Facebook Comments Box

Friday, October 31, 2014

BAADA YA LORI KUFELI BREAK USO KWA USO NA SIMBA MTOTO WAMI


Basi la Simba mtoto linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Tanga limegongana uso kwa uso na Lori la mizigo katikati ya Daraja la Mto Wami mkoani Pwani, Dereva wa lori hilo amefariki papo hapo na wengine kujeruhiwa.

Kitongoni blog inaendelea kutafuta taarifa zaidi za tukio hilo.

Wednesday, October 29, 2014

ROLI LA MAFUTA LAANGUKA NA KUUNGUA LOTE KIMARA KWA THOMAS

Lori la mafuta limeanguka na kuungua lote eneo la kimara kwa Thomas. Ajali hiyo imesababisha foleni kubwa kwa magari yanayo elekea kimara. Lori hilo limeanguka katika kituo cha magari yaendayo kasi. Hamna mtu alie jeruhiwa au kufa.




Tuesday, October 28, 2014

AJALI KONA YA JETI: LORI LAIANGUKIA HIACE


Kumetokea ajali mbaya mida hii maeneo ya Jeti Lumo mwisho wa lami ambapo gari kubwa la mizigo limeangua daladala iliyokuwa kituoni.


Ajali hiyo imetokea wakati gari hilo semi-trailer ikikata kona pale mwisho wa lami ambapo kontena lilianguka na kutua juu ya bodi ya daladala.


Mtoa taarifa wangu amesema hali ni mbaya na bado hajajua idadi ya vifo na majeruhi ujumla.Pia gari imepondeka sana jambo ambalo linaashiria hatari zaidi.


Kuna gari la kunyanyua makontena limeshafika pale lakini limeshindwa kutoa msaada wa uhakika kutokana na kuzidiwa uzito na kontena ambapo likijaribu kunyanyua kontena ushuka.

Hamna mtu yoyote aliepoteza maisha maana Hiace hiyo ilikuwa imepaki kusubiri muda wake wa kupakia abiria.



ABUBAKAR SALUM "SURE BOY" ACHAGULIWA MCHEZAJI BORA WA OKTOBA



Bodi ya ligi kuu soka Tanzania bara TPL Bord imemtangaza mchezaji  wa Azam FC Salum Abubakar  ‘Sure  Boy’ kuwa mchezaji bora wa mwezi oktoba katika ligi kuu soka Tanzania Bara.

Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Bodi ya ligi, Mkurugenzi wa Masindano wa TFF Boniface Wambura amesema mchezaji uyo amechaguliwa baada ya kuwasinda kwa vigezo wachezaji wenzake katika michezo ya mwezi  uu wa oktoba.
Mwezi  uliopita  mchezaji  wa Mbeya City Antony Matogolo aliibuka  mchezaji bora wa  mwezi  septemba na kuambulia  kitita cha shilingi milioni moja.


NAHODHA NA GOLIKIPA WA AFRIKA KUSINI AUAWA NCHINI HUMO



Nahodha na golikipa wa timu ya Taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa enzi za uhai wake.

Nahodha na golikipa wa timu ya Taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa amefariki dunia baada ya kupigwa risasi. Jeshi la polisi la nchi hiyo limesema. Tukio hilo limeripotiwa kutokea katika nyumba ya mpenzi wake iliyopo katika mji wa Vosloorus kusini mwa Johannesburg.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliichezea klabu ya Orlando Pirates na alicheza mechi nne zilizopita za timu yake ya taifa katika mechi za kufuzu za fainali ya mataifa ya Afrika.

Jumamosi alikuwepo katika tukio la timu yake pindi waliposonga mbele katika nusu fainali ya ligi ya Afrika kusini.
Katika maelezo yake Jeshi la polisi la afrika kusini limesema kwamba Meyiwa ameripotiwa kufariki wakati akiwasili hospitalini.

Chanzo: BBC

Sunday, October 26, 2014

SIMBA YAWASIMAMISHA KIEMBA,KISIGA NA CHANONGO

AMRI KIEMBA
Klabu ya Simba SC imewasimamisha wachezaji wake watatu kutokana na kile ninachodhaniwa wachezaji hao kuwa sehemu ya klabu hiyo kufanya vibaya, wachezaji waliosimamishwa ni viungo Amri Kiemba,Shabani Kisiga na Haruna Chanongo,hapo jana jijini Mbeya Simba ililazimishwa sare ya tano msimu huu na Prisons.
Shabaan Kisiga

Taarifa kutoka chanzo cha kuaminika ndani ya klabu hiyo kinasema pia benchi la ufundi limepewa changamoto ya kuakikisha timu hiyo inakusanya pointi tisa  kutoka kwenye michezo mitatu inafuata kama ikishindikana basi benchi Zima la ufundi nalo litapigwa chini.

Habari zaidi zikisema kuwa mshambuliaji wa kigeni Hamis Tambwe akipewa onyo kwa kuhusishwa na Simba ukawa huku Ramadhan Singano nae akipewa onyo kali pia.

 Kocha msaidizi Matola na mtoa tiba kwa vitendo Bwana Gembe wamesimamishwa kwa muda usio julikana.


PICHA: MAADHIMISHO YA GROUP LA KANDADA: TEAM ISMAIL YAFUNGWA NA TEAM DIZO MOJA

Katika maadhimisho ya Group la kandanda la Facebook kutimiza miaka minne. Ilifanyika mechi kati ya Team Ismail na Timu Dizo moja. Team Dizo iliibuka na ushindi wa magoli manne kwa moja. Team zote zilionesha soka safi na la kupendeza.

chini ni picha za bonanza hilo.

mtanange ukiendelea

Kipindi cha Pili Nassoro Binslum akiwa tayari kuanza kazi


wakati wa zawadi







wakishangilia ushindi wa taem Dizzo one





keki na kombe

mameneja wa timu mbili wakipongezana


mfungaji wa mabao matatu "hat trick" akipewa zawadi ya mpira

keki ikikatwa


Patrick Dumulinyi muanzilishi wa group la kandanda akilishwa keki



STAND UNITED WAKIINGIA UWANJANI NA TINGATINGA WAKIWA NA MBUNGE WAO

Hii ndio njia ambayo stand united waliitumia kuingia uwanjani. Mwenye shati la kitenge ni mbunge wa shinyanga mjini ambae pia ni Naibu waziri mh Masele. 

Hii inatakiwa kukemewa ni hatari.





Friday, October 24, 2014

KUELEKEA EL CLASICO ANGALIA PREVIEW HII



HATIMAYE DIAMOND ASALIMISHA SARE ZA JESHI

Kushoto ni Ney wamitego, Diamond Platnum, na Dancer wa Diamond wakiwa katika jukwaa la Fiesta hivi karibuni wakiwa wamevalia mavazi ya Jeshi.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul 'Diamond', amekiri kuhojiwa na polisi baada ya kukutwa na hatia ya kuvaa mavazi yanayoaminika kuwa ni sare ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Hata hivyo msanii huyo alidai kwamba mavazi hayo hayakuwa sare za jeshi hilo na kwamba yeye aliyanunua alipokuwa Ujerumani ingawa baada ya kuhojiwa aliyasalimisha.

Diamond alipanda jukwaani Jumamosi iliyopita katika onyesho la Fiesta jijini Dar es Salaam akiwa na mavazi hayo jambo ambalo liliibua mjadala kwa watu walio wengi.

Diamond alikiri kupata ujumbe uliomtaka kufika Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam na madansa wake akiwa na nguo hizo,
"Awali Meneja wangu alishikiliwa kwa muda na mimi nikatakiwa kufika na zile nguo nikiwa na madansa wangu ambao pia walizivaa, nilifanya hivyo na kuziacha nguo baada ya taratibu zote za kisheria kukamilika," alisema.

"Nisingeweza kukaidi amri ya dola, nilifika na yale mavazi na nikahojiwa kwa saa kadhaa. Nikaeleza kwamba yalikuwa yakifanana tu na ya jeshi na hayakuwa sare rasmi za jeshi, kikubwa nilihitaji kumaliza tatizo," alisema.



Q.CHILLAH AELEZEA NANI MKALI KATI YA DIAMOND NA ALI KIBA

Msanii wa Bongo Fleva Q. Chillah

Mapya yanazidi kuibuka kuhusu ushindani wa Diamond na Ali Kiba ambapoushindani huo ulianzia katika hitimisho la tamasha la Fiesta lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club Dar. 

Mashabiki wa wasanii hawa wawili wanavutana huku kila mmoja akisema mwenzake ana kipaji na anamfunika mwenzake. Inasemekana kuwa kuna baadhi ya mashabiki walikodiwa kwa ajili ya kumzomea Diamond wakati akitoa burudani siku ya Fiesta na hilo lilithibitishwa na Babu Tale ambaye ni meneja wa Diamond.

kwa sasa katika mziki wa Bongo Flava kumekuwa na fitina nyingi wakati mwingine wasanii kwa wasanii wanachonganishwa na mwisho wa siku unakuwa ugomvi, kwa mfano sasa hivi bifu la Ali Kiba na Diamond.

Q Chief : "Yote wanayopitia ni changamoto ambazo pengine hawakuwahi kuzania kwamba watapitia. Mimi nimepitia situation ambazo zimenijenga kuwa "sugu" na "Legendary" ndiyo maana ya kuwa mkongwe unapitia situation ambazo watu wengine wanakulazimisha ufike huko. 

Hata kama upo level fulani wanakushusha kwa kufikiria kwamba wanaweza kukushusha. Unapandishwa na watu, unapandishwa na mwenyezi Mungu, unashushwa na watu, unashushwa na mwenyezi Mungu. 

Mfano niliangalia Fiesta kwenye TV sikwenda kwa sababu nilikuwa na mambo yangu Studio, hakuna kitu kigeni nlichokiona, nimeona msanii wa marekani anafunikwa na msanii wa Tanzania ambaye ni Ali Kiba. 

Nmeona Ali Kiba ambaye amekaa kimya kwa miaka mitatu bila Airtime na watu wamemzungumzia vibaya, vizuri na nini wamemkubali tena. Ikiwa ni mtu yule yule ambaye wamemkataa na wakumuweka mtu mwingine juu. 

Hakuna kitu kisichowezekana, matokeo uliyoyaona juzi ndio matokeo yanayotokea na yataendelea kutokea. Hakuna Mungu wa hii kazi, hakunaga mfalme wa hii kazi ila kuna masultan wa Hii Kazi.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU