Facebook Comments Box

Thursday, September 4, 2014

MTUHUMIWA WA UGAIDI AONESHA ALIVYO LAWITIWA NA POLISI

NA KULWA MZEE, DAR ES SALAAM

MMOJA wa watuhumiwa wa ugaidi katika kesi
inayomkabili Kiongozi wa Jumuiya za Uamsho na
Mihadhara ya Kiislamu (JUMIKI) Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmed (43), amevunja ukimya mahakamani baada ya kuonyesha suruali ilivyolowa kwenye makalio akisema ni madhara ya kulawitiwa na kuingizwa miti na polisi.

Mshtakiwa huyo, Salum Ally Salum, aliamua kufanya hivyo jana ili kuithibitishia mahakama kile walichodai ni unyama waliotendewa na polisi wakati wakihojiwa.
“Mheshimiwa hakimu, angalia (anageuka na kuinua suruali katika eneo la makalio), haya ndiyo madhara niliyopata kwa kuingiliwa nyuma na kuingizwa jiti,” alidai.

Baada ya mshtakiwa huyo kuzungumza, Hakimu Hellen Riwa alimshauri kutoa taarifa kwa uongozi wa Magereza ili aweze kupata matibabu ya haraka kwani akiendelea kukaa hivyo anaweza kupata madhara makubwa.
Kwa upande wake, Sheikh Farid, alimuomba Rais
Jakaya Kikwete kuunda tume huru ya kuchunguza vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa.

Sheikh Farid aliieleza mahakama kuwa Tanzania
hakuna ugaidi, na kwamba balaa hilo lisiombwe
kutokea hapa nchini. Alisema kuwa yanayowakuta hivi sasa ni kutokana na
kudai mamlaka ya nchi yao kwani kuna mgogoro
mkubwa unaoendelea. Sheikh Farid alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Hellen Riwa, wakati kesi yake na wenzake 19 ilipokuwa ikitajwa na kuunganishwa na washtakiwa wengine wawili, Sheikh Mselem Ali Mselem na Abdallah Said Ali.
“Mheshimiwa Hakimu, naomba mahakama ikunjue kifua itusikilize tunayotaka kusema, tunataka ufafanuzi kutoka kwako, kwanza nathibitisha kwamba madhila, unyanyasaji, ukatili tulifanyiwa na polisi wakati wa mahojiano.
“Tatizo letu mheshimiwa ni matibabu, gerezani hakuna matibabu, kuna wenzetu tangu tulipoingia humo miezi miwili sasa, wanalala hospitali, dawa hakuna, inafikia hatua tunaagiza kutoka nje.
“Mheshimiwa hali ni mbaya, watu wanatokwa hadi na usaha, yote hayo ni kwa sababu ya ukatili waliotufanyia polisi, tutakapokwenda katika Mahakama Kuu ya Tanganyika iliyovaa koti la Tanzania tutazungumza mengi.

“Tunahitaji iundwe Tume Huru ya Uchunguzi,
tunaomba Rais Kikwete aunde tume yenye haki, tume ndiyo itatoa ukweli, hiki ndicho kilio chetu.
“Niliuliza hapa mahakamani Zanzibar ni nchi? Yule rais ni rais wa timu ya mpira?” alihoji Sheikh Farid.
Alidai sheria ya ugaidi ni sheria ya dhuluma ambayo ipo kwa ajili ya kuwanyonga Waislamu na kwamba kuna mgogoro mkubwa wa Utanganyika.

“Tanzania hakuna ugaidi hapa, tusiombe balaa hilo, sisi kosa letu ni kudai mamlaka ya nchi yetu,” alidai.
Hakimu Riwa akijibu hoja ya Sheikh Farid, alisema mahakama imewaruhusu kuandika barua kuomba kuundwa kwa tume huru kisha mahakama itajua pa kuipeleka.

Kabla ya kuwasilisha hoja hizo za malalamiko,
washtakiwa walibadilishiwa mashtaka na kusomewa upya mashtaka manne na mawakili wa Serikali, Peter Njike na George Barasa.
Inadaiwa katika shtaka la kwanza, washtakiwa wote kwa pamoja kati ya Januari 2013 na Juni 2014 maaeneo mbalimbali ndani ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, walikua njama na kuingiza watu nchini kushiriki vitendo vya kigaidi.

Katika shtaka la pili, washtakiwa wote wanadaiwa kuwaingiza watu nchini kushiriki vitendo vya ugaidi huku wakijua ni kosa.
“Mheshimiwa, shtaka la tatu linamkabili mshtakiwa Farid na Mselem, mnadaiwa kati ya Januari 2013 na Juni 2014, maeneo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mliwaajiri Sadick Absaloum na Farah Omary kushiriki kutenda vitendo vya kigaidi.

“Shtaka la nne linamkabili Farid, unadaiwa kuhifadhi watu waliotenda vitendo vya kigaidi, huku ukijua ni kosa. Ulimuhifadhi Sadick Absaloum na Farah Omary huku ukijua kwamba walitenda ugaidi,” alidai Balasa. Washtakiwa hawakutakiwa kujibu lolote, upelelezi wa kesi haujakamilika. Mahakama iliahirisha kesi hiyo
hadi Septemba 17, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Jamal Swalehe, Nassoro Abdallah, Hassan Suleiman, Anthari Ahmed, Mohammed Yusuph, Abdallah Hassani, Hussein Ally, Juma Juma.
Wengine ni Saidi Ally, Hamisi Salum, Saidi Amour
Salum, Abubakar Mngodo, Salum Ali Salum, Salum Amour Salum, Alawi Amir, Rashid Nyange, Amir Hamis Juma, Kassim Nassoro, Said Sharifu, Sheikh Mselem Ali Mselem na Abdallah Said Ali.

 CHANZO: MTANZANIA


AKAMATWA BAADA YA KUJIFANYA AFISA USALAMA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
PRESS RELEASE
02/09/2014
 
ANAYEJIFANYA AFISA USALAMA WA TAIFA ANASWA DAR ES SALAAM

Mtu mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda
Maalum Dar es Salaam kutokana na makosa mbalimbali ya kujifanya ni mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa. Mtu huyo anayejulikana kwa jina la GUNNER S/O SAIMON MEENA, Miaka 40, Mkazi wa Kinyerezi Segerea anatuhumiwa kuwasumbua wafanyabiashara mbalimbali jijini Dar es Salaam kwa kuwasingizia au kuwatuhumu kwamba wanahusika na makosa yenye kuhatarisha usalama.

Kwa muda mrefu Jeshi la Polisi limekuwa likimtafuta mtu huyo kutokana na malalamiko mengi ambayo yamekuwa yakijitokeza na uchunguzi unaonyesha kwamba jina lake halipo katika orodha ya watumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Tukio la mwisho lililomfanya akamatwe ni pale
alipomtishia mfanyabiashara mwenye asili ya Kisomali aitwaye ABDI S/O MOHAMED DALMAR. Katika tishio hilo la kutishia mtuhumiwa GUNNER S/O SAIMON MEENA ambaye ni Afisa Usalama feki alidai apatiwe kiasi cha fedha za kitanzania T SHS 25,000,000/= (SHILINGI MILLIONI ISHIRINI NA TANO) ama sivyo angechukuliwa
hatua chini ya sheria ya Usalama wa Taifa.

Mlalamikaji alitoa taarifa na ndipo mtuhumiwa
akakamatwa katika mtego wa Polsi. Uchunguzi zaidi wa shauri hili unafanyika na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya jalada la kesi yake kupitiwa na mwanasheria wa Serikali.

S. H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM


MAGAZETI YA LEO: ALHAMISI 04/09/2014




Wednesday, September 3, 2014

MAGAZETI YA LEO: JUMATANO 03/09/2014




DR SLAA ATOA MSAADA WA MADAWATI MTAMBANI

Dr Willibrod Slaa jana amekabidhi Madawati 60 kwa Shule ya
Mvumoni Seminary iliyoko Msikiti wa Mtambani Kinondoni.
Msaada huu ni kutimiza ahadi aliyoitoa Dr. Wilbrod Slaa Katibu Mkuu wa chadema kwa niaba ya chama alipotembelea msikiti huo kutoa pole za Chama kutokana na ajali ya moto iliyoteketeza mali mbalimbali pamoja na madawati 60 ambayo yalikuwa yakitumika na wanafunzi wa kidato cha nne msikitini hapo.

msikiti wa mtambani ulipata ajali ya moto siku kadhaa zilizopita na kusababisha hasara kubwa lakini cha muhimu ilikuwa ni kuwawezesha wanafunzi wa kitado cha nne shuleni hapo ambao tayari wameanza mitihani juzi.



Tuesday, September 2, 2014

MAGAZETI YA LEO: JUMANNE TAREHE 02/09/2014




ORODHA YA WACHEZAJI WALIOSAJILIWA ULAYA

PREMIER LEAGUE
 
Falcao (Monaco to Manchester United) Loan - reported fee £6m
 
Danny Welbeck (Manchester United to Arsena) £16m
 
Daley Blind (Ajax to Manchester United) £14m
 
Abel Hernandez (Palermo to Hull City) Undisclosed, reported to be £9.5m
 
Hatem Ben Arfa (Newcastle to Hull City) Loan
 
Ricardo Alvarez (Inter Milan to Sunderland) Loan
 
Sebastian Coates (Liverpool to Sunderland) Loan
 
Nathaniel Chalobah (Chelsea to Burnley) loan
 
George Boyd (Hull to Burnley) £3million
 
Modibo Diakite (released by Sunderland) Free
 
Modou Barrow (Ostersunds FK to Swansea) Undisclosed
 
Benjamin Stambouli (Montpellier to Tottenham) Undisclosed
 
Sebastian Coates (Liverpool to Sunderland) Loan
 
Mohamed Diame (West Ham to Hull) Undisclosed
 
Zeki Fryers (Tottenham to Crystal Palace) £3m
 
Sandro (Tottenham to QPR) £10m
 
Gaston Ramirez (Southampton to Hull) Loan
 
Oussama Assaidi (Liverpool to Stoke) Loan
 
James McArthur (Wigan to Crystal Palace) £7m
 
Niko Kranjcar (Dynamo Kiev to QPR) Loan
 
Kevin Doyle (Wolves to QPR) Loan
 
Morgan Amalfitano (Marseille to West Ham) Undisclosed
 
Toby Alderweireld (Atletico Madrid to Southampton) Loan
 
Sadio Mane (Red Bull Salzburg to Southampton) £11.8m
 
Tom Lawrence (Manchester United to Leicester) £1m
 
Nick Powell (Manchester United to Leicester) Loan
 
Michael Keane (Manchester United to Burnley) Loan
 
LA LIGA
 
Javier Hernandez (Man Utd - Real Madrid) Loan
 
Alessio Cerci (Torino to Atletico Madrid) undisclosed
 
Yassine Bounou (Atletico Madrid to Real Zaragoza) loan
 
Jose Canas (Swansea to Espanyol) Free
 
Alvaro Negredo (Manchester City to Valencia) Initial loan, obligation
to buy £23.7m
 
SERIE A
 
Marco van Ginkel (Chelsea to AC Milan) Loan
 
Saphir Taider (Southampton to Inter) Loan return
 
Javier Saviola (Olympiacos to Verona) Undisclosed

Giacomo Bonaventura (Atalanta to AC Milan) €7m

Joao Pedro (Estoril to Cagliari) Exchange for Matias Cabrera

Micah Richards (Manchester City to Fiorentina) Loan

Mapou Yanga-Mbiwa (Newcastle to Roma) Loan

Djamel Mesbah (Parma to Sampdoria) Undisclosed

Juan Antonio (Sampdoria to Parma - loan to Feralpi Salò) Undisclosed

Marco Donadel (Napoli to free agent)

BUNDESLIGA

Julian Green (Bayern Munich to Hamburg) Loan

Lewis Holtby (Tottenham to Hamburg) Loan

LIGUE 1

Valentin Roberge (Sunderland to Reims) Loan

Benjamin Stambouli (Montpellier to Tottenham) Undisclosed

Carlos Eduardo (Porto to Nice) Loan

Doria (Marseille to Brazil) Undisclosed

CHAMPIONSHIP

Ignasi Miquel (Arsenal to Norwich) £1m

Shane Duffy (Everton to Blackburn) Undisclosed

Jelle Vossen (RC Genk to Middlesbrough) Loan

Adam Forshaw (Brentford to Wigan) Undisclosed

Andy Delort (Tours to Wigan) Undisclosed

Brian Montenegro (Nacional Asuncion to Leeds) Loan

Royston Drenthe (Reading to Sheffield Wednesday) Loan

Bruno Ecuele Manga (FC Lorient to Cardiff City) Reported fee £5m

William Kvist (Stuttgart to Wigan) Undisclosed

Danny Gabbidon (Unattached to Cardiff City) Free

Souleymane Doukara (Catania to Leeds) Undisclosed

Jamal Blackman (Chelsea to Middlesbrough) loan

Emyr Huws (Manchester City to Wigan) Undisclosed

Matt Smith (Leeds to Fulham) Undisclosed

Jos Hooiveld (Southampton to Norwich) Loan

Glenn Murray (Crystal Palace to Reading) Loan

Frank Nouble (Ipswich to Coventry) Loan

Louis Thompson (Swindon to Norwich) Undisclosed, loaned back

Ryan Tunnicliffe (Fulham to Blackburn) Loan

Matt Smith (Leeds to Fulham) Undisclosed

Jason Steele (Middlesborough to Blackburn) Loan

Mark Hudson (Cardiff to Huddersfield) Undisclosed

SELECTED OTHERS

Emmanuel Frimpong (Unattached to FC Ufa) Free

Karim El Ahmadi (Aston Villa to Feyenoord) Undisclosed

Jonathan Obika (Tottenham to Swindon) Undisclosed

Tomislav Gomelt (Tottenham to Bari) Loan

Souleymane Coulibaly (Tottenham to Bari) Undisclosed

Matej Delac (Chelsea to Arles) Loan

Holmbert Fridjonsson (Celtic to Brondy) Loan

Dylan McGeouch (Celtic to Hibernian) Loan

Ryo Miyaichi (Arsenal to FC Twente) Loan

Raul Rusescu (Sevilla to Steaua Bucharest) Loan

John Arne Riise (APOEL) Free

Blerim Dzemaili (Napoli to Galatasaray) Undisclosed

Goran Pandev (Napoli to Galatasaray) Undisclosed

Stefan Scepovic (Sporting Gijon to Celtic) £2.3m

Jose Campana (Sampdoria to FC Porto) Loan

Alex Kacaniklic (Fulham to Copenhagen) Loan


Monday, September 1, 2014

TAARIFA YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA JUU YA UPEPO MKALI




MAKOMANDOO WA NEPAL WALINDA NYUMBA YA MNYARWANDA KARIBU NA AIRPORT

Komandoo Sidhee Bahadurkatuwal (kulia) kutoka Nepal akionesha nyumba ya Mrwanda aliyokuwa akiilinda kupitia kampuni ya Ulinzi ya Advanced Security karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam,

akiwa na makomandoo wenzake kutoka Nepal,
Maofisa wa Uhamiaji wakimhoji mama wa kitanzania
aliyeolewa na mnyarwanda ambao nyumba yao ilikuwa
ikilindwa na Komandoo kutoka Nepal

Baadhi ya makomandoo wa kijeshi kutoka Nepal wakiwa
wamevalia sare ya Kampuni ya Ulinzi ya Advanced katika
nyumba hiyo.


MAGAZETI YA LEO: JUMATATU 01 SEPTEMBA 2014




Sunday, August 31, 2014

MWANAZUONI MKUBWA ALHABIB UMAR IBN HAFIDH AWASILI KENYA

Mwanazuoni Mkubwa duniani Alhabib Umar bin Salim bin Hafidh jana amewasili jijini Nairobi Kenya katika ziara ya mwaliko wa Sheikh Al-Amoudy ambapo atakuwa nchini humo kwa muda wa wiki moja.




Katika ziara hiyo Alhabib Umar atafungua Markaz ya Dar Al-Mudathir iliyoko Malindi ambapo ni tawi la chuo cha Dar al Mustafa kilichoko Yemen. Mbali na Nairobi na Malindi sehemu zingine atakazotembelea ni Eldoret,Mombasa na atafungua misikiti kadhaa.




Angalia ziara yake kamili Alhabib Umar hapo chini.

-SAT. 30th AUG. -NAIROBI
Arrival: 7PM
-SUN.31st AUG. -NAIROBI/MALINDI
Muslim Children's Home & Imtiaz Sunni MOsque in Nairobi:AM

Flight to Malindi:PM

-MON. 1st SEP. -MALINDI/MAMRUI/MALINDI
Ziyara of Ash-Sharif Sa'eed al-Beidh, Mamrui:AM
Opening of Dar al-Mudathir, branch of Dar al-Mustafa, Malindi:PM
Opening forum with scholars and public, Malindi: 4:15PM

-TUESDAY 2nd SEPT. - MALINDI/MOMBASA

Opening of Masjid Abu Bakr Siddiq at Kwachocha, Malindi: 11AM
Programme at Masjid Konzi, Mombasa: 6:45PM

-WED. 3rd SEPT. - MOMBASA

Opening of Masjid Nur, Kikambala: 11AM
Hawl of Imam al Haddad RA at Memon Villa Hall: 6:45PM
-THUR. 4th SEPT. -MACKINNON RD/MAKINDU
-FRI. 5th SEPT. -MAKINDU/ELDORET
Jumuah at Makindu: 12:30PM
Flight to Eldoret from Nairobi: PM
-SAT. 6th SEPT. -ELDORET/NAIROBI
Opening of Majma'ul Khayrat Insitute, Eldoret: AM


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU