Facebook Comments Box

Thursday, August 14, 2014

HADITHI FUPI YENYE MAFUNZO KWA WANA NDOA

Siku moja niliingia nyumbani nikamkuta mke wangu akiniandalia chakula cha usiku. Nilimshika mkono na kumwambia: “Nina jambo ninalotaka kukueleza.” Alikaa na kunisikiliza kwa makini. Dalili za wasiwasi nilikuwa nikizishuhudia machoni mwake. Ghafla nilijikuta katika hali ya kushindwa kukifungua kinywa changu.
Lakini ilikuwa ni lazima ajue ninachokifikiria, hivyo nilipiga moyo konde, nikamwambia kwa upole: “Ninataka tuachane.” Hakuonekana kuudhika kwa hoja niliyokuwa nimeiwasilisha mbele yake, bali aliniuliza kwa sauti ya upole kabisa: “Kwa nini?” Nilijaribu kulikwepa hilo swali, hivyo
alighadhibika sana na kuniambia kwa sauti ya juu: “Wewe si mwanaume!” Usiku ule hatukusemeshana, na muda wote alikuwa akilia. Nilitambua kuwa alitaka kujua kitu gani kimetokea katika ndoa yetu. Lakini sikuweza kumpa jibu lenye kuridhisha; kwa sababu sikuwa na mapenzi naye tena, moyo wangu ulikuwa umetekwa na binti mwingine aitwaye Jane. Nilimsikitikia sana!
Huku nikiwa na hisia za hatia moyoni mwangu, niliandika pendekezo la
talaka ambalo lilieleza kuwa atachukua nyumba yetu, gari na shea ya asilimia 30 ya kampuni yangu. Mke wangu aliitazama karatasi hiyo kisha akaichana na kuitupa kwenye ndoo ya takataka.
Huyu ni mwanamke aliyekuwa ameishi nami kwa muda wa miaka kumi alikuwa
amegeuka kuwa kama mgeni kwangu. Nilisikitika sana na kumuomba radhi kwa kumpotezea muda, rasilimali na nguvu zake lakini sikuweza kutengua kauli yangu kwa sababu nilikuwa nikimpenda sana Jane na nilikuwa nimezama kweli kweli ndani ya huba lake na kuwa teja wa penzi lake. Hatimaye alilia kwa sauti mbele yangu, jambo ambalo nilikuwa nikitarajia kuliona.
Kilio chake kwangu kilikuwa kama faraja. Wazo la talaka lililonitawala kwa wiki kadhaa lilikuwa likizidi kupata nguvu na sasa lilionekana kuwa wazi kabisa. Siku iliyofuata nilirudi nyumbani nikiwa nimechelewa na kumkuta akiandika kiandika kitu mezani. Sikutaka kula chochote zaidi ya kuelekea moja kwa moja kitandani kwa sababu nilikuwa nimechoka sana kutokana na mishemishe za siku hiyo nikiwa na Jane. Niliposhtuka, bado alikuwa hajatoka mezani. Sikujali hata kidogo, nikageuka na kuendelea kuuchapa usingizi. Asubuhi alinipatia masharti ya talaka: hakutaka
mali yoyote kutoka kwangu, bali alitaka kuwe na muhula wa mwezi mmoja kabla ya talaka.
Alitaka kwamba katika kipindi hicho tujaribukuishi kama kawaida kwa kadiri iwezekanavyo. Hoja yake ilikuwa wazi: mtoto wetu alitarajia kufanya mitihani ya shule ndani ya mwezi huo na hakutaka tumchanganye kwa tukio la talaka. Hili nililikubali. Lakini alikuwa na nyongeza:
alinitaka nikumbuke siku ya ndoa yetu nilipomnyanyua kumpeleka chumbani kwetu. Alitaka kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mzima niwe nambeba kila siku asubuhi kumtoa chumbani mpaka mbele ya mlango wa nje ya nyumba. Nilihisi kuwa alikuwa ameshikwa na wendawazimu. Nilikubali ombi lake kwa sababu niliona kuwa mwezi mmoja sio kitu, kwani nilitaka tuachane.
Nilimsimulia Jane kuhusu masharti ya talaka yaliyotolewa na mke wangu. Alicheka sana na kuona kuwa ni upuuzi. “Hata akitumia hila gani lazima apewe talaka,” alisema Jane kwa masihara. Tangu nilipoelezea nia yangu ya kutaka kuachana naye, hatukuwa na uhusiano wa kimwili na mke wangu. Hivyo nilipombeba siku ya kwanza, sote tulionekana kutokuwa na uchangamfu. Mtoto wetu alifurahi na kupiga makofi: “Baba amembeba mama”. Kauli yake ilinipa maumivu moyoni. Kutoka chumbani mpaka barazani, kisha mlangoni, nilitembea mita kumi nikiwa nimembeba mikononi mwangu. Aliyafumba macho yake na kuniambia
kwa upole na ulaini: “Usimwambie mtoto wetu kama tunaachana.” Nilikubali kwa kutikisha kichwa huku
nikiwa nimefadhaika. Nilipofika nje
nilimshusha akaenda kituoni kusubiri basi, nami nikachukua gari langu na kwenda ofisini nikiwa peke yangu. Siku ya pili tulijaribu kutoonesha hali yoyote ya mifarakano. Aliegemea kifuani kwangu nikahisi manukato mazuri ya blauzi yake. Nilibaini kuwa sikuwa nimemtazama vizuri mke wangu kwa muda mrefu. Uso wake ulikuwa umeanza kuwa na mikunjo na nywele zake zilikuwa zimeanza kubadilika. Ndoa yetu ilikuwa imemfanya achoke. Kwa dakika kadhaa niliduwaa na kuwaza kile nilichokuwa nimemfanyia.
Siku ya nne nilipombeba nilihisi aina ya
ukaribu na mvuto ikirejea. Huyu ni mwanamke aliyekuwa amenipa miaka
kumi ya uhai na maisha yake. Siku ya tano na ya sita, kwa mara nyingine, niliona hali ya ukaribu na mvuto fulani ikirejea kati yetu. Sikumsimulia Jane kuhusu hali hii. Kadiri siku zilivyosonga mbele ndivyo nilivyozidi wepesi wa kumbeba. Yumkini ilisababishwa na
ile hali ya kumbeba kila siku kiasi cha kumuona kuwa ni mwepesi. Asubuhi moja alikuwa akichagua nguo ya kuvaa. Alijaribu nguo kadhaa lakini hakupata
inayomfaa. Alishusha pumzi na kusema: “Nguo zangu zote hazinienei,
zimekuwa kubwa”. Nilibaini kuwa alikuwa
amekonda na ndiyo maana niliweza kumbeba kwa urahisi. Nilisikitika kwa
sababu nilihisi kuwa alikuwa amebeba mambo mengi moyoni mwake. Hivyo nilimsogelea na kukipapasa kichwa chake. Ni wakati huo ambapo mtoto wetu aliingia na kusema: “Baba sasa ni muda wa kumbeba mama”. Tukio la kumuona
baba yake akiwa amembeba mama yake
lilimuathiri na kuwa sehemu muhimu sana ya maisha yake. Mke wangu alimuita na kumkumbatia kwa upendo.
Niligeuza uso wangu pembeni, sikutaka
kuangalia tukio hilo nisije nikabadilisha uamuzi wangu wa talaka. Nilimnyanyua na kumbeba mke wangu,nikatembea kutoka chumbani, sebuleni mpaka nje. Aliizungusha mikono yake mizuri shingoni kwangu, nami nikamshikilia vizuri; ilikuwa kana kwamba ni siku ile ya harusi yetu. Lakini wepesi wa mwili wake ulinifanya niwe mwenye huzuni. Siku ya
mwisho nilipombeba niliingiwa na uzito
wa kupiga hatua. Wakati huo mtoto wetu tayari alikuwa shule. Nilimshikilia vizuri na kusema: “Sikuwa nimejua kuwa maisha yetu yamekosa mvuto”. Niliwasha gari kuelekea ofisini, niliamua kupita kwa Jane.
Nilipofika nilitoka haraka bila hata kuubana mlango wa gari. Nilikuwa na wasiwasi nisije nikaghairi nia yangu…
Nikapandisha ngazi. Jane alipofungua
mlango nilimwambia: “Samahani Jane, sitaki kuachana na mke wangu”. Alinitazama kwa mshtuko na kunigusa kwenye paji la uso. “Una homa?” alisema. Niliutoa mkono wake na kumwambia: “Samahani Jane, sitaki kumuacha mke wangu. Yawezekana maisha yangu na mke wangu yalikosa uchangamfu kwa sababu hatukuwa karibu, sio kwa sababu hatukupendana. Sasa nimebaini kwamba kwa kuwa nilimbeba siku ya ndoa yetu, ninapaswa kuendelea kufanya hivyo mpaka kifo kitutengenishe.” Jane alionekana kushtuka sana. Alinizaba kibao, akaubamiza mlango na kuanza kulia. Nilimuacha nikapanda gari na kuondoka. Njiani nilipita kwenye duka la maua nikaagiza shada la maua kwa ajili ya mke wangu. Muuzaji akaniuliza ujumbe unaotakiwa kuandikwa juu ya kadi nikatabasamu na kumwambia aandike: “Kila siku asubuhi nitakubeba mpaka kifo kitakapotutenga nisha”.
Jioni nilifika nyumbani nikiwa na maua mkononi, tabasamu usoni, nikapandisha ngazi mpaka ndani. Nilipofika chumbani mke wangu alikuwa amelala akiwa amefariki dunia. Kumbe alikuwa akipambana na KANSA kwa miezi kadhaa lakini sikujua kwa sababu nilikuwa nimetekwa na Jane. Bila mimi kufahamu, kumbe marehemu mke wangu alijua kwamba muda si mrefu atafariki dunia na alitaka kuniokoa dhidi ya fikra yoyote mbaya kutoka kwa mtoto wetu kama tungeachana muda mfupi kabla ya kifo chake. Angalau machoni mwa mwanangu naonekana kuwa mume
mwenye upendo…
WAPENDANAO NATAKA MJIFUNZE
(1) Wengi wanatengana si kwa sababu hawapendani, bali hawapeani muda wa kusikilizana.
(2)Wengi wanaamini ukiachana na mpendwa wako ni lazima muwe maadui.
(3)Busara ndani ya pendo ni zaidi ya mali na pesa.....
(4) Kaa karibu na mkeo na familia yako muda wote ili ujue nini kinawasibu na uwasaidie katika utatuzi.
(5)Mkeo/mmeo hupenda wewe uwe na furaha hata kama yeye anaumia.


MAGAZETI YA LEO ALHAMISI 14/08/2014

 



ANGALIA JINSI KIBONDE NA GARNER WALIVYO FIKISHWA MAHAKAMANI

Watangazaji Ephraim Kibonde (wa kwanza kushoto) na
mwenzake Gardner Habash (wa pili kulia) wakielekea
kizimbani.

Watangazaji hao wakiongozwa na maofisa wa polisi
kuelekea mahakamani.

...Wakiingia mahakamani.

MTANGAZAJI wa Clouds FM, Ephraim Kibonde na
mwenzake, Gardner Habash wa Times FM leo
wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya
Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kusababisha ajali na
kudharau amri ya polisi na kutoa lugha ya matusi.
Watangazaji hao wamesomewa mashitaka hayo na Wakili
wa Serikali, Salim Mohammed mbele ya Hakimu Aniseta
Wambura.
Kibonde na Gadna wanadaiwa kutenda makosa hayo
Jumamosi ya Agosti 9, mwaka huu saa 12 asubuhi, katika
eneo la Makumbusho, ambapo Kibonde akiwa anaendesha
gari walilokuwa wamepanda aliligonga gari la raia mmoja
wa kigeni (Mzungu) na kukimbia.
Kesi yao imeahirishwa mpaka Septemba 10 mwaka huu
itakaposikilizwa tena.(Picha na Shakoor Jongo / GPL)


MKE WA AFANDE SELE (MAMA TUNDA) AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia hivi pune ni kuwa msanii mkongwe Selemani Msindi maarufu kama Afande sele amefiwa na mke wake. Habari kamili zitakujia hapa baada ya muda mfupi ujao
Afande sele akiwa na marehemu mke wake na mtoto wake Tunda



Wednesday, August 13, 2014

PICHA: MSIKITI WA MTAMBANI UNAUNGUA MOTO SASA HIVI

 

Juu ni picha mbalimbali zikionesha msikiti wa mtambani ukiungua moto. Hii ni sehemu ambayo hutumika katika harakati na kupigania haki waislam Tanzania. Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.
Hili ni pigo kubwa kwa waislam wa tanzania.

Inna lilahi wa inna ilayhi rajiuun.

Sekondari ya kiislam ya Mivumono (Mivuno Islamic Secondary) iliyopo
ndani ya msikiti wa Mtambani Kinondoni B, jijini Dar es Salaam.
Moto huo uliteketeza eneo lililokuwa likitumika kama mabweni ya
wanafunzi wa shule hiyo, maabara na ofisi za walimu, eneo hilo
limeteketea kabisa kiasi kwamba hakuna kilichoweza kuokolewa.
Chanzo cha moto huo kinadaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme
iliyokuwepo kwenye bweni la wasichana wanafunzi wa shule hiyo ila
hadi moto huo unafanikiwa kuzimwa hakuna mtu yeyote aliyepoteza
maisha wala kujeruhiwa.


VIDEO: JINSI YA KUJIKINGA USIPATE EBOLA

Ugonjwa wa Ebola umezuka Afrika ya Magharibi na kuuwa watu zaidi ya elfu moja na kuwa idadi kubwa zaidi kutokea katika historia ya ugonjwa huo. Shirika la afya duniani limetangaza ugonjwa huo kama janga duniani.
Hapa nchini kwetu tanzania bado haujafika ila kuna taarifa za kuwa nchi jirani kama Rwanda umeshafika. Hapa chini ni video ya jinsi ya kujilinda usipate ugonjwa huo.





CHANZO: BBC SWAHILI



MKOLOMBIA ABAMBWA NA DAWA ZA KULEVYA JULIUS NYERERE AIRPORT

Mkuu wa Kikosi maalumu cha kupambana na dawa za kulevya nchini Bw. Godfrey Nzowa akionesha jinsi raia wa Colombia Andres Filipe Ballesteros mwenye umri wa miaka 28 alivyo ficha dawa hizo aina ya cocain ndani ya Belt ya Suruali yake kama anavyoonekana hapo pichani muda mfupi baada ya kutiwa hatiani uwanjani hapo

Bw. Nzowa akionesha jinsi madawa hayo yalivyo shonewa ndani ya belt ya suruali ya mtuhumiwa ambayo alikuwa ameivaa.


PICHA YA CITY TRAIN NDANI YA DAR ES SALAAM



Kuna uwezekano mkubwa watu wa zamani wa hapa jijini Dar es Salaam wanalijua vizuri hili basi lakini leo hii lilikuwa kama kituko wakati likikatiza katika mitaa ya jiji la dar es salaam. Zamani shirika la usafiri dar es salaam (UDA)  walikuwa na mabasi kama haya mengi ambayo yalikuwa msaada mkubwa sana kwa wananchi wa Dar es salaam.



HII NDIO STUDIO YA KISASA YA BBC SWAHILI DAR ES SALAAM

Mkuu wa Habari wa BBC Idhaa ya Ulimwengu, Bi. Nikki Clarke akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kituo cha kurushia Matangazo cha Idhaa ya Kiswahili ya BBC jijini Dar es Salaam, katika Jengo lao lililopo Mikocheni.

Kushoto ni Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Ali Saleh.
Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Ali Saleh (wa tatu kulia) akiwapatia maelekezo Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Dkt. Salim Ahmed Salim na Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ya namna Idhaa hiyo inavyoandaa vipindi yake na inavyopeleka hewani wakati wa hafla ya Uzinduzi rasmi wa Kituo cha kurushia Matangazo cha Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Habari wa BBC Idhaa ya Ulimwengu, Bi. Nikki Clarke akibadilishana mawazo na aliewahi kuwa Mkuu wa Idhaa hiyo, Bw. Tiddo Mhando wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC jijini Dar es Salaam, Hassan Mhelela (kushoto) akizungumza katika hafla hiyo pamoja na kuitambulisha timu yake.

Baadhi ya Wageni waalikwa wakiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wakuu wa BBC waliokuwepo kwenye hafla hiyo, Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa zamani wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Bw. Tiddo Mhando (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Bw. Ali Saleh pamoja na Mtangazaji Sussani Mongi.


taswira za Studio ya BBC swahili jijini Dar es Salaam.
Wadau Salim Kikeke na Nicolas wakipitia habari kabla ya kuipeleka hewani.

BBC Idhaa ya Ulimwengu, imezindua ofisi zake jijini Dar es Salaam. Ofisi za Dar es Salaam zina studio ambazo zinatumika kuandaa matangazo maarufu ya redio ya asubuhi, Amka na BBC, na pia kuendesha tovuti ya bbcswahili.com.

Katika kuadhimisha uzinduzi huo, vipindi vingine viwili vya BBC Idhaa ya Kiswahili, Dira ya Dunia ya redio na ya TV vitaandaliwa kutoka Dar es Salaam katika siku hiyo ya Jumatatu Agosti 11. Ufunguzi wa ofisi za Dar es Salaam ni matokeo ya mikakati ya BBC Idhaa ya Ulimwengu ya kuhamisha uandaaji wa vipindi vya redio na tovuti kutoka London kwenda Afrika Mashariki.

Ofisi mpya ina vifaa vya kisasa vinavyoweza kutayarisha vipindi vya redio, TV na huduma za habari kwa njia ya simu za mkononi. Amka na BBC, kipindi cha nusu saa ambacho hutangazwa Jumatatu hadi Ijumaa humulika matukio na taarifa zitakazojiri katika siku, sasa kitaandaliwa Dar es Salaam na watayarishaji na watangazaji 15.

Ofisi mpya pia zina watayarishaji wanaoandaa taarifa mbalimbali za kanda ya Afrika Mashariki na Kati kwa ajili ya vipindi vya TV vya Focus on Africa na Dira ya Dunia. Mkuu wa Habari wa BBC Idhaa ya ulimwengu Nikki Clarke amesema: 

“Uzinduzi wa ofisi zetu za Dar es Salaam ni hatua kubwa katika safari yetu iliyoanza muda mrefu kidogo, katika kuwapa wanachotaka wasikilizaji katika nchi zinazozungumza Kiswahili, na ambao husikiliza BBC wanapotaka kupata taarifa wanazoziamini na zenye uhakika. 

Takriban watu milioni 12.4 – ambao ni kama nusu ya idadi ya watu wazima nchini Tanzania, husikiliza matangazo ya redio ya BBC kila wiki.

Na sasa moja ya kipindi maarufu cha BBC, Amka na BBC, kimekuja karibu zaidi na wasikilizaji.” Ofisi ya Dar es Salaam, ina studio mbili za redio ambazo zinaweza kutumika na hadi watu sita kwa wakati
mmoja, na hivyo ni muafaka kabisa kwa kipindi kichangamfu cha Amka na BBC kwa ajili ya mijadala na mahojiano ya kuvutia.

Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Ali Saleh anasema : “Ofisi mpya zinatoa nafasi bora kabisa kwa watayarishaji wa BBC nchini Tanzania kuimarisha ukusanyaji wa habari na kutoa taarifa kutoka
katika eneo la Afrika Mashariki na Kati. Amka na BBC itakuwa na uwezo mkubwa zaidi kutoa taarifa na habari mchanganyiko, za Afrika Mashariki na pia za dunia, pamoja na mahojiano ya moja kwa moja na watu mbalimbali, lakini pia makala na habari za kijamii.” Idhaa ya Kiswahili ya BBC imekuwa kitovu cha hatua ya BBC Idhaa ya Ulimwengu ya kuimarisha kuwepo kwake katika sekta ya habari barani Afrika.

Baada ya ufunguzi wa ofisi ya Nairobi mwaka 1998, BBC Idhaa ya Ulimwengu ilikuwa shirika la kwanza la habari la kimataifa kuwa na kituo cha uandaaji habari barani Afrika. Mwaka 2006 Amka na BBC ilihamishwa kutoka London kwenda Nairobi, na BBC Idhaa ya Ulimwengu, kwa mara nyingine tena ikawa shirika la kwanza la kimataifa la habari kuandaa na kutangaza vipindi kutoka barani Afrika.

Katika hatua ya kuhamisha utayarisaji wa vipindi na taarifa za kwenye tovuti, kipindi maarufu cha jioni cha redio, Dira ya Dunia sasa kinatayarishwa Nairobi. Mwisho// Kwa taarifa zaidi wasiliana na afisa wa idara ya mawasiliano ya BBC Idhaa ya Ulimwengu – Lala Najafova, lala.najafova@bbc.co.uk. Kwa wahariri: BBC Idhaa ya Ulimwengu ni shirika la utangazaji la kimataifa lenye idhaa nyingi za lugha mbalimbali zinazotoa huduma ya matangazo ya redio, TV, kwenye mtandao wa internet na pia simu za mkononi. BBC Idhaa ya Ulimwengu hutumia njia mbalimbali kuwafikia wasikilizaji wake wapatao milioni 191 duniani kote. 

BBC huwafikia watu milioni 265 duniani kote kila wiki kwa huduma zake kutoka BBC Idhaa ya Ulimwengu, BBC News TV na bbc.com.

chanzo:full shangwe
Chumba cha Habari cha BBC Jijini Dar.


Tuesday, August 12, 2014

MBUNGE WA CHADEMA AELEZA KWANINI KARUDI BUNGENI


Mh Said Arfi
Na Magreth Kinabo Dodoma; 
Mjumbe wa Bunge  Maalum la Katiba Said Arfi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)amezitaja sababu za kurejea katika bunge hilo, kuwa ni hofu ya  Mwenyezi Mungu.

Aidha Arfi ameitaja sababu nyingine ni kwamba amerudi katikaBunge hilo, ili kuhakikisha kwamba anaisadia nchi kupita katika mchakato wa Katiba mpya kwa amani na utulivu kwa kutumia kipaji chake na kuwatumikia Watanzania. Kauli hiyo imetolewa mjini Dodoma na mjumbe huyo, wakati akihojiwa na kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na Shirika la Utangazaji la Tanzania(TBC).

Akizungumza katika kipindi hicho, huku akinukuu kitabu cha Nabii Musa, Arfi alisema Mwenyezi Mungu hapendezwi na mtu mwenye jeuri na anayejivuna. “Nimejitathimini na kuona mimi mwenyewe nina nafasi gani… maaskofu, mapadre, wachungaji na masheikh. Viongozi wetu wametusii turudi napata kiburi wapi cha kutokurudi,” alihoji Arfi.

Akirejea katika kitabu cha Qruan anasema Mwenyezi Mungu hapendezwi na mtu mwenye kiburi na anayejivuna. Aliongeza kuwa viongozi hao “ wana nafasi kubwa pia wanaheshima ndio maana nimeweza kurudi,””alisema. Mjumbe huyo alisema sasa ni wakati wa kila mtu kueleza ukweli, kwani amerejea katika Bunge hilo, amepata bahati ya kuchangia katika sura ya nne katika kifungu cha 43na 44 kinachohusu haki za msingi. “Nimepata fursa ya kutoa mapendekezo ya haki za wazee nisingewezakuwasilisha kama ningekuwa nje. Pia haki za wafanyakazi,” alisema.

Akizungumzia kuhusu wajumbe wenzake waliosusia Bunge hilo, aliwataka kutanguliza maslahi ya taifa huku akisisitiza kwamba atajitahidi kuwashawishi wajumbe walioko nje ya Bunge hilo ili waweze kurejea. Arfi aliwahakikishia wananchi kuwa  wanawatengenezea Katiba itakayowasaidia kubadilisha maisha ya watu wote.


MAGAZETI YA LEO: JUMANNE 12/08/2014

   
 



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU