Facebook Comments Box

Sunday, August 31, 2014

YANGA YATANGAZA KAMATI ZAKE

Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Wajumbe Wenza wa Kamati ya Utendaji ya YANGA (Maendelo ya Michezo), Ndugu Seif Ahmed na Engineer Isaac Chanji, wanapenda
kutoa taarifa kupitia vyombo vya habari kwa wanaYANGA,
wameunda Kamati ndogo chini ya Kamati ya Utendaji ya YANGA zifuatazo:
 
1) KAMATI YA UFUNDI
 
Wajumbe:
1) Duduma, Nassoro
2) Lamlembe, Roger
3) Malulu, Pascal
4) Msolla, Peter
5) Zangira, Steve
 
2) KAMATI YA SOKA YA VIJANA NA WANAWAKE
Wajumbe:
1) Katwila, Shaban
2) Kabisa, Jessica (Advocate)
3) Mazwile, Isack
4) Mwita, George
5) Tembele, Ally Mayay
 
3) KAMATI YA MASHINDANO
Wajumbe:
1) Cheyo, Magembe
2) Didi, Ibrahim
3) Hussein, Ndama Risasi
4) Katabalo, Moses
5) Katunzi, Mudhamiri
6) Kihanga, Pascal
7) Kingo, Ray Shauri
8) Kleb, Abdallah Bin
9) Luhago, David
10) Lukumay, Samwel
11) Macha, Innocent
12) Maige, Jackson
13) Mahende, Mugaya
14) Makay, Sule
15) Malebo, Michael
16) Malume, Paul
17) Matata
18) Mbise, Anandumi Timothy
19) Mlangwa, David
20) Mogha, John
21) Mutaboyerwa, Joseph John
22) Ntimizi, Said
23) Nyambaya, Lameck
24) Nyika, Hussein
25) Nyumbamkaly,
26) Ramadhan, Fulgence
27) Rashid, Ahmed
28) Suleman, Majid
29) Tenga, Frank
30) Tindwa, Beda
31) Zakaria, Dr.
 
Ifahamike kwamba, kutakuwa na nyongeza ya uteuzi wa Wajumbe wengine wa Kamatiza YANGA zilizotajwa hapo juu.
Ndugu Seif Ahmed na Engineer Isaac Chanji Wajumbe Wenza wa
Kamati ya Utendaji ya YANGA (Maendelo ya Michezo) watakuwa
Wenyekiti Wenza wa Kamati zilizotajwa hapo juu.
Kamati ya Utendaji ya YANGA, ina karibisha Wajumbe waliotajwa
katika Kamati zilizotajwa hapo juu kwa dhamira njema kuwa
watasaidia kujenga YANGA bora, na wanaomba ushirikiano kutoka
kwa wanaYanga wote ili Wajumbe walioteuliwa waweze ketenda
kazi zao vyema kwa manufaa ya YANGA.
(YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO)
(BENO NJOVU)
KATIBU MKUU WA YANGA


SIMBA YAVUNA MAGOLI KWA KMKM

Beki wa Simba "baba ubaya" akipambana na mchezaji wa KMKM
SIMBA SC imewafunga mabingwa wa Zanzibar, KMKM mabao 5 - 0 katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara usiku huu uwanja wa Amaan,Zanzibar.

KMKM inayofundishwa na Ally Bushiri ‘Bush’ ambayo Jumatano wiki hii ilifungwa 2 - 0 na Yanga SC, leo iligeuzwa asusa na Wekundu wa Msimbazi.

Simba SC ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza mabao 4-0, yaliyotiwa kimiani na Hamis Tambwe mawili, Amir Kiembe na Shabaan Kisiga 'malone' moja kila mmoja.

Viongozi wa Simba wakiongozwa na Hans pope
Amri Kiemba ndiye aliyefungua karamu ya mabao ya Simba SC hii leo, dakika ya tatu ya mchezo baada ya kupewa pasi nzuri na kiungo Mrundi, Pierre Kwizera na kuwatoka wachezaji wawili wa KMKM kabla ya kufumua shuti kali lililogonga mwamba wa ndani wa lango.

Amisi Tambwe akafuatia dakika ya 14 baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa Salim Amour kufuatia yeye mwenyewe kupiga mkwaju wa penati, baada ya Kiungo Haroun Chanongo kuangushwa kwenye boksi.

Tambwe tena akafunga bao la tatu dakika ya 23 akimalizia krosi maridadi ya Ramadhan Singano 'Messi' kabla ya kisiga kufunga la nne dakika ya 37, kufuatia kazi nzuri ya Kiemba.

Mchezaji ambae yupo katika mgogoro na ambae hajajua hatma yake kama atacheza au hata cheza ligi Emmanuel Okwi akiwa katika benchi la simba akiangalia kama anaweza kupata namba katika kikosi hicho cha Simba.
Kipindi ha pili, kocha Mzambia, Patrick Phiri alibadilisha kikosi kizima akimuacha Nahodha Joseph Owino na dakika ya 60 Elias Maguri akahitimisha karamu ya mabao kwa bao safi la tano.

Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi aliyetangaza juzi kurejea Simba SC kutoka kwa mahasimu wao Yanga SC usiku wa jana alikuwepo, lakini alibaki benchi muda wote wa mchezo.

Hamis Tambwe na Singano wakishangilia Goli
Viongozi wa Simba SC wakiongozwa Makamu wa
Rais, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ na Mwenyekiti
Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe, Kassim
Dewji, Musley Ruwey, Mohammed Nassor ‘Steven
Seagal’, Crescentius Magori, Said Tuliy na
wengineo walikuwepo kushuhudia mchezo huo.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa:
Ivo Mapunda/
Hussein Sharrif ‘Cassilas’ dk46/Peter Manyika
dk84, Miraj Adam/Abdi Banda dk46/Nassor
Mssoud ‘Cholo’dk84, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’/
William Lucian ‘Gallas’ dk46/Mohammed Hussein
‘Tshabalala’ dk84, Joram Mgeveke/Hassan Isihaka
dk46, Joseph Owino, Pierre Kwizera/Abdallah
Seseme dk46, Haroun Chanongo/Twaha Ibrahim
‘Messi’ dk46, Amri Kiemba/Ibrahim Hajibu dk46,
Amisi Tambwe/Elias Maguri dk46, Shaaban Kisiga
‘Malone’/Awadh Juma dk46 na Ramadhani Singano
‘Messi’/Uhuru Suleiman dk46.
KMKM; Salim Amour, Pandu Hajji, Faki Hamad/
Makame Hajji dk30, Juma Rashid/Nassor Ali dk30,
Halfan Khamisi/Mudrik Muhibu dk30, Moka
Shaaban, Ame Khamis, Abdi Kassim ‘Babbi’, Haji
Simba/Kassim Nemshi dk30, Maulid Ibrahim na
Khamis Ali.


WAZIRI MKUU AKIMBILIA AFRIKA YA KUSINI

Jeshi la Lesotho
Sawa Waziri mkuu nchini Lesotho Tom Thabane ameiambia BBC kwamba amelitoroka taifa hilo baada ya kupata vitisho vya maisha yake.

Akizungumza kutoka nchini Afrika kusini,Bwana Thabane amesema kuwa vitendo vya jeshi nchini humo vya kusitisha huduma za serikali na kusababisha mapinduzi.
 
Awali Ripoti kutoka mji mkuu wa maseru zilisema kuwa jeshi lilizingira makao makuu ya polisi na kuzuia matangazo ya radio pamoja na mtandao wa simu katika mji mkuu wa Maseru.

Uchaguzi uliozongwa na utata nchini humo miaka miwili iliopita ulisababisha kuundwa kwa serikali ya muungano isio dhabiti.
Licha ya mazungumzo ya kuleta amani mnamo mwezi Juni ,hali ya wasiwasi ilitanda huku majirani wa taifa hiilo wakionya dhidi ya
mbinu yoyote isio ya kikatiba.
 
Taifa hilo limezungukwa na Afrika kusini na hutegemea sana jirani yake kwa maslahi pamoja na nafasi za kazi.

Chanzo: BBC SWAHILI


Saturday, August 30, 2014

HII NDIO TIMU ANAYOENDA RADAMEL FALCAO

Mchezaji wa Monaco Radamel Falcao ameuthibitishia ulimwengu kuwa atajiunga na Madrid. Mchezaji huyo alituma ujumbe wa furaha katika akaunti yake ya tweeter na baadae kuufuta ujumbe huo ila tayari watu tulikuwa tumesha upiga picha.
 Wadadavuaji wengine wanasema huenda akaunti yake itakuwa imetekwa na maharamia wa mtandao maarufu kwa jina la kiingereza la "hackers "
Chini ni picha ya ujumbe huo.




RAIS KIKWETE ATEMBELEA SOKO LA MAZAO KIBAIGWA



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea soko la nafaka la kimataifa la Kibaigwa mkoani Dodoma katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo Agosti 28, 2014 , ambapo alijionea shehena kubwa sana ya mahindi iliyoletwa kutoka mashambani na kusafirishwa kila pembe ya nchi. Mwaka huu, kama ilivyokuwa mwaka jana, mavuno ya mahindi yamekuwa makubwa kiasi hata cha kupatikana kwa mavuno ya ziada yanayolemea maghala yaliyopo, ikiwa ni muendelezo wa mafanikio ya sera ya kilimo kwanza ambayo imekuwa ikileta matokeo mazuri kila mwaka. (picha hii na zote zinazofuata hapo chini ni kutoka Ikulu).














SALUM MWALIMU ACHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA CHADEMA

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA Zanzibar Bi Maryam Ahmed Omar akimkabidhi fomu Salum Mwalim fomu ya kugombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho kundi la Zanzibar katika hafla fupi iliyofanyika ofisi kuu za CHADEMA kisiwani humo.

Mmoja wa wachama wa CHADEMA Zanzibar Bikwao Khamis akitia saini ya fomu ya udhamini wa Salum Mwalim (aliyesimama wa kwanza kushoto) anaegombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho kundi la Zanzibar. Mwalim alichukua na kurudisha fomu hiyo Jumamosi Agosti 30, 2014 katika Ofisi za Chadema Zanzibar

Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Jumbe Idrisa akitia saini ya fomu ya udhamini wa Salum Mwalim (aliyesimama wa kwanza kushoto) anaegombea nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu ya chjama hicho kundi la Zanzibar. Mwalim alichukua na kurudisha fomu hiyo Jumamosi Agosti 30, 2014 katika Ofisi za Chadema Zanzibar

Salum Mwalim anayewania nafasi ya ujumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA kundi la Zanzibar akitia saini kitambu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi kuu za chama hicho Zanzibar kwa lengo la kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

Mbunge wa CHADEMA viti Maalum wa CHADEMA Mwanamrisho Abama akimdhamini Mgombe Ujumbe wa Kamati Kuu wa Chama hicho Salum Mwalim katika ofisi za chama Zanzibar. Mwalim alichukua na kurudisha fomu hiyo Jumamosi Agosti 30, 2014 katika Ofisi za CHADEMA Zanzibar.


MAJAMBAZI YABAKA NA KUPORA MILIONI 20

Watu wanaosadikiwa kuwa majambazi wanadaiwa kumvamia mwalimu mmoja, wampora zaidi ya Sh. milioni 20 na kumbaka
mwalimu mwingine na kutokomea.

Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Nassa Ginery, wilayani Busega mkoani Simiyu.
Polisi mkoa wa Simiyu imethibitisha kutokea kwa tukio hilo usiku wa kuamkia juzi.
Akisimulia tukio, mwalimu aliyepatwa na mkasa huo, Samwel Mbochi alisema watu hao waliruka ukuta wa nyumba yake na kumvamia na kuanza kumshambulia mwilini na kudai awape pesa.
Alisema kuwa pesa hizo alikuwa ameziandaa kwa ajili ya kununua bidhaa kesho yake kwa kuwa amekuwa akijishughulisha na biashara
ya duka.

Alisema baada ya kuchukua pesa hizo, watu hao walimvamia mpangaji wake katika chumba kingine ambaye pia ni mwalimu na kumbaka kwa zamu kisha kutokomea kusikojulikana.
Afisa upelelezi wa makosa ya jinai mkoani Simiyu, Evance Mwijage jana alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo. Mwijage alisema atawataja watu waliohusika kwenye tukio hilo
mara baada ya kupata taarifa rasmi kutoka polisi. 

CHANZO: NIPASHE


MAGAZETI YA LEO: JUMAMOSI TAREHE 30/08/2014





VIDEO: INSTAGRAM WAANZISHA HYPERLAPSE NA KAMERA YA KIPEKEE KWA MBWA

CHANZO: BBC SWAHILI

YANGA NA OKWI WAITWA NA TFF KWENYE KIKAO

Chini ni barua ambazo TFF wamewaandikia klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi kuwaita kwenye kikao cha kamati.



VIONGOZI WA SHURA YA MAIMAM WAMTEMBELEA DR SLAA

Viongozi wa Shura ya Maimam leo asubuhi wamemtembelea Dr. Slaa ofisini kwake iliyopo mtaa wa Ufipa Kinondoni. Lengo la ziara hiyo ni
kumweleza Dr. Slaa juu ya udhalilishaji wanaofanyiwa Masheikh 19 wanaotuhumiwa kwa kesi ya Ugaidi wakiwa chini ya vyombo vya
sheria.

Hivi karibuni imeripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari kuwa Mashekh hao wamekuwa wakidhalilishwa kijinsia na kuharibiwa sehemu za siri. Viongozi hao wamemwomba Dr. Slaa na Chama chake kuwaunga mkono katika kupaza sauti juu ya udhalilishaji huo na kumwomba ushirikiano katika maswala ya kisheria hasa ikizingatiwa kuwa CHADEMA ni wahanga wa matukio hayo ya udhalilishaji kwa vijana waliobambikwa kesi za ugaidi


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU