Tahrir Afrika Mashariki inalaani vikali kitendo hiki na twasema yafuatayo:-

Ukatili wa polisi wa Kenya umezidi sana hasa kwa Waislamu ; Huku kukiwa kuna magenge ya-nayotekeleza mauaji kama vile Baghdad boys na Mungiki ambayo wengi ya wafuasi wake ni wakristo hatujashuhudia hata kanisa moja likivamiwa na polisi kama inavyofanywa kwa Waislamu. Bali polisi katika kuendeleza maonevu kwa Waislamu, huwapachika majina radicalists na
extremists kuhalalisha unyama wao dhidi yao. Na hii ndio sura kamili ya polisi leo ndani ya nidhamu za kibepari namna
wanavyotumiwa katika kuwafanyia unyama Waislamu. Madai ya kuwa kuna Waislamu wabaya na Waislamu wazuri
‘radicalists and moderates ni njama tu kuwagawanya Waislamu.

Na hata kama kuna tofauti baina ya Waislamu kifikra na kimisimamo,basi waachiwe wenyewe Waislamu kwani Uislamu uliwawekea utaratibu maalum wa kutatua kasoro hizo. Hivyo haijakuwa halali kwa serikali kuendeleza mateso kwa Waislamu kwa kisingizio hicho. Tunakataa miito hii pamoja na vita
kupambana na ugaidi kwani vyote hivyo ni kuushambulia Uislamu na Waislamu.

Udhalilifu huu umetokamana kukosekanwa na waakilishi wa kikweli  wa mambo ya Waislamu. Hata wale baadhi ya wanasiasa wanaojitokeza ati kukashifu unyamu huo, wao hufanya hivyo kwa lengo tu la kujitafutia umaarufu wa kisiasa. Ushahidi wa haya ni kuwa hao hao ndio huwadaa raia kuwa kushiriki kwao ndani ya nidhamu za kidemokrasia ndio njia ya kuzuia dhulma juu ya Waislamu. Na ukweli ni kuwa nidhamu za kidemokrasia ndio chanzo cha balaa zote zinazoshuhudiwa na watu wote Waislamu na wasokuwa waislamu.

Madhila haya leo ni sehemu tu ya miongoni mwa mengi yanayofanyiwa Waislamu kote dunia  na hayatokoma leo hadi pale Waislamu watapoweza kufanya kazi ya kubeba ulinganizi wa Kiislamu kwa lengo la kusimamisha utawala halisi wa Kiislamu Khilafah katika moja wapo ya nchi za Kiislamu.  Utawala huo ndio
utakaohifadhi kikweli Waislamu na Wasokuwa Waislamu na kuwakinga dhidi ya shari za maadui zao.

KUMB: 04 / 1436 AH   
25th Muharram 1436 AH
18/11/2014 CE
Shabani Mwalimu
Mwakilishi kwa Vyombo Vya Habari Hizb ut-Tahrir Afrika
Mashariki



RASMI: JAJA AONDOKA YANGA: NAFASI YAKE YAPEWA MBRAZILI MWINGINE

Kiungo mkabaji raia wa Brazil Emerson De Oliveira Neves Rouqe anatarajiwa kuwasili siku ya jumanne mchana jijini Dar es salaam kwa ajili ya majaribio katika klabu ya Young Africans na endapo atafuzu moja kwa moja atajiunga na mabingwa mara 24 wa Ligi Kuu Tanzania bara.

Emerson mwenye umri wa miaka 24 ambaye kwa sasa anachezea timu ya Bonsucesso FC iliyopo ligi daraja la pili nchini kwao Brazil, msimu uliopita alikuwa akicheza soka la kulipwa nchini Poland katika timu ya Piotrkow Trybunalski FC iliyopo Ligi Daraja la pili nchini humo.

Ujio wa Emerson kuja kufanya majaribio nchini unakuja kufuatia mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Brazil pia Geilson Santos "Jaja" kushindwa kurejea nchini baada ya kwenda kwao Brazil na kutoa taarifa kwamba hataweza kurejea tena nchini kutokana kukabiliwa na matatizo ya kifamilia.
Awali ilikua familia ya Jaja ije nchini katika kipindi cha mapumziko, lakini waliomba yeye Jaja ndio aende Brazil na mara baada ya kufika huko matatizo ya kifamilia aliyokutana nayo yamepelekea kushindwa kurejea nchini
 kuitumikia klabu yake na kuomba abakie kwao kwa ajili ya kutatua matatizo hayo.
Kuondoka kwa Jaja kunafanya klabu ya Young Africans kubakia na wachezaji wanne tu wa kimataifa ambao ni Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hamis Kizza na Andrey Coutinho hivyo endapo Emerson atafuzu  atakuwaa
 anakamilisha idadi ya wachezaji watano wa kimataifa.

Endapo Emerson atafuzu majaribo pamoja na vipimo atajiunga na kikosi cha kocha mbrazil Marcio Maximo katika nafasi ya kiungo mkabaji ikiwa ni sehemu ya kuboresha timu kuelekea kwenye michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya kimataifa.
Aidha kikosi cha Young African baada ya kuwa mapumzikoni kwa takribani wiki mbili, kinatarajiwa kuanza mazoezi siku ya jumatatu katika Uwanja wa shule ya sekondari Loyola kujiandaa na mchezo wa Nani Mtani Jembe
pamoja na mzunguko wa nane wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania bara.


Sunday, November 9, 2014

MWANAMUZIKI MKONGWE AMIGOLAS AFARIKI DUNIA

AMIGOLAS
Mwanamuziki mkongwe wa Bendi ya Africans Stars maarufu kama Twanga pepeta amefariki dunia katika hospitali ya taifa ya Muhimbili.
Marehemu alipelekwa hapo akiwa nasumbuliwa na matatizo ya moyo.


PICHA YANGA ILIPO WAONESHA MGAMBO MATAA YA MJINI

Timu ya Young Africans Sports Club jana imewaonesha Mgambo JKT mataa ya mjini baada ya kuwachabanga mabao mawili kwa bila. Mabao ya Yanga yamefungwa na Simon Msuva katika kipindi cha pili.
Kiungo mbrazili Coutinho akitafuta njia ya kumtoka beki wa mgambo

Kikosi cha Yanga

Kikosi cha Mgambo JKT

Msuva akishangilia bao lake la pili




PICHA ZA BARABARA YA UKONGA MAZIZINI ILIYOTUMIA MILIONI 90 ILIVYO SASA



Hii ndiyo ile barabara ya Ukonga Mazizini- Moshi Bar ambayo inadaiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 90 kuikarabati kwa kiwango cha changarawe kwa umbali wa kilometa tatu. Picha hizi ni madimbwi ya mwanzo tu ya hizo kilometa tatu.



Meya Jerry Silaa wa Ilala ambaye ni Diwani wa Gongo la Mboto alipotembelea aliwaambia wananchi kuwa fedha za ujenzi huo ni kutoka mfuko wao. 
Picha zifuatazo ni za siku Meya Silaa alipotembelea ujenzi.



Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa jana amefanya ziara fundi ya ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Ukonga Moshi Bar ya kilometa 3 kwa kiwango cha changarawe awamu ya kwanza, ikiwa ni utekelezaji wa miradi ya dharura kulingana na uharibifu wa miundo mbinu uliotokea baada ya mvua kubwa kunyesha. Mradi huo unagharimu kiasi cha shilingi millioni 90. Pesa za ujenzi huo zinatoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Pia barabara hiyo itawekwa lami kwa awamu ya pili ndani ya mwaka huu kwa kilomita tatu.



Greda likirekebisha Barabara ya Ukonga-Mazizini kulekea Moshi Bar



Mwonekano wa barabara hiyo


SHEREHE ZA JANDO BUTIAMA



Wanamwita "Dokta" wa kijiji cha Ryamisanga wilayani Butiama akiendelea na shughuli yake ya kumtahiri kijana kwa dakika 17 bila ganzi.



Baadhi ya vijana ambao wameshatahiriwa wakimtizama mwenzao ambaye anafanyiwa tohara



"Dokta" akijiandaa kuifanya kazi yake




Mashuhuda







Baadaye ni vinywaji



Msosi kama huu pia ulikuwepo



Picha, maelezo na Shomi Binda: HIVI NDIVYO TOHARA ZA KABILA LA KIKURYA ZINAVYOFANYIKA

WIMBO AMBAO LOKASSA YA MBONGO AMEMUIMBIA RAIS KIKWETE





Saturday, November 8, 2014

HATIMAYE SITTI MTEMVU AACHIA TAJI

Katika hali isiyotarajiwa mlimbwende alichukua taji la urembo la Tanzania mwanadada Sitti Mtemvu ameachia taji hilo. Katika barua ambayo amewaandikia wandaaji wa shindano hilo ameeleza jinsi anavyo andamwa na watu mbalimbali juu ya umri wake.

Barua aliyo andika ni hiyo hapo chini


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU